Showing posts with label attitude. Show all posts
Showing posts with label attitude. Show all posts

Wednesday, August 23, 2017

UDHIBITI BINAFSI

Nafsi isiyo na udhibibiti binafsi ni sawa na mji usiokuwa na kuta

Moja ya changamoto kubwa ya kinafsi ni ukosefu wa udhibiti binafsi. Udhibiti binafsi na uwezo wa kinafsi wa kuratibu na kuzuia kila ambacho kinaweza kuingia katika nafsi husika na hapo ndipo tabia ya udhibiti binafsi inapokuja. Ulimwengu ni kama jalala yenye kila aina ya mambo, yenye kuharibu nafsi, yenye kujenga, yenye kuleta tabia na mitazamo asi au chanya, hivo ukitaka usalama wa kinafsi ni lazima uwe na udhibiti binafsi.

Haijalishi kwamba umepewa macho, kinywa au masikio, uimara wako unatokana na kutumia milango hiyo katika mambo ya msingi pekee. Udhibiti binafsi sio tu kudhibiti haja za mwili wako bali pia ni kudhibiti milango inayoingiza habari ndani yako. Huwezi kuwa na uimara kama ni mtu wa kutazama kila kitu, mtu wa kusikiza kila kitu, mtu wa kuchangia kila kitu, mtu wa kufatilia kila kitu au mtu wa kuongea kila kitu, hapana. Hautakuwa mtu mwenye utashi mzuri wa kihisia na hata kiakili.

Kuna tamaa za kinafsi kama shauku ya kutaka kufahamu mambo yasiyo na tija kwako, au kutaka kusikiza maswala yasiyoongeza thamani kwako au kutaka kufatilia watu wasio katika mlengwa wa yale yanayokuhusu. Ni tamaa tu ya kinafsi kutaka kuburudishwa na yanayowatokea wengine pengine hata kama hayana faida kwako. Usichofahamu ni kwamba unaijaza nafsi yako na mambo ambayo yanaongeza mzigo au yanakupa mtazamo ambao hauna tija kwako. Hakuna changamoto kubwa kama uchaguzi. Pale unapokuwa katika mazingira yanayokupasa uchague kuburudisha nafsi au kujenga nafsi.

Tafuta burudani ya kinafsi kwa mambo yanayohusiana na mambo ya msingi yanayokujenga. Kuwa na udhibiti binafsi, na wengi ambao hawana udhibiti binafsi wamejikuta katika matatizo mengi ya msongo wa mawazo au hata mikwaruzano isiyo na tija na watu wengine. Hata kama jambo lipo mbele yako sio lazima uburudishe nafsi yako kulifatilia. Hata kama hoja iko mbele yako sio lazima kuburudisha nafsi yako kuchangia. Hata kama maneno yanasemwa juu yako sio lazima kuruhusu nafsi yako kujibu, hata kama una shauku ya kuwafatilia watu sio lazima uruhusu nafsi yako kuwafatilia. Kama jambo badala ya kukusaidia linakujaza ujinga dhibiti nafsi yako na uliache.

Hakika usipokuwa mtu wa kudhibiti nafsi yako utakuwa mtu mwenye kubeba kila aina ya uchafu.

Thursday, May 18, 2017

IMANI NI MSINGI WA AMANI YA NAFSI

Imani ni kuwa na hakika ya mambo yasiyoeleweka au ambayo hayajabainishwa kwa wakati huo. Imani hukupa nuru ya kutambua mafumbo ya kinafsi na maswali yasiyo na majibu yenye kuleta taharuki katika nafsi.

Nafsi inaweza kupitia mambo fulani ambayo yanaikosesha amani na kuifanya ibaki katika hamaki kutojua ni nini kinachofuata au nawezaje kutoka katika hali fulani ya mkwamo wa kihisia au kimtazamo na kiakili. Hapo ndipo imani huja kuleta amani.

Imani inatakiwa iongoze hisia na iziweke katika hali ya utulivu. Ni vigumu kupata tulizo la kihisia bila kuweka mfumo bora wa kiimani, Ukitazamia kutoka katika mkwamo huo, ukitazamia utulivu wa hisia na ukitazamia uzuri na mambo mema yajayo.

Muda wote imani hujengeka katika msingi imara wa hatma ya kesho yenye furaha, faraja na uzuri na pia hujengeka katika faida ya leo katika mazingira hayo magumu. Imani hutazama fundisho, hutazama uzuri na  hutazama uimara unaotokana na ugumu na changamoto husika.

Siku zote ukitaka kuwa na amani katika nafsi yako boresha mfumo wako wa imani, boresha mfumo wako wa kuamini, jikite katika kutengeneza imani zenye tija, imani zenye kukujenga na kukuimarisha. Na ukishapata msingi husika iache imani hiyo iamuru hisia zako zitii.

Imani ikisema nitatoka katika hii hali, ikasema nitavuka katika hili daraja la maumivu, ikasema nitapata kilicho bora, Hakuna hisia ya maumivu itakayoweza kukushikilia kwa muda mrefu au hata kukuzamisha. Utakuwa ni mtu mwenye amani muda wote.

Thibitisha imani zako kwa kuzipa msingi imara kwa kuzifanya sheria za nafsi yako. Imani juu ya uzuri wako, imani juu ya stahiki yako na yale unayoyatarajia na yenye kukupa amani ya nafsi, hakikisha unajijenga na kujithibitisha katika imani hizo kwa kusimama bila kuyumba kama hisia za taharuki na uchungu zikija.

Huwezi kuwa na amani ya nafsi kama huna imani na hali fulani, kama huna imani na jambo fulani, kama huna imani na watu fulani. Ni vyema ukajiimarisha katika imani na siku zote hakikisha imani yako inajengeka katika kweli. Huwezi jenga imani kwa kitu cha uongo. Imani lazima isimame katika misingi ya kweli, fikra chanya, ubora wa nafsi na utu.

Saturday, May 6, 2017

ALWAYS KEEP A JOYFUL DEMEANOR

Our strength lies in our ability to always keep a joyful demeanor in the face of our problems-Nickvaleries

Life has its ups and downs, Life has negative situations that can hit us or hurt us and we find it hard to be joyful but joy has to be founded from our souls.

When we believe in our worth and have the mentality that there is always something better ahead and that we will always receive the desires of our souls then we generate a joyful spirit and demeanor.

There is no reason to stay in sorrow and pain when you know that the best is out there heading your way and you ought to be ready and step towards it. Pain and sorrow will try to drown you in a state of emotional stagnation but rise up, smile and say to yourself that am heading to my best. Darkness is for a night but joy comes in the morning.

Always choose to be joyful and find joy at whatever costs by changing your belief from a victim to a victor of circumstances. If things change dont stay there drowning yourself. Get up and heal your soul of the pain and choose to keep a joyful demeanor.

Just say to yourself it is well with my soul then believe that you are heading for the best out there. Tell your heart you are not hurt but you are strengthened then find your rythm and be happy. Smile for your beauty and peace awaits.

The Universe will always smile back if you smile at it. Its just a matter of time till you find love, happiness and joy again. But for now keep a joyful demeanor and attitude.

Tuesday, May 2, 2017

USICHUKULIE KILA JAMBO KIHISIA

Ukitaka kuwa na furaha usipende kuchukulia kila jambo kinafsi au kihisia. Kuna mambo mengine ni ya kifikra tu na yamekaa kimtazamo tu ambayo hayatakiwi kuchukuliwa kihisia.

Ukitaka kuwa na utashi wa kihisia na uweze kuratibu hisia zako katika mlengwa chanya yakupasa kuziacha hisia zako katika mfumo tulivo kadri uwezavyo. Kuna mambo ukiyachukulia kihisia utaziweka hisia zako kwenye mfumo wa taharuki kwa wakati mwingi na itakupunguzia msisimko wa maisha ulio katika muundo chanya.

Je wawezaje kutochukulia mambo kihisia? Tambua kuwa kila wazo au mtazamo unapaswa kupokelewa kiakili na kuratibiwa kabla ya kusukumwa na hisia fulani. Ni vizuri ukiratibu mawazo na mitazamo unayopokea na kuiratibu kabla ya kujua ni hisia gani uiachilie ili isukume hilo jambo.

Ni muhimu sana kulishikilia wazo au mtazamo katika mfumo chanya hata kama limekuja katika muundo hasi. Lione hilo wazo kama njia ya kukuboresha, yaone hayo maoni kama njia ya kukuboresha kisha yape hisia chanya ndipo uyapokee. Usikubali kuanza kupokea kihisia wazo ambalo hujariratibu kwa akili.

Mfano mtu anaweza kukwambia jambo ambalo unaona kabisa linaweza lisiwe chanya kwako, badala ya kulipokea kwa hisia hasi jaribu kuliona ilo jambo kama wazo la kukuboresha na sio kukuharibu, kisha chukua hisia ya amani na furaha kwa kutambua kuwa hilo wazo limekuja kukuboresha..kisha chukua hisia ya morali na ari ya kulitafutia ufumbuzi na kulishughulikia hilo jambo na sio vinginevyo. Ukilipokea kama vile limekuja kukuumiza utaingiwa na taharuki ya kinafsi pengine hata kujenga ukuta kulizuia hilo suala na kuonekana kuwa ni mtu dhaifu kinafsi pengine hata mtu hasiyependa kuambiwa ukweli.

Nakushauri tena usilipokee kila jambo kihisia kabla ya kuriratibu kiutashi na kiakili ili kukujenga utashi wa kihisia itakayokupa furaha wakati wote.

Sunday, April 23, 2017

TAFUTA AMANI YA NAFSI

Hakuna jambo lenye msingi katika uimara na utashi wa nafsi kama amani ya nafsi - Nickvaleries

Huwezi kukua katika utashi wa nafsi pasipo kuwa na amani ya nafsi. Imani ikikaa katika nafsi humuwezesha mtu kustahimili misukosuko ya nje kwasababu kinachoweza kuzamisha meli sio bahari bali maji yanayoingia ndani ya meli.

Ukiweza kuiacha nafsi yako katika usalama kwa kujenga ukuta kuzuia yale yanayotokea yasiondoe amani ya nafsi utaweza kustahimili mengi. Ukikosa amani lazima utakosa imani na ukikosa imani hata utendaji wako na maneno yako yatakwenda kinyume na uhalisia.

Jiulize ni mambo gani ambayo unayaruhusu katika nafsi yako...Je yanaimarisha ngome za utulivu wako au yanabomoa amani ya nafsi yako na kukupa hali ya taharuki. Waweza kuwa na vyote ukakosa amani na ukikosa amani ukakosa imani huweza kuwa na furaha.

Hakuna furaha mahali palipokosa amani...Huwezi kuwa na furaha ya nafsi au kufurahia yale mazuri yanayokuzunguka kama ukikosa amani.  Tafuta kuwa na amani na jiimarishe kinafsi ukiziimarisha ngome za nafsi yako.

Jitahidi kujenga ngome zenye usalama ndani yako kiasi cha kusimama imara kinafsi hata kama mazingira ni yenye taharuki..sikiliza ulimwengu una taharuki na ukikosa amani jua huwezi kuwa na furaha.

Amani inaweza patikana kwa kuimarisha misingi ya uaminifu, mawasiliano, utashi wakihisia na utu. Tambua kwamba kila jambo linafanyika kuwa jema na wewe ni mwenye hatma njema na kuna mambo mengi mazuri ambayo yako mbele yako.

Taswira yako ni ya muhimu sana ukitaka kuwa na amani. Je unaangalia nini na unasikiliza nini? Hakikisha umejiimarisha kuratibu kila kinachoingia katika nafsi yako.

Usipende kuyapa muda mwingi mawazo na mazingira yanayoondoa amani yako. Itenge nafsi yako ili iwe na amani.


Saturday, March 25, 2017

MUDA WAKO WA UPEKEE NA NAFSI YAKO

Ukitaka kuwa na furaha anza kwa kufurahia muda wako wa upekee.

Moja ya changamoto tulizonazo kama binadamu ni upweke. Upweke sio ukosefu wa wenza au watu wa kutuzunguka. Upweke ni pale mtu anaposhindwa kuufurahia upekee wake na anaposhindwa kuwa na uhusiano na uhalisia wa nafsi yake.

Kuna malalamiko mengi unasikia hata katika mahusiano mmoja wao anasema nilijihisi mpweke ndo maana nilikusaliti, au mwingine anaingia katika ulevi au hata mikanda ya ngono kwa sababu ya upweke. Tafsiri yetu ya upweke ni kukosa watu wa kutengeneza muungano wa kinafsi au watu wa kuburudisha nafsi zetu.

Nafsi ya binadamu kila wakati inahitaji kurutubishwa kwa kutengewa muda wa kupata uwepo. Nafsi yako ni utu wako wa ndani. Mtu wako wa ndani anahitaji wewe umtengee muda kumsikiliza, kumdadisi, kuzungumza naye, kumburudisha na hata kumponya na aina yeyote ya maumivu.

Lazima ujitengee muda wako wako bora wa kutengeneza mguso wa kimaelewano na nafsi yako. Watu wengi wameshindwa kuwa watu wa namna hiyo kupelekea kupigwa na upweke kila wakati anapokosa mguso wa nje wa watu wanaomzunguka.

Rafiki yako wa kwanza na wa karibu ni nafsi yako. Itengee muda nafsi yako ili ipate ukaribu wako. Na wakati wa kuzungumza na nafsi yako jua kwamba unaongea na mtu wako wa karibu. Acha kuongea na nafsi yako kwa ukali au kuihukumu kwa makosa ya nyuma. Itie moyo nafsi yako, ikumbushe uwezo wako. Panda mbegu chanya ndani ya nafsi yako, itie moyo, iponye kwa makosa ya nyuma na iahidi mambo mazuri huko mbele, iburudishe kwa lugha nzuri yenye mguso chanya lakini kuu kuliko yote iweke huru.

Watu wengi wamekuwa wakitumia wakati wao wa upekee kwa kulala, kuangalia mitandao ya kijamii au hata kutafuta magenge ya umbea kutafuta jambo la kufanya kuondoa upweke nk. Huo sio wakati wake. Huo ni wakati wa kujenga uhusiano na nafsi yako. Ni sawa na aina yeyote ya uhusiano. Lakini uhusiano wako na nafsi ndiyo jambo la msingi kwanza.

Ukiwa na tabia ya kuwa na muda mwingi na nafsi yako hautokuwa mtu wa kulalamika upweke. Na hautokuwa mtu wa kutafuta vileta msisimko vya nje kama pombe, anasa na ngono pale unapojihisi mpweke. Utaufurahia muda wako wa upekee, nafsi yako itarutubishwa na utakuwa ni mtu mwenye furaha muda mwingi.

Angalizo ni kwamba katika muda wako wa upekee na nafsi yako hakikisha unatengeneza mazingira chanya. Huwezi kutengeneza mazingira hasi ya mawazo na hisia hasi au muingiliano na mambo yasiyojenga halafu utegemee nafsi yako itajiachilia. Nafsi yako itajenga ukuta wa kujihami maana ndivo mwanadamu alivo kiakili katika maisha yanayoonekana kama mapambano.

Pia usipende kuipa nafsi yako maumivu yasiyokuwa na sababu na mara nyingi pale akili yako inaposhindwa kuendana na misingi ya nafsi yako. Na usipende kuipa nafsi yako vifungo kwa kufuata njia ambazo unajua nafsi yako haiwi huru kuchanua.

Sunday, March 12, 2017

HOW TO DEAL WITH FEAR

Do you know that fear is false evidence appearing real? Sometimes in life you will be faced with situations whereby there will be evidences that are false appearing real. Fear will torment you and leave you paralysed. The only cure to fear is faith. Believe beyond circumstances. 

Clear your mind of the Past : You will always be free as your mind is free. The battlefield is always in your mind. Its a point where strongholds of the past are. The strong holds of fear and other dissapointments. Experience should make you wiser in terms of strategies and how you perceive life. But always free your mind as much as possible.

Something is about to happen in your life: Things happen all the time, good or bad but its always dark before dawn. We pass through darkness to experience the light. We pass through trouble to appreciate calmness. No darkness comes after darkness until afternoon passes. Always believe that the next phase of your life will always be better than the previous. Try to find the rainbow after the storm because its there. Dont be afraid that later will be like the former. There will always be changes in every stage of your life.

Find beauty and peace: You will never be happy unless you are at a state of beauty and peace and tranquility. We often look at the beauty without but not the beauty within. We all want to be in tune with our inner self. Our core values and our inner being, but we often times try to find this in the wrong places. We should always be in the quest to find beauty and nirvana and where its connected.

Monday, January 16, 2017

GHARAMA NA KIPIMO CHA UVUMILIVU

Je wajua kila jambo bora huja na gharama ya uvumilivu. Kila jambo unalohitaji katika maisha huja na gharama ya uvumilivu huku ukikua katika nidhamu katika hicho kipindi cha uvumilivu. Kuna wakati unaweza dhani unaishi katika ndoto pale unapozungumza mambo pasipo kuyaona katika uhalisia.

Imani ni kuwa na uhakika wa mambo ambayo unayo katika fikra lakini bado hayajadhiirika. Unaweza omba msitu lakini ukapata mbegu ya msitu na ukaanza kujiuliza hii mbegu naifanyia nini. Unaweza kuwa na maono ya kujenga familia bora yenye kila hitaji muhimu likiwa limekamilika lakini ukajikuta unapata mwenza ambaye amekamilika katika hitaji la kinafsi lakini mahitaji ya kimali bado inakubidi uvumilie pengine hata uwekeze muda zaidi. Ni wewe kutambua kuwa hiyo uliyonayo ni mbegu bora inayohitaji udongo mzuri ili ichipue yale unayohitaji.

Hitaji la nafsi ni changamoto kubwa na wengi wamekuwa wakipata mahitaji mengine lakini wamekuwa wakiishi pasipo kuridhika kwakuwa mahitaji ya kinafsi wamekuwa wakiyakosa. Tambua kuwa kuna nyakati ambazo uvumilivu na imani yako itawekwa katika kipimo ili kuimarika katika uthabiti wa kimaamuzi. Kila jambo huwa zuri kwa muda kama likijengwa juu ya uaminifu, maono na nia thabiti ya kulisababisha lile jambo litokee katika uhalisia wake.

Lazima ufike kipindi ambacho imani yako itakuwa katika kipimo, lazima ifike kipindi utajiuliza je haya mambo ninayoyatazamia ni ndoto tu za mchana au kweli nitakuja kuyathibitisha. Unapofika katika kipindi hicho uimara wako na imani yako na fikra chanya ndizo zitakazokuvusha kuyapata yale unayoyahitaji na kuyatazamia.

Hakuna ndoto kwa mtu mwenye dhamira ya dhati na kila wakati anahangaika kutafuta njia za kutekeleza yale anayoyaona katika maono yake. Bali ni hatma ya muda na uvumilivu wa huyu mtu akisimama imara katika kutegemea yaliyo bora na yale anayoyatazamia. Usijione kuwa mwenye ndoto tu pengine labda unatazamia mambo ambayo kwa sasa huwezi yapata. Tambua kuwa dhamira ya dhati na utayari wa kujitoa huku ukichanganya na uvumilivu ukiendelea kukua kinafsi vitathibitisha ndoto zako na maono yako.

Wednesday, January 11, 2017

WEKEZA KATIKA UIMARA WA NDANI

Nyumba imara ni ile yenye msingi imara. Msingi mara nyingi hufukiwa chini lakini ndio uimara wa jengo zima ulipo. Vivyo hivyo uimara wako kwa mambo yanayoonekana unatokana na uimara wako wa ndani, uimara wa nafsi. Japo nje waweza onekana imara lakini kipimo pekee cha uimara wako wa ndani ni mtikisiko.

Mtikisiko mkubwa utakaopata ni pale ambapo misingi yako ya ndani itatikiswa. Pale ambapo utawekwa katika mazingira ambayo yatakubidi upime mitazamo yako, upime sheria zako, upime utaratibu wako na kuu kuliko yote upime utambulisho wako. Na ndio maana katika kipindi cha mtikisiko unaweza poteza dira ya utambulisho wako, imani yako na hata utaratibu wako.

Mtikisiko unapoingia lazima uingie uzito wakati huo huo inaingia hali ya hamaki na taharuki. Hapo ndipo utajikuta unafanya maamuzi ambayo hayana faida kwako, hapo utajikuta unaingiwa na ukungu katika macho yako ya ndani ya maono yako.

Hali hiyo ni ya kawaida hasa pale unapotoka katika mfumo mmoja kwenda mwingine, kawaida moja kwenda nyingine. Pale unapotaka kuishi mitazamo yako na ndoto zako kwa mkupuo. Pale unapotaka kukimbia kabla hujapasha joto miguu kwa kutembea. Ni vema ukapasha joto miguu yako na kufurahia kabla hujaanza kukimbia.

Uhuru wa nafsi unahitaji nidhamu na maono yaliyo sambamba na uhalisia. Jaribu kwenda kwa utaratibu lakini ukiwa na uharaka wa kifikra kuchukua maamuzi. Kuwa muwazi juu ya hali yako na utafute watu wachache ambao watakuchoma sindano ya hamasa na watakuamini. Ambao wako tayari kusimama na kukupa moyo.

Unaweza kujiimarisha kwa kuendelea kujipa hamasa na kuwa na fikra chanya, ukichukulia kila changamoto kama njia ya kujiimarisha. Usitafute kujipa kisingizio kama unajua unaweza kujiimarisha. Kila wakati ongeza nguvu yako ya ndani kwa kusimama tena hata kama umechoka. Misuli huja kwa kuongeza zaidi, kujiinua zaidi na kuamini ipo siku mambo yatakuwa mazuri.

Sunday, November 20, 2016

LEARN TO IGNORE

The race of life is the one with a lot of obstacles, a lot of hindrances and a lot of oppositions, we all know that and we all have experienced that at some point in life, but there comes the most critical of all a lot of intimidations. If you havent master the art of ignoring voices then you will always fall victim.

When you are walking your walk always know that there are people who will come to intimidate you and try to misfocus you with words. Listen always be ready for that for people will hit you where it hurts you the most, sometimes even people you cant imagine but always guide your heart and mind. Many have grabbed a victim mindset simply because they take everything thrown unto them personal

Don't be intimidated...Learn to ignore, choose not to give full attention to distractions, Its obvious that some will be people very close to you in whom there opinions can have a big impact in you, but one of the greatest thing you need to do is detach yourself from the emotions brought about by people. Its true that you might sometimes fall prey in the predatorial world but stand up, ignore the predators and move on. What doesnt kill you makes you stronger.

Just because people are close doesn't mean that their opinions of you will always be right. Don't let the pressure get into you...Don't be intimidated, learn to ignore the impacts of their words. Learn to ignore, Ignore the negative feelings, ignore the negative emotions. Ignore what seems to bring you down. I challenge you to ignore those voices that keep running through your mind all the times telling you that you are somebody's victim. No you arent. Train your mind to cancel off and ignore.

Say to yourself, i choose to ignore all distractions. One African proverb says a lion doesn't turn back when dogs bark, also the noise of frogs doesn't hinder the elephant from drinking water from the stream. When you have an understanding of what people go through then it wont trouble you when they voice out their opinions out of emotions. Just ignore and move on. Choose to mind your own business and move on. No need to give an airtime to the calls that dont compliment you. Focus on the good. 

Tuesday, October 25, 2016

UTUMIE VEMA MUDA WA KUSUBIRI

Moja ya changamoto katika maisha ni pale ambapo matarajio yetu yanachelewa, pale ambapo unasubiri jambo fulani likamilike. Ni sawa na kupanda mbegu chini ya ardhi na kusubiri mti uchipuke. Muda mwingi tumekuwa tukiona wakati huo ni mrefu na hata kuingiwa na hisia za huzuni na kuchoka pale tunapoona matokeo yamekawia.

Inapaswa ujifunze kuwa wakati wa kusubiri huwa mrefu na wenye uchungu pale ambapo kwa muda huo unasimama katika mambo mengine huku ukisubiria. Hata mkulima huwa akipanda mbegu hakai akisubiria. 

Jizamishe katika mambo uyapendayo hadi usahau kuwa ulikuwa unasubiria jambo fulani.
Subira yenye furaha ni ile subira ambayo unaifanya huku unaendelea kufanya mambo uyapendayo. Hata katika mahusiano yakupasa kuwekeza pia kuhusiana na nafsi yako wakati uko katika mahusiano na mtu mwingine, mahusiano haimaanishi uiache nafsi yako katika ukame ukisubiria muitikio wa nafsi unayohusiana nayo.

Mfano umepanga kukutana na mtu na hajafika huwa unafanya nini huku ukisubiri?, mfano upo katika foleni sehemu huwa unafanya nini ukisubiria?, mfano umeingia katika mgahawa chakula kimechelewa huwa unafanya nini ukisubiria? Dunia haitakiwi kusimama wakati wewe ukisubiria muitikio wa mtu au jambo. Endelea kufurahisha nafsi yako kwa kufanya yale uyapendayo la sivyo utakuwa unaingiwa na huzuni ukiona jambo linachelewa.

Unasubiri jambo gani katika maisha, iwe katika mahusiano au eneo lolote, usisimamishe dunia ya nafsi yako ukisubiria, kuna mambo mengi unaweza kufanya wakati unasubiria kuna vitabu hujasoma, kuna tabia na vipawa unaweza vikuza, kuna marafiki unaweza wasiliana nao, unaweza kwenda kutembea. Kuna mambo mengi nafsi yako ingependa kuyafanya na bado hujayafanya...tumia huo muda.

Jifunze pia kutembea na kitabu kidogo cha kunakiri mambo au yafundishe macho yako kuona uzuri wa mambo yanayokuzunguka, jenga akili ya kudadisi, andika mambo unayoyaona, changamoto mbalimbali, sikiliza audio za kukujenga, waweza enda kusaidia mtu mwingine, tembelea marafiki na jamĆ a na mzungumze, kuna sehemu unaweza itajika kusubiri muitikio wa jambo fulani, wewe endelea kuishi dunia iliyomo nafsini mwako.

Hata katika mahusiano watu wamekuwa wakilaumiana kwakuwa husubiri miitikio ya watu fulani lakini huchelewa kuitikia, wakati unasubiri waweza fanya mambo mengine, waweza andika mambo yanayokufurahisha katika mahusiano nk, jizamishe katika mambo ya nafsi yako na vipawa vyako, wekeza katika ufahamu wako.

Sunday, September 4, 2016

PATA MAPUMZIMKO UONGEZE UFANISI

Moja ya mambo ambayo unatakiwa ujijengee katika maisha yako ni kupumzisha akili yako. Akili ambayo inakosa mapumziko huwa na uzito kuchukua hatua na hata kupata majibu ya maswali yanayokuzunguka.

Kupumzika ni zaidi ya kulala au kutofanya kazi bali kupumzisha akili ni kuacha kwa muda kufanya mambo fulani au kujishughulisha kwa mambo fulani. Maisha bila mapumziko hukosa msisimko na kuna wakati utajikuta bila ari ya utendaji kwasababu hukuweza kuupa mwili na akili mapumziko.

Muda wa kupumzika sio muda wa kuendelea kutumia simu au kuangalia runinga. Unachofanya pale ni kuendelea kuishughulisha akili na kujiweka wazi kwa fikra asi zinazochosha akili. Muda wa mapumziko ni muda wa kuweka pembeni stress na mawazo juu ya misukosuko na changamoto zinazokuzunguka.

Kuna watu ambao husema kupumzisha akili hakuyafanyi matatizo yaondoke, ni kweli lakini kupumzisha akili ni kuiwezesha kupata majibu ya matatizo hayo. Usidhani kuwa kupumzika ni kupoteza muda au kuwa mzembe.

Kuna usemi unasema kuwa "more than working hard, work smart", bila akili nguvu hupotea. Lazima akili ipumzishwe ili ilete ufanisi unaotakiwa. Njia nzuri ya kupumzika ni wakati wa kukaa kufurahia uzuri wa maisha na kutafakari mema.

Maandiko husema kuwa siku ya saba Mungu alipumzika na kufurahia uumbaji wake. Wakati wa mapumziko ni wakati wa kufurahi uzuri wa maisha. Katika wakati huu iache akili yako ifurahie uzuri wa maisha na mambo mazuri. Wengine hujitenga kabisa kwa muda na watu wengine.

Ukiona unakosa furaha ya maisha na msisimko wa kazi jiulize ni wakati gani uliopumzika, ni wakati gani umepumzisha nafsi yako, mara ya mwisho kufurahia uzuri wa maisha na kutafakari mazuri ni lini?

Friday, August 26, 2016

KWANINI HATUTENDEI KAZI TUNAYOYAJUA

Changamoto kubwa tuliyonayo ni kujua sana, kusoma sana lakini hatutendi yale tunayoyajua. Ni sawa na kuingiza vitu vingi ndani yako lakini utoaji wake au utendaji wake ni mdogo. Wengi hawasongi mbele kwasababu wanajua sana lakini wanatenda kidogo.

Huwa najiuliza maswali mengi hasa pale napokijua kitu lakini nashindwa kukitendea kazi. Huwa najiuliza nini tatizo? Hasa hasa pale unapokuja kuona mtu mwingine akikitendea kazi kile ulichokijua wewe na akapiga hatua.

Hata maandiko husema muwe watendaji wa neno na sio wasikilizaji tu. Na yule ajuaye jambo na kutolitenda huhesabika kwake kama uovu.. Kwanini? Kwasababu ufahamu unapaswa kukuweka huru na sio kukufanya mfungwa. Unapojua kitu ni nafasi kwako kukifanyia kazi ili kikusaidie. Kukijua tu na kuishia pale haisaidii.

Ni kwanini watu hatutendei kazi yale tunayoyajua? Baada ya kutafakari na kuchunguza kwa makini nimekuja kugundua sababu kuu inayopelekea watu tusitendee kazi tunachokijua imefungwa katika mitazamo yetu na tabia zetu za ndani.

1. MTAZAMO BINAFSI: Hii ndiyo changamoto ya kwanza inayosababisha watu wasitendee kazi wanayoyajua. Watu wengi wana mitazamo binafsi iliyo asi ambayo hupambanua na kuua nguvu ya utendaji, ukiwa na mtazamo asi siku zote utakichambua unachokijua na kuua msukumo wako kukitendea kazi. Ni muhimu sana kujenga mtazamo binafsi ulio chanya.

2. KUKOSA UJASIRI : Watu wengi hawatendei kazi wanayoyajua kutokana na kukosa ujasiri wa kutenda. Wengi wamefungwa katika mitazamo ya watu wengine mfano ndugu wa karibu nk. Mawazo yao yakiyumbishwa kidogo wanakosa ujasiri wa kutenda. Zaidi ya vyote ni muhimu kuwa na ujasiri wa kufanya jambo hata ukikutana na vipingamizi. Lazima ujiamini katika kutenda.

3. IMANI HABA : Hili neno limekuwa lenye kufahamika sana hata katika vitabu vya dini, watu wengi hushindwa kutenda mambo kutokana na kuwa na imani isiyo thabiti. Lazima jambo unalolifahamu ulijengee msingi wa kiimani. Haiishii kulitambua bali inakupasa uliamini. Usipoliamini huwezi kulifanyia kazi

4. KUKOSA NIDHAMU: Nidhamu ni tabia ya ndani ambayo mtu huijenga. Nidhamu itakuwezesha kustahimili na kutoka katika comfort zone ( uwanda wa starehe) na kustahimili misukosuko na kuweza kusonga mbele. Nidhamu itakulazimu kufanya jambo hata usilojisikia kulifanya huku ukiwa na taswira ya matokeo chanya.

5. KUKOSA MIFUMO YA UTENDAJI: Hii ni changamoto kuu hasa pale unaposhindwa kuandaa mifumo ya utendaji kuhamisha nadharia kuwa vitendo. Mifumo ya utendaji ni malengo, muda, nguvu na uwezeshaji mwingine. Usipojenga mifumo bora ya utendaji itakuwia vigumu kutenda yale unayoyajua. Yakupasa uwekeze zaidi.
Pasipo kutathmini kwa makini hizo sababu tutaendelea kuwa watu wa kujua mambo pasipo kutenda.

ACHA KUJILINGANISHA NA WATU WENGINE

Moja ya changamoto ambayo huwafanya watu wengi wasiishi katika furaha ni tabia ya kujilinganisha na watu wengine. Washindi hawajipimi kwa maendeleo ya wengine bali kwa maendeleo waliyonayo jana. Bill gates muanzilishi wa Microsoft aliwahi kusema kuwa kujilinganisha na wengine ni kujitukana mwenyewe.

Ukipenda kujilinganisha na watu wengine kuna hatari ya kudharau uwezo wako na kuanza kutazama  madhaifu yako na hii itakujengea tabia ya kutofurahi hata kwa vitu ulivonavo huku ukiwa unatazama zaidi vitu vya wengine au mafanikio ya wengine.

Ukijilinganisha na wengine utaua msukumo wako wa mafanikio kwasababu kuna ambao wamekutangulia katika safari ya maendeleo, kuna ambao wamepitia vikwazo vingi au kuna ambao wamepitia njia rahisi zaidi hivo si busara kujilinganisha na watu.

Weka malengo yako na ujipime kwa malengo yako na siyo malengo ya watu wengine. Kila mtu ana malengo na mitazamo yake na dhana kuu ya maendeleo ni mfumo uliotumika na sio matokeo. Matokeo hayawezi kuwa sawa kama mifumo ni tofauti hivo ukitazama tu matokeo unaweza ingiwa na hasira kwa kutopata matokeo sawa na mwenzako.

Ukipenda kujilinganisha ma wengine utaishi kama kivuli na hautokuwa na utambulisho wako. Wanaoshindwa huangalia zaidi wanaoshinda badala ya kuangalia ushindi. Usiridhike na mafanikio yako ya nyuma...unaweza kuwa zaidi ya hapo.

JE UNAWEZAJE KUJENGA TABIA YA KUTOJILINGANISHA NA WENGINE

1. JITAMBUE : Inakupasa kujitambua wewe ni nani, vipawa vyako, uwezo wako, maarifa yako na yale unayoweza kuyafanya. Jipime kwa hayo mambo na ujiulize Je unaweza kufanya zaidi ya hapo?

2. JENGA MIFUMO: Siku zote husipokuwa na mifumo ya utendaji yako iliyojengwa na mitazamo uliyonayo kuhusu maisha lazima utajaribu kujilinganisha na matokeo yanayopatikana na mifumo inayotumiwa na wengine.

3. EPUKA MANENO YA WATU : Mara nyingi tunajikuta wahanga wa kujilinganisha na wengine kutokana na misukumo tunayoipata kutoka kwa watu wanaotuzunguka kama wazazi, watu wa karibu n.k...Lakini lazima uwe na uwezo wa kutotafakari sana maneno ya watu hasa wale wanaokushinikiza kuwa kama watu wengine.

4. KUMBUKA WEWE NDIO KIONGOZI WA MAISHA YAKO: Inakupasa utambue wewe ni kiongozi wa maisha yako, maisha yako ni kama kampuni hivo yakupasa kujua mtu pekee ambayo ana wajibika zaidi ni wewe. Hata mzazi wako sio kiongozi wa maisha yako zaidi yako wewe. Hii itakusaidia kuwa na mtazamo wa ubunifu zaidi juu ya maisha yako.

5. ANGALIA MBELE : Dereva bora ni yule anayeangalia mbele anapoendesha gari na sio kuangalia pembeni wanaomu overtake au walio ktk mwendo sawa na yeye. Siku zote usitumie muda wako mwingi kutazama wanaoku overtake. Unaweza jifunza jambo lakini si busara kujilinganisha na waƓ

Kumbuka kipimo pekee cha mafanikio yako ni malengo yako na uwezo wako na sio kujilinganisha na wengine.


Wednesday, August 24, 2016

JENGA TABIA YA UKIMYA

Napozungumzia tabia ya ukimya nazungumzia ukimya wa nafsi na ukimya wa tabia na hata mazingira kwa ujumla. Jamii kwasasa imezungukwa na vivutio na purukushani nyingi ambazo haziruhusu au hazisababisha ukimya. Shida kubwa ni kwamba baada ya purukushani za kila siku kinachobaki katika nafsi ni upweke unaotokana na kutojenga muda muafaka kusikiliza nafsi yako na kutafakari.

Ukimya kwanza unakuwezesha kujitambua kwa kuwa utakuwezesha kujitafakari kwa utulivu vipawa na uwezo wako na kukuwezesha kufikiri kwa makini juu ya hatma ya maisha yako.Pia ukimya utakuwezesha kutambua ni maeneo gani katika maisha yako yanahitaji uangalizi ili kukuongezea thamani. Pia utakuwezesha kusikiza miongozo inayotoka ndani ya nafsi yako.

Utajua ni nini unachotaka na ni nini unachokiamini kwasababu umezungukwa na kelele nyingi za maisha...Kelele za mitazamo ya watu, maneno ya watu na hata changamoto za maisha. Usipojenga tabia ya ukimya utakuwa ni mtu mwenye hisia za upweke mara kwa mara maana muda mwingi utajikuta umeenda tofauti na nafsi yako na kufuata mvuto wa kelele zinazokuzunguka.

Kumbuka palipo na ukimya ndipo maarifa, hekima na amani ya nafsi hukaa, pia katika ukimya kunajengeka tabia ya kuwa macho juu ya mahitaji na hisia za wengine. Mahusiano ya watu ambao hawajajenga tabia hii huwa na lawama, malalamiko na mikwaruzano ya hapa na pale kwasababu ya kukosa ule muamko na kuwa macho juu ya mahitaji na hisia za wengine.

Mambo ya kufanya na kuzingatia ili kujenga tabia ya ukimya:-
1. Pendelea kuwa na tabia ya kukaa mwenyewe ukitafakari juu ya maisha yako pasipo vurugu au purukushani kutoka kwa watu wengine

2. Jenga tabia ya kutembea au kutembelea maeneo yenye utulivu na malihai kama miti, bustani nk

3. Penda kuwa msikilizaji, mtazamaji na mtu anayetafakari zaidi kwa kile anachokiona.

4. Penda kupangilia vitu vizuri maana siku zote mlundikano wa vitu hautokuruhusu kuwa na muda mzuri wa kutafakari.

5. Jenga tabia za kiimani kama kusali na kusikiza nyimbo za taratibu zenye kuinua nafsi.

Tuesday, August 23, 2016

OUR ATTITUDE MATTERS

The process of human change begins within us. We all have tremendous potential. We all desire good results from our efforts. Most of us are willing to work hard and to pay the price that success and happiness demand.

Each of us has the ability to put our unique human potential into action and to acquire a desired result. But the one thing that determines the level of our potential, that produces the intensity of our activity, and that predicts the quality of the result we receive is our attitude.

Attitude determines how much of the future we are allowed to see. It decides the size of our dreams and influences our determination when we are faced with new challenges. No other person on earth has dominion over our attitude.

People can affect our attitude by teaching us poor thinking habits or unintentionally misinforming us or providing us with negative sources of influence, but no one can control our attitude unless we voluntarily surrender that control. No one else "makes us angry." We make ourselves angry when we surrender control of our attitude.

What someone else may have done is irrelevant. We choose, not they. They merely put our attitude to a test. If we select a violent attitude by becoming hostile, angry, jealous or suspicious, then we have failed the test.

If we condemn ourselves by believing that we are unworthy, then again,we have failed the test. If we care at all about ourselves, then we must accept full responsibility for our own feelings. We must learn to guard against those feelings that have the capacity to lead our attitude down the wrong path and to strengthen those feelings that can lead us confidently into a better future.

If we want to receive the rewards the future holds in trust for us, then we must exercise the most important choice given to humanity by maintaining total dominion over our attitude. Our attitude is an asset, a treasure of great value, which must be protected accordingly.

Beware of the vandals and thieves among us who would injure our positive attitude or seek to steal it away. Having the right attitude is one of the basics that success requires.

Monday, August 22, 2016

FAIDA YA JUU SANA KATIKA KAZI

Faida ya juu sana aipatayo mtu kwa kufanya kazi sio anachokipata katika kazi hiyo bali ni anachokuwa katika kazi hiyo -John Ruskin

Watu wengi hutenda mambo au hufanya kazi fulani ili apate mapato fulani mfano mafao, pesa nk. Si jambo baya kufanya kazi au kujishughulisha katika mambo fulani kwa mapato fulani lakini sio mtazamo endelevu wa maendeleo. Robert Kiyosaki aliwahi kusema kuwa katika kazi yeyote angalia zaidi hiyo kazi ina manufaa gani zaidi katika kukuongezea maarifa na thamani.

Wekeza zaidi katika kuongeza thamani na hiyo ndiyo iwe faida yako namba moja. Unapojali zaidi thamani inayoongezeka ndani yako unajijengea msingi wa maendeleo endelevu. Thamani ya mtu ni uwezo alionao ndani yake na thamani ya mtu itamuwezesha kuendelea katika mazingira tofauti tofauti.

Unapowekeza katika kuwa na maendeleo ya nafsi mfano mitazamo chanya, maarifa endelevu, uwezo wa kustahimili na tabia za uwajibikaji unajijengea thamani zaidi ya pesa unazopata.
Kama unachofanya kinakuza mfuko wako lakini hakikuzi nafsi yako na kukujenga basi hakikusaidii sana maana pasipo thamani ukija kupoteza hayo mafao ni vigumu kutengeneza mazingira ya kuzalisha.

Thamani yako itakuwezesha kuwa na ufanisi katika eneo lolote. Hivo kwa mujibu wa John Ruskin hiyo ndiyo faida ya juu sana unayoweza kuipata. Hivo badala ya kuangalia zaidi malipo utakayopata angalia zaidi mabadiliko au thamani unayopata au utakayopata katika jambo ulifanyalo.

Friday, August 12, 2016

PROBLEMS AS OPPORTUNITIES

The factor that triggers your creativity and activates your positive mind is pressing problems. It is only when you are experiencing the pressure of problems and obstacles that you are motivated to perform at your mental best. Facing and solving the inevitable problems and difficulties of life make you stronger and smarter, and bring out the very best in you.

Most people do not understand the nature of problems. Problems are a normal and necessary part of life. They are inevitable and unavoidable. Problems come in spite of your best efforts to avoid them. Problems, therefore, come unbidden.

The only part of a problem over which you have any control is your response to your problems. Effective people respond positively and constructively to problems. In this way, they demonstrate that they have developed high levels of “response-ability”. They have developed the ability to respond effectively when unexpected or undesired difficulties occur.

Problems of all kinds bring out your very best qualities. They make you strong and resourceful. The more pressing your problems, and the more emotion you invest in solving those problems,the more creative you will become. Each time you solve a problem constructively, you become smarter and more effective. As a result,you prepare yourself for even bigger and more important problems to solve.