Showing posts with label Progress. Show all posts
Showing posts with label Progress. Show all posts

Thursday, May 18, 2017

IMANI NI MSINGI WA AMANI YA NAFSI

Imani ni kuwa na hakika ya mambo yasiyoeleweka au ambayo hayajabainishwa kwa wakati huo. Imani hukupa nuru ya kutambua mafumbo ya kinafsi na maswali yasiyo na majibu yenye kuleta taharuki katika nafsi.

Nafsi inaweza kupitia mambo fulani ambayo yanaikosesha amani na kuifanya ibaki katika hamaki kutojua ni nini kinachofuata au nawezaje kutoka katika hali fulani ya mkwamo wa kihisia au kimtazamo na kiakili. Hapo ndipo imani huja kuleta amani.

Imani inatakiwa iongoze hisia na iziweke katika hali ya utulivu. Ni vigumu kupata tulizo la kihisia bila kuweka mfumo bora wa kiimani, Ukitazamia kutoka katika mkwamo huo, ukitazamia utulivu wa hisia na ukitazamia uzuri na mambo mema yajayo.

Muda wote imani hujengeka katika msingi imara wa hatma ya kesho yenye furaha, faraja na uzuri na pia hujengeka katika faida ya leo katika mazingira hayo magumu. Imani hutazama fundisho, hutazama uzuri na  hutazama uimara unaotokana na ugumu na changamoto husika.

Siku zote ukitaka kuwa na amani katika nafsi yako boresha mfumo wako wa imani, boresha mfumo wako wa kuamini, jikite katika kutengeneza imani zenye tija, imani zenye kukujenga na kukuimarisha. Na ukishapata msingi husika iache imani hiyo iamuru hisia zako zitii.

Imani ikisema nitatoka katika hii hali, ikasema nitavuka katika hili daraja la maumivu, ikasema nitapata kilicho bora, Hakuna hisia ya maumivu itakayoweza kukushikilia kwa muda mrefu au hata kukuzamisha. Utakuwa ni mtu mwenye amani muda wote.

Thibitisha imani zako kwa kuzipa msingi imara kwa kuzifanya sheria za nafsi yako. Imani juu ya uzuri wako, imani juu ya stahiki yako na yale unayoyatarajia na yenye kukupa amani ya nafsi, hakikisha unajijenga na kujithibitisha katika imani hizo kwa kusimama bila kuyumba kama hisia za taharuki na uchungu zikija.

Huwezi kuwa na amani ya nafsi kama huna imani na hali fulani, kama huna imani na jambo fulani, kama huna imani na watu fulani. Ni vyema ukajiimarisha katika imani na siku zote hakikisha imani yako inajengeka katika kweli. Huwezi jenga imani kwa kitu cha uongo. Imani lazima isimame katika misingi ya kweli, fikra chanya, ubora wa nafsi na utu.

Monday, November 21, 2016

KIWANGO CHA MAANDALIZI YAKO KIKOJE?

Kuna dhana inayosema njia pekee ya kutabiri hatma yako ni kuitengeneza na ukishindwa kujiandaa unajiandaa kushindwa. Ni dhana zenye ukweli kabisa katika maisha yetu ya kila siku. Maandalizi ni jambo ambalo linaweza kukuonyesha hatma ya mchezo, yawezekana dhana hii isiwe na uhalisia wa jumla katika maeneo mengine hasa pale watu wanapojiandaa lakini bado wanashindwa. Jambo la muhimu ni je unajiandaa kwa kipimo gani na pia unajiandaa katika msingi upi.

Kutokujiandaa na kujiandaa kwa jambo lisilo na uwiano na hatma yako inaweza leta changamoto sawa jambo hilo linapofika. Kuna mambo yanaweza fika ukashindwa kuyahimili kwasababu hukuwa na maàndalizi imara kuyahimili hayo mambo.

Nataka nizungumzie juu ya maswali ambayo watu wanakuwa nayo hasa wanapokuwa wakisubiria jambo fulani litokee, mara nyingi hukaa wakitazama wengine ambao wanategemea jambo hilo hilo au lenye usawa wa namna hiyo wakisonga mbele na kulipata huku wao wakiendelea kusubiri, Maandalizi yanaweza kuwa ya muda mrefu au muda mfupi inategemea na uzito wa jambo lako.

Ukienda katika sehemu ya mgahawa ukaagiza chakula cha thamani sana au chakula kinachohitaji maandalizi utasubiri sana na pengine utashangaa mwingine anayekuja kuomba kinywaji akiandaliwa na kupata mapema, ukadhani labda unafanyiwa makusudi, hapana maandalizi ya chakula chako yanahitaji muda kwasababu umeomba chakula kinachohitaji umakini, muda na uwekezaji mkubwa kukiandaa, hivo haimaanishi kuwa umefanya makosa kuagiza chakula hicho.

Wengi wamejikuta wakibadilisha matazamio yao na kuamua kufanya mambo tofauti na matazamio yao kwasababu maandalizi yao yamekuwa ya muda mrefu. Tatizo halikuwa katika muda wa maandalizi bali tatizo lilikuwa katika uwezo wa kusubiri na misukumo ya kulitwaa jambo lile kwa wakati huo.

Cha msingi ni kuhakikisha unajiandaa katika kila jambo unalolihitaji, usiseme nitajiandaa hilo jambo likija, muda mwingine unaweza jiandaa lakini usifanikiwe kwa wakati huo, haimaanishi maandalizi yako hayakuwa na mantiki, hapana endelea na maandalizi. Katika maandalizi kuna tabia zinaimarika, kuna uwezo unajengeka ndani mwako ambao utakuwezesha kuwa na ufanisi katika hilo jambo litakapokuja.

Tambua kwamba maandalizi siku zote ni jambo endelevu, usichukie vipindi vya maandalizi na kila wakati jua unajiandaa kwa jambo fulani. Haijalishi maandalizi yako yanachukua muda gani. Usiupime muda wa maandalizi pima kiwango cha maandalizi yako. Maandalizi huongeza thamani yako na uwezo wako

Monday, November 14, 2016

USITAFAKARI MAJUTO, TAFAKARI FUNDISHO

Katika maisha tunapitia mambo mengi, njia nyingi na tunakutana na vitu vingi, nafasi nyingi na hata vipindi vingi ambavyo tunatakiwa tufanye maamuzi juu ya mambo kadha wa kadha tunayokutana nayo. Kama binadamu wenye uhuru wa kufanya uchaguzi na utashi kila wakati huwa tunatumia njia zozote zile tulizonazo kufanya maamuzi.

Maamuzi yetu ndiyo ambayo hutengeneza hatima ya maisha yetu au matokeo yanayokuja baada ya hapo. Maamuzi mazuri huleta matokeo mazuri na maamuzi mabaya pia huleta matokeo mabaya. Kila mtu ameshapitia hali ya kufanya maamuzi na kila mtu ametumia uhuru wake wa kinafsi kufanya maamuzi. Changamoto kubwa ni matokeo ya maamuzi yetu na jinsi tunavopokea matokeo ya maamuzi yetu.

Maisha siku zote ni safari endelevu yenye changamoto mbali mbali na safari hiyo huwa vumilivu pale inapoendeka kwa maarifa na ujuzi wa wapi unaelekea. Maisha huhitaji dira na dira ndo itakuelekeza kasi ya kwenda nayo hata njia za kupita kufikia hatma yako. Maarifa ni muhimu sana.

Mara nyingi tumekuwa na mapokeo tofauti tofauti ya matokeo ya maamuzi yetu ambayo wengi wetu yametusababishia kukwama kwa muda mrefu katika dimbwi la maumivu na tukaishia kulalamika, kulaumu, kuwa na mitazamo hasi na hata kupata matatizo mbali mbali ya nafsi. Mara nyingi tumekuwa watu wa majuto badala ya mafunzo

Jambo la muhimu ni kutafakari mafunzo uliyoyapata na uyatumie hayo kama mawe ya kukanyagia kwenda mbele, usikae unajilaumu au unatafakari kwa makosa ya nyuma hata kama yameleta matokeo mabovu katika maisha, badala ya kusema ningejua tafakari aya sasa umejua utafanya nini. Huwezi kubadilisha makosa ya nyuma ila unaweza kufanya mabadiliko ili makosa ya nyuma yasijirudie.

Wengi tunakaa zaidi tunatafakari majuto badala ya kutafakari mafunzo na kufanya yanayohitajika kusonga mbele halafu baadaye unajikuta unarudia kosa lile lile au unapita tena njia ile ile. Badili mtazamo hata kama matokeo ya maamuzi yako mabaya yanaendelea kukutesa kuwa na ujasiri wa kusema nitafanya hivi badala ya ningefanya hivi.

Kumbuka kila mtu ameshafanya kosa fulani ambalo limemgharimu au linamgharimu hadi sasa lakini cha msingi ni kutafakari funzo badala ya majuto.

Tuesday, October 25, 2016

UTUMIE VEMA MUDA WA KUSUBIRI

Moja ya changamoto katika maisha ni pale ambapo matarajio yetu yanachelewa, pale ambapo unasubiri jambo fulani likamilike. Ni sawa na kupanda mbegu chini ya ardhi na kusubiri mti uchipuke. Muda mwingi tumekuwa tukiona wakati huo ni mrefu na hata kuingiwa na hisia za huzuni na kuchoka pale tunapoona matokeo yamekawia.

Inapaswa ujifunze kuwa wakati wa kusubiri huwa mrefu na wenye uchungu pale ambapo kwa muda huo unasimama katika mambo mengine huku ukisubiria. Hata mkulima huwa akipanda mbegu hakai akisubiria. 

Jizamishe katika mambo uyapendayo hadi usahau kuwa ulikuwa unasubiria jambo fulani.
Subira yenye furaha ni ile subira ambayo unaifanya huku unaendelea kufanya mambo uyapendayo. Hata katika mahusiano yakupasa kuwekeza pia kuhusiana na nafsi yako wakati uko katika mahusiano na mtu mwingine, mahusiano haimaanishi uiache nafsi yako katika ukame ukisubiria muitikio wa nafsi unayohusiana nayo.

Mfano umepanga kukutana na mtu na hajafika huwa unafanya nini huku ukisubiri?, mfano upo katika foleni sehemu huwa unafanya nini ukisubiria?, mfano umeingia katika mgahawa chakula kimechelewa huwa unafanya nini ukisubiria? Dunia haitakiwi kusimama wakati wewe ukisubiria muitikio wa mtu au jambo. Endelea kufurahisha nafsi yako kwa kufanya yale uyapendayo la sivyo utakuwa unaingiwa na huzuni ukiona jambo linachelewa.

Unasubiri jambo gani katika maisha, iwe katika mahusiano au eneo lolote, usisimamishe dunia ya nafsi yako ukisubiria, kuna mambo mengi unaweza kufanya wakati unasubiria kuna vitabu hujasoma, kuna tabia na vipawa unaweza vikuza, kuna marafiki unaweza wasiliana nao, unaweza kwenda kutembea. Kuna mambo mengi nafsi yako ingependa kuyafanya na bado hujayafanya...tumia huo muda.

Jifunze pia kutembea na kitabu kidogo cha kunakiri mambo au yafundishe macho yako kuona uzuri wa mambo yanayokuzunguka, jenga akili ya kudadisi, andika mambo unayoyaona, changamoto mbalimbali, sikiliza audio za kukujenga, waweza enda kusaidia mtu mwingine, tembelea marafiki na jamàa na mzungumze, kuna sehemu unaweza itajika kusubiri muitikio wa jambo fulani, wewe endelea kuishi dunia iliyomo nafsini mwako.

Hata katika mahusiano watu wamekuwa wakilaumiana kwakuwa husubiri miitikio ya watu fulani lakini huchelewa kuitikia, wakati unasubiri waweza fanya mambo mengine, waweza andika mambo yanayokufurahisha katika mahusiano nk, jizamishe katika mambo ya nafsi yako na vipawa vyako, wekeza katika ufahamu wako.

Monday, October 17, 2016

BADILI TASWIRA WAKO

Changamoto kubwa katika maisha ni kuwa na mitazamo mibovu. Taswira uliyonayo juu ya mambo inatokana na hazina uliyoweka moyoni mwako. Jinsi unavowekeza ndani yako ndo jinsi unavojenga taswira nzuri katika maisha yako. Mambo unayoyaona mazito kwako inatokana na nguvu au hazina uliyowekeza ndani yako.

Usipowekeza katika kukua siku zote hautakuwa mtu mwenye taswira nzuri....ukiwa na hazina ndogo au nguvu ndogo ya kiroho siku zote taswira yako itakuwa na tatizo...na ukikosa taswira nzuri utakuwa ni mtu mwenye kulaumu na kuona kama maisha hayakutendei haki. Maisha yapo siku zote lakini wenye nguvu ndio wanaoweza kustahimili hivo wekeza kuwa na nguvu katika nafsi yako.

Chukua kila tatizo linalokuja kwako na ulione kama jiwe la kwenda kiwango kingine. Chukua maumivu na uyaone kama fursa ya kujiimarisha zaidi roho yako. Usilalamike, wewe ni kiongozi wa maisha yako na kila jambo hufuata mkondo unaouweka wewe. Hukuzaliwa umfurahishe kila mtu hivo acha kufungwa katika mawazo au shuruti za watu. Unatakiwa uwe huru.

Ili taswira yako iwe nzuri ibadilishe, unapokuwa unatafuta taswira ya picha na camera lazima uhakikishe picha ya maisha yako unaiweka katika mraba, kuna vitu vya kuondoa katika taswira hiyo, unaweza kubadili umbali nk. Vivyo hivo katika maisha yako ukitaka upate taswira unayoitaka kuna watu inabidi uachane nao, kuna mambo inabidi uachane nayo, kuna vitu inabidi uviondoe katika taswira. Haijalishi vikoje kama unaona havipo katika taswira yako yakupasa uviondoe.

Usipokua, siku zote taswira yako itakuwa ndogo, kuna mambo mengine hujayajua au kuna mambo mengine huyaoni kwasababu huna taswira nzuri na hii hutokana na kutokuwa na hazina na nguvu ndani yako.


Saturday, September 17, 2016

JENGA MSUKUMO WA NDANI

Binadamu yeyote hutenda mambo kutokana na msukumo fulani. Misukumo iko ya aina mbili. Kuna msukumo wa nje na msukumo wa ndani. Watu wengi hutenda mambo kutokana na msukumo wa nje ambao unahusisha mazingira fulani au faida na matokeo fulani. Sio jambo baya kuwa na misukumo ya nje inayopelekea wewe kutenda jambo lakini changamoto ni kwamba ukiwa na msukumo wa nje zaidi inaweza pelekea kuwa na mguso tofauti.

Misukumo ya nje inaweza kubadilika muda wowote na hii itakupelekea kupoteza kabisa ile ari ya utendaji. Unaposukumwa kutenda jambo kwa ajili ya faida fulani itapelekea kuwa na hamaki pale hasara inapokuja au kukosekana kwa faida husika. Ukisukumwa zaidi na mazingira jua hayo mazingira yanaweza kubadilika muda wowote mfano unaweza pangiwa kutoka Dar es salaam kwenda dodoma. Hii itakusumbua sana katika kupata uwiano wa kihisia.

Ni muhimu kujenga msukumo wa ndani uliojengwa katika msingi wa mambo matatu..Moja ni Uongozi wa maisha yako, Thamani na mwisho ni kusudi.

Uongozi wa maisha yako ni msukumo wa ndani ulio na mtazamo na uthibiti wa muelekeo wa maisha yako. Ukijua ya kwamba wewe ndio mwenye jukumu ya kutengeneza muelekeo wa maisha yako itakupa msukumo wa utendaji kwa maana utajua kila wakati kuwa unalolifanya linatengeneza muelekeo wa maisha yako.

Thamani ni msukumo wa ndani uliojijenga katika mtazamo kuwa kila jambo unalolitenda unalifanya ili likujengee uwezo na ufanisi, likufanye mtu mwenye uwezo zaidi na mwenye ufanisi zaidi...uwe mtu wa thamani na bora. Ndio maana faida kubwa katika kazi sio unachokipata baada ya kazi bali ni unavokuwa baada ya kazi ( Thamani yako)

Kusudi ni msukumo wa jambo uliojijenga katika mtazamo kuwa unafanya jambo kwasababu lina maana kwako na jamii inayokuzunguka. Utasukumwa kufanya jambo kwa sababu lina maana kubwa ndani yako na kwa jamii yako.

Ukiwa na misukumo hiyo mitatu ya ndani katika kila jambo ulifanyalo, kila siku utakuwa na ari na msisimko kufanya mambo na hautopoteza hamu ya kuamka asubuhi kuiendea siku kwa furaha.

Tuesday, September 6, 2016

POWER OF PASSION IN PROGRESS

The greatest virtue one can have that assures progress is passion. Passion is the driving force of motivation. Without passion the heart lacks meaning, the actions lacks enthusiasm and the mind lacks creativity.

When you have passion you inspire innovation. When you always work in the circle of the usual that means you lack the passion.

Passion inspires excellence. If you lack the passionate heart concerning something then it isn't worth it. The bible says God looks for a passionate heart. When you are passionate about something you go the extra mile.

Passion develops Perseverance  which means you can push forward even when all odds are against you. Passion brings about internal peace and joy to do what you want. 

Which means you do something with the satisfaction. As the self actualization concept of Abraham Maslow with passion you have satisfaction which is the highest need of a person.

Always understand your passion and most of all develop passion about the things you do.

How can you develop passion to progress:-
1. Discover your talents and abilities : the greatest discovery a man can do isn't discovering an ipad, light bulb or anything tangible but the discovery of one's talents and abilities. Never undermine your talent discovery. A talent is something you do easily and effectively and excellently with little strength but brings maximum satisfaction and joy. A talent isn't a hobby..a hobby is something you love to do but a talent is something you can do excellently that others cant.

2. Love yourself : Realise that you are a limited edition and you are a miracle in this world. You aren't an accident nor is your life an accident. Troubles and mistakes don't define you but only shape you, people's opinion don't define you and you have so much greatness in you. You can do anything you put your mind into and you deserve all what life can offer, You deserve to be happy, live a good life and have good relationships. If you begin to look at yourself in that focus you begin to develop passion to progress.

3.  Have a Positive mindset: You need to have a mindset that things are working for good and you aren't at a disadvantage. Develop that positive mindset about life. Ignore the negative opinions that always come into your mind most of the times.
If you want to progress you must develop passion.

Friday, September 2, 2016

JINSI YA KUKABILIANA NA VIKWAZO

Moja ya changamoto tunazokumbana nazo katika maisha ni vikwazo vinavotukwamisha kufikia malengo au yale tunayoyahitaji. Kuna vikwazo vya nje na vikwazo vya ndani. Maana halisi ya kikwazo ni jambo linalokuzuia kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

Vikwazo vinaweza kuwa watu, tabia au hata mifumo ya utendaji. Unapokuwa mtu wa kutafakari maono yako na hapo ulipo utatambua ni aina gani ya kikwazo unachokumbana nacho. Kikwazo siku zote kina namna yake ya kukiangalia ili uweze kukiondoa au kukivuka.

Lazima ujitafakari ni kikwazo cha namna gani unachokumbana nacho na ni nini unaweza kufanya kukivuka hicho kikwazo. Pasipo kukaa chini kujitafakari vikwazo vinaweza kuwa sababu yako ya kulaumu, kulalamika na kujenga mtazamo asi wa maisha.

Njia pekee ya kuvuka kikwazo ni lazima kwanza ujue na uwe na picha halisi ya lengo lako au hatma yako, kisha lazima utulize akili na kisha ukitazame kikwazo kilichopo mbele yako na ukitambue kuwa ni kikwazo cha namna gani.

Kisha ni muhimu sasa kuangalia kikwazo hicho kina mguso gani katika mfumo wako wa kukabili mambo, je hicho kikwazo kinahitaji ufanye mabadiliko gani kwa upande wako, kisha yakupasa uangalie fursa zilizopo za kuweza kukivuka hicho kikwazo.

Kumbuka usipokaa ukatafakari utakuwa unavamia vikwazo na vinakuwa na mguso wa ndani katika nafsi yako kupelekea wewe kukosa kabisa ari na hata morali ya kufanya mambo kupelekea kukata tamaa na kupoteza kabisa mtazamo chanya na maisha.

Sunday, August 28, 2016

HAKUNA AJALI, KILA JAMBO LINA KUSUDI

"Huwa hakuna ajali.. Bali kuna kusudi ambalo bado hatujalitambua "-Deepak Chopra

Katika moja ya mafundisho yake mhamasishaji na mkufunzi wa maswala ya kujitambua Deepak chopra alisema huwa hakuna ajali bali kuna kusudi ambalo bado hatujalitambua. Kauli hii ni yenye mtazamo chanya hasa pale tunapokosa majibu ya baadhi ya maswali tuliyonayo katika maisha.

Siku zote kusudi la jambo hufungwa katika muda na maarifa. Kuna usemi ambao wengi wetu huwa tunao hasa pale tunapokosa majibu huwa tunasema limetokea la kutokea tukiweka mtazamo kwamba jambo ilo ni kama muujiza au limetokea kutoka hali ya kutokuwepo. Lakini inatupasa tubadili mitazamo.

Katika kila jambo tusilopata majibu tutambue kuwa kuna kusudi ambalo halijadhiirishwa bado kwa wakati huo hivo inatupasa kutambua yatupasa kuwekeza katika kujikuza kimaarifa huku tukiendelea kutambua kuwa muda muafaka tutakuwa watu wenye ufahamu zaidi juu ya yale yanayotokea.

Hakuna jambo linalotokea kwa ajali...lazima kuwe na kusudi...iwe ni kukukumbusha jambo, kukufundisha jambo au kukuimarisha katika jambo. Lakini ni lazima tujenge tabia ya uvumilivu hadi pale tunapopata maarifa mapana ya jambo hilo.

Muda mwingi tumekuwa ni watu wa kuchukua maamuzi bila maarifa yeyote tunapokuwa katika hali ya kukosa ufahamu juu ya kusudi fulani. Inabidi turuhusu muda na kukua katika maarifa.Kuna ambao wanajifunga katika makubaliano baada ya dakika kumi na tano za hisia kali bila kuruhusu muda kupoza hisia hizo na kupata maarifa juu ya kusudi hilo kabla hawajachukua maamuzi.

Chukua muda wako vizuri huku ukikua ktk maarifa kutambua kusudi la jambo maana hakuna jambo linalotokea kama ajali.

Friday, August 26, 2016

ACHA KUJILINGANISHA NA WATU WENGINE

Moja ya changamoto ambayo huwafanya watu wengi wasiishi katika furaha ni tabia ya kujilinganisha na watu wengine. Washindi hawajipimi kwa maendeleo ya wengine bali kwa maendeleo waliyonayo jana. Bill gates muanzilishi wa Microsoft aliwahi kusema kuwa kujilinganisha na wengine ni kujitukana mwenyewe.

Ukipenda kujilinganisha na watu wengine kuna hatari ya kudharau uwezo wako na kuanza kutazama  madhaifu yako na hii itakujengea tabia ya kutofurahi hata kwa vitu ulivonavo huku ukiwa unatazama zaidi vitu vya wengine au mafanikio ya wengine.

Ukijilinganisha na wengine utaua msukumo wako wa mafanikio kwasababu kuna ambao wamekutangulia katika safari ya maendeleo, kuna ambao wamepitia vikwazo vingi au kuna ambao wamepitia njia rahisi zaidi hivo si busara kujilinganisha na watu.

Weka malengo yako na ujipime kwa malengo yako na siyo malengo ya watu wengine. Kila mtu ana malengo na mitazamo yake na dhana kuu ya maendeleo ni mfumo uliotumika na sio matokeo. Matokeo hayawezi kuwa sawa kama mifumo ni tofauti hivo ukitazama tu matokeo unaweza ingiwa na hasira kwa kutopata matokeo sawa na mwenzako.

Ukipenda kujilinganisha ma wengine utaishi kama kivuli na hautokuwa na utambulisho wako. Wanaoshindwa huangalia zaidi wanaoshinda badala ya kuangalia ushindi. Usiridhike na mafanikio yako ya nyuma...unaweza kuwa zaidi ya hapo.

JE UNAWEZAJE KUJENGA TABIA YA KUTOJILINGANISHA NA WENGINE

1. JITAMBUE : Inakupasa kujitambua wewe ni nani, vipawa vyako, uwezo wako, maarifa yako na yale unayoweza kuyafanya. Jipime kwa hayo mambo na ujiulize Je unaweza kufanya zaidi ya hapo?

2. JENGA MIFUMO: Siku zote husipokuwa na mifumo ya utendaji yako iliyojengwa na mitazamo uliyonayo kuhusu maisha lazima utajaribu kujilinganisha na matokeo yanayopatikana na mifumo inayotumiwa na wengine.

3. EPUKA MANENO YA WATU : Mara nyingi tunajikuta wahanga wa kujilinganisha na wengine kutokana na misukumo tunayoipata kutoka kwa watu wanaotuzunguka kama wazazi, watu wa karibu n.k...Lakini lazima uwe na uwezo wa kutotafakari sana maneno ya watu hasa wale wanaokushinikiza kuwa kama watu wengine.

4. KUMBUKA WEWE NDIO KIONGOZI WA MAISHA YAKO: Inakupasa utambue wewe ni kiongozi wa maisha yako, maisha yako ni kama kampuni hivo yakupasa kujua mtu pekee ambayo ana wajibika zaidi ni wewe. Hata mzazi wako sio kiongozi wa maisha yako zaidi yako wewe. Hii itakusaidia kuwa na mtazamo wa ubunifu zaidi juu ya maisha yako.

5. ANGALIA MBELE : Dereva bora ni yule anayeangalia mbele anapoendesha gari na sio kuangalia pembeni wanaomu overtake au walio ktk mwendo sawa na yeye. Siku zote usitumie muda wako mwingi kutazama wanaoku overtake. Unaweza jifunza jambo lakini si busara kujilinganisha na waô

Kumbuka kipimo pekee cha mafanikio yako ni malengo yako na uwezo wako na sio kujilinganisha na wengine.


Friday, August 19, 2016

FEAR OF THE UNKNOWN

The Fear of the unknown is the Psychological paralysis caused by mystery of the unknown. Its one of the greatest challenges to progress because it kills the enthusiasm and the morale to progress to the clouds of what you haven't experienced or what you don't know.

This has paralysed many people with big ideas, it has paralysed individuals and caused them to be ANTAGONISTS to the FORCE OF CHANGE. Human being delights in COMFORT ZONE and any idea of CHANGE that hasn't been experienced before is often excused by the fear of the unknown.

But you can overcome the FEAR OF THE UNKNOWN by evaluating the vision and putting it down into realistic attributes, then GRAB on FAITH and DISCIPLINE while exercising the POSITIVE MINDSET.
Negativity gives power to the FEAR OF THE UNKNOWN. In life we need to understand that we either CHANGE willfully or THE FORCE OF CHANGE affects us violently leaving us with scars. Now that requires us to overcome the fear of the unknown.

The unknown is a mystery and it should be approached with enthusiasm and the joy of exploration...for whatever you don't know holds a part of your soul you haven't discovered yet...Pursue the experience and let Go of the fear of unknown.

Believe that God is there in the unknown ready to make it known to you. Let your life be of adventures and explore new experiences and overcome the fear of the unknown that keeps you from knowing the unknown.

Monday, August 15, 2016

HUWEZI FANIKIWA ZAIDI YA MAWAZO YAKO

Watu wengi hupenda mafanikio na kukua lakini hawafanikiwi wala kukua. Kwasababu ya sheria moja ambayo ni kwamba huwezi fanikiwa zaidi ya mawazo yako. Maisha yako ya nje ni zao la mawazo yako.

Hakuna jambo linaloweza kutokea kama hujalifikiria kwa wakati wowote katika maisha yako. Unaweza kupenda kufanikiwa lakini je ulishawahi kufikiria na kutafakari mafanikio. Huwezi kuwa na fikra za ukomo halafu uwe na ziada. Mfumo wako wa fikra unadhiirika kwa kauli zako na mitazamo yako juu ya jambo fulani.

Ukishakiri kwamba jambo haliwezekani ni kwasababu umefikiria haliwezekani na halitokuja kuwezekana kwako hadi ubadilishe jinsi unavoliwaza hilo jambo. Hapo pekee ndo utaweza kufungua ubongo wako juu ya njia za kuliweza.

Myles munroe alishawahi kusema ugumu wa jambo fulani unatokana na ufahamu wako juu ya jambo husika hivo badala ya kushikiria mtazamo wako, wekeza kupata ufahamu zaidi juu ya hilo jambo. Huwezi ishi nje ya mitazamo yako maana mitazamo yako siku zote itachonga muundo wa maisha yako.

Friday, August 12, 2016

PROBLEMS AS OPPORTUNITIES

The factor that triggers your creativity and activates your positive mind is pressing problems. It is only when you are experiencing the pressure of problems and obstacles that you are motivated to perform at your mental best. Facing and solving the inevitable problems and difficulties of life make you stronger and smarter, and bring out the very best in you.

Most people do not understand the nature of problems. Problems are a normal and necessary part of life. They are inevitable and unavoidable. Problems come in spite of your best efforts to avoid them. Problems, therefore, come unbidden.

The only part of a problem over which you have any control is your response to your problems. Effective people respond positively and constructively to problems. In this way, they demonstrate that they have developed high levels of “response-ability”. They have developed the ability to respond effectively when unexpected or undesired difficulties occur.

Problems of all kinds bring out your very best qualities. They make you strong and resourceful. The more pressing your problems, and the more emotion you invest in solving those problems,the more creative you will become. Each time you solve a problem constructively, you become smarter and more effective. As a result,you prepare yourself for even bigger and more important problems to solve.