Showing posts with label Knowledge. Show all posts
Showing posts with label Knowledge. Show all posts

Wednesday, February 22, 2017

BENEFITS OF KNOWLEDGE AND ADVENTURE FOR EMOTIONAL INTELLIGENCE

Our minds and souls are constantly in need of exploration and discovery. The reason why we act differently and evolve is because our souls seek new horizons. Our minds need to be refreshend and expanded so as we can stable in our actions and in our ways. As it is said Lunacy is doing the same thing the same way and expecting different results.

We act in a lunacy form whenever we fail to expand our minds and let our souls explore its limitlessness. Knowledge is essential for expanding our minds increasing our possibilities and widening the limits that have been set by ignorance. We must grow in knowledge so as to be free. Emotional intelligence being the ability to perceive, assess and manage our emotions is a crucial attribute to our stability as human beings.

If we invest in knowledge while we let our souls experience wonder we invest in the attribute of emotional intelligence. We not only grow in our ability to manage our emotions but we develop control as to how we can relate our knowledge in a practical way to see wonder and adventure.

How can Knowledge and adventure be used simultaneously for emotional intelligence

1. Always read books of a specific topic in the specific moment at the specific place. That's Practical investment of knowledge.

2. Knowledge has to be put into practise, acquiring knowledge without practising it is a wastage of time. Ensure to always acquire the kind of knowledge you can practise.

3. Explore new horizons, listen don't let your life become a routine of activities that don't allow your soul to explore and experience the adventures of your life time.

4. Visit nature occasionally and meditate on it. This will open your mind and trigger your soul to explore the adventures of naturality.

Always remember that without emotional intelligence we will always be unstable human beings. If emotions aren't managed and assessed skillfully then we will always be human beings of so many imbalances and we will live life not realising the beauty of it.


Sunday, August 28, 2016

HAKUNA AJALI, KILA JAMBO LINA KUSUDI

"Huwa hakuna ajali.. Bali kuna kusudi ambalo bado hatujalitambua "-Deepak Chopra

Katika moja ya mafundisho yake mhamasishaji na mkufunzi wa maswala ya kujitambua Deepak chopra alisema huwa hakuna ajali bali kuna kusudi ambalo bado hatujalitambua. Kauli hii ni yenye mtazamo chanya hasa pale tunapokosa majibu ya baadhi ya maswali tuliyonayo katika maisha.

Siku zote kusudi la jambo hufungwa katika muda na maarifa. Kuna usemi ambao wengi wetu huwa tunao hasa pale tunapokosa majibu huwa tunasema limetokea la kutokea tukiweka mtazamo kwamba jambo ilo ni kama muujiza au limetokea kutoka hali ya kutokuwepo. Lakini inatupasa tubadili mitazamo.

Katika kila jambo tusilopata majibu tutambue kuwa kuna kusudi ambalo halijadhiirishwa bado kwa wakati huo hivo inatupasa kutambua yatupasa kuwekeza katika kujikuza kimaarifa huku tukiendelea kutambua kuwa muda muafaka tutakuwa watu wenye ufahamu zaidi juu ya yale yanayotokea.

Hakuna jambo linalotokea kwa ajali...lazima kuwe na kusudi...iwe ni kukukumbusha jambo, kukufundisha jambo au kukuimarisha katika jambo. Lakini ni lazima tujenge tabia ya uvumilivu hadi pale tunapopata maarifa mapana ya jambo hilo.

Muda mwingi tumekuwa ni watu wa kuchukua maamuzi bila maarifa yeyote tunapokuwa katika hali ya kukosa ufahamu juu ya kusudi fulani. Inabidi turuhusu muda na kukua katika maarifa.Kuna ambao wanajifunga katika makubaliano baada ya dakika kumi na tano za hisia kali bila kuruhusu muda kupoza hisia hizo na kupata maarifa juu ya kusudi hilo kabla hawajachukua maamuzi.

Chukua muda wako vizuri huku ukikua ktk maarifa kutambua kusudi la jambo maana hakuna jambo linalotokea kama ajali.

Friday, August 26, 2016

KWANINI HATUTENDEI KAZI TUNAYOYAJUA

Changamoto kubwa tuliyonayo ni kujua sana, kusoma sana lakini hatutendi yale tunayoyajua. Ni sawa na kuingiza vitu vingi ndani yako lakini utoaji wake au utendaji wake ni mdogo. Wengi hawasongi mbele kwasababu wanajua sana lakini wanatenda kidogo.

Huwa najiuliza maswali mengi hasa pale napokijua kitu lakini nashindwa kukitendea kazi. Huwa najiuliza nini tatizo? Hasa hasa pale unapokuja kuona mtu mwingine akikitendea kazi kile ulichokijua wewe na akapiga hatua.

Hata maandiko husema muwe watendaji wa neno na sio wasikilizaji tu. Na yule ajuaye jambo na kutolitenda huhesabika kwake kama uovu.. Kwanini? Kwasababu ufahamu unapaswa kukuweka huru na sio kukufanya mfungwa. Unapojua kitu ni nafasi kwako kukifanyia kazi ili kikusaidie. Kukijua tu na kuishia pale haisaidii.

Ni kwanini watu hatutendei kazi yale tunayoyajua? Baada ya kutafakari na kuchunguza kwa makini nimekuja kugundua sababu kuu inayopelekea watu tusitendee kazi tunachokijua imefungwa katika mitazamo yetu na tabia zetu za ndani.

1. MTAZAMO BINAFSI: Hii ndiyo changamoto ya kwanza inayosababisha watu wasitendee kazi wanayoyajua. Watu wengi wana mitazamo binafsi iliyo asi ambayo hupambanua na kuua nguvu ya utendaji, ukiwa na mtazamo asi siku zote utakichambua unachokijua na kuua msukumo wako kukitendea kazi. Ni muhimu sana kujenga mtazamo binafsi ulio chanya.

2. KUKOSA UJASIRI : Watu wengi hawatendei kazi wanayoyajua kutokana na kukosa ujasiri wa kutenda. Wengi wamefungwa katika mitazamo ya watu wengine mfano ndugu wa karibu nk. Mawazo yao yakiyumbishwa kidogo wanakosa ujasiri wa kutenda. Zaidi ya vyote ni muhimu kuwa na ujasiri wa kufanya jambo hata ukikutana na vipingamizi. Lazima ujiamini katika kutenda.

3. IMANI HABA : Hili neno limekuwa lenye kufahamika sana hata katika vitabu vya dini, watu wengi hushindwa kutenda mambo kutokana na kuwa na imani isiyo thabiti. Lazima jambo unalolifahamu ulijengee msingi wa kiimani. Haiishii kulitambua bali inakupasa uliamini. Usipoliamini huwezi kulifanyia kazi

4. KUKOSA NIDHAMU: Nidhamu ni tabia ya ndani ambayo mtu huijenga. Nidhamu itakuwezesha kustahimili na kutoka katika comfort zone ( uwanda wa starehe) na kustahimili misukosuko na kuweza kusonga mbele. Nidhamu itakulazimu kufanya jambo hata usilojisikia kulifanya huku ukiwa na taswira ya matokeo chanya.

5. KUKOSA MIFUMO YA UTENDAJI: Hii ni changamoto kuu hasa pale unaposhindwa kuandaa mifumo ya utendaji kuhamisha nadharia kuwa vitendo. Mifumo ya utendaji ni malengo, muda, nguvu na uwezeshaji mwingine. Usipojenga mifumo bora ya utendaji itakuwia vigumu kutenda yale unayoyajua. Yakupasa uwekeze zaidi.
Pasipo kutathmini kwa makini hizo sababu tutaendelea kuwa watu wa kujua mambo pasipo kutenda.