Showing posts with label Emotions. Show all posts
Showing posts with label Emotions. Show all posts

Wednesday, September 27, 2017

FREEDOM OF THE SOUL

One of the greatest challenges to the soul is freedom. The soul is in constant craving for freedom and it always strive to acquire freedom by any means.

 In life no matter how successful you can be, freedom is crucial for your soul to flourish, freedom enhances security and grounds for expressing the attributes for impact. Unless souls are free there will always be constant struggle.

We can choose to be free by letting our souls sink into themselves and to discover what we are made of and choosing to connect. Connection is a product of freedom.

Without freedom there is no connection whatsoever thats why its our duty to always free ourselves from the ties of our souls.


Monday, September 11, 2017

NAFASI YA MAZUNGUMZO YAKO KATIKA UTASHI WAKO WA KIHISIA

Je wajua kuwa mazungumzo yako ni kipimo cha utashi wako wa kihisia? Je wajua ya kwamba mazungumzo yako yana mchango katika uimara wa utashi wako wa kihisia. Jiulize tu swali moja, unazungumza nini?

Mfumo wako wa mazungumzo au uwasilishaji mawazo yako ni kipimo cha utashi wako wa kihisia. Jinsi unavozungumza juu ya maswala yenye miguso ya kihisia ndivo jinsi utashi wako wa kihisia ulivo. Watu wengi hudhani kuwa uhuru wa kuzungumza katika kutoa mitazamo ya kihisia ni sawa na uhuru wa kuzungumza katika maswala ya kiakili na kifikra, hapana. Uhuru wa kihisia unahitaji mguso wa kinafsi na ufahamu wa aina ya utu wa nafsi husika.

Watu wengi wamejikuta wanazungumza katika lugha hasi yenye harufu ya ukosefu wa imani na ladha ya uchungu wa maumivu kwakuwa ndivo utashi wao wa kihisia ulivo. Wengi wanazungumza nyuma ya pazia la woga na hofu wakionekana ni watu wenye uimara mkubwa kifikra kumbe kihisia ni nafsi ambazo zina hofu hata ya kupatwa na mawimbi ya kihisia. Ukiweza tambua miundo ya lugha na mitazamo utatambua kuwa kuna changamoto kubwa katika utashi wa kihisia.

Tambua ya kwamba kimjazacho mtu ndicho kimtokacho. Inatakiwa tutambue ni nini haswa hutujaza nafsi zetu. Kuna mazungumzo tunayopenda kuyapa nafasi pengine kwa utamu wake  wa kimaudhui wenye kuburudisha nafsi zenye shauku ya kutaka ufahamu pengine hata kama maudhui haina tija wala faida lakini mazungumzo hayo ndiyo yanajaza nafsi zetu magugu yanayoenda kusababisha udhaifu wa kihisia. Shauku isiyo na nidhamu ni adhabu kwa hisia na nafsi. Lazima ujifunze kuratibu mazumgumzo.

Kuna mazungumzo pia tunayofanya ambayo hutudhoofisha nafsi zetu na kutupa misukosuko ya kihisia isiyo na tija. Hivo ni muhimu kutambua na kufahamu aina ya mazungumzo na mguso wake kwa hisia zako

Hatuwezi kuwa watu wenye nafsi imara na utashi wa kihisia bila kuwa watu wenye kuratibu aina ya mazungumzo tunayofanya. Ni jambo gumu sana kuwa mtu mwenye mazungumzo yasiyo na tija kuwa na utashi wa kihisia pengine ni rahisi hata ngamia kupenya katika tundu la sindano. Lazima uwe makini na mazungumzo yako.

Ratibu vyema mazungumzo yako ili safari yako ya utashi wa kihisia iweze kuimarika.

Wednesday, August 23, 2017

UDHIBITI BINAFSI

Nafsi isiyo na udhibibiti binafsi ni sawa na mji usiokuwa na kuta

Moja ya changamoto kubwa ya kinafsi ni ukosefu wa udhibiti binafsi. Udhibiti binafsi na uwezo wa kinafsi wa kuratibu na kuzuia kila ambacho kinaweza kuingia katika nafsi husika na hapo ndipo tabia ya udhibiti binafsi inapokuja. Ulimwengu ni kama jalala yenye kila aina ya mambo, yenye kuharibu nafsi, yenye kujenga, yenye kuleta tabia na mitazamo asi au chanya, hivo ukitaka usalama wa kinafsi ni lazima uwe na udhibiti binafsi.

Haijalishi kwamba umepewa macho, kinywa au masikio, uimara wako unatokana na kutumia milango hiyo katika mambo ya msingi pekee. Udhibiti binafsi sio tu kudhibiti haja za mwili wako bali pia ni kudhibiti milango inayoingiza habari ndani yako. Huwezi kuwa na uimara kama ni mtu wa kutazama kila kitu, mtu wa kusikiza kila kitu, mtu wa kuchangia kila kitu, mtu wa kufatilia kila kitu au mtu wa kuongea kila kitu, hapana. Hautakuwa mtu mwenye utashi mzuri wa kihisia na hata kiakili.

Kuna tamaa za kinafsi kama shauku ya kutaka kufahamu mambo yasiyo na tija kwako, au kutaka kusikiza maswala yasiyoongeza thamani kwako au kutaka kufatilia watu wasio katika mlengwa wa yale yanayokuhusu. Ni tamaa tu ya kinafsi kutaka kuburudishwa na yanayowatokea wengine pengine hata kama hayana faida kwako. Usichofahamu ni kwamba unaijaza nafsi yako na mambo ambayo yanaongeza mzigo au yanakupa mtazamo ambao hauna tija kwako. Hakuna changamoto kubwa kama uchaguzi. Pale unapokuwa katika mazingira yanayokupasa uchague kuburudisha nafsi au kujenga nafsi.

Tafuta burudani ya kinafsi kwa mambo yanayohusiana na mambo ya msingi yanayokujenga. Kuwa na udhibiti binafsi, na wengi ambao hawana udhibiti binafsi wamejikuta katika matatizo mengi ya msongo wa mawazo au hata mikwaruzano isiyo na tija na watu wengine. Hata kama jambo lipo mbele yako sio lazima uburudishe nafsi yako kulifatilia. Hata kama hoja iko mbele yako sio lazima kuburudisha nafsi yako kuchangia. Hata kama maneno yanasemwa juu yako sio lazima kuruhusu nafsi yako kujibu, hata kama una shauku ya kuwafatilia watu sio lazima uruhusu nafsi yako kuwafatilia. Kama jambo badala ya kukusaidia linakujaza ujinga dhibiti nafsi yako na uliache.

Hakika usipokuwa mtu wa kudhibiti nafsi yako utakuwa mtu mwenye kubeba kila aina ya uchafu.

Tuesday, June 20, 2017

ITAJIRISHE NAFSI YAKO

Nafsi yako ni hazina kubwa maana ndio kiunganishi cha mwili wako na uhai wako au tunaweza sema roho yako. Nafsi yenye nguvu ni ile inayoweza kudhibiti fikra na kuratibu hisia na kuziweka katika mfumo utakaoleta tija katika maisha na tija kwa yale yanayokuzunguka.

Nafsi imara ni ile inayoweza kuchuja fikra na mawazo na kuhakikisha yanaleta mguso chanya kwa hisia ili zilete msukumo wa utendaji. Huwezi kuwa na nafsi imara kama haudhibiti fikra zako na kama hauratibu hisia zako. Hisia zinatakiwa zipokee msukumo chanya kutoka katika fikra zilizoratibiwa vizuri.

Utatu wa kinafsi yaani hisia, akili na utashi unahitaji kuchunguzwa na kila mwenye nafsi. Inapaswa kama binadamu uhakikishe sheria au misingi ya imani yako imejikita kujenga nafsi imara na sio nafsi dhaifu. Je ni mambo gani yanaingia zaidi katika nafsi yako, je watu wanaokuzunguka wana mguso upi katika nafsi yako? Hayo mambo ni ya kuchunguza sana.

Waweza kuitajirisha nafsi yako kiasi cha kwamba ikawa inatoa misimamo na hisia zenye uwiano, ni jambo lenye changamoto pale akili yako na hisia zikawa na mgongano katika namna inavogusa watu. Utashi wa kimawazo usio na utashi wa kihisia siku zote hauleti matokeo sawa. Unaweza kuwa na utashi wa kimawazo ila pasipo na utashi wa kihisia ukasababisha maafa makubwa.

Je mawazo yako yanaleta mguso gani wa kihisia. Waweza jua jambo lakini ukaliwasilisha likasababisha maafa au hata maudhi. Tajirisha nafsi yako kiasi cha kwamba utashi wako wa kiakili uuwiane na utashi wako wa kihisia. Nikupe mfano wa zawadi, ukipeleka zawadi kwa mtu na umeinunua kwa gharama siku zote lazima uifunge katika boxi la zawadi na uliwekee gift paper. Vivyo hivo ukiwa unatoa madini ya mawazo, ushauri na marekebisho lazima utumie utashi wa kihisia ili anayepokea afurahishwe na kuguswa na zawadi yako.

Hata Kama zawadi ulioifunga sio nzuri sana ila namna ulivoifunga inaweza ikamgusa mtu na akaipokea.

Tajirisha nafsi yako kwa kuweka uwiano katika ukuaji wa utaahi wa kihisia na utashi wa kiakili

Thursday, May 25, 2017

KUTOKA KATIKA UCHOVU WA KINAFSI

Uchovu wa kinafsi ni hali ya nafsi ya mtu kukosa nguvu ya kusimama ili kuweza kuhimili mitikisiko hasi. Ni hali ambayo kama ikiingia humjenga mtu kutaka ukombozi wa kinafsi na pumziko.

Kila uchovu unahitaji pumziko lakini njia za kupata pumziko ina utofauti. Kuna pumziko la kudumu na lile lisilo la kudumu. Watu wengi wamekuwa wakishindwa kutofautisha mapumziko hayo kutokana na kukosa taswira hada hasa pale uchovu unapokuwa mkubwa.

Changamoto kubwa ni uchaguzi wa pumziko la nafsi yako maana waweza fanya uchaguzi wa kudumu au wa muda mfupi ambao utakupa uchovu mkuu baada ya ganzi ya pumziko hilo kuisha.

Ili uweze kuchagua pumziko la kudumu ni lazima ujue chanzo kikuu cha uchovu wako wa kinafsi maana vichocheo vya uchovu huo mara nyingi ni kama mchwa ambao hukula taratibu nguvu yako ya kinafsi na kukuacha mchovu.

Unaweza pata uchovu wa kinafsi pale unapojaribu jambo linashindikana au pale unapotaka kubadili jambo inashindikana, unapotaka kubadili hali fulani lakini inashindikana au inaweza ikawa jambo fulani linakushambulia kila wakati ambalo unajaribu kuliepuka, au yawezakana ni watu ndo wanakupa uchovu wa kinafsi pale wanapoila amani yako, wanaposhambulia nguvu yako ya kusimama, na kutenda yale yanayovuruga misingi yako. Unaweza pata uchovu wa kinafsi na pengine ukajaribu kupata pumziko lakini ukashindwa katika uchaguzi wako ni lipi pumziko hasa unalohitaji.

Ukishindwa kujua hasa ni pumziko gani unalohitaji waweza jikuta unapata pumziko la muda mfupi ambalo likawa kama kilevi cha nafsi kisichokupa suluhisho la kinafsi la kudumu bali kinakupa nafuu ya muda mfupi tu.

Ukitaka kuondoa uchovu wa kinafsi siku zote jaribu kujitia nguvu kwa kuelekea zaidi pale ambapo panakutia nguvu, panakupa amani, panakupa mguso chanya, pana uwiano na kile unachokiamini, na pana misingi ya kiutu yenye uhusiano na nafsi yako.

Uchovu wa kinafsi humkuta kila mtu kwa wakati fulani lakini tofauti inakuja katika uchaguzi wa mapumziko. Waweza jikuta unajiingiza katika pumziko la muda mfupi ambalo badala ya kuitia nguvu nafsi yako linazidi kukudhoofisha.

Chagua vyema pumziko la nafsi yako ili uweze kuushinda uchovu wa kinafsi.

Monday, May 15, 2017

CHUNGA MOYO WAKO

Chunga moyo wako maana hiyo ndiyo bustani ya amani na furaha yako. Nafsi yako hustawi katika bustani ya moyo wako. Katika bustani ya moyo wako kunaweza kuwa na maua ya furaha, amani na faraja au magugu ya maumivu na uchungu. Kuwa muangalifu sana kwa kuchunga moyo wako kila wakati ni nini kinachoota.

Kuna mawazo na maneno ambayo ukiyaruhusu yaingie moyoni yanaenda kuweka majeraha ambayo kupona kwake kutakuchukua muda sana. Majeraha hayo yatajenga mfumo wa kifikra wa kujihami ili kuzuia maumivu mengine. Hasara ya fikra za kujihami ni kwamba utashindwa kufurahia uhuru na uzuri wa maisha kwa kuwa utaishi kwa kujihami.

Moyo wako unatakiwa ulindwe kama ngome imara. Ukiruhusu maumivu au matatizo yakaingia katika bustani ya moyo wako yataenda kuotesha magugu ya mawazo na fikra hasi. Kuna maneno ukiyaruhusu kuingia siku moja yatautesa moyo wako wakati wote. 

Safisha moyo wako kwa kuondoa yale ambayo yanauumiza na kutesa moyo wako. Yale ambayo kila ukiyafikiria unasikia kama kichomi ndani ya moyo wako, yale ambayo kila ukiyapa nafasi katika akili yanakububujisha machozi ya uchungu moyoni mwako.

Tambua kuwa moyo wako unatakiwa kustawisha amani, furaha na upendo. Ukiwa na moyo wenye uchungu inageuka kuwa sumu inayodhoofisha nafsi yako na akili yako. Utakuwa mtu mwenye vifungo badala ya uhuru.

Chunga moyo wako na uache katika amani. Usiuache umekaa katika dimbwi la maumivu au usiuache ushikilie uchungu unaokuumiza, usiuache ushikilie maneno makali au misumari ya mitazamo hasi juu yako. Usiruhusu moyo wako udunde kwa kasi kwa kukosa amani au kuwa na taharuki, Jipe utulivu kwa kuruhusu uzuri na furaha istawishe moyo wako.

Ruhusu yale yenye furaha na amani na yenye uzuri na utulivu ndio yakae katika moyo wako. Stawisha moyo wako ili ukutunze na uachilie yale yenye furaha, amani na pumziko. Kama vile damu inavoingia na kutoka katika mkondo wa mishipa ya damu, wewe pia tengeneza mkondo wa kuingiza furaha nyingi, amani nyingi na faraja nyingi moyoni mwako kwa kukaa na watu au mazingira yatakayosaidia hivo vitu lakini ondoa moyoni mkondo wa maumivu, uchungu na yale yanayoutatiza moyo

Lazima kuwe na uwiano baina ya yanayotoka na yanayoingia, usipende kuingiza mawazo hasi, Itafute hiyo furaha na amani ili ustawishe bustani ya moyo wako.

Fikra chanya au mazingira chanya sio tu yale yanayokusukuma kufanikiwa bali pia kuustawisha moyo wako na kuuacha katika hali ya utulivu.

Saturday, May 6, 2017

ALWAYS KEEP A JOYFUL DEMEANOR

Our strength lies in our ability to always keep a joyful demeanor in the face of our problems-Nickvaleries

Life has its ups and downs, Life has negative situations that can hit us or hurt us and we find it hard to be joyful but joy has to be founded from our souls.

When we believe in our worth and have the mentality that there is always something better ahead and that we will always receive the desires of our souls then we generate a joyful spirit and demeanor.

There is no reason to stay in sorrow and pain when you know that the best is out there heading your way and you ought to be ready and step towards it. Pain and sorrow will try to drown you in a state of emotional stagnation but rise up, smile and say to yourself that am heading to my best. Darkness is for a night but joy comes in the morning.

Always choose to be joyful and find joy at whatever costs by changing your belief from a victim to a victor of circumstances. If things change dont stay there drowning yourself. Get up and heal your soul of the pain and choose to keep a joyful demeanor.

Just say to yourself it is well with my soul then believe that you are heading for the best out there. Tell your heart you are not hurt but you are strengthened then find your rythm and be happy. Smile for your beauty and peace awaits.

The Universe will always smile back if you smile at it. Its just a matter of time till you find love, happiness and joy again. But for now keep a joyful demeanor and attitude.

Tuesday, May 2, 2017

USICHUKULIE KILA JAMBO KIHISIA

Ukitaka kuwa na furaha usipende kuchukulia kila jambo kinafsi au kihisia. Kuna mambo mengine ni ya kifikra tu na yamekaa kimtazamo tu ambayo hayatakiwi kuchukuliwa kihisia.

Ukitaka kuwa na utashi wa kihisia na uweze kuratibu hisia zako katika mlengwa chanya yakupasa kuziacha hisia zako katika mfumo tulivo kadri uwezavyo. Kuna mambo ukiyachukulia kihisia utaziweka hisia zako kwenye mfumo wa taharuki kwa wakati mwingi na itakupunguzia msisimko wa maisha ulio katika muundo chanya.

Je wawezaje kutochukulia mambo kihisia? Tambua kuwa kila wazo au mtazamo unapaswa kupokelewa kiakili na kuratibiwa kabla ya kusukumwa na hisia fulani. Ni vizuri ukiratibu mawazo na mitazamo unayopokea na kuiratibu kabla ya kujua ni hisia gani uiachilie ili isukume hilo jambo.

Ni muhimu sana kulishikilia wazo au mtazamo katika mfumo chanya hata kama limekuja katika muundo hasi. Lione hilo wazo kama njia ya kukuboresha, yaone hayo maoni kama njia ya kukuboresha kisha yape hisia chanya ndipo uyapokee. Usikubali kuanza kupokea kihisia wazo ambalo hujariratibu kwa akili.

Mfano mtu anaweza kukwambia jambo ambalo unaona kabisa linaweza lisiwe chanya kwako, badala ya kulipokea kwa hisia hasi jaribu kuliona ilo jambo kama wazo la kukuboresha na sio kukuharibu, kisha chukua hisia ya amani na furaha kwa kutambua kuwa hilo wazo limekuja kukuboresha..kisha chukua hisia ya morali na ari ya kulitafutia ufumbuzi na kulishughulikia hilo jambo na sio vinginevyo. Ukilipokea kama vile limekuja kukuumiza utaingiwa na taharuki ya kinafsi pengine hata kujenga ukuta kulizuia hilo suala na kuonekana kuwa ni mtu dhaifu kinafsi pengine hata mtu hasiyependa kuambiwa ukweli.

Nakushauri tena usilipokee kila jambo kihisia kabla ya kuriratibu kiutashi na kiakili ili kukujenga utashi wa kihisia itakayokupa furaha wakati wote.

Sunday, April 23, 2017

TAFUTA AMANI YA NAFSI

Hakuna jambo lenye msingi katika uimara na utashi wa nafsi kama amani ya nafsi - Nickvaleries

Huwezi kukua katika utashi wa nafsi pasipo kuwa na amani ya nafsi. Imani ikikaa katika nafsi humuwezesha mtu kustahimili misukosuko ya nje kwasababu kinachoweza kuzamisha meli sio bahari bali maji yanayoingia ndani ya meli.

Ukiweza kuiacha nafsi yako katika usalama kwa kujenga ukuta kuzuia yale yanayotokea yasiondoe amani ya nafsi utaweza kustahimili mengi. Ukikosa amani lazima utakosa imani na ukikosa imani hata utendaji wako na maneno yako yatakwenda kinyume na uhalisia.

Jiulize ni mambo gani ambayo unayaruhusu katika nafsi yako...Je yanaimarisha ngome za utulivu wako au yanabomoa amani ya nafsi yako na kukupa hali ya taharuki. Waweza kuwa na vyote ukakosa amani na ukikosa amani ukakosa imani huweza kuwa na furaha.

Hakuna furaha mahali palipokosa amani...Huwezi kuwa na furaha ya nafsi au kufurahia yale mazuri yanayokuzunguka kama ukikosa amani.  Tafuta kuwa na amani na jiimarishe kinafsi ukiziimarisha ngome za nafsi yako.

Jitahidi kujenga ngome zenye usalama ndani yako kiasi cha kusimama imara kinafsi hata kama mazingira ni yenye taharuki..sikiliza ulimwengu una taharuki na ukikosa amani jua huwezi kuwa na furaha.

Amani inaweza patikana kwa kuimarisha misingi ya uaminifu, mawasiliano, utashi wakihisia na utu. Tambua kwamba kila jambo linafanyika kuwa jema na wewe ni mwenye hatma njema na kuna mambo mengi mazuri ambayo yako mbele yako.

Taswira yako ni ya muhimu sana ukitaka kuwa na amani. Je unaangalia nini na unasikiliza nini? Hakikisha umejiimarisha kuratibu kila kinachoingia katika nafsi yako.

Usipende kuyapa muda mwingi mawazo na mazingira yanayoondoa amani yako. Itenge nafsi yako ili iwe na amani.


Wednesday, February 22, 2017

BENEFITS OF KNOWLEDGE AND ADVENTURE FOR EMOTIONAL INTELLIGENCE

Our minds and souls are constantly in need of exploration and discovery. The reason why we act differently and evolve is because our souls seek new horizons. Our minds need to be refreshend and expanded so as we can stable in our actions and in our ways. As it is said Lunacy is doing the same thing the same way and expecting different results.

We act in a lunacy form whenever we fail to expand our minds and let our souls explore its limitlessness. Knowledge is essential for expanding our minds increasing our possibilities and widening the limits that have been set by ignorance. We must grow in knowledge so as to be free. Emotional intelligence being the ability to perceive, assess and manage our emotions is a crucial attribute to our stability as human beings.

If we invest in knowledge while we let our souls experience wonder we invest in the attribute of emotional intelligence. We not only grow in our ability to manage our emotions but we develop control as to how we can relate our knowledge in a practical way to see wonder and adventure.

How can Knowledge and adventure be used simultaneously for emotional intelligence

1. Always read books of a specific topic in the specific moment at the specific place. That's Practical investment of knowledge.

2. Knowledge has to be put into practise, acquiring knowledge without practising it is a wastage of time. Ensure to always acquire the kind of knowledge you can practise.

3. Explore new horizons, listen don't let your life become a routine of activities that don't allow your soul to explore and experience the adventures of your life time.

4. Visit nature occasionally and meditate on it. This will open your mind and trigger your soul to explore the adventures of naturality.

Always remember that without emotional intelligence we will always be unstable human beings. If emotions aren't managed and assessed skillfully then we will always be human beings of so many imbalances and we will live life not realising the beauty of it.


Monday, January 16, 2017

GHARAMA NA KIPIMO CHA UVUMILIVU

Je wajua kila jambo bora huja na gharama ya uvumilivu. Kila jambo unalohitaji katika maisha huja na gharama ya uvumilivu huku ukikua katika nidhamu katika hicho kipindi cha uvumilivu. Kuna wakati unaweza dhani unaishi katika ndoto pale unapozungumza mambo pasipo kuyaona katika uhalisia.

Imani ni kuwa na uhakika wa mambo ambayo unayo katika fikra lakini bado hayajadhiirika. Unaweza omba msitu lakini ukapata mbegu ya msitu na ukaanza kujiuliza hii mbegu naifanyia nini. Unaweza kuwa na maono ya kujenga familia bora yenye kila hitaji muhimu likiwa limekamilika lakini ukajikuta unapata mwenza ambaye amekamilika katika hitaji la kinafsi lakini mahitaji ya kimali bado inakubidi uvumilie pengine hata uwekeze muda zaidi. Ni wewe kutambua kuwa hiyo uliyonayo ni mbegu bora inayohitaji udongo mzuri ili ichipue yale unayohitaji.

Hitaji la nafsi ni changamoto kubwa na wengi wamekuwa wakipata mahitaji mengine lakini wamekuwa wakiishi pasipo kuridhika kwakuwa mahitaji ya kinafsi wamekuwa wakiyakosa. Tambua kuwa kuna nyakati ambazo uvumilivu na imani yako itawekwa katika kipimo ili kuimarika katika uthabiti wa kimaamuzi. Kila jambo huwa zuri kwa muda kama likijengwa juu ya uaminifu, maono na nia thabiti ya kulisababisha lile jambo litokee katika uhalisia wake.

Lazima ufike kipindi ambacho imani yako itakuwa katika kipimo, lazima ifike kipindi utajiuliza je haya mambo ninayoyatazamia ni ndoto tu za mchana au kweli nitakuja kuyathibitisha. Unapofika katika kipindi hicho uimara wako na imani yako na fikra chanya ndizo zitakazokuvusha kuyapata yale unayoyahitaji na kuyatazamia.

Hakuna ndoto kwa mtu mwenye dhamira ya dhati na kila wakati anahangaika kutafuta njia za kutekeleza yale anayoyaona katika maono yake. Bali ni hatma ya muda na uvumilivu wa huyu mtu akisimama imara katika kutegemea yaliyo bora na yale anayoyatazamia. Usijione kuwa mwenye ndoto tu pengine labda unatazamia mambo ambayo kwa sasa huwezi yapata. Tambua kuwa dhamira ya dhati na utayari wa kujitoa huku ukichanganya na uvumilivu ukiendelea kukua kinafsi vitathibitisha ndoto zako na maono yako.

Sunday, November 20, 2016

LEARN TO IGNORE

The race of life is the one with a lot of obstacles, a lot of hindrances and a lot of oppositions, we all know that and we all have experienced that at some point in life, but there comes the most critical of all a lot of intimidations. If you havent master the art of ignoring voices then you will always fall victim.

When you are walking your walk always know that there are people who will come to intimidate you and try to misfocus you with words. Listen always be ready for that for people will hit you where it hurts you the most, sometimes even people you cant imagine but always guide your heart and mind. Many have grabbed a victim mindset simply because they take everything thrown unto them personal

Don't be intimidated...Learn to ignore, choose not to give full attention to distractions, Its obvious that some will be people very close to you in whom there opinions can have a big impact in you, but one of the greatest thing you need to do is detach yourself from the emotions brought about by people. Its true that you might sometimes fall prey in the predatorial world but stand up, ignore the predators and move on. What doesnt kill you makes you stronger.

Just because people are close doesn't mean that their opinions of you will always be right. Don't let the pressure get into you...Don't be intimidated, learn to ignore the impacts of their words. Learn to ignore, Ignore the negative feelings, ignore the negative emotions. Ignore what seems to bring you down. I challenge you to ignore those voices that keep running through your mind all the times telling you that you are somebody's victim. No you arent. Train your mind to cancel off and ignore.

Say to yourself, i choose to ignore all distractions. One African proverb says a lion doesn't turn back when dogs bark, also the noise of frogs doesn't hinder the elephant from drinking water from the stream. When you have an understanding of what people go through then it wont trouble you when they voice out their opinions out of emotions. Just ignore and move on. Choose to mind your own business and move on. No need to give an airtime to the calls that dont compliment you. Focus on the good. 

Thursday, November 10, 2016

KUDHIBITI HISIA HASI

Magugu siku zote huota hata sehemu ambazo hazitakiwi, hayaitaji mbegu..yenyewe huota bila kupandwa wala nini, vivo hivo na hisia hasi, huwa haziitaji kazi kubwa kukaa katika nafsi yako. Zinaweza kukuhijia wakati wowote na kwa namna yeyote lakini hisia chanya zinahitaji kupangiliwa, kurutubishwa na kupaliliwa.

Moyo wako kuna wakati unaweza patwa na hisia hasi ambazo zinakuja kutokana na jambo lolote, inawezekana ni uchovu wa kimwili au kiakili, mtu fulani kukukatisha tamaa, mtu fulani kuzungumza na wewe vibaya nk...yamkini ni mtu wako wa karibu, au mtu ambaye ana mguso wa tofauti ndani ya moyo wako. Lakini ni vyema ukatengeneza mzani wa kupima hisia hasi na kuzikata badala ya kuzipa hifadhi kwa muda mrefu ndani yako.

Ukizipa hifadhi kwa muda mrefu zina tabia ya kuchoma nafsi yako na kila zikichoma nafsi yako zinakujengea hali ya kutaka kuzitoa. Na hapo wengi wamejikuta wakizitoa kwa msukumo unaosababisha maafa zaidi. Njia pekee ya kuzidhibiti hisia hasi ni kupumzisha nafsi yako kwa muda huku ukijaribu kuingiza hisia chanya.

Hisia chanya zinahitaji nidhamu kuziimarisha ndani ya nafsi yako, kwasababu asilimia kubwa ya watu wamezungukwa na mazingira hasi mfano ndugu walalamishi, marafiki wasiojali, wapendwa wasiokuelewa na wasioheshima uhuru wako na furaha yako. Inabidi ujipe likizo ya kinafsi. Ikiwezekana jijengee utaratibu hata wa kufunga kuendekeza hisia hasi kwa kipindi fulani kama jinsi ambavyo dini hufunga chakula au starehe fulani waweza funga kutoziendekeza hisia hasi.

Jenga utaratibu katika maisha yako wa kutozipa hifadhi hisia hasi wala kuziendekeza kwa muda mrefu. Hisia ni mfano wa mimea, kuna mimea bora na kuna magugu. Hisia hasi ni kama magugu. Tafuta kuwa mtu mwenye hisia chanya kila wakati. Ni sawa na chumba chenye uchafu na kila aina ya takataka...usipoweza kuondoa visivohitajika, chumba kitajaa na hewa itakuwa haizunguki vizuri. Usipoweza kupunguza hifadhi ya hisia hasi ndani ya nafsi yako, nafsi yako itajaa na hewa nzuri ya mazingira chanya haitozunguka vizuri ndani yako.


Sunday, October 23, 2016

TENGENEZA MKONDO MZURI WA MAWASILIANO

Moja ya changamoto katika maisha ni pale tunaposhindwa kutengeneza mkondo mzuri wa mawasiliano na hii upelekea mikwaruzano na hata hali ya taharuki na hata hali ya mashaka juu ya mustakabali mzima wa mambo.

Mahusiano pasipo mawasiliano mazuri ya kinafsi ni chanzo kikubwa cha huzuni na hata kuumizana, waweza kuwa na nia njema lakini ukishindwa kutengeneza mkondo mzuri wa mawasiliano unaweza eleweka vibaya. Au unaweza kumuumiza mtu mwingine, ni muhimu sana ukawa mtu wa kuwa unazungumza.

Ni lazima ujenge hali nzuri na msingi imara ili uweze kuwasiliana na mwenzako au yule ambaye unataka kuwasilisha kile unachoona kinakutatiza. Wakati mwingi huwa tunadhani kwamba ni lazima tutafute misamiati mizuri ya mawasiliano, ni kweli pia kuna wakati unaweza kuwasilisha jambo fulani likapokelewa usivyodhania ndo maana kuna wakati unaweza kuwa na hofu fulani.

Ni muhimu kujenga msingi wa uwazi na ukweli na uwe huru maana pasipo uhuru wa nafsi juu ya jambo fulani huwezi kujenga mkondo mzuri wa mawasiliano ndio maana ni muhimu kuwa na msingi mzuri wa kihisia ukitaka kuwa na mkondo mzuri wa mawasiliano...Tambua ya kwamba unapokuwa huru kuzungumza ndio utakuwa na uhuru wa kuwa vile unavotaka.

Kuna sauti nyingi ambazo zinaweza kuja katika akili yako kukuzuia kujenga mkondo mzuri wa mawasiliano, kukosa amani ya nafsi, hofu au hata kutotaka kufikiriwa au kutazamiwa vibaya ndio maana inakupasa uwe na uhuru na amani ya nafsi na utambue kuwa wewe ni nafsi huru na unatakiwa uwe huru kuwasilisha yaliyo katika nafsi yako.

Jifunze kuzungumza kama unadhani huwezi kuzungumza yaliyo ndani ya nafsi yako, tambua nafsi yako ina uzuri na ukuu ambao kama ukishindwa kuzungumza inakuwa vigumu kueleweka....iache nuru yako ing'ae...usihofie kuzungumza. Usipozungumza unaweza jikuta upo katika hali ya taharuki na ukaishi kama mfungwa wakati ukisema ukweli utakuwa huru

Hekima ni kutambua njia na muda muafaka wa kuzungumza lakini mawasiliano ya nafsi ni jambo la msingi sana, yatakuweka huru. Ukitaka sana kufurahisha watu pia inaweza kuwa changamoto yako kuzungumza, pia usipotaka kuwaumiza watu inaweza kuwa changamoto yako kuzungumza lakini ni vyema ukawa huru katika nafsi.

Thursday, October 13, 2016

SAUTI TATU KATIKA MAHUSIANO

Mahusiano yetu huguswa na sauti ambazo zinaleta changamoto na ni sauti ambazo zinamchango katika uimara wa mahusiano yako au kuanguka kwa mahusiano yako. Bila sauti hizo kuwa katika uwiano  sawa basi sauti moja ikiizidi nyenzake inaweza sababisha changamoto.

Sauti hizo zimegawanyika katika makundi matatu, ya kwanza ni sauti ya nafsi ; Hii ni sauti ambayo kila mtu anakuwa nayo kiasili nayo ni sauti ya uhuru, furaha na amani. Kila nafsi inataka kuwa katika uhusiano ambapo itakuwa huru na yenye furaha na amani, sauti hii inalia kutoka ndani ya nafsi ya mtu na ndio maana kuna ambao husema kuwa katika uhusiano ambao utakuwa huru na mwenye furaha na amani.

Sauti ya pili ni sauti ya Jamii; hii ni sauti inayotoka katika jamii inayotuzunguka juu ya mahusiano yetu. Hii sauti inaweza ikawa sauti ya wazazi au sauti ya malezi na makuzi ambayo tumeyapitia. Sauti hii mara nyingi hutuambia kuwa ni nani anatufaa, au ni nani tunatakiwa tuwe naye au ni mahusiano gani ambayo inabidi tuwe nayo.

Sauti ya tatu ni sauti ya akili zetu; Binadamu huwa na hali ya kupenda kutafakari na kutumia akili katika kufanya maamuzi na pengine kuna wakati hutumia zaidi akili katika mambo fulani juu ya nini hasa jambo sahihi la kufanya.

Ili kujenga uhusiano imara lazima hizi sauti ziwe na uwiano...sauti ya nafsi inabidi iwe kama msingi itakayobeba sauti nyingine zote. Sauti ya nafsi ikizifunika sauti nyingine zote unaweza pelekea kufanya mambo ambayo yanaweza kutokubalika katika jamii na ukajikuta unakosa kabisa ushirikiano na wengine lakini sauti ya jamii ikiizidi sauti ya nafsi utajikuta unaingia katika mahusiano ambayo katika jamii unasifika lakini ndani ya nafsi yako unakosa furaha na unakuwa na upweke ambao jamii haiwezi kukusaidia.

Pia inakupasa sauti ya nafsi iwe na uwiano na sauti ya akili ili akili yako iweze kuwekeza zaidi...maana nafsi na akili zikiwa na uwiano ile amani na furaha hudhiirika katika fikra za ubunifu zaidi katika kuimarisha mahusiano hayo.

Kama unaona sauti ya jamii ni kubwa na inakutisha hakikisha sauti ya nafsi na sauti ya akili vinaungana kuishurutisha sauti ya jamii itulie.

Changamoto na jambo la msingi kwa kila mtu ni kuhakikisha hizo sauti zina uwiano ili kujenga mahusiano imara.


Saturday, October 1, 2016

USIOGOPE KUKUTANA NA HOFU YAKO

Moja ya changamoto tunazopitia katika maisha ni hofu ya kukutana na hofu zetu na hofu ya mguso utakaotokana na hofu zetu. Huwezi kuwa huru kutoka katika hofu unayohofia kukutana nayo. Siku zote kuwa tayari kukutana na hofu zako na jivike ujasiri wa kuweza kuzidhibiti hofu zako.

Katika maisha lazima uwe na ujasiri wa kusonga mbele na kujua kuwa iko siku utakutana na hofu zako. Lazima ujipange jinsi ya kukabiliana na hofu yako na uwe jasiri maana hofu yako siku zote ndio gereza lako. Kuna wakati katika maisha inakubidi kuvuka daraja lenye kutia hofu kwa ujasiri ukitazamia maono uliyonayo katika maisha.

Amani ya nafsi ikishakaa ndani yako itakupa ujasiri wa kukabiriana na hofu yako ndio maana mwanafilosofia mmoja aliwahi kusema kuwa kama hakuna adui ndani ...adui wa nje haweza kutuathiri. Na hapa anapozungumzia adui sio lazima awe adui anayekupinga bali kuna maadui wa furaha yako na maono makubwa ambao wanaweza kuja kama watu wa karibu wakikushauri au mazingira fulani yakikukwamisha.

Lazima ujivike ujasiri na useme kwa jambo lolote nitasonga mbele na niko tayari kukutana na hofu yangu. Bila kuwa na huo ujasiri hofu yako itaendelea kukuzuia kusonga mbele. Na njia pekee ya kuweza kuishinda hofu yako ni kuwa mkweli kwa nafsi yako, kuwa mkweli kwa kile nafsi yako inataka na pia kuikubali amani iliyo ndani yako maana amani ya nafsi siku zote ni ya msingi sana. Ukisha kuwa mkweli uweke wazi ukweli ulio ndani yako, usiuogope, wala usiogope jinsi watu watakavoupokea huo ukweli.

Njia ya maisha siku zote ni ya kufanya maamuzi na kusonga mbele. Muda wa kukaa kutafakari kwa sababu ya hofu iliyo mbele yako ni kujikwamisha mwenyewe. Songa mbele kama una imani na kweli iliyo ndani yako. Amini tu kwamba kila jambo linafanyika kuwa jema. Maamuzi siku zote hutujenga, pasipo maamuzi tutaendelea kukaa katika hali ya mazoea ambayo pengine yangekuja kutuumiza.
Kuwa jasiri na Hofu zako zitakimbia. Usipokuwa jasiri hofu zako zitaendelea kukufunga sehemu ulipo.

Thursday, September 22, 2016

UHURU NA UDHIBITI WA KIHISIA

Uhuru wa kihisia ni pale unapoweza kudhibiti na kuelekeza hisia zako katika muundo na mpangilio uutakao. Hili si jambo rahisi kwa maana hisia huja kutokana na mabadiliko ya ndani ya mwili na hata hujengeka katika msingi wa nafsi ya mtu hivo uhuru wa kihisia unawezekana pale tu unapojenga tabia inayoitwa Nidhamu.

Nidhamu itakuwezesha kudhibiti hisia zako kwa namna kwamba utaweza kuzielekeza au kuamua muitikio na hata namna ya kukabili hali fulani zinazojitokeza. Uhuru wa kihisia kwanza unajengwa na kuitambua nafsi yako....nguvu na mapungufu yake kisha kujenga msingi wa kimaamuzi unaotokana na sheria utakazozijenga katika akili yako.

Hisia ni kama upepo, huja na hupoa na pengine hata kupotea kabisa, upepo huo unaweza kuwa kimbunga kwako au unaweza kuwa kama kipupwe kutokana na misingi ya kinidhamu ulioijenga katika nafsi yako ambayo inakupa uhuru wa kuamua jinsi hisia zako zinavodhibitiwa. Kudhibiti hisia ni sawa na kujenga mifereji ili kudhibiti mikondo ya maji isilete madhara au isielekee kusikotakiwa.

Ukiwa mfungwa wa hisia inamaana utendaji wako au muitikio wako katika mambo utatokana na msukumo wa hisia ulizonazo. Umeshawahi kuwa hisia nzito juu ya mtu fulani au jambo fulani kwa wakati fulani na ukatamani kulifuatilia lakini baada ya muda unapoteza hiyo hisia? Na hii hasa ndio changamoto ya kufanya maamuzi kwa kufuata hisia.

Jenga utaratibu wa kinidhamu wa kuratibu hisia zako kisha zielekeze kuongeza msukumo ktk sheria ulizozijenga na wala usiruhusu hisia zako zikuelekeze kupingana na sheria zako...namaanisha usiruhusu hisia pinzani zipate nguvu. Hisia zote zielekeze unapotaka ziende. Na hii inahitaji mazoezi.

Warren buffet aliwahi kusema kuwa mtu asiyeweza kudhibiti hisia zake hawezi kudhibiti pesa zake. Na hilo ni jambo la kweli kabisa, usipoweza kuwa nidhamu ya kihisia huwezi kuwe na nidhamu ya kiuchumi

Pia usipokuwa na uhuru wa kihisia utakuwa mhanga wa maumivu mengi ikiwemo mahusiano au hata namna watu wanavoleta upinzani katika maisha yako. Watu wasio na uhuru wa kihisia mara nyingi hushindwa kuchanganua ni aina gani ya mahusiano ni mazuri kwao na yatakayowajenga, kwao hisia zikishatawala wanashindwa hata kuruhusu akili zao kuchanganua.

Maisha bila uhuru wa kihisia ni kama msitu maana kila aina ya mabadiliko yatakuwa na mguso kwako na utataka kuitikia kila ambavyo hisia zitakutuma. Lazima uwe huru kuzidhibiti hisia la sivyo zitakuzamisha.

Tuesday, August 23, 2016

OUR ATTITUDE MATTERS

The process of human change begins within us. We all have tremendous potential. We all desire good results from our efforts. Most of us are willing to work hard and to pay the price that success and happiness demand.

Each of us has the ability to put our unique human potential into action and to acquire a desired result. But the one thing that determines the level of our potential, that produces the intensity of our activity, and that predicts the quality of the result we receive is our attitude.

Attitude determines how much of the future we are allowed to see. It decides the size of our dreams and influences our determination when we are faced with new challenges. No other person on earth has dominion over our attitude.

People can affect our attitude by teaching us poor thinking habits or unintentionally misinforming us or providing us with negative sources of influence, but no one can control our attitude unless we voluntarily surrender that control. No one else "makes us angry." We make ourselves angry when we surrender control of our attitude.

What someone else may have done is irrelevant. We choose, not they. They merely put our attitude to a test. If we select a violent attitude by becoming hostile, angry, jealous or suspicious, then we have failed the test.

If we condemn ourselves by believing that we are unworthy, then again,we have failed the test. If we care at all about ourselves, then we must accept full responsibility for our own feelings. We must learn to guard against those feelings that have the capacity to lead our attitude down the wrong path and to strengthen those feelings that can lead us confidently into a better future.

If we want to receive the rewards the future holds in trust for us, then we must exercise the most important choice given to humanity by maintaining total dominion over our attitude. Our attitude is an asset, a treasure of great value, which must be protected accordingly.

Beware of the vandals and thieves among us who would injure our positive attitude or seek to steal it away. Having the right attitude is one of the basics that success requires.