Showing posts with label Identity. Show all posts
Showing posts with label Identity. Show all posts

Thursday, March 16, 2017

KUWA NA UHUSIANO NA UHALISIA WAKO

Kila binadamu ana uhalisia wake na utofauti wake, binadamu wanaweza fanana tabia lakini kuna msingi wa ndani kabisa wa kinafsi unaowatofautisha. Huu msingi wa kinafsi ndio uhalisia wa yule mtu. Mtu yeyote anayetoka katika uhalisia wake anapoteza utambulisho wake na akipoteza utambulisho wake anapoteza mambo mengi ya kinafsi yaliyomo ndani yake maana inambidi atafute uhalisia mwingine na alazimike kuishi katika uhalisia huo.

Kuna mambo mengi ya kinafsi ambayo mtu hupoteza na kuu kuliko yote ni amani ya nafsi na furaha ya ndani. Hapo ndipo unakutana na mtu ana kila kitu lakini hana furaha wala amani, yamkini kuna mambo kadha wa kadha yanayomtatiza lakini kuu kuliko yote ni kupoteza uhalisia wake. Kuna mambo yanayompa mtu ujasiri wa ndani, kuna misingi ya kinafsi ambayo mtu anakuwa nayo inayompambanua. Akipoteza hivo vitu au akitoka nje ya hivo vitu utaona mabadiliko yake kimtazamo na hata kihisia.

Katika uratibu wa kihisia na kutengeneza uimara wa kihisia mtu lazima arudi katikà uhalisia wake. Watu wengi wamepoteza dira katika mambo mengi kwasababu walitoka katika uhalisia wao ndipo wanakuja kushtuka wameshapotea na wakajikuta wanaishi kama wahanga wa mambo pasipo kujua nini cha kufanya.

Jitambue na jitambulishe na jiimarishe katika uhalisia wako maana utakapokuja kutoka katika uhalisia huo utajaribu kuwa kitu au mtu ambaye haumuelewi hata wewe. Unakuwa kama mtu usiyejitambua, Rudi katika uhalisia wako ili urudishe ile morali na msukumo na msisimko wa ndani kufanya mambo.

Ukiwa katika uhalisia wako mazingira ndo yatalazimika kuendana na uhalisia wako lakini tofauti na hapo wewe ndo utalazimika kuendana na mazingira. Uhalisia hukupa wewe uhuru wa kujipambanua na kujiwasilisha katika jamii ili uwe na mguso chanya. Uhalisia wako ndio hupelekea wewe kutambua kusudi lako na hata kuongeza thamani yako ili ulitende kusudi lako. Hivo ni muhimu sana kuwa katika uhalisia wako.

Jamii au mazingira yasikufanye upoteze uhalisia wako. Jamii ndo inapaswa ipishe njia ili uhalisia wako uweze kuwa na mguso na hii itawezekana tu ukisimama katika kulinda uhalisia wako

Friday, October 28, 2016

IMANI YAKO HUJENGA KAWAIDA YAKO

Imani mara nyingi hutokana na uzoefu juu ya jambo fulani, uzoefu huo hujiimarisha katika ubongo wako na kutengeneza mfumo wa kisheria ambao utatawala mitazamo yako na utakujengea kawaida yako. Na mara nyingi kawaida hiyo hujenga utamaduni ambao utakusanya mambo ya kuthibitisha na kuendana na utamaduni huo.

Unapojenga imani fulani siku zote imani hiyo huvuta mazingira husika ya kuthibitisha imani hiyo. Mfano unapojenga imani kuwa katika mahusiano jinsia fulani sio ya kuaminika imani hiyo huvuta mazingira hayo, imani hiyo itakuongoza kuchagua watu wasioaminika na hata itakujenga kutafuta mazingira yasio aminifu katika mahusiano yako ili kuthibitisha imani hiyo.

Siku zote akili hujisikia furaha pale inapothibitisha mitazamo yake na malengo yake..ndio maana siku zote ukithibitisha jambo ulilokuwa na wasiwasi nalo hata kama linaumiza akili yako itasema nilijua tu....tafsiri ya neno nilijua ni kuipa thamani akili yako kwa uthibitisho huo na kuijengea thamani kwa imani hiyo.

Ni muhimu utambue kuwa unatakiwa kutafakari sana kabla hujakiweka kitu kama imani yako kwasababu imani hiyo itakutengenezea kawaida yako. Na siku zote kawaida yako ndio ulimwengu wako. Watu wengi wamejijengea kawaida mbaya hadi pale jambo zuri linapokuja wanalikataa na kuliona haliwastahili. Kuna watu wamejijengea kawaida kiasi cha kwamba jaribio lolote la kutoka hapo ni maumivu kwao.

Usijenge msingi wa kiimani ambao unaona kabisa ni asi kwasababu huo msingi utavuta mazingira ya kuthibitisha hayo uliyoyaweka kama sheria. Hakikisha kabla hujaliamini jambo na kuliweka katika akili yako litafakari. Usije kufungwa na kawaida ambayo itakutesa. Mfano mtu anaweza akaja kukwambia yaani mie kila mahusiano yangu naumizwa...unamuuliza je unadhani kwanini....mtu anakwambia mie nadhani nina mkosi au wanaume wote ni wahuni, au wanawake wote hawaaminiki...Tayari kishajenga imani ambayo inavuta mazingira kuthibitisha imani hiyo.

Ni jambo la muhimu sana kuongeza maarifa juu ya jambo usilolijua badala ya kujijengea imani ambazo zitakujengea kawaida yako. Pia ni kubadilisha taswira yako, ni nini hasa unaangalia au ni wapi hasa mtazamo wako ulipo maana taswira siku zote hukutengenezea imani itakayokujengea kawaida itakayovuta mazingira kuthibitisha mambo husika.

Monday, October 3, 2016

TAMBUA UNACHOTAKA KATIKA MAISHA

Moja ya changamoto kubwa ambayo watu wengi huwa tunayo ni kutofahamu nini tunachotaka au tunachohitaji katika maisha. Watu wengi hudhani wanajua wanachokitaka au wanachokihitaji lakini ukiangalia matendo yao utatambua kuwa wengi hawajui wanachokitaka katika maisha. Usipojua unachotaka katika maisha utakuwa ni mtu wa kuzunguka zunguka kujaribu jaribu kila kitu kuona kina mguso gani kwako.

Kuna dhana nyingi sana ambazo tunazo ju ya yale tunayotaka katika maisha na unaweza ukapewa kila ulichodhani unakitaka kisha ukaja kugundua kuwa bado kuna kitu kingine unachokitaka. Na utakuwa ni mtu usiye na furaha wala amani kwasababu hujui unachokitaka. Pengine hata ukawa mtu mwenye lawama katika kila jambo kwasababu wewe mwenyewe hujui unachokitaka.

Pengine pia unaweza jua unachokitaka lakini unadhani ni jambo la kufikirika, huo mtazamo unaweza kukufanya ukaendelea kuwa kama mtumwa anayezunguka jangwani asijue anapoelekea. Kuna mwanafilosofia mmoja aliwahi kusema kuwa Watu wengi hawajui wanachokitaka hadi uwaonyeshe wanachokitaka. Ni muhimu sana kujua unachokitaka.

Njia pekee ya kujua unachokitaka ni kujitathmini nafsi yako na kujitambua utu wako ndipo utajua ni nini unachohitaji. Mwanafilosofia mmoja aliwahi kusema kuwa kama hakuna adui ndani adui wa nje hawezi kutudhuru. Nafsi yako ya ndani imeundwaje? Pengine ushawahi kujiuliza ni jambo gani linakupa amani na unaamini ndio jambo ambalo ukilipata kama msingi wa maisha yako utaweza kupata mambo mengine yote?

Kila nafsi inahitaji uhuru na amani na furaha na wengi wetu tumedhani tukipata vitu basi nafsi yetu ndo itakuwa imepata inachotaka. Hapana!! Nafsi yako inahitaji kukua na jambo lolote linaloweza kuinyanyua nafsi yako ndilo jambo unalohitaji. Nafsi yako inahitaji thamani na jambo linaloweza kuipa thamani nafsi yako ndilo unalohitaji. Nafsi yako inahitaji amani na jambo lolote linaloweza kukupa amani ya nafsi ndilo unalohitaji.

Ukishajua msingi hasa wa mahitaji ya nafsi yako itakuwezesha kutambua ni nini unachohitaji katika maisha, iwe ni katika uchaguzi wa kazi, iwe ni katika mahusiano au nyanja yeyote ya maisha. Utatambua marafiki wa nafsi yako, utatambua hata mwenzi wa nafsi yako, utatambua hata kusudi la maisha yako.

Tuesday, September 6, 2016

TENGENEZA UTARATIBU WA KIUONGOZI WA MAISHA YAKO

Pasipo utaratibu mambo huenda mrama. Pasipo uongozi thabiti lazima kuwe na machafuko. Ili uweze kuwa na uthibiti katika maisha lazima kuwe na utaratibu na lazima kuwe na uongozi thabiti. Wewe ni kiongozi wa maisha yako.

Usipokuwa na uongozi binafsi na utaratibu wako wa utendaji lazima utakuwa mtumwa wa uongozi na utaratibu wa mwingine. Mikwaruzo hutokea pale mamlaka zinapokinzana. Pale ambapo kunakosekana uwiano baina ya uongozi binafsi na uongozi unaokuzunguka. Pale ambapo kunakosekana uwiano baina ya utaratibu binafsi na utaratibu unaokuzunguka.

Usipokuwa kiongozi wa maisha yako utawapa wengine fursa ya kushinikiza mambo katika maisha yako na hii itakujengea hali ya kukosa furaha kwa maana utakuwa unashindana na nafsi yako inayotaka kuwa kiongozi lakini imekosa utaratibu wa kiungozi.

Uhuru siku zote una gharama, Huwezi kuwa huru kama unaogopa gharama ya kuwa huru. Nafsi yako inataka kuwa huru lakina usipojenga utaratibu na uongozi wa ndani wa hisia na maamuzi ni vigumu sana nafsi yako kuwa huru.

Je unawezaje kujenga utaratibu na uongozi wa maisha yako:-
1. Usisimame katika msingi wa hisia: siku zote ili kuwa na utaratibu na uongozi katika maisha lazima ujenge msingi imara katika nafsi yako. Na hisia sio msingi imara maana hisia hubadilika kila wakati, huwezi kuwa kiongozi wa maisha yako kama unaenda kwa hisia. Ukienda kwa hisia utajikuta unaendelea kuvipa nafasi vitu ambavyo havitakiwi kupewa nafasi kwa wakati huo.

2. Ongeza maarifa na ufahamu : Huwezi kuwa huru na kuwa kiongozi wa maisha yako kama ufahamu na maarifa yako vina ukomo. Hakuna jambo baya kama uhuru na ujinga. Huwezi kuwa mjinga halafu ukawa kiongozi wa maisha yako. Ujinga ni utumwa ndio maana kuna maandiko yanasema Utaijua kweli nayo kweli itakufanya huru.

3. Tengeneza sheria za maisha yako: lazima utengeneze msingi mgumu tofauti na hisia. Ukishakuwa na maarifa tengeneza sheria zako mwenyewe na hakikisha huzivunji sheria hizo maana ni changamoto na itakuumiza zaidi pale unapovunja sheria zako mwenyewe.

4. Fanya vitu kulingana na vipawa na karama zako : Huwezi kuwa kiongozi bora wa maisha yako kama haujipambanui na wengine. Usiwe mtu wa kufata upepo...Zig ziglar alishawahi kusema kuwa Uongozi sio kufuata njia iliyopitwa na watu bali ni kutafuta njia yako na kuacha alama. Ukiwa mtu wa kujilinganisha na wengine huwezi kuwa na utaratibu wako mwenyewe.

5. Jiamini : Dhana ya kujiamini ni pana sana. Katika jambo lolote lile usipojiamini huwezi fanya chochote, jiamini katika maamuzi yako, jiamini katika unayofanya. Wengi wanashindwa hata kufanya maamuzi magumu kwasababu ya kukosa kujiamini. Kama unataka kuwa kiongozi wa maisha yako jiamini ikiwemo huweze kufanya maamuzi na kuwa tayari kuwajibika kutokana na maamuzi yako.

* Hakuna jambo litakalokupa amani na furaha kama kutambua kuwa una uthibiti wa maisha yako. Ni jambo litakaloongeza ari ya utendaji wako na pia kukupa morali na msisimko wa kila siku wa maisha.

Friday, August 19, 2016

NJIA ZA KUDHIHIRISHA MAONO YAKO

"Whatever you vividly imagine, ardently desire, sincerely believe, and enthusiastically act upon must inevitably come to pass!" - Paul J. Meyer

Tafakari ya ufasaha ni ngazi ya kwanza kabisa ya kufikia unachokitaka. Mara nyingi huwa tunatafakari bila ufasaha. Tunabeba maono makubwa lakini hatukai chini kutafakari maono hayo kwa ufasaha. Ni muhimu kukaa chini kutafakari kwa ufasaha maono uliyonayo.

Hitaji kutoka ndani ya nafsi ni ngazi ya pili kwa mujibu wa paul meyer ya kufikia malengo. Lazima maono yako uyatengenezee sababu na msingi wa ndani wa kihisia. Tengeneza msukumo wa ndani wa uhitaji katika kufikia malengo yako...Lazima utengeneze sababu ya kwanini unatakiwa ufikie malengo hayo.

Amini kutoka moyoni ni ngazi ya tatu kwa mujibu wa Paul meyer, ni lazima uwe na imani thabiti juu ya maono yako na imani hiyo isitetereshwe na aina yeyote ya mazingira. Ukiwa na maono lakini ukashindwa kuyaamini maono yako jua hautoweza kuyafikia.

Kisha unatakiwa uchukue hatua kwa msisimko na mhemko chanya. Lazima uchukue hatua kwa msisimko na mhemko chanya la sivyo hutoweza kuyafanya hayo maono yako dhahiri. Hatua iliyo na msisimko itakuwezesha kushinda vipingamizi au misukumo na changamoto hasi.
Kwa mujibu wa Paul meyer chochote kitafanikiwa ukifata hizo njia.

Thursday, August 11, 2016

IMPACTS OF YOUR COMPANIONS TO YOUR SUCCESS

Learn to surround yourself with people who will make impact, encourage and support you. Don't waste most of your time with people who don't care about your future but cares about what you drink this weekend and always want you to depend on them than be independent.

Surround yourself with people who will assist you to chase your dreams and wish you to be independent in life than dependent. People who want to see you succeeding in life and take care of your own bill.

Most of us would have been successful by now but the company we keep is dragging us down because they enjoy when people depend on them. Is time to have people who wish us good than those who want us to depend on them.

Your company either makes you or breaks you. Your company is either a burden or a drive. You have to be careful with the company you keep if you want to succeed. Most successful people have success connections and they don't entertain people below their league because they believe they don't have any challenge to offer them.

If eagles fly alone no matter the crowd of other birds that fly together. Eagles fly with their kind. Thus its very important to choose well the company we hang out with.

There are three kinds of company, the comrades, the confidants, the constituents.
The Comrades are people who walk with you because you have a common goal and once the goal is gone they also leave. Most school friends and colleagues are comrades,
The constituents are people who walk with you because they want something from you and once they get what they want they go,most people fall in this that's why relationships fail and hurt, friendship break etc.
The confidants are the people who stick with you unconditionally...they will be with you in the valleys,hills, good times and bad times etc.
You have to evaluate well the company you keep if you want to succeed.