Showing posts with label Feelings. Show all posts
Showing posts with label Feelings. Show all posts

Monday, September 11, 2017

NAFASI YA MAZUNGUMZO YAKO KATIKA UTASHI WAKO WA KIHISIA

Je wajua kuwa mazungumzo yako ni kipimo cha utashi wako wa kihisia? Je wajua ya kwamba mazungumzo yako yana mchango katika uimara wa utashi wako wa kihisia. Jiulize tu swali moja, unazungumza nini?

Mfumo wako wa mazungumzo au uwasilishaji mawazo yako ni kipimo cha utashi wako wa kihisia. Jinsi unavozungumza juu ya maswala yenye miguso ya kihisia ndivo jinsi utashi wako wa kihisia ulivo. Watu wengi hudhani kuwa uhuru wa kuzungumza katika kutoa mitazamo ya kihisia ni sawa na uhuru wa kuzungumza katika maswala ya kiakili na kifikra, hapana. Uhuru wa kihisia unahitaji mguso wa kinafsi na ufahamu wa aina ya utu wa nafsi husika.

Watu wengi wamejikuta wanazungumza katika lugha hasi yenye harufu ya ukosefu wa imani na ladha ya uchungu wa maumivu kwakuwa ndivo utashi wao wa kihisia ulivo. Wengi wanazungumza nyuma ya pazia la woga na hofu wakionekana ni watu wenye uimara mkubwa kifikra kumbe kihisia ni nafsi ambazo zina hofu hata ya kupatwa na mawimbi ya kihisia. Ukiweza tambua miundo ya lugha na mitazamo utatambua kuwa kuna changamoto kubwa katika utashi wa kihisia.

Tambua ya kwamba kimjazacho mtu ndicho kimtokacho. Inatakiwa tutambue ni nini haswa hutujaza nafsi zetu. Kuna mazungumzo tunayopenda kuyapa nafasi pengine kwa utamu wake  wa kimaudhui wenye kuburudisha nafsi zenye shauku ya kutaka ufahamu pengine hata kama maudhui haina tija wala faida lakini mazungumzo hayo ndiyo yanajaza nafsi zetu magugu yanayoenda kusababisha udhaifu wa kihisia. Shauku isiyo na nidhamu ni adhabu kwa hisia na nafsi. Lazima ujifunze kuratibu mazumgumzo.

Kuna mazungumzo pia tunayofanya ambayo hutudhoofisha nafsi zetu na kutupa misukosuko ya kihisia isiyo na tija. Hivo ni muhimu kutambua na kufahamu aina ya mazungumzo na mguso wake kwa hisia zako

Hatuwezi kuwa watu wenye nafsi imara na utashi wa kihisia bila kuwa watu wenye kuratibu aina ya mazungumzo tunayofanya. Ni jambo gumu sana kuwa mtu mwenye mazungumzo yasiyo na tija kuwa na utashi wa kihisia pengine ni rahisi hata ngamia kupenya katika tundu la sindano. Lazima uwe makini na mazungumzo yako.

Ratibu vyema mazungumzo yako ili safari yako ya utashi wa kihisia iweze kuimarika.

Thursday, May 25, 2017

KUTOKA KATIKA UCHOVU WA KINAFSI

Uchovu wa kinafsi ni hali ya nafsi ya mtu kukosa nguvu ya kusimama ili kuweza kuhimili mitikisiko hasi. Ni hali ambayo kama ikiingia humjenga mtu kutaka ukombozi wa kinafsi na pumziko.

Kila uchovu unahitaji pumziko lakini njia za kupata pumziko ina utofauti. Kuna pumziko la kudumu na lile lisilo la kudumu. Watu wengi wamekuwa wakishindwa kutofautisha mapumziko hayo kutokana na kukosa taswira hada hasa pale uchovu unapokuwa mkubwa.

Changamoto kubwa ni uchaguzi wa pumziko la nafsi yako maana waweza fanya uchaguzi wa kudumu au wa muda mfupi ambao utakupa uchovu mkuu baada ya ganzi ya pumziko hilo kuisha.

Ili uweze kuchagua pumziko la kudumu ni lazima ujue chanzo kikuu cha uchovu wako wa kinafsi maana vichocheo vya uchovu huo mara nyingi ni kama mchwa ambao hukula taratibu nguvu yako ya kinafsi na kukuacha mchovu.

Unaweza pata uchovu wa kinafsi pale unapojaribu jambo linashindikana au pale unapotaka kubadili jambo inashindikana, unapotaka kubadili hali fulani lakini inashindikana au inaweza ikawa jambo fulani linakushambulia kila wakati ambalo unajaribu kuliepuka, au yawezakana ni watu ndo wanakupa uchovu wa kinafsi pale wanapoila amani yako, wanaposhambulia nguvu yako ya kusimama, na kutenda yale yanayovuruga misingi yako. Unaweza pata uchovu wa kinafsi na pengine ukajaribu kupata pumziko lakini ukashindwa katika uchaguzi wako ni lipi pumziko hasa unalohitaji.

Ukishindwa kujua hasa ni pumziko gani unalohitaji waweza jikuta unapata pumziko la muda mfupi ambalo likawa kama kilevi cha nafsi kisichokupa suluhisho la kinafsi la kudumu bali kinakupa nafuu ya muda mfupi tu.

Ukitaka kuondoa uchovu wa kinafsi siku zote jaribu kujitia nguvu kwa kuelekea zaidi pale ambapo panakutia nguvu, panakupa amani, panakupa mguso chanya, pana uwiano na kile unachokiamini, na pana misingi ya kiutu yenye uhusiano na nafsi yako.

Uchovu wa kinafsi humkuta kila mtu kwa wakati fulani lakini tofauti inakuja katika uchaguzi wa mapumziko. Waweza jikuta unajiingiza katika pumziko la muda mfupi ambalo badala ya kuitia nguvu nafsi yako linazidi kukudhoofisha.

Chagua vyema pumziko la nafsi yako ili uweze kuushinda uchovu wa kinafsi.

Monday, May 15, 2017

CHUNGA MOYO WAKO

Chunga moyo wako maana hiyo ndiyo bustani ya amani na furaha yako. Nafsi yako hustawi katika bustani ya moyo wako. Katika bustani ya moyo wako kunaweza kuwa na maua ya furaha, amani na faraja au magugu ya maumivu na uchungu. Kuwa muangalifu sana kwa kuchunga moyo wako kila wakati ni nini kinachoota.

Kuna mawazo na maneno ambayo ukiyaruhusu yaingie moyoni yanaenda kuweka majeraha ambayo kupona kwake kutakuchukua muda sana. Majeraha hayo yatajenga mfumo wa kifikra wa kujihami ili kuzuia maumivu mengine. Hasara ya fikra za kujihami ni kwamba utashindwa kufurahia uhuru na uzuri wa maisha kwa kuwa utaishi kwa kujihami.

Moyo wako unatakiwa ulindwe kama ngome imara. Ukiruhusu maumivu au matatizo yakaingia katika bustani ya moyo wako yataenda kuotesha magugu ya mawazo na fikra hasi. Kuna maneno ukiyaruhusu kuingia siku moja yatautesa moyo wako wakati wote. 

Safisha moyo wako kwa kuondoa yale ambayo yanauumiza na kutesa moyo wako. Yale ambayo kila ukiyafikiria unasikia kama kichomi ndani ya moyo wako, yale ambayo kila ukiyapa nafasi katika akili yanakububujisha machozi ya uchungu moyoni mwako.

Tambua kuwa moyo wako unatakiwa kustawisha amani, furaha na upendo. Ukiwa na moyo wenye uchungu inageuka kuwa sumu inayodhoofisha nafsi yako na akili yako. Utakuwa mtu mwenye vifungo badala ya uhuru.

Chunga moyo wako na uache katika amani. Usiuache umekaa katika dimbwi la maumivu au usiuache ushikilie uchungu unaokuumiza, usiuache ushikilie maneno makali au misumari ya mitazamo hasi juu yako. Usiruhusu moyo wako udunde kwa kasi kwa kukosa amani au kuwa na taharuki, Jipe utulivu kwa kuruhusu uzuri na furaha istawishe moyo wako.

Ruhusu yale yenye furaha na amani na yenye uzuri na utulivu ndio yakae katika moyo wako. Stawisha moyo wako ili ukutunze na uachilie yale yenye furaha, amani na pumziko. Kama vile damu inavoingia na kutoka katika mkondo wa mishipa ya damu, wewe pia tengeneza mkondo wa kuingiza furaha nyingi, amani nyingi na faraja nyingi moyoni mwako kwa kukaa na watu au mazingira yatakayosaidia hivo vitu lakini ondoa moyoni mkondo wa maumivu, uchungu na yale yanayoutatiza moyo

Lazima kuwe na uwiano baina ya yanayotoka na yanayoingia, usipende kuingiza mawazo hasi, Itafute hiyo furaha na amani ili ustawishe bustani ya moyo wako.

Fikra chanya au mazingira chanya sio tu yale yanayokusukuma kufanikiwa bali pia kuustawisha moyo wako na kuuacha katika hali ya utulivu.

Saturday, May 6, 2017

ALWAYS KEEP A JOYFUL DEMEANOR

Our strength lies in our ability to always keep a joyful demeanor in the face of our problems-Nickvaleries

Life has its ups and downs, Life has negative situations that can hit us or hurt us and we find it hard to be joyful but joy has to be founded from our souls.

When we believe in our worth and have the mentality that there is always something better ahead and that we will always receive the desires of our souls then we generate a joyful spirit and demeanor.

There is no reason to stay in sorrow and pain when you know that the best is out there heading your way and you ought to be ready and step towards it. Pain and sorrow will try to drown you in a state of emotional stagnation but rise up, smile and say to yourself that am heading to my best. Darkness is for a night but joy comes in the morning.

Always choose to be joyful and find joy at whatever costs by changing your belief from a victim to a victor of circumstances. If things change dont stay there drowning yourself. Get up and heal your soul of the pain and choose to keep a joyful demeanor.

Just say to yourself it is well with my soul then believe that you are heading for the best out there. Tell your heart you are not hurt but you are strengthened then find your rythm and be happy. Smile for your beauty and peace awaits.

The Universe will always smile back if you smile at it. Its just a matter of time till you find love, happiness and joy again. But for now keep a joyful demeanor and attitude.

Tuesday, May 2, 2017

USICHUKULIE KILA JAMBO KIHISIA

Ukitaka kuwa na furaha usipende kuchukulia kila jambo kinafsi au kihisia. Kuna mambo mengine ni ya kifikra tu na yamekaa kimtazamo tu ambayo hayatakiwi kuchukuliwa kihisia.

Ukitaka kuwa na utashi wa kihisia na uweze kuratibu hisia zako katika mlengwa chanya yakupasa kuziacha hisia zako katika mfumo tulivo kadri uwezavyo. Kuna mambo ukiyachukulia kihisia utaziweka hisia zako kwenye mfumo wa taharuki kwa wakati mwingi na itakupunguzia msisimko wa maisha ulio katika muundo chanya.

Je wawezaje kutochukulia mambo kihisia? Tambua kuwa kila wazo au mtazamo unapaswa kupokelewa kiakili na kuratibiwa kabla ya kusukumwa na hisia fulani. Ni vizuri ukiratibu mawazo na mitazamo unayopokea na kuiratibu kabla ya kujua ni hisia gani uiachilie ili isukume hilo jambo.

Ni muhimu sana kulishikilia wazo au mtazamo katika mfumo chanya hata kama limekuja katika muundo hasi. Lione hilo wazo kama njia ya kukuboresha, yaone hayo maoni kama njia ya kukuboresha kisha yape hisia chanya ndipo uyapokee. Usikubali kuanza kupokea kihisia wazo ambalo hujariratibu kwa akili.

Mfano mtu anaweza kukwambia jambo ambalo unaona kabisa linaweza lisiwe chanya kwako, badala ya kulipokea kwa hisia hasi jaribu kuliona ilo jambo kama wazo la kukuboresha na sio kukuharibu, kisha chukua hisia ya amani na furaha kwa kutambua kuwa hilo wazo limekuja kukuboresha..kisha chukua hisia ya morali na ari ya kulitafutia ufumbuzi na kulishughulikia hilo jambo na sio vinginevyo. Ukilipokea kama vile limekuja kukuumiza utaingiwa na taharuki ya kinafsi pengine hata kujenga ukuta kulizuia hilo suala na kuonekana kuwa ni mtu dhaifu kinafsi pengine hata mtu hasiyependa kuambiwa ukweli.

Nakushauri tena usilipokee kila jambo kihisia kabla ya kuriratibu kiutashi na kiakili ili kukujenga utashi wa kihisia itakayokupa furaha wakati wote.

Tuesday, March 28, 2017

JENGA UTASHI WA KIHISIA

Uimara wa mtu katika nafsi umejikita zaidi katika utashi wake wa kihisia. Binadamu ni kiumbe chenye nafsi na nafsi ya mtu imeundwa katika mfumo wa hisia. Hisia za mtu pia zimeundwa katika mfumo wa utu wake. Kila mtu ana muundo wake wa kiutu ambao ndio msingi hasa wa uratibu wa hisia za mtu huyo.

Hisia ni misukumo na mihemko ya kinafsi ambayo hujitokeza kutoka kipindi hadi kipindi kutokana na mabadiliko ya ndani au nje. Yaweza ikawa mabadiliko ya kimazingira au mabadiliko ya tabia za mwili. Changamoto kubwa ya hisia ni kwamba ni kama upepo, huja na kufika katika kilele lakini baadaye hushuka katika ukawaida na pengine hushuka zaidi ya hapo.

Hapo ndipo wengi hujikuta wanasema leo najihisi niko chini sana kihisia au nimezama katika hisia na hata wengi hutumia kauli za vitabu vya dini na kusema leo nimezama katika bonde la uvuli wa mauti. Lakini hao hao watu nyakati nyingine utasikia anasema leo nina msisimko au leo niko hewani. Yote hayo ni mabadiliko ya kihisia.

Hisia zinaweza kuwa nzuri kama zikitumika vizuri lakini changamoto kubwa ni pale mfumo wa uratibu wa kimaamuzi katika akili unapofungwa katika hisia ambazo zinapanda na kushuka. Kuna ambao wamekuwa na utashi wakufikiria lakini wamekosa utashi wa kihisia.

Utashi wa kihisia ni uwezo wa kuratibu hisia zako na kuzielekeza vile unavotaka. Watu wengi tumekuwa na utashi wa ki akili lakini tumekosa jambo la muhimu sana ambalo ni utashi wa kihisia kupelekea yale tunayoyajenga kwa akili zetu yanaharibiwa na hisia zetu.

Waweza fikiria jambo zuri na ukaliwekea mikakati madhubuti lakini kinapofika kipindi cha mtikisiko unaogusa hisia ,wengi wetu tumejikuta tukiruhusu hisia zetu ziharibu hata ule mtazamo chanya wa yale tuliyoyajenga kwa akili zetu.

Watu wengi waliofanikiwa au wakuu wamejikuta wakianguka na kufanya maamuzi mabovu kwasababu ya kukosa utashi wa kihisia na wamejikuta wakizama katika dimbwi ambalo pengine kusababisha zile imaya walizozijenga kwa akili nyingi kuanguka kutokana na kukosa utashi wa kihisia.

Wekeza sana kuwa utashi wa kihisia uweze kutambua ni hisia zipi zinakujenga na zipi zinakubomoa. Hisia zipi zinakuimarisha na hisia zipi zinakudhoofisha, hisia zipi zinakuinua na hisia zipi zinakuangusha. Ukiwa na utashi wa namna hiyo utaweza kuzitumia hisia hizo ziweze kukutumikia na sio wewe kutumikia hisia zako.

Je wawezaje kuwa na Utashi wa kihisia

1. Pambanua hisia zako pindi zinapokuja na utambua mlengwa wa kila hisia.

2. Tambua chanzo cha hisia husika au mifumo sababishi ya kutokea kwa hisia hizo.

3. Jifunze kuzimudu hisia kila zinapokuja kwa kuifanya nafsi yako izungumze na hisia hizo

4. Tambua kuwa hisia sio jambo baya na wala sio udhaifu bali ni muundo wa kinafsi hivo hisia zako zikubali kuwa ni zako na wewe ndio mwenye kuwajibika kwa hisia hizo. Usitafute kisingizio juu ya hisia zako.

5. Jiimarishe katika uvumilivu ili uweze kuziratibu hisia zako na kuratibu mkondo wa hisia zako maana hisia ni kama mkondo wa maji

6. Pendelea kutenga muda wako wa upekee ukizungumza na nafsi yako ili uweze kuthibitika katika uimara wa kihisia.

Hakuna jambo la msingi na lenye kufaa kama kuwa na utashi wa kihisia maana maisha yako yanaweza kuwa yenye furaha na amani au kuwa na shida na maumivu kama hauna utashi wa kihisia.

Saturday, March 25, 2017

MUDA WAKO WA UPEKEE NA NAFSI YAKO

Ukitaka kuwa na furaha anza kwa kufurahia muda wako wa upekee.

Moja ya changamoto tulizonazo kama binadamu ni upweke. Upweke sio ukosefu wa wenza au watu wa kutuzunguka. Upweke ni pale mtu anaposhindwa kuufurahia upekee wake na anaposhindwa kuwa na uhusiano na uhalisia wa nafsi yake.

Kuna malalamiko mengi unasikia hata katika mahusiano mmoja wao anasema nilijihisi mpweke ndo maana nilikusaliti, au mwingine anaingia katika ulevi au hata mikanda ya ngono kwa sababu ya upweke. Tafsiri yetu ya upweke ni kukosa watu wa kutengeneza muungano wa kinafsi au watu wa kuburudisha nafsi zetu.

Nafsi ya binadamu kila wakati inahitaji kurutubishwa kwa kutengewa muda wa kupata uwepo. Nafsi yako ni utu wako wa ndani. Mtu wako wa ndani anahitaji wewe umtengee muda kumsikiliza, kumdadisi, kuzungumza naye, kumburudisha na hata kumponya na aina yeyote ya maumivu.

Lazima ujitengee muda wako wako bora wa kutengeneza mguso wa kimaelewano na nafsi yako. Watu wengi wameshindwa kuwa watu wa namna hiyo kupelekea kupigwa na upweke kila wakati anapokosa mguso wa nje wa watu wanaomzunguka.

Rafiki yako wa kwanza na wa karibu ni nafsi yako. Itengee muda nafsi yako ili ipate ukaribu wako. Na wakati wa kuzungumza na nafsi yako jua kwamba unaongea na mtu wako wa karibu. Acha kuongea na nafsi yako kwa ukali au kuihukumu kwa makosa ya nyuma. Itie moyo nafsi yako, ikumbushe uwezo wako. Panda mbegu chanya ndani ya nafsi yako, itie moyo, iponye kwa makosa ya nyuma na iahidi mambo mazuri huko mbele, iburudishe kwa lugha nzuri yenye mguso chanya lakini kuu kuliko yote iweke huru.

Watu wengi wamekuwa wakitumia wakati wao wa upekee kwa kulala, kuangalia mitandao ya kijamii au hata kutafuta magenge ya umbea kutafuta jambo la kufanya kuondoa upweke nk. Huo sio wakati wake. Huo ni wakati wa kujenga uhusiano na nafsi yako. Ni sawa na aina yeyote ya uhusiano. Lakini uhusiano wako na nafsi ndiyo jambo la msingi kwanza.

Ukiwa na tabia ya kuwa na muda mwingi na nafsi yako hautokuwa mtu wa kulalamika upweke. Na hautokuwa mtu wa kutafuta vileta msisimko vya nje kama pombe, anasa na ngono pale unapojihisi mpweke. Utaufurahia muda wako wa upekee, nafsi yako itarutubishwa na utakuwa ni mtu mwenye furaha muda mwingi.

Angalizo ni kwamba katika muda wako wa upekee na nafsi yako hakikisha unatengeneza mazingira chanya. Huwezi kutengeneza mazingira hasi ya mawazo na hisia hasi au muingiliano na mambo yasiyojenga halafu utegemee nafsi yako itajiachilia. Nafsi yako itajenga ukuta wa kujihami maana ndivo mwanadamu alivo kiakili katika maisha yanayoonekana kama mapambano.

Pia usipende kuipa nafsi yako maumivu yasiyokuwa na sababu na mara nyingi pale akili yako inaposhindwa kuendana na misingi ya nafsi yako. Na usipende kuipa nafsi yako vifungo kwa kufuata njia ambazo unajua nafsi yako haiwi huru kuchanua.

Sunday, March 12, 2017

HOW TO DEAL WITH FEAR

Do you know that fear is false evidence appearing real? Sometimes in life you will be faced with situations whereby there will be evidences that are false appearing real. Fear will torment you and leave you paralysed. The only cure to fear is faith. Believe beyond circumstances. 

Clear your mind of the Past : You will always be free as your mind is free. The battlefield is always in your mind. Its a point where strongholds of the past are. The strong holds of fear and other dissapointments. Experience should make you wiser in terms of strategies and how you perceive life. But always free your mind as much as possible.

Something is about to happen in your life: Things happen all the time, good or bad but its always dark before dawn. We pass through darkness to experience the light. We pass through trouble to appreciate calmness. No darkness comes after darkness until afternoon passes. Always believe that the next phase of your life will always be better than the previous. Try to find the rainbow after the storm because its there. Dont be afraid that later will be like the former. There will always be changes in every stage of your life.

Find beauty and peace: You will never be happy unless you are at a state of beauty and peace and tranquility. We often look at the beauty without but not the beauty within. We all want to be in tune with our inner self. Our core values and our inner being, but we often times try to find this in the wrong places. We should always be in the quest to find beauty and nirvana and where its connected.

Wednesday, February 22, 2017

BENEFITS OF KNOWLEDGE AND ADVENTURE FOR EMOTIONAL INTELLIGENCE

Our minds and souls are constantly in need of exploration and discovery. The reason why we act differently and evolve is because our souls seek new horizons. Our minds need to be refreshend and expanded so as we can stable in our actions and in our ways. As it is said Lunacy is doing the same thing the same way and expecting different results.

We act in a lunacy form whenever we fail to expand our minds and let our souls explore its limitlessness. Knowledge is essential for expanding our minds increasing our possibilities and widening the limits that have been set by ignorance. We must grow in knowledge so as to be free. Emotional intelligence being the ability to perceive, assess and manage our emotions is a crucial attribute to our stability as human beings.

If we invest in knowledge while we let our souls experience wonder we invest in the attribute of emotional intelligence. We not only grow in our ability to manage our emotions but we develop control as to how we can relate our knowledge in a practical way to see wonder and adventure.

How can Knowledge and adventure be used simultaneously for emotional intelligence

1. Always read books of a specific topic in the specific moment at the specific place. That's Practical investment of knowledge.

2. Knowledge has to be put into practise, acquiring knowledge without practising it is a wastage of time. Ensure to always acquire the kind of knowledge you can practise.

3. Explore new horizons, listen don't let your life become a routine of activities that don't allow your soul to explore and experience the adventures of your life time.

4. Visit nature occasionally and meditate on it. This will open your mind and trigger your soul to explore the adventures of naturality.

Always remember that without emotional intelligence we will always be unstable human beings. If emotions aren't managed and assessed skillfully then we will always be human beings of so many imbalances and we will live life not realising the beauty of it.


Sunday, November 20, 2016

LEARN TO IGNORE

The race of life is the one with a lot of obstacles, a lot of hindrances and a lot of oppositions, we all know that and we all have experienced that at some point in life, but there comes the most critical of all a lot of intimidations. If you havent master the art of ignoring voices then you will always fall victim.

When you are walking your walk always know that there are people who will come to intimidate you and try to misfocus you with words. Listen always be ready for that for people will hit you where it hurts you the most, sometimes even people you cant imagine but always guide your heart and mind. Many have grabbed a victim mindset simply because they take everything thrown unto them personal

Don't be intimidated...Learn to ignore, choose not to give full attention to distractions, Its obvious that some will be people very close to you in whom there opinions can have a big impact in you, but one of the greatest thing you need to do is detach yourself from the emotions brought about by people. Its true that you might sometimes fall prey in the predatorial world but stand up, ignore the predators and move on. What doesnt kill you makes you stronger.

Just because people are close doesn't mean that their opinions of you will always be right. Don't let the pressure get into you...Don't be intimidated, learn to ignore the impacts of their words. Learn to ignore, Ignore the negative feelings, ignore the negative emotions. Ignore what seems to bring you down. I challenge you to ignore those voices that keep running through your mind all the times telling you that you are somebody's victim. No you arent. Train your mind to cancel off and ignore.

Say to yourself, i choose to ignore all distractions. One African proverb says a lion doesn't turn back when dogs bark, also the noise of frogs doesn't hinder the elephant from drinking water from the stream. When you have an understanding of what people go through then it wont trouble you when they voice out their opinions out of emotions. Just ignore and move on. Choose to mind your own business and move on. No need to give an airtime to the calls that dont compliment you. Focus on the good. 

Monday, November 14, 2016

USITAFAKARI MAJUTO, TAFAKARI FUNDISHO

Katika maisha tunapitia mambo mengi, njia nyingi na tunakutana na vitu vingi, nafasi nyingi na hata vipindi vingi ambavyo tunatakiwa tufanye maamuzi juu ya mambo kadha wa kadha tunayokutana nayo. Kama binadamu wenye uhuru wa kufanya uchaguzi na utashi kila wakati huwa tunatumia njia zozote zile tulizonazo kufanya maamuzi.

Maamuzi yetu ndiyo ambayo hutengeneza hatima ya maisha yetu au matokeo yanayokuja baada ya hapo. Maamuzi mazuri huleta matokeo mazuri na maamuzi mabaya pia huleta matokeo mabaya. Kila mtu ameshapitia hali ya kufanya maamuzi na kila mtu ametumia uhuru wake wa kinafsi kufanya maamuzi. Changamoto kubwa ni matokeo ya maamuzi yetu na jinsi tunavopokea matokeo ya maamuzi yetu.

Maisha siku zote ni safari endelevu yenye changamoto mbali mbali na safari hiyo huwa vumilivu pale inapoendeka kwa maarifa na ujuzi wa wapi unaelekea. Maisha huhitaji dira na dira ndo itakuelekeza kasi ya kwenda nayo hata njia za kupita kufikia hatma yako. Maarifa ni muhimu sana.

Mara nyingi tumekuwa na mapokeo tofauti tofauti ya matokeo ya maamuzi yetu ambayo wengi wetu yametusababishia kukwama kwa muda mrefu katika dimbwi la maumivu na tukaishia kulalamika, kulaumu, kuwa na mitazamo hasi na hata kupata matatizo mbali mbali ya nafsi. Mara nyingi tumekuwa watu wa majuto badala ya mafunzo

Jambo la muhimu ni kutafakari mafunzo uliyoyapata na uyatumie hayo kama mawe ya kukanyagia kwenda mbele, usikae unajilaumu au unatafakari kwa makosa ya nyuma hata kama yameleta matokeo mabovu katika maisha, badala ya kusema ningejua tafakari aya sasa umejua utafanya nini. Huwezi kubadilisha makosa ya nyuma ila unaweza kufanya mabadiliko ili makosa ya nyuma yasijirudie.

Wengi tunakaa zaidi tunatafakari majuto badala ya kutafakari mafunzo na kufanya yanayohitajika kusonga mbele halafu baadaye unajikuta unarudia kosa lile lile au unapita tena njia ile ile. Badili mtazamo hata kama matokeo ya maamuzi yako mabaya yanaendelea kukutesa kuwa na ujasiri wa kusema nitafanya hivi badala ya ningefanya hivi.

Kumbuka kila mtu ameshafanya kosa fulani ambalo limemgharimu au linamgharimu hadi sasa lakini cha msingi ni kutafakari funzo badala ya majuto.

Thursday, November 10, 2016

KUDHIBITI HISIA HASI

Magugu siku zote huota hata sehemu ambazo hazitakiwi, hayaitaji mbegu..yenyewe huota bila kupandwa wala nini, vivo hivo na hisia hasi, huwa haziitaji kazi kubwa kukaa katika nafsi yako. Zinaweza kukuhijia wakati wowote na kwa namna yeyote lakini hisia chanya zinahitaji kupangiliwa, kurutubishwa na kupaliliwa.

Moyo wako kuna wakati unaweza patwa na hisia hasi ambazo zinakuja kutokana na jambo lolote, inawezekana ni uchovu wa kimwili au kiakili, mtu fulani kukukatisha tamaa, mtu fulani kuzungumza na wewe vibaya nk...yamkini ni mtu wako wa karibu, au mtu ambaye ana mguso wa tofauti ndani ya moyo wako. Lakini ni vyema ukatengeneza mzani wa kupima hisia hasi na kuzikata badala ya kuzipa hifadhi kwa muda mrefu ndani yako.

Ukizipa hifadhi kwa muda mrefu zina tabia ya kuchoma nafsi yako na kila zikichoma nafsi yako zinakujengea hali ya kutaka kuzitoa. Na hapo wengi wamejikuta wakizitoa kwa msukumo unaosababisha maafa zaidi. Njia pekee ya kuzidhibiti hisia hasi ni kupumzisha nafsi yako kwa muda huku ukijaribu kuingiza hisia chanya.

Hisia chanya zinahitaji nidhamu kuziimarisha ndani ya nafsi yako, kwasababu asilimia kubwa ya watu wamezungukwa na mazingira hasi mfano ndugu walalamishi, marafiki wasiojali, wapendwa wasiokuelewa na wasioheshima uhuru wako na furaha yako. Inabidi ujipe likizo ya kinafsi. Ikiwezekana jijengee utaratibu hata wa kufunga kuendekeza hisia hasi kwa kipindi fulani kama jinsi ambavyo dini hufunga chakula au starehe fulani waweza funga kutoziendekeza hisia hasi.

Jenga utaratibu katika maisha yako wa kutozipa hifadhi hisia hasi wala kuziendekeza kwa muda mrefu. Hisia ni mfano wa mimea, kuna mimea bora na kuna magugu. Hisia hasi ni kama magugu. Tafuta kuwa mtu mwenye hisia chanya kila wakati. Ni sawa na chumba chenye uchafu na kila aina ya takataka...usipoweza kuondoa visivohitajika, chumba kitajaa na hewa itakuwa haizunguki vizuri. Usipoweza kupunguza hifadhi ya hisia hasi ndani ya nafsi yako, nafsi yako itajaa na hewa nzuri ya mazingira chanya haitozunguka vizuri ndani yako.


Saturday, October 1, 2016

USIOGOPE KUKUTANA NA HOFU YAKO

Moja ya changamoto tunazopitia katika maisha ni hofu ya kukutana na hofu zetu na hofu ya mguso utakaotokana na hofu zetu. Huwezi kuwa huru kutoka katika hofu unayohofia kukutana nayo. Siku zote kuwa tayari kukutana na hofu zako na jivike ujasiri wa kuweza kuzidhibiti hofu zako.

Katika maisha lazima uwe na ujasiri wa kusonga mbele na kujua kuwa iko siku utakutana na hofu zako. Lazima ujipange jinsi ya kukabiliana na hofu yako na uwe jasiri maana hofu yako siku zote ndio gereza lako. Kuna wakati katika maisha inakubidi kuvuka daraja lenye kutia hofu kwa ujasiri ukitazamia maono uliyonayo katika maisha.

Amani ya nafsi ikishakaa ndani yako itakupa ujasiri wa kukabiriana na hofu yako ndio maana mwanafilosofia mmoja aliwahi kusema kuwa kama hakuna adui ndani ...adui wa nje haweza kutuathiri. Na hapa anapozungumzia adui sio lazima awe adui anayekupinga bali kuna maadui wa furaha yako na maono makubwa ambao wanaweza kuja kama watu wa karibu wakikushauri au mazingira fulani yakikukwamisha.

Lazima ujivike ujasiri na useme kwa jambo lolote nitasonga mbele na niko tayari kukutana na hofu yangu. Bila kuwa na huo ujasiri hofu yako itaendelea kukuzuia kusonga mbele. Na njia pekee ya kuweza kuishinda hofu yako ni kuwa mkweli kwa nafsi yako, kuwa mkweli kwa kile nafsi yako inataka na pia kuikubali amani iliyo ndani yako maana amani ya nafsi siku zote ni ya msingi sana. Ukisha kuwa mkweli uweke wazi ukweli ulio ndani yako, usiuogope, wala usiogope jinsi watu watakavoupokea huo ukweli.

Njia ya maisha siku zote ni ya kufanya maamuzi na kusonga mbele. Muda wa kukaa kutafakari kwa sababu ya hofu iliyo mbele yako ni kujikwamisha mwenyewe. Songa mbele kama una imani na kweli iliyo ndani yako. Amini tu kwamba kila jambo linafanyika kuwa jema. Maamuzi siku zote hutujenga, pasipo maamuzi tutaendelea kukaa katika hali ya mazoea ambayo pengine yangekuja kutuumiza.
Kuwa jasiri na Hofu zako zitakimbia. Usipokuwa jasiri hofu zako zitaendelea kukufunga sehemu ulipo.

Thursday, September 22, 2016

UHURU NA UDHIBITI WA KIHISIA

Uhuru wa kihisia ni pale unapoweza kudhibiti na kuelekeza hisia zako katika muundo na mpangilio uutakao. Hili si jambo rahisi kwa maana hisia huja kutokana na mabadiliko ya ndani ya mwili na hata hujengeka katika msingi wa nafsi ya mtu hivo uhuru wa kihisia unawezekana pale tu unapojenga tabia inayoitwa Nidhamu.

Nidhamu itakuwezesha kudhibiti hisia zako kwa namna kwamba utaweza kuzielekeza au kuamua muitikio na hata namna ya kukabili hali fulani zinazojitokeza. Uhuru wa kihisia kwanza unajengwa na kuitambua nafsi yako....nguvu na mapungufu yake kisha kujenga msingi wa kimaamuzi unaotokana na sheria utakazozijenga katika akili yako.

Hisia ni kama upepo, huja na hupoa na pengine hata kupotea kabisa, upepo huo unaweza kuwa kimbunga kwako au unaweza kuwa kama kipupwe kutokana na misingi ya kinidhamu ulioijenga katika nafsi yako ambayo inakupa uhuru wa kuamua jinsi hisia zako zinavodhibitiwa. Kudhibiti hisia ni sawa na kujenga mifereji ili kudhibiti mikondo ya maji isilete madhara au isielekee kusikotakiwa.

Ukiwa mfungwa wa hisia inamaana utendaji wako au muitikio wako katika mambo utatokana na msukumo wa hisia ulizonazo. Umeshawahi kuwa hisia nzito juu ya mtu fulani au jambo fulani kwa wakati fulani na ukatamani kulifuatilia lakini baada ya muda unapoteza hiyo hisia? Na hii hasa ndio changamoto ya kufanya maamuzi kwa kufuata hisia.

Jenga utaratibu wa kinidhamu wa kuratibu hisia zako kisha zielekeze kuongeza msukumo ktk sheria ulizozijenga na wala usiruhusu hisia zako zikuelekeze kupingana na sheria zako...namaanisha usiruhusu hisia pinzani zipate nguvu. Hisia zote zielekeze unapotaka ziende. Na hii inahitaji mazoezi.

Warren buffet aliwahi kusema kuwa mtu asiyeweza kudhibiti hisia zake hawezi kudhibiti pesa zake. Na hilo ni jambo la kweli kabisa, usipoweza kuwa nidhamu ya kihisia huwezi kuwe na nidhamu ya kiuchumi

Pia usipokuwa na uhuru wa kihisia utakuwa mhanga wa maumivu mengi ikiwemo mahusiano au hata namna watu wanavoleta upinzani katika maisha yako. Watu wasio na uhuru wa kihisia mara nyingi hushindwa kuchanganua ni aina gani ya mahusiano ni mazuri kwao na yatakayowajenga, kwao hisia zikishatawala wanashindwa hata kuruhusu akili zao kuchanganua.

Maisha bila uhuru wa kihisia ni kama msitu maana kila aina ya mabadiliko yatakuwa na mguso kwako na utataka kuitikia kila ambavyo hisia zitakutuma. Lazima uwe huru kuzidhibiti hisia la sivyo zitakuzamisha.

Thursday, September 15, 2016

ACHA YA JANA...ISHI YA LEO

Usiruhusu yale ya jana yachukue muda mwingi wa leo- Willy rogers

Moja ya changamoto kubwa katika maisha yako ya leo ni kumbukumbu ya jana yako. Jana yako unaweza kuitumia katika tathmini yako kukuwezesha kuwa na mtazamo chanya na wa fadhila hasa ukikumbuka ulipotoka na kushukuru kwa hapo ulipo huku ukitazama unapoelekea.

Changamoto kubwa ni pale jana yako inapochukua muda mwingi kihisia na hata kimtazamo kiasi cha kukufanya kushindwa kuiishi leo yako. Jana yako inaweza kuwa mtego wako hasa pale unapokuwa na hisia zilizoshikamana na jana hiyo. 

Kuna watu wengi wameshindwa kuachilia jana yao kiasi cha kutotazama fursa katika leo yao na kuacha fursa hizo zikipotea.

Wengi wameingia katika mahusiano leo na kumbukumbu la jana yao...Wengi wao wanataka kuishi leo lakini bado hawajaachana na jana yao. Ukiona unatamani sana jana ni dhahiri umepoteza dira ya leo na kesho yako. Kuna mambo mengi ya jana bado hutaki kuyaachilia na yamekuwa mzigo kwa leo yako.

Huwezi furahia leo yako kama jana yako inachukua sehemu kubwa ya moyo wako, akili yako na nafsi yako. Wengi leo wanaingia katika mahusiano huku bado hawajaacha kutazamia mahusiano ya jana yao. Wanajaribu hata kulinganisha leo na jana yao. Kuna wengine ambao pia hawajaacha machungu ya jana yafe, bado wanayapa nafasi katika akili yao kufikia hatua ya kuteswa na hofu ya kuishi leo katika ukamilifu.

Sikiza leo haiwezi kuja kama jana haijafa, Kesho haiwezi tokea kama leo haijaisha. Acha kuchelewesha furaha ya leo, fursa ya leo, nuru ya leo kwa kuendelea kukaa katika giza la jana..Weka pembeni na uiishi leo yako kwa furaha. Acha ya jana yawe ya jana...Ganga ya leo.

Sunday, August 28, 2016

HAKUNA AJALI, KILA JAMBO LINA KUSUDI

"Huwa hakuna ajali.. Bali kuna kusudi ambalo bado hatujalitambua "-Deepak Chopra

Katika moja ya mafundisho yake mhamasishaji na mkufunzi wa maswala ya kujitambua Deepak chopra alisema huwa hakuna ajali bali kuna kusudi ambalo bado hatujalitambua. Kauli hii ni yenye mtazamo chanya hasa pale tunapokosa majibu ya baadhi ya maswali tuliyonayo katika maisha.

Siku zote kusudi la jambo hufungwa katika muda na maarifa. Kuna usemi ambao wengi wetu huwa tunao hasa pale tunapokosa majibu huwa tunasema limetokea la kutokea tukiweka mtazamo kwamba jambo ilo ni kama muujiza au limetokea kutoka hali ya kutokuwepo. Lakini inatupasa tubadili mitazamo.

Katika kila jambo tusilopata majibu tutambue kuwa kuna kusudi ambalo halijadhiirishwa bado kwa wakati huo hivo inatupasa kutambua yatupasa kuwekeza katika kujikuza kimaarifa huku tukiendelea kutambua kuwa muda muafaka tutakuwa watu wenye ufahamu zaidi juu ya yale yanayotokea.

Hakuna jambo linalotokea kwa ajali...lazima kuwe na kusudi...iwe ni kukukumbusha jambo, kukufundisha jambo au kukuimarisha katika jambo. Lakini ni lazima tujenge tabia ya uvumilivu hadi pale tunapopata maarifa mapana ya jambo hilo.

Muda mwingi tumekuwa ni watu wa kuchukua maamuzi bila maarifa yeyote tunapokuwa katika hali ya kukosa ufahamu juu ya kusudi fulani. Inabidi turuhusu muda na kukua katika maarifa.Kuna ambao wanajifunga katika makubaliano baada ya dakika kumi na tano za hisia kali bila kuruhusu muda kupoza hisia hizo na kupata maarifa juu ya kusudi hilo kabla hawajachukua maamuzi.

Chukua muda wako vizuri huku ukikua ktk maarifa kutambua kusudi la jambo maana hakuna jambo linalotokea kama ajali.

Friday, August 26, 2016

KWANINI HATUTENDEI KAZI TUNAYOYAJUA

Changamoto kubwa tuliyonayo ni kujua sana, kusoma sana lakini hatutendi yale tunayoyajua. Ni sawa na kuingiza vitu vingi ndani yako lakini utoaji wake au utendaji wake ni mdogo. Wengi hawasongi mbele kwasababu wanajua sana lakini wanatenda kidogo.

Huwa najiuliza maswali mengi hasa pale napokijua kitu lakini nashindwa kukitendea kazi. Huwa najiuliza nini tatizo? Hasa hasa pale unapokuja kuona mtu mwingine akikitendea kazi kile ulichokijua wewe na akapiga hatua.

Hata maandiko husema muwe watendaji wa neno na sio wasikilizaji tu. Na yule ajuaye jambo na kutolitenda huhesabika kwake kama uovu.. Kwanini? Kwasababu ufahamu unapaswa kukuweka huru na sio kukufanya mfungwa. Unapojua kitu ni nafasi kwako kukifanyia kazi ili kikusaidie. Kukijua tu na kuishia pale haisaidii.

Ni kwanini watu hatutendei kazi yale tunayoyajua? Baada ya kutafakari na kuchunguza kwa makini nimekuja kugundua sababu kuu inayopelekea watu tusitendee kazi tunachokijua imefungwa katika mitazamo yetu na tabia zetu za ndani.

1. MTAZAMO BINAFSI: Hii ndiyo changamoto ya kwanza inayosababisha watu wasitendee kazi wanayoyajua. Watu wengi wana mitazamo binafsi iliyo asi ambayo hupambanua na kuua nguvu ya utendaji, ukiwa na mtazamo asi siku zote utakichambua unachokijua na kuua msukumo wako kukitendea kazi. Ni muhimu sana kujenga mtazamo binafsi ulio chanya.

2. KUKOSA UJASIRI : Watu wengi hawatendei kazi wanayoyajua kutokana na kukosa ujasiri wa kutenda. Wengi wamefungwa katika mitazamo ya watu wengine mfano ndugu wa karibu nk. Mawazo yao yakiyumbishwa kidogo wanakosa ujasiri wa kutenda. Zaidi ya vyote ni muhimu kuwa na ujasiri wa kufanya jambo hata ukikutana na vipingamizi. Lazima ujiamini katika kutenda.

3. IMANI HABA : Hili neno limekuwa lenye kufahamika sana hata katika vitabu vya dini, watu wengi hushindwa kutenda mambo kutokana na kuwa na imani isiyo thabiti. Lazima jambo unalolifahamu ulijengee msingi wa kiimani. Haiishii kulitambua bali inakupasa uliamini. Usipoliamini huwezi kulifanyia kazi

4. KUKOSA NIDHAMU: Nidhamu ni tabia ya ndani ambayo mtu huijenga. Nidhamu itakuwezesha kustahimili na kutoka katika comfort zone ( uwanda wa starehe) na kustahimili misukosuko na kuweza kusonga mbele. Nidhamu itakulazimu kufanya jambo hata usilojisikia kulifanya huku ukiwa na taswira ya matokeo chanya.

5. KUKOSA MIFUMO YA UTENDAJI: Hii ni changamoto kuu hasa pale unaposhindwa kuandaa mifumo ya utendaji kuhamisha nadharia kuwa vitendo. Mifumo ya utendaji ni malengo, muda, nguvu na uwezeshaji mwingine. Usipojenga mifumo bora ya utendaji itakuwia vigumu kutenda yale unayoyajua. Yakupasa uwekeze zaidi.
Pasipo kutathmini kwa makini hizo sababu tutaendelea kuwa watu wa kujua mambo pasipo kutenda.

Tuesday, August 23, 2016

OUR ATTITUDE MATTERS

The process of human change begins within us. We all have tremendous potential. We all desire good results from our efforts. Most of us are willing to work hard and to pay the price that success and happiness demand.

Each of us has the ability to put our unique human potential into action and to acquire a desired result. But the one thing that determines the level of our potential, that produces the intensity of our activity, and that predicts the quality of the result we receive is our attitude.

Attitude determines how much of the future we are allowed to see. It decides the size of our dreams and influences our determination when we are faced with new challenges. No other person on earth has dominion over our attitude.

People can affect our attitude by teaching us poor thinking habits or unintentionally misinforming us or providing us with negative sources of influence, but no one can control our attitude unless we voluntarily surrender that control. No one else "makes us angry." We make ourselves angry when we surrender control of our attitude.

What someone else may have done is irrelevant. We choose, not they. They merely put our attitude to a test. If we select a violent attitude by becoming hostile, angry, jealous or suspicious, then we have failed the test.

If we condemn ourselves by believing that we are unworthy, then again,we have failed the test. If we care at all about ourselves, then we must accept full responsibility for our own feelings. We must learn to guard against those feelings that have the capacity to lead our attitude down the wrong path and to strengthen those feelings that can lead us confidently into a better future.

If we want to receive the rewards the future holds in trust for us, then we must exercise the most important choice given to humanity by maintaining total dominion over our attitude. Our attitude is an asset, a treasure of great value, which must be protected accordingly.

Beware of the vandals and thieves among us who would injure our positive attitude or seek to steal it away. Having the right attitude is one of the basics that success requires.

Sunday, August 21, 2016

MSISIMKO WA MAISHA

Je umekosa msisimko wa maisha? Jizamishe katika kazi unayoiamini kwa moyo wako wote, iishi kazi hiyo, na utapata furaha ambayo haukuidhania-Dale Carnegie

Moja ya changamoto kubwa kwa watu sasa hivi ni kukosa msisimko na msukumo wa maisha, Moja ya viashiria vya kukosa msisimko wa maisha ni upweke, lawama na kukosa msukumo wa kufanya mambo. Watu wanakosa ile furaha ya kuamka jumatatu asubuhi, wengine hadi wanaingiwa na hisia hasi ikifika jumapili jioni.

Changamoto hii inatokana na mazoea ya watu ya kufanya mambo wasiyoyapenda, mambo ambayo hayana uhusiano na hulka zao. Watu wanafanya kazi lakini kwa lengo moja nalo ni kupata pesa pasipo kuwa na ridhaa katika nafsi zao. Kwa mujibu ya mwanasaikolojia Abraham maslow binadamu anasukumwa kukua na mambo mengi lakini kuu kuliko yote ni nafsi yake kuridhika.

Nafsi yako isiporidhika na kuridhia kazi unayofanya jua kabisa lazima utakosa msukumo na furaha katika kazi hiyo. Utaanza kuingiwa na hisia hasi kila unapokumbuka kwamba kesho yake kuna kazi. Steve Jobs aliwahi kusema kuwa kama hujapata kitu unachokipenda endelea kutafuta maana maana kuu ya maisha ni kutafuta kusudi lako na kulifanya.

Kama kwa mtazamo wa Dale carnegie inatupasa kujizamisha katika kazi tunayoiamini kwa mioyo yote na kuziishi kazi hizo utapata furaha na hautokaa kusubiri Jumatatu ifike uruke katika kazi ya moyo wako na uzuri ni kwamba ukiishi kazi ya moyo wako hautokuwa na likizo.

Friday, August 19, 2016

FEAR OF THE UNKNOWN

The Fear of the unknown is the Psychological paralysis caused by mystery of the unknown. Its one of the greatest challenges to progress because it kills the enthusiasm and the morale to progress to the clouds of what you haven't experienced or what you don't know.

This has paralysed many people with big ideas, it has paralysed individuals and caused them to be ANTAGONISTS to the FORCE OF CHANGE. Human being delights in COMFORT ZONE and any idea of CHANGE that hasn't been experienced before is often excused by the fear of the unknown.

But you can overcome the FEAR OF THE UNKNOWN by evaluating the vision and putting it down into realistic attributes, then GRAB on FAITH and DISCIPLINE while exercising the POSITIVE MINDSET.
Negativity gives power to the FEAR OF THE UNKNOWN. In life we need to understand that we either CHANGE willfully or THE FORCE OF CHANGE affects us violently leaving us with scars. Now that requires us to overcome the fear of the unknown.

The unknown is a mystery and it should be approached with enthusiasm and the joy of exploration...for whatever you don't know holds a part of your soul you haven't discovered yet...Pursue the experience and let Go of the fear of unknown.

Believe that God is there in the unknown ready to make it known to you. Let your life be of adventures and explore new experiences and overcome the fear of the unknown that keeps you from knowing the unknown.