Showing posts with label Thoughts. Show all posts
Showing posts with label Thoughts. Show all posts

Thursday, May 18, 2017

IMANI NI MSINGI WA AMANI YA NAFSI

Imani ni kuwa na hakika ya mambo yasiyoeleweka au ambayo hayajabainishwa kwa wakati huo. Imani hukupa nuru ya kutambua mafumbo ya kinafsi na maswali yasiyo na majibu yenye kuleta taharuki katika nafsi.

Nafsi inaweza kupitia mambo fulani ambayo yanaikosesha amani na kuifanya ibaki katika hamaki kutojua ni nini kinachofuata au nawezaje kutoka katika hali fulani ya mkwamo wa kihisia au kimtazamo na kiakili. Hapo ndipo imani huja kuleta amani.

Imani inatakiwa iongoze hisia na iziweke katika hali ya utulivu. Ni vigumu kupata tulizo la kihisia bila kuweka mfumo bora wa kiimani, Ukitazamia kutoka katika mkwamo huo, ukitazamia utulivu wa hisia na ukitazamia uzuri na mambo mema yajayo.

Muda wote imani hujengeka katika msingi imara wa hatma ya kesho yenye furaha, faraja na uzuri na pia hujengeka katika faida ya leo katika mazingira hayo magumu. Imani hutazama fundisho, hutazama uzuri na  hutazama uimara unaotokana na ugumu na changamoto husika.

Siku zote ukitaka kuwa na amani katika nafsi yako boresha mfumo wako wa imani, boresha mfumo wako wa kuamini, jikite katika kutengeneza imani zenye tija, imani zenye kukujenga na kukuimarisha. Na ukishapata msingi husika iache imani hiyo iamuru hisia zako zitii.

Imani ikisema nitatoka katika hii hali, ikasema nitavuka katika hili daraja la maumivu, ikasema nitapata kilicho bora, Hakuna hisia ya maumivu itakayoweza kukushikilia kwa muda mrefu au hata kukuzamisha. Utakuwa ni mtu mwenye amani muda wote.

Thibitisha imani zako kwa kuzipa msingi imara kwa kuzifanya sheria za nafsi yako. Imani juu ya uzuri wako, imani juu ya stahiki yako na yale unayoyatarajia na yenye kukupa amani ya nafsi, hakikisha unajijenga na kujithibitisha katika imani hizo kwa kusimama bila kuyumba kama hisia za taharuki na uchungu zikija.

Huwezi kuwa na amani ya nafsi kama huna imani na hali fulani, kama huna imani na jambo fulani, kama huna imani na watu fulani. Ni vyema ukajiimarisha katika imani na siku zote hakikisha imani yako inajengeka katika kweli. Huwezi jenga imani kwa kitu cha uongo. Imani lazima isimame katika misingi ya kweli, fikra chanya, ubora wa nafsi na utu.

Wednesday, November 23, 2016

MAKE YOUR THOUGHTS FUTURE ORIENTED

One of the greatest challenges to thinking is the directions of your thoughts, Are your thoughts future oriented or past oriented? Is the direction of your thoughts forward or backwards? Backward oriented thoughts are a resistance to future pursuit. The quest to the future needs a future oriented mindset.

If you are constantly thinking backwards rather than thinking forwards then you create a resistance in your forward movement. When you think backward you create a force that pulls you backwards to the past. But if you think forward you create a force that pulls you forward to your future.

You can never move in a direction where your thoughts aren't directed, Don't ever fall in the trap of the mind of thinking backwards. Thinking backwards is thinking about things past, its entertaining past thoughts, its your reluctance to delete the past from your system. The duty of the past is to give you a motivation to create a platform for the future you want. Once you find the gear of the future, drive in the future mode and set your mind there.

Never inter-change your present gear with your past gear, its dangerous, You can only change your present gear with your future gear to increase the momentum and increase a boost of enthusiasm. How do you inter change present gear with future gear....Its by consuming some of the future ideas and dreams and instill them in the present, You cant consume all of them or else your present will be crowded and you wont find pleasure in the process

Its very important to think forward, just analyse yourself in the times you sit down to think what are the directions of your thoughts? Present, Past or future. Ask yourself also when you want to act on something and thoughts come in your mind in your analysis where are those thoughts from? Past or future... If you realise that its your past that brings out most of your thoughts then its time to change.

Make the future be the source of your thoughts and let the future interchange gears of motivation in your quest to pursue life.

Monday, November 14, 2016

USITAFAKARI MAJUTO, TAFAKARI FUNDISHO

Katika maisha tunapitia mambo mengi, njia nyingi na tunakutana na vitu vingi, nafasi nyingi na hata vipindi vingi ambavyo tunatakiwa tufanye maamuzi juu ya mambo kadha wa kadha tunayokutana nayo. Kama binadamu wenye uhuru wa kufanya uchaguzi na utashi kila wakati huwa tunatumia njia zozote zile tulizonazo kufanya maamuzi.

Maamuzi yetu ndiyo ambayo hutengeneza hatima ya maisha yetu au matokeo yanayokuja baada ya hapo. Maamuzi mazuri huleta matokeo mazuri na maamuzi mabaya pia huleta matokeo mabaya. Kila mtu ameshapitia hali ya kufanya maamuzi na kila mtu ametumia uhuru wake wa kinafsi kufanya maamuzi. Changamoto kubwa ni matokeo ya maamuzi yetu na jinsi tunavopokea matokeo ya maamuzi yetu.

Maisha siku zote ni safari endelevu yenye changamoto mbali mbali na safari hiyo huwa vumilivu pale inapoendeka kwa maarifa na ujuzi wa wapi unaelekea. Maisha huhitaji dira na dira ndo itakuelekeza kasi ya kwenda nayo hata njia za kupita kufikia hatma yako. Maarifa ni muhimu sana.

Mara nyingi tumekuwa na mapokeo tofauti tofauti ya matokeo ya maamuzi yetu ambayo wengi wetu yametusababishia kukwama kwa muda mrefu katika dimbwi la maumivu na tukaishia kulalamika, kulaumu, kuwa na mitazamo hasi na hata kupata matatizo mbali mbali ya nafsi. Mara nyingi tumekuwa watu wa majuto badala ya mafunzo

Jambo la muhimu ni kutafakari mafunzo uliyoyapata na uyatumie hayo kama mawe ya kukanyagia kwenda mbele, usikae unajilaumu au unatafakari kwa makosa ya nyuma hata kama yameleta matokeo mabovu katika maisha, badala ya kusema ningejua tafakari aya sasa umejua utafanya nini. Huwezi kubadilisha makosa ya nyuma ila unaweza kufanya mabadiliko ili makosa ya nyuma yasijirudie.

Wengi tunakaa zaidi tunatafakari majuto badala ya kutafakari mafunzo na kufanya yanayohitajika kusonga mbele halafu baadaye unajikuta unarudia kosa lile lile au unapita tena njia ile ile. Badili mtazamo hata kama matokeo ya maamuzi yako mabaya yanaendelea kukutesa kuwa na ujasiri wa kusema nitafanya hivi badala ya ningefanya hivi.

Kumbuka kila mtu ameshafanya kosa fulani ambalo limemgharimu au linamgharimu hadi sasa lakini cha msingi ni kutafakari funzo badala ya majuto.

Friday, October 28, 2016

IMANI YAKO HUJENGA KAWAIDA YAKO

Imani mara nyingi hutokana na uzoefu juu ya jambo fulani, uzoefu huo hujiimarisha katika ubongo wako na kutengeneza mfumo wa kisheria ambao utatawala mitazamo yako na utakujengea kawaida yako. Na mara nyingi kawaida hiyo hujenga utamaduni ambao utakusanya mambo ya kuthibitisha na kuendana na utamaduni huo.

Unapojenga imani fulani siku zote imani hiyo huvuta mazingira husika ya kuthibitisha imani hiyo. Mfano unapojenga imani kuwa katika mahusiano jinsia fulani sio ya kuaminika imani hiyo huvuta mazingira hayo, imani hiyo itakuongoza kuchagua watu wasioaminika na hata itakujenga kutafuta mazingira yasio aminifu katika mahusiano yako ili kuthibitisha imani hiyo.

Siku zote akili hujisikia furaha pale inapothibitisha mitazamo yake na malengo yake..ndio maana siku zote ukithibitisha jambo ulilokuwa na wasiwasi nalo hata kama linaumiza akili yako itasema nilijua tu....tafsiri ya neno nilijua ni kuipa thamani akili yako kwa uthibitisho huo na kuijengea thamani kwa imani hiyo.

Ni muhimu utambue kuwa unatakiwa kutafakari sana kabla hujakiweka kitu kama imani yako kwasababu imani hiyo itakutengenezea kawaida yako. Na siku zote kawaida yako ndio ulimwengu wako. Watu wengi wamejijengea kawaida mbaya hadi pale jambo zuri linapokuja wanalikataa na kuliona haliwastahili. Kuna watu wamejijengea kawaida kiasi cha kwamba jaribio lolote la kutoka hapo ni maumivu kwao.

Usijenge msingi wa kiimani ambao unaona kabisa ni asi kwasababu huo msingi utavuta mazingira ya kuthibitisha hayo uliyoyaweka kama sheria. Hakikisha kabla hujaliamini jambo na kuliweka katika akili yako litafakari. Usije kufungwa na kawaida ambayo itakutesa. Mfano mtu anaweza akaja kukwambia yaani mie kila mahusiano yangu naumizwa...unamuuliza je unadhani kwanini....mtu anakwambia mie nadhani nina mkosi au wanaume wote ni wahuni, au wanawake wote hawaaminiki...Tayari kishajenga imani ambayo inavuta mazingira kuthibitisha imani hiyo.

Ni jambo la muhimu sana kuongeza maarifa juu ya jambo usilolijua badala ya kujijengea imani ambazo zitakujengea kawaida yako. Pia ni kubadilisha taswira yako, ni nini hasa unaangalia au ni wapi hasa mtazamo wako ulipo maana taswira siku zote hukutengenezea imani itakayokujengea kawaida itakayovuta mazingira kuthibitisha mambo husika.

Thursday, October 13, 2016

SAUTI TATU KATIKA MAHUSIANO

Mahusiano yetu huguswa na sauti ambazo zinaleta changamoto na ni sauti ambazo zinamchango katika uimara wa mahusiano yako au kuanguka kwa mahusiano yako. Bila sauti hizo kuwa katika uwiano  sawa basi sauti moja ikiizidi nyenzake inaweza sababisha changamoto.

Sauti hizo zimegawanyika katika makundi matatu, ya kwanza ni sauti ya nafsi ; Hii ni sauti ambayo kila mtu anakuwa nayo kiasili nayo ni sauti ya uhuru, furaha na amani. Kila nafsi inataka kuwa katika uhusiano ambapo itakuwa huru na yenye furaha na amani, sauti hii inalia kutoka ndani ya nafsi ya mtu na ndio maana kuna ambao husema kuwa katika uhusiano ambao utakuwa huru na mwenye furaha na amani.

Sauti ya pili ni sauti ya Jamii; hii ni sauti inayotoka katika jamii inayotuzunguka juu ya mahusiano yetu. Hii sauti inaweza ikawa sauti ya wazazi au sauti ya malezi na makuzi ambayo tumeyapitia. Sauti hii mara nyingi hutuambia kuwa ni nani anatufaa, au ni nani tunatakiwa tuwe naye au ni mahusiano gani ambayo inabidi tuwe nayo.

Sauti ya tatu ni sauti ya akili zetu; Binadamu huwa na hali ya kupenda kutafakari na kutumia akili katika kufanya maamuzi na pengine kuna wakati hutumia zaidi akili katika mambo fulani juu ya nini hasa jambo sahihi la kufanya.

Ili kujenga uhusiano imara lazima hizi sauti ziwe na uwiano...sauti ya nafsi inabidi iwe kama msingi itakayobeba sauti nyingine zote. Sauti ya nafsi ikizifunika sauti nyingine zote unaweza pelekea kufanya mambo ambayo yanaweza kutokubalika katika jamii na ukajikuta unakosa kabisa ushirikiano na wengine lakini sauti ya jamii ikiizidi sauti ya nafsi utajikuta unaingia katika mahusiano ambayo katika jamii unasifika lakini ndani ya nafsi yako unakosa furaha na unakuwa na upweke ambao jamii haiwezi kukusaidia.

Pia inakupasa sauti ya nafsi iwe na uwiano na sauti ya akili ili akili yako iweze kuwekeza zaidi...maana nafsi na akili zikiwa na uwiano ile amani na furaha hudhiirika katika fikra za ubunifu zaidi katika kuimarisha mahusiano hayo.

Kama unaona sauti ya jamii ni kubwa na inakutisha hakikisha sauti ya nafsi na sauti ya akili vinaungana kuishurutisha sauti ya jamii itulie.

Changamoto na jambo la msingi kwa kila mtu ni kuhakikisha hizo sauti zina uwiano ili kujenga mahusiano imara.


Friday, August 19, 2016

FEAR OF THE UNKNOWN

The Fear of the unknown is the Psychological paralysis caused by mystery of the unknown. Its one of the greatest challenges to progress because it kills the enthusiasm and the morale to progress to the clouds of what you haven't experienced or what you don't know.

This has paralysed many people with big ideas, it has paralysed individuals and caused them to be ANTAGONISTS to the FORCE OF CHANGE. Human being delights in COMFORT ZONE and any idea of CHANGE that hasn't been experienced before is often excused by the fear of the unknown.

But you can overcome the FEAR OF THE UNKNOWN by evaluating the vision and putting it down into realistic attributes, then GRAB on FAITH and DISCIPLINE while exercising the POSITIVE MINDSET.
Negativity gives power to the FEAR OF THE UNKNOWN. In life we need to understand that we either CHANGE willfully or THE FORCE OF CHANGE affects us violently leaving us with scars. Now that requires us to overcome the fear of the unknown.

The unknown is a mystery and it should be approached with enthusiasm and the joy of exploration...for whatever you don't know holds a part of your soul you haven't discovered yet...Pursue the experience and let Go of the fear of unknown.

Believe that God is there in the unknown ready to make it known to you. Let your life be of adventures and explore new experiences and overcome the fear of the unknown that keeps you from knowing the unknown.

Monday, August 15, 2016

HUWEZI FANIKIWA ZAIDI YA MAWAZO YAKO

Watu wengi hupenda mafanikio na kukua lakini hawafanikiwi wala kukua. Kwasababu ya sheria moja ambayo ni kwamba huwezi fanikiwa zaidi ya mawazo yako. Maisha yako ya nje ni zao la mawazo yako.

Hakuna jambo linaloweza kutokea kama hujalifikiria kwa wakati wowote katika maisha yako. Unaweza kupenda kufanikiwa lakini je ulishawahi kufikiria na kutafakari mafanikio. Huwezi kuwa na fikra za ukomo halafu uwe na ziada. Mfumo wako wa fikra unadhiirika kwa kauli zako na mitazamo yako juu ya jambo fulani.

Ukishakiri kwamba jambo haliwezekani ni kwasababu umefikiria haliwezekani na halitokuja kuwezekana kwako hadi ubadilishe jinsi unavoliwaza hilo jambo. Hapo pekee ndo utaweza kufungua ubongo wako juu ya njia za kuliweza.

Myles munroe alishawahi kusema ugumu wa jambo fulani unatokana na ufahamu wako juu ya jambo husika hivo badala ya kushikiria mtazamo wako, wekeza kupata ufahamu zaidi juu ya hilo jambo. Huwezi ishi nje ya mitazamo yako maana mitazamo yako siku zote itachonga muundo wa maisha yako.