Showing posts with label Vision. Show all posts
Showing posts with label Vision. Show all posts

Wednesday, November 23, 2016

MAKE YOUR THOUGHTS FUTURE ORIENTED

One of the greatest challenges to thinking is the directions of your thoughts, Are your thoughts future oriented or past oriented? Is the direction of your thoughts forward or backwards? Backward oriented thoughts are a resistance to future pursuit. The quest to the future needs a future oriented mindset.

If you are constantly thinking backwards rather than thinking forwards then you create a resistance in your forward movement. When you think backward you create a force that pulls you backwards to the past. But if you think forward you create a force that pulls you forward to your future.

You can never move in a direction where your thoughts aren't directed, Don't ever fall in the trap of the mind of thinking backwards. Thinking backwards is thinking about things past, its entertaining past thoughts, its your reluctance to delete the past from your system. The duty of the past is to give you a motivation to create a platform for the future you want. Once you find the gear of the future, drive in the future mode and set your mind there.

Never inter-change your present gear with your past gear, its dangerous, You can only change your present gear with your future gear to increase the momentum and increase a boost of enthusiasm. How do you inter change present gear with future gear....Its by consuming some of the future ideas and dreams and instill them in the present, You cant consume all of them or else your present will be crowded and you wont find pleasure in the process

Its very important to think forward, just analyse yourself in the times you sit down to think what are the directions of your thoughts? Present, Past or future. Ask yourself also when you want to act on something and thoughts come in your mind in your analysis where are those thoughts from? Past or future... If you realise that its your past that brings out most of your thoughts then its time to change.

Make the future be the source of your thoughts and let the future interchange gears of motivation in your quest to pursue life.

Tuesday, November 8, 2016

INVEST IN YOURSELF

How do you picture yourself? How do you see your life? How do you see your soul? How do you see your spirit? Do you see any area you can add more value in you. There is still more you can add in your life. You still have room for more. Invest in excellence. You still have more you can add.

Listen when you stop growing you start dying. And dying can start from your soul, mind and even your spirit. You slowly start to settle for whats below you. You slowly start to settle for what doesn't compliment you. Listen challenges should boost you to invest in yourself more.

Negative thinking will just drown you in negativity. Choose to direct your thoughts towards creating value in life. You can still be the best version of yourself. Refuse to settle in despair. Life is bigger than that...rise higher. A country like america invested in every sector to be the world superpower. Invest in every sector of your life. Your health, your skills, your financial life. Invest more and let you be needed for the value you have.

Feed your faith and your fears will flee, choose to distinguish yourself...Don't fit in, fit out with character and excellence. Be the best version of yourself for when you do that you will always stand out with an impact. Commit yourself in being a person of value and character. Enrich your soul with everything needful for you. Don't settle down crying and complaining. It wont help.

Walk in wisdom, choose to be a man of excellence. Focus on being a person that impacts the world and inspire people. Be the best person you would feel great to be around. Doubts should not be part of you, worry should leave you. Let you soul free to enjoy the beauty of life without regrets. Any pain you have, use it for greatness. Don't drown in it. Use it. Your purpose is greater than anything.


Friday, October 28, 2016

IMANI YAKO HUJENGA KAWAIDA YAKO

Imani mara nyingi hutokana na uzoefu juu ya jambo fulani, uzoefu huo hujiimarisha katika ubongo wako na kutengeneza mfumo wa kisheria ambao utatawala mitazamo yako na utakujengea kawaida yako. Na mara nyingi kawaida hiyo hujenga utamaduni ambao utakusanya mambo ya kuthibitisha na kuendana na utamaduni huo.

Unapojenga imani fulani siku zote imani hiyo huvuta mazingira husika ya kuthibitisha imani hiyo. Mfano unapojenga imani kuwa katika mahusiano jinsia fulani sio ya kuaminika imani hiyo huvuta mazingira hayo, imani hiyo itakuongoza kuchagua watu wasioaminika na hata itakujenga kutafuta mazingira yasio aminifu katika mahusiano yako ili kuthibitisha imani hiyo.

Siku zote akili hujisikia furaha pale inapothibitisha mitazamo yake na malengo yake..ndio maana siku zote ukithibitisha jambo ulilokuwa na wasiwasi nalo hata kama linaumiza akili yako itasema nilijua tu....tafsiri ya neno nilijua ni kuipa thamani akili yako kwa uthibitisho huo na kuijengea thamani kwa imani hiyo.

Ni muhimu utambue kuwa unatakiwa kutafakari sana kabla hujakiweka kitu kama imani yako kwasababu imani hiyo itakutengenezea kawaida yako. Na siku zote kawaida yako ndio ulimwengu wako. Watu wengi wamejijengea kawaida mbaya hadi pale jambo zuri linapokuja wanalikataa na kuliona haliwastahili. Kuna watu wamejijengea kawaida kiasi cha kwamba jaribio lolote la kutoka hapo ni maumivu kwao.

Usijenge msingi wa kiimani ambao unaona kabisa ni asi kwasababu huo msingi utavuta mazingira ya kuthibitisha hayo uliyoyaweka kama sheria. Hakikisha kabla hujaliamini jambo na kuliweka katika akili yako litafakari. Usije kufungwa na kawaida ambayo itakutesa. Mfano mtu anaweza akaja kukwambia yaani mie kila mahusiano yangu naumizwa...unamuuliza je unadhani kwanini....mtu anakwambia mie nadhani nina mkosi au wanaume wote ni wahuni, au wanawake wote hawaaminiki...Tayari kishajenga imani ambayo inavuta mazingira kuthibitisha imani hiyo.

Ni jambo la muhimu sana kuongeza maarifa juu ya jambo usilolijua badala ya kujijengea imani ambazo zitakujengea kawaida yako. Pia ni kubadilisha taswira yako, ni nini hasa unaangalia au ni wapi hasa mtazamo wako ulipo maana taswira siku zote hukutengenezea imani itakayokujengea kawaida itakayovuta mazingira kuthibitisha mambo husika.

Monday, October 17, 2016

BADILI TASWIRA WAKO

Changamoto kubwa katika maisha ni kuwa na mitazamo mibovu. Taswira uliyonayo juu ya mambo inatokana na hazina uliyoweka moyoni mwako. Jinsi unavowekeza ndani yako ndo jinsi unavojenga taswira nzuri katika maisha yako. Mambo unayoyaona mazito kwako inatokana na nguvu au hazina uliyowekeza ndani yako.

Usipowekeza katika kukua siku zote hautakuwa mtu mwenye taswira nzuri....ukiwa na hazina ndogo au nguvu ndogo ya kiroho siku zote taswira yako itakuwa na tatizo...na ukikosa taswira nzuri utakuwa ni mtu mwenye kulaumu na kuona kama maisha hayakutendei haki. Maisha yapo siku zote lakini wenye nguvu ndio wanaoweza kustahimili hivo wekeza kuwa na nguvu katika nafsi yako.

Chukua kila tatizo linalokuja kwako na ulione kama jiwe la kwenda kiwango kingine. Chukua maumivu na uyaone kama fursa ya kujiimarisha zaidi roho yako. Usilalamike, wewe ni kiongozi wa maisha yako na kila jambo hufuata mkondo unaouweka wewe. Hukuzaliwa umfurahishe kila mtu hivo acha kufungwa katika mawazo au shuruti za watu. Unatakiwa uwe huru.

Ili taswira yako iwe nzuri ibadilishe, unapokuwa unatafuta taswira ya picha na camera lazima uhakikishe picha ya maisha yako unaiweka katika mraba, kuna vitu vya kuondoa katika taswira hiyo, unaweza kubadili umbali nk. Vivyo hivo katika maisha yako ukitaka upate taswira unayoitaka kuna watu inabidi uachane nao, kuna mambo inabidi uachane nayo, kuna vitu inabidi uviondoe katika taswira. Haijalishi vikoje kama unaona havipo katika taswira yako yakupasa uviondoe.

Usipokua, siku zote taswira yako itakuwa ndogo, kuna mambo mengine hujayajua au kuna mambo mengine huyaoni kwasababu huna taswira nzuri na hii hutokana na kutokuwa na hazina na nguvu ndani yako.


Monday, October 3, 2016

TAMBUA UNACHOTAKA KATIKA MAISHA

Moja ya changamoto kubwa ambayo watu wengi huwa tunayo ni kutofahamu nini tunachotaka au tunachohitaji katika maisha. Watu wengi hudhani wanajua wanachokitaka au wanachokihitaji lakini ukiangalia matendo yao utatambua kuwa wengi hawajui wanachokitaka katika maisha. Usipojua unachotaka katika maisha utakuwa ni mtu wa kuzunguka zunguka kujaribu jaribu kila kitu kuona kina mguso gani kwako.

Kuna dhana nyingi sana ambazo tunazo ju ya yale tunayotaka katika maisha na unaweza ukapewa kila ulichodhani unakitaka kisha ukaja kugundua kuwa bado kuna kitu kingine unachokitaka. Na utakuwa ni mtu usiye na furaha wala amani kwasababu hujui unachokitaka. Pengine hata ukawa mtu mwenye lawama katika kila jambo kwasababu wewe mwenyewe hujui unachokitaka.

Pengine pia unaweza jua unachokitaka lakini unadhani ni jambo la kufikirika, huo mtazamo unaweza kukufanya ukaendelea kuwa kama mtumwa anayezunguka jangwani asijue anapoelekea. Kuna mwanafilosofia mmoja aliwahi kusema kuwa Watu wengi hawajui wanachokitaka hadi uwaonyeshe wanachokitaka. Ni muhimu sana kujua unachokitaka.

Njia pekee ya kujua unachokitaka ni kujitathmini nafsi yako na kujitambua utu wako ndipo utajua ni nini unachohitaji. Mwanafilosofia mmoja aliwahi kusema kuwa kama hakuna adui ndani adui wa nje hawezi kutudhuru. Nafsi yako ya ndani imeundwaje? Pengine ushawahi kujiuliza ni jambo gani linakupa amani na unaamini ndio jambo ambalo ukilipata kama msingi wa maisha yako utaweza kupata mambo mengine yote?

Kila nafsi inahitaji uhuru na amani na furaha na wengi wetu tumedhani tukipata vitu basi nafsi yetu ndo itakuwa imepata inachotaka. Hapana!! Nafsi yako inahitaji kukua na jambo lolote linaloweza kuinyanyua nafsi yako ndilo jambo unalohitaji. Nafsi yako inahitaji thamani na jambo linaloweza kuipa thamani nafsi yako ndilo unalohitaji. Nafsi yako inahitaji amani na jambo lolote linaloweza kukupa amani ya nafsi ndilo unalohitaji.

Ukishajua msingi hasa wa mahitaji ya nafsi yako itakuwezesha kutambua ni nini unachohitaji katika maisha, iwe ni katika uchaguzi wa kazi, iwe ni katika mahusiano au nyanja yeyote ya maisha. Utatambua marafiki wa nafsi yako, utatambua hata mwenzi wa nafsi yako, utatambua hata kusudi la maisha yako.

Saturday, October 1, 2016

USIOGOPE KUKUTANA NA HOFU YAKO

Moja ya changamoto tunazopitia katika maisha ni hofu ya kukutana na hofu zetu na hofu ya mguso utakaotokana na hofu zetu. Huwezi kuwa huru kutoka katika hofu unayohofia kukutana nayo. Siku zote kuwa tayari kukutana na hofu zako na jivike ujasiri wa kuweza kuzidhibiti hofu zako.

Katika maisha lazima uwe na ujasiri wa kusonga mbele na kujua kuwa iko siku utakutana na hofu zako. Lazima ujipange jinsi ya kukabiliana na hofu yako na uwe jasiri maana hofu yako siku zote ndio gereza lako. Kuna wakati katika maisha inakubidi kuvuka daraja lenye kutia hofu kwa ujasiri ukitazamia maono uliyonayo katika maisha.

Amani ya nafsi ikishakaa ndani yako itakupa ujasiri wa kukabiriana na hofu yako ndio maana mwanafilosofia mmoja aliwahi kusema kuwa kama hakuna adui ndani ...adui wa nje haweza kutuathiri. Na hapa anapozungumzia adui sio lazima awe adui anayekupinga bali kuna maadui wa furaha yako na maono makubwa ambao wanaweza kuja kama watu wa karibu wakikushauri au mazingira fulani yakikukwamisha.

Lazima ujivike ujasiri na useme kwa jambo lolote nitasonga mbele na niko tayari kukutana na hofu yangu. Bila kuwa na huo ujasiri hofu yako itaendelea kukuzuia kusonga mbele. Na njia pekee ya kuweza kuishinda hofu yako ni kuwa mkweli kwa nafsi yako, kuwa mkweli kwa kile nafsi yako inataka na pia kuikubali amani iliyo ndani yako maana amani ya nafsi siku zote ni ya msingi sana. Ukisha kuwa mkweli uweke wazi ukweli ulio ndani yako, usiuogope, wala usiogope jinsi watu watakavoupokea huo ukweli.

Njia ya maisha siku zote ni ya kufanya maamuzi na kusonga mbele. Muda wa kukaa kutafakari kwa sababu ya hofu iliyo mbele yako ni kujikwamisha mwenyewe. Songa mbele kama una imani na kweli iliyo ndani yako. Amini tu kwamba kila jambo linafanyika kuwa jema. Maamuzi siku zote hutujenga, pasipo maamuzi tutaendelea kukaa katika hali ya mazoea ambayo pengine yangekuja kutuumiza.
Kuwa jasiri na Hofu zako zitakimbia. Usipokuwa jasiri hofu zako zitaendelea kukufunga sehemu ulipo.

Thursday, September 15, 2016

ACHA YA JANA...ISHI YA LEO

Usiruhusu yale ya jana yachukue muda mwingi wa leo- Willy rogers

Moja ya changamoto kubwa katika maisha yako ya leo ni kumbukumbu ya jana yako. Jana yako unaweza kuitumia katika tathmini yako kukuwezesha kuwa na mtazamo chanya na wa fadhila hasa ukikumbuka ulipotoka na kushukuru kwa hapo ulipo huku ukitazama unapoelekea.

Changamoto kubwa ni pale jana yako inapochukua muda mwingi kihisia na hata kimtazamo kiasi cha kukufanya kushindwa kuiishi leo yako. Jana yako inaweza kuwa mtego wako hasa pale unapokuwa na hisia zilizoshikamana na jana hiyo. 

Kuna watu wengi wameshindwa kuachilia jana yao kiasi cha kutotazama fursa katika leo yao na kuacha fursa hizo zikipotea.

Wengi wameingia katika mahusiano leo na kumbukumbu la jana yao...Wengi wao wanataka kuishi leo lakini bado hawajaachana na jana yao. Ukiona unatamani sana jana ni dhahiri umepoteza dira ya leo na kesho yako. Kuna mambo mengi ya jana bado hutaki kuyaachilia na yamekuwa mzigo kwa leo yako.

Huwezi furahia leo yako kama jana yako inachukua sehemu kubwa ya moyo wako, akili yako na nafsi yako. Wengi leo wanaingia katika mahusiano huku bado hawajaacha kutazamia mahusiano ya jana yao. Wanajaribu hata kulinganisha leo na jana yao. Kuna wengine ambao pia hawajaacha machungu ya jana yafe, bado wanayapa nafasi katika akili yao kufikia hatua ya kuteswa na hofu ya kuishi leo katika ukamilifu.

Sikiza leo haiwezi kuja kama jana haijafa, Kesho haiwezi tokea kama leo haijaisha. Acha kuchelewesha furaha ya leo, fursa ya leo, nuru ya leo kwa kuendelea kukaa katika giza la jana..Weka pembeni na uiishi leo yako kwa furaha. Acha ya jana yawe ya jana...Ganga ya leo.

Sunday, August 28, 2016

HAKUNA AJALI, KILA JAMBO LINA KUSUDI

"Huwa hakuna ajali.. Bali kuna kusudi ambalo bado hatujalitambua "-Deepak Chopra

Katika moja ya mafundisho yake mhamasishaji na mkufunzi wa maswala ya kujitambua Deepak chopra alisema huwa hakuna ajali bali kuna kusudi ambalo bado hatujalitambua. Kauli hii ni yenye mtazamo chanya hasa pale tunapokosa majibu ya baadhi ya maswali tuliyonayo katika maisha.

Siku zote kusudi la jambo hufungwa katika muda na maarifa. Kuna usemi ambao wengi wetu huwa tunao hasa pale tunapokosa majibu huwa tunasema limetokea la kutokea tukiweka mtazamo kwamba jambo ilo ni kama muujiza au limetokea kutoka hali ya kutokuwepo. Lakini inatupasa tubadili mitazamo.

Katika kila jambo tusilopata majibu tutambue kuwa kuna kusudi ambalo halijadhiirishwa bado kwa wakati huo hivo inatupasa kutambua yatupasa kuwekeza katika kujikuza kimaarifa huku tukiendelea kutambua kuwa muda muafaka tutakuwa watu wenye ufahamu zaidi juu ya yale yanayotokea.

Hakuna jambo linalotokea kwa ajali...lazima kuwe na kusudi...iwe ni kukukumbusha jambo, kukufundisha jambo au kukuimarisha katika jambo. Lakini ni lazima tujenge tabia ya uvumilivu hadi pale tunapopata maarifa mapana ya jambo hilo.

Muda mwingi tumekuwa ni watu wa kuchukua maamuzi bila maarifa yeyote tunapokuwa katika hali ya kukosa ufahamu juu ya kusudi fulani. Inabidi turuhusu muda na kukua katika maarifa.Kuna ambao wanajifunga katika makubaliano baada ya dakika kumi na tano za hisia kali bila kuruhusu muda kupoza hisia hizo na kupata maarifa juu ya kusudi hilo kabla hawajachukua maamuzi.

Chukua muda wako vizuri huku ukikua ktk maarifa kutambua kusudi la jambo maana hakuna jambo linalotokea kama ajali.

Friday, August 19, 2016

NJIA ZA KUDHIHIRISHA MAONO YAKO

"Whatever you vividly imagine, ardently desire, sincerely believe, and enthusiastically act upon must inevitably come to pass!" - Paul J. Meyer

Tafakari ya ufasaha ni ngazi ya kwanza kabisa ya kufikia unachokitaka. Mara nyingi huwa tunatafakari bila ufasaha. Tunabeba maono makubwa lakini hatukai chini kutafakari maono hayo kwa ufasaha. Ni muhimu kukaa chini kutafakari kwa ufasaha maono uliyonayo.

Hitaji kutoka ndani ya nafsi ni ngazi ya pili kwa mujibu wa paul meyer ya kufikia malengo. Lazima maono yako uyatengenezee sababu na msingi wa ndani wa kihisia. Tengeneza msukumo wa ndani wa uhitaji katika kufikia malengo yako...Lazima utengeneze sababu ya kwanini unatakiwa ufikie malengo hayo.

Amini kutoka moyoni ni ngazi ya tatu kwa mujibu wa Paul meyer, ni lazima uwe na imani thabiti juu ya maono yako na imani hiyo isitetereshwe na aina yeyote ya mazingira. Ukiwa na maono lakini ukashindwa kuyaamini maono yako jua hautoweza kuyafikia.

Kisha unatakiwa uchukue hatua kwa msisimko na mhemko chanya. Lazima uchukue hatua kwa msisimko na mhemko chanya la sivyo hutoweza kuyafanya hayo maono yako dhahiri. Hatua iliyo na msisimko itakuwezesha kushinda vipingamizi au misukumo na changamoto hasi.
Kwa mujibu wa Paul meyer chochote kitafanikiwa ukifata hizo njia.

Tuesday, August 16, 2016

JE UNA UHUSIANO NA UNACHOKIFANYA

Changamoto kubwa watu wengi wanayokutana nayo katika mambo wayafanyayo ni kukosa uhusiano wa kihisia baina yake na akifanyacho. Lazima kuwe na msingi na uhusiano wa kihisia na kinafsi baina yako wewe na unachokifanya.

Ukikosa huo uhusiano lazima ukose hisia ya kuridhia na kuridhika kwa kile ukifanyacho. Bado katika nafsi yako kunakuwa na utupu ambao husababisha hisia za upweke katika kila ukifanyacho. Kuna watu wengi wanafanya kazi au shughuli lakini wana upweke kwa yale wayafanyayo.

Nafsi yako inakosa uwiano na kile ukifanyacho. Uwezo wako unakosa msukumo kuelekea kile ukifanyacho. Ni changamoto kubwa pale unapotaka likizo ili upumzike kihisia ktk kile ukifanyacho maana kazi ya nafsi yako huwa haina likizo ya kihisia.

Ukiona msukumo wako unapungua na hauna ile shauku ya kuongeza msukumo kiutendaji katika jambo fulani ni dhahiri wewe na hilo jambo hamna uhusiano wa kimsingi wa kinafsi na kihisia. Lazima kuwe na uhusiano, tafuta jambo ambalo lina mahusiano na nafsi yako.

Friday, August 12, 2016

PROBLEMS AS OPPORTUNITIES

The factor that triggers your creativity and activates your positive mind is pressing problems. It is only when you are experiencing the pressure of problems and obstacles that you are motivated to perform at your mental best. Facing and solving the inevitable problems and difficulties of life make you stronger and smarter, and bring out the very best in you.

Most people do not understand the nature of problems. Problems are a normal and necessary part of life. They are inevitable and unavoidable. Problems come in spite of your best efforts to avoid them. Problems, therefore, come unbidden.

The only part of a problem over which you have any control is your response to your problems. Effective people respond positively and constructively to problems. In this way, they demonstrate that they have developed high levels of “response-ability”. They have developed the ability to respond effectively when unexpected or undesired difficulties occur.

Problems of all kinds bring out your very best qualities. They make you strong and resourceful. The more pressing your problems, and the more emotion you invest in solving those problems,the more creative you will become. Each time you solve a problem constructively, you become smarter and more effective. As a result,you prepare yourself for even bigger and more important problems to solve.

Wednesday, August 10, 2016

NANI MUANDAAJI WA SCRIPT YA MAISHA YAKO?

Ni utaratibu kwa waigizaji wa filamu kuandikiwa muongozo wa jinsi ya kucheza tamthilia au filamu kwa kuvaa uhusika wa watu walio katika nadharia. Wao huvaa uhusika na kucheza kwa muongozo wa mtayarishaji mkuu.

Katika maisha yako ni nani mtayarishaji mkuu wa script unazocheza? Kuna kipindi lazima uvae uhusika wa mtu fulani aliye katika nadharia nawe umuweke katika matendo lakini ni muhimu sana kutambua ni nani mtayarishaji mkuu wa script zako.

Mtayarishaji mkuu anaweza akawa Mzazi wako, ndugu zako na hata majirani zako inategemea na nani umempa funguo ya kukushurutisha, unapompa utayarishaji mkuu mtu mwingine unaishi katika maono au nadharia ya mtu mwingine. Naye ndo anakuwa mtengeneza utaratibu wa maisha yako. Ni sawa na mtumwa, yeye huishi akifata utaratibu wa Bwana wake.

Unapoacha kuwapa watu wengine utayarishaji mkuu wa script za maisha yako ndipo unapoanza kuishi maisha yako, ndipo unapoanza kuishi ndoto zako na maono yako, tofauti na hapo unakuwa mtumwa wa maono na nadharia za watu wengine.

Changamoto kubwa ni kutengeneza script ya maisha yako na usimame imara kama msimamizi mkuu kwa vitendo na usikilize mawazo yale yanayoendana na hiyo script yako na sio siri ni lazima utapata upinzani kutoka kwa wale ambao wanataka kuwa watayarishaji wa script ya maisha yako na mara nyingi ni watu wale ambao hata wao walitayarishiwa script za maisha yao wanataka kuendeleza utamaduni huo.

Andaa miongozo, andaa script na uhakikishe unajenga mianya ya watu watakaokuwezesha kucheza vizuri script yako, wawe ni marafiki, wakufunzi nk.
Kumbuka unaanza kuishi maisha yako pale unapokuwa mtayarishaji wa script ya maisha yako .