Showing posts with label Self development. Show all posts
Showing posts with label Self development. Show all posts

Friday, July 27, 2018

POWERFUL WAYS OF HAPPINESS IN THE WORLD

Have you realised that the happiness rate is decreasing in the world... People now lament, complain and cry more than ever

Jesus said in the world there is trouble but be of CHEER for i have overcomed the world.

The Kingdom of God isnt in food and drinks but joy and peace in the holy ghost....which means the kingdom of God isnt in materials but in the inward environment of the soul...There are those with so much materials but dont have the kingdom so never envy those with materials but find peace and joy.

Have you realised that the bible says seek the Kingdom of God and all others ( materials) will be added the he later says the kingdom of God is in joy and peace in the holy spirit...What do you understand??? Its simple...seek Joy and peace in your life and success will come...Some put it the other way round...NO, the reason you arent successful in the spirit is because you have no joy nor peace in you.

You complain too much instead of being joyful and praise the lord...You worry to much of money instead of having peace for he is able to do exceedingly, abundantly more than you can imagine....You worry and stress instead of Being at peace for all things work for Good for they that love God.

You will say you dont know what am going through...Well God knows and he is the one who said All things will work for good...Not I.

...Your mindset, speech and actions....One thing i have realised we as human beings should always evolve...and there is no greater pain than staying dormant....so each day make a goal and a devotion then hit it. Reduce your regrets by making everyday count...Do things that will make you happy and joyful daily.

So how can you find happiness in the world..

Its simple...Gravitate in Your identity, meditate in his promises...Focus on the light for so many times we fall into the temptation of following the darkness...

Listen search your spirit...understand your potentials, thank God for your strength and ask him to capitalize in your weakness.... Serve his kingdom with your God given talent. Invest in his kingdom...Change your perception and tie your life in your purpose.

Chase only what will cultivate your soul...Refuse to give you ear to negativity of the world...I believe the greatest transformation is in the way we use our tongues for in that area we find Life and death...

Happiness comes when you focus on God, his promises will give you peace...your mindset will change and you will be prophesying greatness.

Prophesy over your life more than you worry...Praise more than you complain...and another thing...Pray more than you stay in silent whining... Refuse to listen to any negative report from anyone that is contrally to the word of God.

Start a weekly devotion and fast...Say in this week i wont complain on anything, i will be thankful for all...and i will laugh at problems than cry and i will talk and prophesy of positive things like a crazy person and i wont talk bad words to hurt my spirit...then see the happiness you will find.

Nickvaleries

Wednesday, September 27, 2017

FREEDOM OF THE SOUL

One of the greatest challenges to the soul is freedom. The soul is in constant craving for freedom and it always strive to acquire freedom by any means.

 In life no matter how successful you can be, freedom is crucial for your soul to flourish, freedom enhances security and grounds for expressing the attributes for impact. Unless souls are free there will always be constant struggle.

We can choose to be free by letting our souls sink into themselves and to discover what we are made of and choosing to connect. Connection is a product of freedom.

Without freedom there is no connection whatsoever thats why its our duty to always free ourselves from the ties of our souls.


Wednesday, August 23, 2017

UDHIBITI BINAFSI

Nafsi isiyo na udhibibiti binafsi ni sawa na mji usiokuwa na kuta

Moja ya changamoto kubwa ya kinafsi ni ukosefu wa udhibiti binafsi. Udhibiti binafsi na uwezo wa kinafsi wa kuratibu na kuzuia kila ambacho kinaweza kuingia katika nafsi husika na hapo ndipo tabia ya udhibiti binafsi inapokuja. Ulimwengu ni kama jalala yenye kila aina ya mambo, yenye kuharibu nafsi, yenye kujenga, yenye kuleta tabia na mitazamo asi au chanya, hivo ukitaka usalama wa kinafsi ni lazima uwe na udhibiti binafsi.

Haijalishi kwamba umepewa macho, kinywa au masikio, uimara wako unatokana na kutumia milango hiyo katika mambo ya msingi pekee. Udhibiti binafsi sio tu kudhibiti haja za mwili wako bali pia ni kudhibiti milango inayoingiza habari ndani yako. Huwezi kuwa na uimara kama ni mtu wa kutazama kila kitu, mtu wa kusikiza kila kitu, mtu wa kuchangia kila kitu, mtu wa kufatilia kila kitu au mtu wa kuongea kila kitu, hapana. Hautakuwa mtu mwenye utashi mzuri wa kihisia na hata kiakili.

Kuna tamaa za kinafsi kama shauku ya kutaka kufahamu mambo yasiyo na tija kwako, au kutaka kusikiza maswala yasiyoongeza thamani kwako au kutaka kufatilia watu wasio katika mlengwa wa yale yanayokuhusu. Ni tamaa tu ya kinafsi kutaka kuburudishwa na yanayowatokea wengine pengine hata kama hayana faida kwako. Usichofahamu ni kwamba unaijaza nafsi yako na mambo ambayo yanaongeza mzigo au yanakupa mtazamo ambao hauna tija kwako. Hakuna changamoto kubwa kama uchaguzi. Pale unapokuwa katika mazingira yanayokupasa uchague kuburudisha nafsi au kujenga nafsi.

Tafuta burudani ya kinafsi kwa mambo yanayohusiana na mambo ya msingi yanayokujenga. Kuwa na udhibiti binafsi, na wengi ambao hawana udhibiti binafsi wamejikuta katika matatizo mengi ya msongo wa mawazo au hata mikwaruzano isiyo na tija na watu wengine. Hata kama jambo lipo mbele yako sio lazima uburudishe nafsi yako kulifatilia. Hata kama hoja iko mbele yako sio lazima kuburudisha nafsi yako kuchangia. Hata kama maneno yanasemwa juu yako sio lazima kuruhusu nafsi yako kujibu, hata kama una shauku ya kuwafatilia watu sio lazima uruhusu nafsi yako kuwafatilia. Kama jambo badala ya kukusaidia linakujaza ujinga dhibiti nafsi yako na uliache.

Hakika usipokuwa mtu wa kudhibiti nafsi yako utakuwa mtu mwenye kubeba kila aina ya uchafu.

Tuesday, June 20, 2017

ITAJIRISHE NAFSI YAKO

Nafsi yako ni hazina kubwa maana ndio kiunganishi cha mwili wako na uhai wako au tunaweza sema roho yako. Nafsi yenye nguvu ni ile inayoweza kudhibiti fikra na kuratibu hisia na kuziweka katika mfumo utakaoleta tija katika maisha na tija kwa yale yanayokuzunguka.

Nafsi imara ni ile inayoweza kuchuja fikra na mawazo na kuhakikisha yanaleta mguso chanya kwa hisia ili zilete msukumo wa utendaji. Huwezi kuwa na nafsi imara kama haudhibiti fikra zako na kama hauratibu hisia zako. Hisia zinatakiwa zipokee msukumo chanya kutoka katika fikra zilizoratibiwa vizuri.

Utatu wa kinafsi yaani hisia, akili na utashi unahitaji kuchunguzwa na kila mwenye nafsi. Inapaswa kama binadamu uhakikishe sheria au misingi ya imani yako imejikita kujenga nafsi imara na sio nafsi dhaifu. Je ni mambo gani yanaingia zaidi katika nafsi yako, je watu wanaokuzunguka wana mguso upi katika nafsi yako? Hayo mambo ni ya kuchunguza sana.

Waweza kuitajirisha nafsi yako kiasi cha kwamba ikawa inatoa misimamo na hisia zenye uwiano, ni jambo lenye changamoto pale akili yako na hisia zikawa na mgongano katika namna inavogusa watu. Utashi wa kimawazo usio na utashi wa kihisia siku zote hauleti matokeo sawa. Unaweza kuwa na utashi wa kimawazo ila pasipo na utashi wa kihisia ukasababisha maafa makubwa.

Je mawazo yako yanaleta mguso gani wa kihisia. Waweza jua jambo lakini ukaliwasilisha likasababisha maafa au hata maudhi. Tajirisha nafsi yako kiasi cha kwamba utashi wako wa kiakili uuwiane na utashi wako wa kihisia. Nikupe mfano wa zawadi, ukipeleka zawadi kwa mtu na umeinunua kwa gharama siku zote lazima uifunge katika boxi la zawadi na uliwekee gift paper. Vivyo hivo ukiwa unatoa madini ya mawazo, ushauri na marekebisho lazima utumie utashi wa kihisia ili anayepokea afurahishwe na kuguswa na zawadi yako.

Hata Kama zawadi ulioifunga sio nzuri sana ila namna ulivoifunga inaweza ikamgusa mtu na akaipokea.

Tajirisha nafsi yako kwa kuweka uwiano katika ukuaji wa utaahi wa kihisia na utashi wa kiakili

Monday, May 15, 2017

CHUNGA MOYO WAKO

Chunga moyo wako maana hiyo ndiyo bustani ya amani na furaha yako. Nafsi yako hustawi katika bustani ya moyo wako. Katika bustani ya moyo wako kunaweza kuwa na maua ya furaha, amani na faraja au magugu ya maumivu na uchungu. Kuwa muangalifu sana kwa kuchunga moyo wako kila wakati ni nini kinachoota.

Kuna mawazo na maneno ambayo ukiyaruhusu yaingie moyoni yanaenda kuweka majeraha ambayo kupona kwake kutakuchukua muda sana. Majeraha hayo yatajenga mfumo wa kifikra wa kujihami ili kuzuia maumivu mengine. Hasara ya fikra za kujihami ni kwamba utashindwa kufurahia uhuru na uzuri wa maisha kwa kuwa utaishi kwa kujihami.

Moyo wako unatakiwa ulindwe kama ngome imara. Ukiruhusu maumivu au matatizo yakaingia katika bustani ya moyo wako yataenda kuotesha magugu ya mawazo na fikra hasi. Kuna maneno ukiyaruhusu kuingia siku moja yatautesa moyo wako wakati wote. 

Safisha moyo wako kwa kuondoa yale ambayo yanauumiza na kutesa moyo wako. Yale ambayo kila ukiyafikiria unasikia kama kichomi ndani ya moyo wako, yale ambayo kila ukiyapa nafasi katika akili yanakububujisha machozi ya uchungu moyoni mwako.

Tambua kuwa moyo wako unatakiwa kustawisha amani, furaha na upendo. Ukiwa na moyo wenye uchungu inageuka kuwa sumu inayodhoofisha nafsi yako na akili yako. Utakuwa mtu mwenye vifungo badala ya uhuru.

Chunga moyo wako na uache katika amani. Usiuache umekaa katika dimbwi la maumivu au usiuache ushikilie uchungu unaokuumiza, usiuache ushikilie maneno makali au misumari ya mitazamo hasi juu yako. Usiruhusu moyo wako udunde kwa kasi kwa kukosa amani au kuwa na taharuki, Jipe utulivu kwa kuruhusu uzuri na furaha istawishe moyo wako.

Ruhusu yale yenye furaha na amani na yenye uzuri na utulivu ndio yakae katika moyo wako. Stawisha moyo wako ili ukutunze na uachilie yale yenye furaha, amani na pumziko. Kama vile damu inavoingia na kutoka katika mkondo wa mishipa ya damu, wewe pia tengeneza mkondo wa kuingiza furaha nyingi, amani nyingi na faraja nyingi moyoni mwako kwa kukaa na watu au mazingira yatakayosaidia hivo vitu lakini ondoa moyoni mkondo wa maumivu, uchungu na yale yanayoutatiza moyo

Lazima kuwe na uwiano baina ya yanayotoka na yanayoingia, usipende kuingiza mawazo hasi, Itafute hiyo furaha na amani ili ustawishe bustani ya moyo wako.

Fikra chanya au mazingira chanya sio tu yale yanayokusukuma kufanikiwa bali pia kuustawisha moyo wako na kuuacha katika hali ya utulivu.

Tuesday, May 2, 2017

USICHUKULIE KILA JAMBO KIHISIA

Ukitaka kuwa na furaha usipende kuchukulia kila jambo kinafsi au kihisia. Kuna mambo mengine ni ya kifikra tu na yamekaa kimtazamo tu ambayo hayatakiwi kuchukuliwa kihisia.

Ukitaka kuwa na utashi wa kihisia na uweze kuratibu hisia zako katika mlengwa chanya yakupasa kuziacha hisia zako katika mfumo tulivo kadri uwezavyo. Kuna mambo ukiyachukulia kihisia utaziweka hisia zako kwenye mfumo wa taharuki kwa wakati mwingi na itakupunguzia msisimko wa maisha ulio katika muundo chanya.

Je wawezaje kutochukulia mambo kihisia? Tambua kuwa kila wazo au mtazamo unapaswa kupokelewa kiakili na kuratibiwa kabla ya kusukumwa na hisia fulani. Ni vizuri ukiratibu mawazo na mitazamo unayopokea na kuiratibu kabla ya kujua ni hisia gani uiachilie ili isukume hilo jambo.

Ni muhimu sana kulishikilia wazo au mtazamo katika mfumo chanya hata kama limekuja katika muundo hasi. Lione hilo wazo kama njia ya kukuboresha, yaone hayo maoni kama njia ya kukuboresha kisha yape hisia chanya ndipo uyapokee. Usikubali kuanza kupokea kihisia wazo ambalo hujariratibu kwa akili.

Mfano mtu anaweza kukwambia jambo ambalo unaona kabisa linaweza lisiwe chanya kwako, badala ya kulipokea kwa hisia hasi jaribu kuliona ilo jambo kama wazo la kukuboresha na sio kukuharibu, kisha chukua hisia ya amani na furaha kwa kutambua kuwa hilo wazo limekuja kukuboresha..kisha chukua hisia ya morali na ari ya kulitafutia ufumbuzi na kulishughulikia hilo jambo na sio vinginevyo. Ukilipokea kama vile limekuja kukuumiza utaingiwa na taharuki ya kinafsi pengine hata kujenga ukuta kulizuia hilo suala na kuonekana kuwa ni mtu dhaifu kinafsi pengine hata mtu hasiyependa kuambiwa ukweli.

Nakushauri tena usilipokee kila jambo kihisia kabla ya kuriratibu kiutashi na kiakili ili kukujenga utashi wa kihisia itakayokupa furaha wakati wote.

Sunday, April 23, 2017

TAFUTA AMANI YA NAFSI

Hakuna jambo lenye msingi katika uimara na utashi wa nafsi kama amani ya nafsi - Nickvaleries

Huwezi kukua katika utashi wa nafsi pasipo kuwa na amani ya nafsi. Imani ikikaa katika nafsi humuwezesha mtu kustahimili misukosuko ya nje kwasababu kinachoweza kuzamisha meli sio bahari bali maji yanayoingia ndani ya meli.

Ukiweza kuiacha nafsi yako katika usalama kwa kujenga ukuta kuzuia yale yanayotokea yasiondoe amani ya nafsi utaweza kustahimili mengi. Ukikosa amani lazima utakosa imani na ukikosa imani hata utendaji wako na maneno yako yatakwenda kinyume na uhalisia.

Jiulize ni mambo gani ambayo unayaruhusu katika nafsi yako...Je yanaimarisha ngome za utulivu wako au yanabomoa amani ya nafsi yako na kukupa hali ya taharuki. Waweza kuwa na vyote ukakosa amani na ukikosa amani ukakosa imani huweza kuwa na furaha.

Hakuna furaha mahali palipokosa amani...Huwezi kuwa na furaha ya nafsi au kufurahia yale mazuri yanayokuzunguka kama ukikosa amani.  Tafuta kuwa na amani na jiimarishe kinafsi ukiziimarisha ngome za nafsi yako.

Jitahidi kujenga ngome zenye usalama ndani yako kiasi cha kusimama imara kinafsi hata kama mazingira ni yenye taharuki..sikiliza ulimwengu una taharuki na ukikosa amani jua huwezi kuwa na furaha.

Amani inaweza patikana kwa kuimarisha misingi ya uaminifu, mawasiliano, utashi wakihisia na utu. Tambua kwamba kila jambo linafanyika kuwa jema na wewe ni mwenye hatma njema na kuna mambo mengi mazuri ambayo yako mbele yako.

Taswira yako ni ya muhimu sana ukitaka kuwa na amani. Je unaangalia nini na unasikiliza nini? Hakikisha umejiimarisha kuratibu kila kinachoingia katika nafsi yako.

Usipende kuyapa muda mwingi mawazo na mazingira yanayoondoa amani yako. Itenge nafsi yako ili iwe na amani.


Tuesday, March 28, 2017

JENGA UTASHI WA KIHISIA

Uimara wa mtu katika nafsi umejikita zaidi katika utashi wake wa kihisia. Binadamu ni kiumbe chenye nafsi na nafsi ya mtu imeundwa katika mfumo wa hisia. Hisia za mtu pia zimeundwa katika mfumo wa utu wake. Kila mtu ana muundo wake wa kiutu ambao ndio msingi hasa wa uratibu wa hisia za mtu huyo.

Hisia ni misukumo na mihemko ya kinafsi ambayo hujitokeza kutoka kipindi hadi kipindi kutokana na mabadiliko ya ndani au nje. Yaweza ikawa mabadiliko ya kimazingira au mabadiliko ya tabia za mwili. Changamoto kubwa ya hisia ni kwamba ni kama upepo, huja na kufika katika kilele lakini baadaye hushuka katika ukawaida na pengine hushuka zaidi ya hapo.

Hapo ndipo wengi hujikuta wanasema leo najihisi niko chini sana kihisia au nimezama katika hisia na hata wengi hutumia kauli za vitabu vya dini na kusema leo nimezama katika bonde la uvuli wa mauti. Lakini hao hao watu nyakati nyingine utasikia anasema leo nina msisimko au leo niko hewani. Yote hayo ni mabadiliko ya kihisia.

Hisia zinaweza kuwa nzuri kama zikitumika vizuri lakini changamoto kubwa ni pale mfumo wa uratibu wa kimaamuzi katika akili unapofungwa katika hisia ambazo zinapanda na kushuka. Kuna ambao wamekuwa na utashi wakufikiria lakini wamekosa utashi wa kihisia.

Utashi wa kihisia ni uwezo wa kuratibu hisia zako na kuzielekeza vile unavotaka. Watu wengi tumekuwa na utashi wa ki akili lakini tumekosa jambo la muhimu sana ambalo ni utashi wa kihisia kupelekea yale tunayoyajenga kwa akili zetu yanaharibiwa na hisia zetu.

Waweza fikiria jambo zuri na ukaliwekea mikakati madhubuti lakini kinapofika kipindi cha mtikisiko unaogusa hisia ,wengi wetu tumejikuta tukiruhusu hisia zetu ziharibu hata ule mtazamo chanya wa yale tuliyoyajenga kwa akili zetu.

Watu wengi waliofanikiwa au wakuu wamejikuta wakianguka na kufanya maamuzi mabovu kwasababu ya kukosa utashi wa kihisia na wamejikuta wakizama katika dimbwi ambalo pengine kusababisha zile imaya walizozijenga kwa akili nyingi kuanguka kutokana na kukosa utashi wa kihisia.

Wekeza sana kuwa utashi wa kihisia uweze kutambua ni hisia zipi zinakujenga na zipi zinakubomoa. Hisia zipi zinakuimarisha na hisia zipi zinakudhoofisha, hisia zipi zinakuinua na hisia zipi zinakuangusha. Ukiwa na utashi wa namna hiyo utaweza kuzitumia hisia hizo ziweze kukutumikia na sio wewe kutumikia hisia zako.

Je wawezaje kuwa na Utashi wa kihisia

1. Pambanua hisia zako pindi zinapokuja na utambua mlengwa wa kila hisia.

2. Tambua chanzo cha hisia husika au mifumo sababishi ya kutokea kwa hisia hizo.

3. Jifunze kuzimudu hisia kila zinapokuja kwa kuifanya nafsi yako izungumze na hisia hizo

4. Tambua kuwa hisia sio jambo baya na wala sio udhaifu bali ni muundo wa kinafsi hivo hisia zako zikubali kuwa ni zako na wewe ndio mwenye kuwajibika kwa hisia hizo. Usitafute kisingizio juu ya hisia zako.

5. Jiimarishe katika uvumilivu ili uweze kuziratibu hisia zako na kuratibu mkondo wa hisia zako maana hisia ni kama mkondo wa maji

6. Pendelea kutenga muda wako wa upekee ukizungumza na nafsi yako ili uweze kuthibitika katika uimara wa kihisia.

Hakuna jambo la msingi na lenye kufaa kama kuwa na utashi wa kihisia maana maisha yako yanaweza kuwa yenye furaha na amani au kuwa na shida na maumivu kama hauna utashi wa kihisia.

Saturday, March 25, 2017

MUDA WAKO WA UPEKEE NA NAFSI YAKO

Ukitaka kuwa na furaha anza kwa kufurahia muda wako wa upekee.

Moja ya changamoto tulizonazo kama binadamu ni upweke. Upweke sio ukosefu wa wenza au watu wa kutuzunguka. Upweke ni pale mtu anaposhindwa kuufurahia upekee wake na anaposhindwa kuwa na uhusiano na uhalisia wa nafsi yake.

Kuna malalamiko mengi unasikia hata katika mahusiano mmoja wao anasema nilijihisi mpweke ndo maana nilikusaliti, au mwingine anaingia katika ulevi au hata mikanda ya ngono kwa sababu ya upweke. Tafsiri yetu ya upweke ni kukosa watu wa kutengeneza muungano wa kinafsi au watu wa kuburudisha nafsi zetu.

Nafsi ya binadamu kila wakati inahitaji kurutubishwa kwa kutengewa muda wa kupata uwepo. Nafsi yako ni utu wako wa ndani. Mtu wako wa ndani anahitaji wewe umtengee muda kumsikiliza, kumdadisi, kuzungumza naye, kumburudisha na hata kumponya na aina yeyote ya maumivu.

Lazima ujitengee muda wako wako bora wa kutengeneza mguso wa kimaelewano na nafsi yako. Watu wengi wameshindwa kuwa watu wa namna hiyo kupelekea kupigwa na upweke kila wakati anapokosa mguso wa nje wa watu wanaomzunguka.

Rafiki yako wa kwanza na wa karibu ni nafsi yako. Itengee muda nafsi yako ili ipate ukaribu wako. Na wakati wa kuzungumza na nafsi yako jua kwamba unaongea na mtu wako wa karibu. Acha kuongea na nafsi yako kwa ukali au kuihukumu kwa makosa ya nyuma. Itie moyo nafsi yako, ikumbushe uwezo wako. Panda mbegu chanya ndani ya nafsi yako, itie moyo, iponye kwa makosa ya nyuma na iahidi mambo mazuri huko mbele, iburudishe kwa lugha nzuri yenye mguso chanya lakini kuu kuliko yote iweke huru.

Watu wengi wamekuwa wakitumia wakati wao wa upekee kwa kulala, kuangalia mitandao ya kijamii au hata kutafuta magenge ya umbea kutafuta jambo la kufanya kuondoa upweke nk. Huo sio wakati wake. Huo ni wakati wa kujenga uhusiano na nafsi yako. Ni sawa na aina yeyote ya uhusiano. Lakini uhusiano wako na nafsi ndiyo jambo la msingi kwanza.

Ukiwa na tabia ya kuwa na muda mwingi na nafsi yako hautokuwa mtu wa kulalamika upweke. Na hautokuwa mtu wa kutafuta vileta msisimko vya nje kama pombe, anasa na ngono pale unapojihisi mpweke. Utaufurahia muda wako wa upekee, nafsi yako itarutubishwa na utakuwa ni mtu mwenye furaha muda mwingi.

Angalizo ni kwamba katika muda wako wa upekee na nafsi yako hakikisha unatengeneza mazingira chanya. Huwezi kutengeneza mazingira hasi ya mawazo na hisia hasi au muingiliano na mambo yasiyojenga halafu utegemee nafsi yako itajiachilia. Nafsi yako itajenga ukuta wa kujihami maana ndivo mwanadamu alivo kiakili katika maisha yanayoonekana kama mapambano.

Pia usipende kuipa nafsi yako maumivu yasiyokuwa na sababu na mara nyingi pale akili yako inaposhindwa kuendana na misingi ya nafsi yako. Na usipende kuipa nafsi yako vifungo kwa kufuata njia ambazo unajua nafsi yako haiwi huru kuchanua.

Thursday, March 16, 2017

KUWA NA UHUSIANO NA UHALISIA WAKO

Kila binadamu ana uhalisia wake na utofauti wake, binadamu wanaweza fanana tabia lakini kuna msingi wa ndani kabisa wa kinafsi unaowatofautisha. Huu msingi wa kinafsi ndio uhalisia wa yule mtu. Mtu yeyote anayetoka katika uhalisia wake anapoteza utambulisho wake na akipoteza utambulisho wake anapoteza mambo mengi ya kinafsi yaliyomo ndani yake maana inambidi atafute uhalisia mwingine na alazimike kuishi katika uhalisia huo.

Kuna mambo mengi ya kinafsi ambayo mtu hupoteza na kuu kuliko yote ni amani ya nafsi na furaha ya ndani. Hapo ndipo unakutana na mtu ana kila kitu lakini hana furaha wala amani, yamkini kuna mambo kadha wa kadha yanayomtatiza lakini kuu kuliko yote ni kupoteza uhalisia wake. Kuna mambo yanayompa mtu ujasiri wa ndani, kuna misingi ya kinafsi ambayo mtu anakuwa nayo inayompambanua. Akipoteza hivo vitu au akitoka nje ya hivo vitu utaona mabadiliko yake kimtazamo na hata kihisia.

Katika uratibu wa kihisia na kutengeneza uimara wa kihisia mtu lazima arudi katikà uhalisia wake. Watu wengi wamepoteza dira katika mambo mengi kwasababu walitoka katika uhalisia wao ndipo wanakuja kushtuka wameshapotea na wakajikuta wanaishi kama wahanga wa mambo pasipo kujua nini cha kufanya.

Jitambue na jitambulishe na jiimarishe katika uhalisia wako maana utakapokuja kutoka katika uhalisia huo utajaribu kuwa kitu au mtu ambaye haumuelewi hata wewe. Unakuwa kama mtu usiyejitambua, Rudi katika uhalisia wako ili urudishe ile morali na msukumo na msisimko wa ndani kufanya mambo.

Ukiwa katika uhalisia wako mazingira ndo yatalazimika kuendana na uhalisia wako lakini tofauti na hapo wewe ndo utalazimika kuendana na mazingira. Uhalisia hukupa wewe uhuru wa kujipambanua na kujiwasilisha katika jamii ili uwe na mguso chanya. Uhalisia wako ndio hupelekea wewe kutambua kusudi lako na hata kuongeza thamani yako ili ulitende kusudi lako. Hivo ni muhimu sana kuwa katika uhalisia wako.

Jamii au mazingira yasikufanye upoteze uhalisia wako. Jamii ndo inapaswa ipishe njia ili uhalisia wako uweze kuwa na mguso na hii itawezekana tu ukisimama katika kulinda uhalisia wako

Sunday, March 12, 2017

HOW TO DEAL WITH FEAR

Do you know that fear is false evidence appearing real? Sometimes in life you will be faced with situations whereby there will be evidences that are false appearing real. Fear will torment you and leave you paralysed. The only cure to fear is faith. Believe beyond circumstances. 

Clear your mind of the Past : You will always be free as your mind is free. The battlefield is always in your mind. Its a point where strongholds of the past are. The strong holds of fear and other dissapointments. Experience should make you wiser in terms of strategies and how you perceive life. But always free your mind as much as possible.

Something is about to happen in your life: Things happen all the time, good or bad but its always dark before dawn. We pass through darkness to experience the light. We pass through trouble to appreciate calmness. No darkness comes after darkness until afternoon passes. Always believe that the next phase of your life will always be better than the previous. Try to find the rainbow after the storm because its there. Dont be afraid that later will be like the former. There will always be changes in every stage of your life.

Find beauty and peace: You will never be happy unless you are at a state of beauty and peace and tranquility. We often look at the beauty without but not the beauty within. We all want to be in tune with our inner self. Our core values and our inner being, but we often times try to find this in the wrong places. We should always be in the quest to find beauty and nirvana and where its connected.

Wednesday, February 22, 2017

BENEFITS OF KNOWLEDGE AND ADVENTURE FOR EMOTIONAL INTELLIGENCE

Our minds and souls are constantly in need of exploration and discovery. The reason why we act differently and evolve is because our souls seek new horizons. Our minds need to be refreshend and expanded so as we can stable in our actions and in our ways. As it is said Lunacy is doing the same thing the same way and expecting different results.

We act in a lunacy form whenever we fail to expand our minds and let our souls explore its limitlessness. Knowledge is essential for expanding our minds increasing our possibilities and widening the limits that have been set by ignorance. We must grow in knowledge so as to be free. Emotional intelligence being the ability to perceive, assess and manage our emotions is a crucial attribute to our stability as human beings.

If we invest in knowledge while we let our souls experience wonder we invest in the attribute of emotional intelligence. We not only grow in our ability to manage our emotions but we develop control as to how we can relate our knowledge in a practical way to see wonder and adventure.

How can Knowledge and adventure be used simultaneously for emotional intelligence

1. Always read books of a specific topic in the specific moment at the specific place. That's Practical investment of knowledge.

2. Knowledge has to be put into practise, acquiring knowledge without practising it is a wastage of time. Ensure to always acquire the kind of knowledge you can practise.

3. Explore new horizons, listen don't let your life become a routine of activities that don't allow your soul to explore and experience the adventures of your life time.

4. Visit nature occasionally and meditate on it. This will open your mind and trigger your soul to explore the adventures of naturality.

Always remember that without emotional intelligence we will always be unstable human beings. If emotions aren't managed and assessed skillfully then we will always be human beings of so many imbalances and we will live life not realising the beauty of it.


Monday, January 16, 2017

GHARAMA NA KIPIMO CHA UVUMILIVU

Je wajua kila jambo bora huja na gharama ya uvumilivu. Kila jambo unalohitaji katika maisha huja na gharama ya uvumilivu huku ukikua katika nidhamu katika hicho kipindi cha uvumilivu. Kuna wakati unaweza dhani unaishi katika ndoto pale unapozungumza mambo pasipo kuyaona katika uhalisia.

Imani ni kuwa na uhakika wa mambo ambayo unayo katika fikra lakini bado hayajadhiirika. Unaweza omba msitu lakini ukapata mbegu ya msitu na ukaanza kujiuliza hii mbegu naifanyia nini. Unaweza kuwa na maono ya kujenga familia bora yenye kila hitaji muhimu likiwa limekamilika lakini ukajikuta unapata mwenza ambaye amekamilika katika hitaji la kinafsi lakini mahitaji ya kimali bado inakubidi uvumilie pengine hata uwekeze muda zaidi. Ni wewe kutambua kuwa hiyo uliyonayo ni mbegu bora inayohitaji udongo mzuri ili ichipue yale unayohitaji.

Hitaji la nafsi ni changamoto kubwa na wengi wamekuwa wakipata mahitaji mengine lakini wamekuwa wakiishi pasipo kuridhika kwakuwa mahitaji ya kinafsi wamekuwa wakiyakosa. Tambua kuwa kuna nyakati ambazo uvumilivu na imani yako itawekwa katika kipimo ili kuimarika katika uthabiti wa kimaamuzi. Kila jambo huwa zuri kwa muda kama likijengwa juu ya uaminifu, maono na nia thabiti ya kulisababisha lile jambo litokee katika uhalisia wake.

Lazima ufike kipindi ambacho imani yako itakuwa katika kipimo, lazima ifike kipindi utajiuliza je haya mambo ninayoyatazamia ni ndoto tu za mchana au kweli nitakuja kuyathibitisha. Unapofika katika kipindi hicho uimara wako na imani yako na fikra chanya ndizo zitakazokuvusha kuyapata yale unayoyahitaji na kuyatazamia.

Hakuna ndoto kwa mtu mwenye dhamira ya dhati na kila wakati anahangaika kutafuta njia za kutekeleza yale anayoyaona katika maono yake. Bali ni hatma ya muda na uvumilivu wa huyu mtu akisimama imara katika kutegemea yaliyo bora na yale anayoyatazamia. Usijione kuwa mwenye ndoto tu pengine labda unatazamia mambo ambayo kwa sasa huwezi yapata. Tambua kuwa dhamira ya dhati na utayari wa kujitoa huku ukichanganya na uvumilivu ukiendelea kukua kinafsi vitathibitisha ndoto zako na maono yako.

Wednesday, January 11, 2017

WEKEZA KATIKA UIMARA WA NDANI

Nyumba imara ni ile yenye msingi imara. Msingi mara nyingi hufukiwa chini lakini ndio uimara wa jengo zima ulipo. Vivyo hivyo uimara wako kwa mambo yanayoonekana unatokana na uimara wako wa ndani, uimara wa nafsi. Japo nje waweza onekana imara lakini kipimo pekee cha uimara wako wa ndani ni mtikisiko.

Mtikisiko mkubwa utakaopata ni pale ambapo misingi yako ya ndani itatikiswa. Pale ambapo utawekwa katika mazingira ambayo yatakubidi upime mitazamo yako, upime sheria zako, upime utaratibu wako na kuu kuliko yote upime utambulisho wako. Na ndio maana katika kipindi cha mtikisiko unaweza poteza dira ya utambulisho wako, imani yako na hata utaratibu wako.

Mtikisiko unapoingia lazima uingie uzito wakati huo huo inaingia hali ya hamaki na taharuki. Hapo ndipo utajikuta unafanya maamuzi ambayo hayana faida kwako, hapo utajikuta unaingiwa na ukungu katika macho yako ya ndani ya maono yako.

Hali hiyo ni ya kawaida hasa pale unapotoka katika mfumo mmoja kwenda mwingine, kawaida moja kwenda nyingine. Pale unapotaka kuishi mitazamo yako na ndoto zako kwa mkupuo. Pale unapotaka kukimbia kabla hujapasha joto miguu kwa kutembea. Ni vema ukapasha joto miguu yako na kufurahia kabla hujaanza kukimbia.

Uhuru wa nafsi unahitaji nidhamu na maono yaliyo sambamba na uhalisia. Jaribu kwenda kwa utaratibu lakini ukiwa na uharaka wa kifikra kuchukua maamuzi. Kuwa muwazi juu ya hali yako na utafute watu wachache ambao watakuchoma sindano ya hamasa na watakuamini. Ambao wako tayari kusimama na kukupa moyo.

Unaweza kujiimarisha kwa kuendelea kujipa hamasa na kuwa na fikra chanya, ukichukulia kila changamoto kama njia ya kujiimarisha. Usitafute kujipa kisingizio kama unajua unaweza kujiimarisha. Kila wakati ongeza nguvu yako ya ndani kwa kusimama tena hata kama umechoka. Misuli huja kwa kuongeza zaidi, kujiinua zaidi na kuamini ipo siku mambo yatakuwa mazuri.

Sunday, November 20, 2016

LEARN TO IGNORE

The race of life is the one with a lot of obstacles, a lot of hindrances and a lot of oppositions, we all know that and we all have experienced that at some point in life, but there comes the most critical of all a lot of intimidations. If you havent master the art of ignoring voices then you will always fall victim.

When you are walking your walk always know that there are people who will come to intimidate you and try to misfocus you with words. Listen always be ready for that for people will hit you where it hurts you the most, sometimes even people you cant imagine but always guide your heart and mind. Many have grabbed a victim mindset simply because they take everything thrown unto them personal

Don't be intimidated...Learn to ignore, choose not to give full attention to distractions, Its obvious that some will be people very close to you in whom there opinions can have a big impact in you, but one of the greatest thing you need to do is detach yourself from the emotions brought about by people. Its true that you might sometimes fall prey in the predatorial world but stand up, ignore the predators and move on. What doesnt kill you makes you stronger.

Just because people are close doesn't mean that their opinions of you will always be right. Don't let the pressure get into you...Don't be intimidated, learn to ignore the impacts of their words. Learn to ignore, Ignore the negative feelings, ignore the negative emotions. Ignore what seems to bring you down. I challenge you to ignore those voices that keep running through your mind all the times telling you that you are somebody's victim. No you arent. Train your mind to cancel off and ignore.

Say to yourself, i choose to ignore all distractions. One African proverb says a lion doesn't turn back when dogs bark, also the noise of frogs doesn't hinder the elephant from drinking water from the stream. When you have an understanding of what people go through then it wont trouble you when they voice out their opinions out of emotions. Just ignore and move on. Choose to mind your own business and move on. No need to give an airtime to the calls that dont compliment you. Focus on the good. 

Thursday, November 10, 2016

KUDHIBITI HISIA HASI

Magugu siku zote huota hata sehemu ambazo hazitakiwi, hayaitaji mbegu..yenyewe huota bila kupandwa wala nini, vivo hivo na hisia hasi, huwa haziitaji kazi kubwa kukaa katika nafsi yako. Zinaweza kukuhijia wakati wowote na kwa namna yeyote lakini hisia chanya zinahitaji kupangiliwa, kurutubishwa na kupaliliwa.

Moyo wako kuna wakati unaweza patwa na hisia hasi ambazo zinakuja kutokana na jambo lolote, inawezekana ni uchovu wa kimwili au kiakili, mtu fulani kukukatisha tamaa, mtu fulani kuzungumza na wewe vibaya nk...yamkini ni mtu wako wa karibu, au mtu ambaye ana mguso wa tofauti ndani ya moyo wako. Lakini ni vyema ukatengeneza mzani wa kupima hisia hasi na kuzikata badala ya kuzipa hifadhi kwa muda mrefu ndani yako.

Ukizipa hifadhi kwa muda mrefu zina tabia ya kuchoma nafsi yako na kila zikichoma nafsi yako zinakujengea hali ya kutaka kuzitoa. Na hapo wengi wamejikuta wakizitoa kwa msukumo unaosababisha maafa zaidi. Njia pekee ya kuzidhibiti hisia hasi ni kupumzisha nafsi yako kwa muda huku ukijaribu kuingiza hisia chanya.

Hisia chanya zinahitaji nidhamu kuziimarisha ndani ya nafsi yako, kwasababu asilimia kubwa ya watu wamezungukwa na mazingira hasi mfano ndugu walalamishi, marafiki wasiojali, wapendwa wasiokuelewa na wasioheshima uhuru wako na furaha yako. Inabidi ujipe likizo ya kinafsi. Ikiwezekana jijengee utaratibu hata wa kufunga kuendekeza hisia hasi kwa kipindi fulani kama jinsi ambavyo dini hufunga chakula au starehe fulani waweza funga kutoziendekeza hisia hasi.

Jenga utaratibu katika maisha yako wa kutozipa hifadhi hisia hasi wala kuziendekeza kwa muda mrefu. Hisia ni mfano wa mimea, kuna mimea bora na kuna magugu. Hisia hasi ni kama magugu. Tafuta kuwa mtu mwenye hisia chanya kila wakati. Ni sawa na chumba chenye uchafu na kila aina ya takataka...usipoweza kuondoa visivohitajika, chumba kitajaa na hewa itakuwa haizunguki vizuri. Usipoweza kupunguza hifadhi ya hisia hasi ndani ya nafsi yako, nafsi yako itajaa na hewa nzuri ya mazingira chanya haitozunguka vizuri ndani yako.


Tuesday, November 8, 2016

INVEST IN YOURSELF

How do you picture yourself? How do you see your life? How do you see your soul? How do you see your spirit? Do you see any area you can add more value in you. There is still more you can add in your life. You still have room for more. Invest in excellence. You still have more you can add.

Listen when you stop growing you start dying. And dying can start from your soul, mind and even your spirit. You slowly start to settle for whats below you. You slowly start to settle for what doesn't compliment you. Listen challenges should boost you to invest in yourself more.

Negative thinking will just drown you in negativity. Choose to direct your thoughts towards creating value in life. You can still be the best version of yourself. Refuse to settle in despair. Life is bigger than that...rise higher. A country like america invested in every sector to be the world superpower. Invest in every sector of your life. Your health, your skills, your financial life. Invest more and let you be needed for the value you have.

Feed your faith and your fears will flee, choose to distinguish yourself...Don't fit in, fit out with character and excellence. Be the best version of yourself for when you do that you will always stand out with an impact. Commit yourself in being a person of value and character. Enrich your soul with everything needful for you. Don't settle down crying and complaining. It wont help.

Walk in wisdom, choose to be a man of excellence. Focus on being a person that impacts the world and inspire people. Be the best person you would feel great to be around. Doubts should not be part of you, worry should leave you. Let you soul free to enjoy the beauty of life without regrets. Any pain you have, use it for greatness. Don't drown in it. Use it. Your purpose is greater than anything.


Saturday, October 1, 2016

USIOGOPE KUKUTANA NA HOFU YAKO

Moja ya changamoto tunazopitia katika maisha ni hofu ya kukutana na hofu zetu na hofu ya mguso utakaotokana na hofu zetu. Huwezi kuwa huru kutoka katika hofu unayohofia kukutana nayo. Siku zote kuwa tayari kukutana na hofu zako na jivike ujasiri wa kuweza kuzidhibiti hofu zako.

Katika maisha lazima uwe na ujasiri wa kusonga mbele na kujua kuwa iko siku utakutana na hofu zako. Lazima ujipange jinsi ya kukabiliana na hofu yako na uwe jasiri maana hofu yako siku zote ndio gereza lako. Kuna wakati katika maisha inakubidi kuvuka daraja lenye kutia hofu kwa ujasiri ukitazamia maono uliyonayo katika maisha.

Amani ya nafsi ikishakaa ndani yako itakupa ujasiri wa kukabiriana na hofu yako ndio maana mwanafilosofia mmoja aliwahi kusema kuwa kama hakuna adui ndani ...adui wa nje haweza kutuathiri. Na hapa anapozungumzia adui sio lazima awe adui anayekupinga bali kuna maadui wa furaha yako na maono makubwa ambao wanaweza kuja kama watu wa karibu wakikushauri au mazingira fulani yakikukwamisha.

Lazima ujivike ujasiri na useme kwa jambo lolote nitasonga mbele na niko tayari kukutana na hofu yangu. Bila kuwa na huo ujasiri hofu yako itaendelea kukuzuia kusonga mbele. Na njia pekee ya kuweza kuishinda hofu yako ni kuwa mkweli kwa nafsi yako, kuwa mkweli kwa kile nafsi yako inataka na pia kuikubali amani iliyo ndani yako maana amani ya nafsi siku zote ni ya msingi sana. Ukisha kuwa mkweli uweke wazi ukweli ulio ndani yako, usiuogope, wala usiogope jinsi watu watakavoupokea huo ukweli.

Njia ya maisha siku zote ni ya kufanya maamuzi na kusonga mbele. Muda wa kukaa kutafakari kwa sababu ya hofu iliyo mbele yako ni kujikwamisha mwenyewe. Songa mbele kama una imani na kweli iliyo ndani yako. Amini tu kwamba kila jambo linafanyika kuwa jema. Maamuzi siku zote hutujenga, pasipo maamuzi tutaendelea kukaa katika hali ya mazoea ambayo pengine yangekuja kutuumiza.
Kuwa jasiri na Hofu zako zitakimbia. Usipokuwa jasiri hofu zako zitaendelea kukufunga sehemu ulipo.

Thursday, September 22, 2016

UHURU NA UDHIBITI WA KIHISIA

Uhuru wa kihisia ni pale unapoweza kudhibiti na kuelekeza hisia zako katika muundo na mpangilio uutakao. Hili si jambo rahisi kwa maana hisia huja kutokana na mabadiliko ya ndani ya mwili na hata hujengeka katika msingi wa nafsi ya mtu hivo uhuru wa kihisia unawezekana pale tu unapojenga tabia inayoitwa Nidhamu.

Nidhamu itakuwezesha kudhibiti hisia zako kwa namna kwamba utaweza kuzielekeza au kuamua muitikio na hata namna ya kukabili hali fulani zinazojitokeza. Uhuru wa kihisia kwanza unajengwa na kuitambua nafsi yako....nguvu na mapungufu yake kisha kujenga msingi wa kimaamuzi unaotokana na sheria utakazozijenga katika akili yako.

Hisia ni kama upepo, huja na hupoa na pengine hata kupotea kabisa, upepo huo unaweza kuwa kimbunga kwako au unaweza kuwa kama kipupwe kutokana na misingi ya kinidhamu ulioijenga katika nafsi yako ambayo inakupa uhuru wa kuamua jinsi hisia zako zinavodhibitiwa. Kudhibiti hisia ni sawa na kujenga mifereji ili kudhibiti mikondo ya maji isilete madhara au isielekee kusikotakiwa.

Ukiwa mfungwa wa hisia inamaana utendaji wako au muitikio wako katika mambo utatokana na msukumo wa hisia ulizonazo. Umeshawahi kuwa hisia nzito juu ya mtu fulani au jambo fulani kwa wakati fulani na ukatamani kulifuatilia lakini baada ya muda unapoteza hiyo hisia? Na hii hasa ndio changamoto ya kufanya maamuzi kwa kufuata hisia.

Jenga utaratibu wa kinidhamu wa kuratibu hisia zako kisha zielekeze kuongeza msukumo ktk sheria ulizozijenga na wala usiruhusu hisia zako zikuelekeze kupingana na sheria zako...namaanisha usiruhusu hisia pinzani zipate nguvu. Hisia zote zielekeze unapotaka ziende. Na hii inahitaji mazoezi.

Warren buffet aliwahi kusema kuwa mtu asiyeweza kudhibiti hisia zake hawezi kudhibiti pesa zake. Na hilo ni jambo la kweli kabisa, usipoweza kuwa nidhamu ya kihisia huwezi kuwe na nidhamu ya kiuchumi

Pia usipokuwa na uhuru wa kihisia utakuwa mhanga wa maumivu mengi ikiwemo mahusiano au hata namna watu wanavoleta upinzani katika maisha yako. Watu wasio na uhuru wa kihisia mara nyingi hushindwa kuchanganua ni aina gani ya mahusiano ni mazuri kwao na yatakayowajenga, kwao hisia zikishatawala wanashindwa hata kuruhusu akili zao kuchanganua.

Maisha bila uhuru wa kihisia ni kama msitu maana kila aina ya mabadiliko yatakuwa na mguso kwako na utataka kuitikia kila ambavyo hisia zitakutuma. Lazima uwe huru kuzidhibiti hisia la sivyo zitakuzamisha.

Thursday, September 15, 2016

ACHA YA JANA...ISHI YA LEO

Usiruhusu yale ya jana yachukue muda mwingi wa leo- Willy rogers

Moja ya changamoto kubwa katika maisha yako ya leo ni kumbukumbu ya jana yako. Jana yako unaweza kuitumia katika tathmini yako kukuwezesha kuwa na mtazamo chanya na wa fadhila hasa ukikumbuka ulipotoka na kushukuru kwa hapo ulipo huku ukitazama unapoelekea.

Changamoto kubwa ni pale jana yako inapochukua muda mwingi kihisia na hata kimtazamo kiasi cha kukufanya kushindwa kuiishi leo yako. Jana yako inaweza kuwa mtego wako hasa pale unapokuwa na hisia zilizoshikamana na jana hiyo. 

Kuna watu wengi wameshindwa kuachilia jana yao kiasi cha kutotazama fursa katika leo yao na kuacha fursa hizo zikipotea.

Wengi wameingia katika mahusiano leo na kumbukumbu la jana yao...Wengi wao wanataka kuishi leo lakini bado hawajaachana na jana yao. Ukiona unatamani sana jana ni dhahiri umepoteza dira ya leo na kesho yako. Kuna mambo mengi ya jana bado hutaki kuyaachilia na yamekuwa mzigo kwa leo yako.

Huwezi furahia leo yako kama jana yako inachukua sehemu kubwa ya moyo wako, akili yako na nafsi yako. Wengi leo wanaingia katika mahusiano huku bado hawajaacha kutazamia mahusiano ya jana yao. Wanajaribu hata kulinganisha leo na jana yao. Kuna wengine ambao pia hawajaacha machungu ya jana yafe, bado wanayapa nafasi katika akili yao kufikia hatua ya kuteswa na hofu ya kuishi leo katika ukamilifu.

Sikiza leo haiwezi kuja kama jana haijafa, Kesho haiwezi tokea kama leo haijaisha. Acha kuchelewesha furaha ya leo, fursa ya leo, nuru ya leo kwa kuendelea kukaa katika giza la jana..Weka pembeni na uiishi leo yako kwa furaha. Acha ya jana yawe ya jana...Ganga ya leo.