Tuesday, August 14, 2018

SOUL ACTIVISM

Today i will speak about soul activism.I have come across a number of people who are passive in their soul and spirits.

What do i mean by soul activitism? Its the act of applying action to achieve results in your soul. Most of us are passive in our potential and abilities. We lay low and live our talents dormant. We dont even walk the course of our purpose nor even have a glimpse of where we should move to.

When we are in a state of dilemma concerning the issues of life. We become passive in our soul. You can stay doing nothing all day, scrolling social media, sleeping waking up, or you might be entangled in activities but your soul remain passive.

What am i saying, In your times of despair or without activity, apply the soul activism even in the small things that have a relationship to your destiny. Dont despise the days of humble beginning, Exercise your gifts even in a small situation.

You want to evolve in your soul, apply soul activism, apply actions to exercise your soul and attitudes. You want to be someone, live the way you want even in the privacy of your room. Dont lay dormant.

Remember effeciency happens when opportunity meets preparation. Always prepare yourself by the process of soul activism.Always act on issues of your soul to produce necessary character results

Dont forget to purchase the copy of "Utashi wa Kihisia" to receive necessary principles of emotional intelligence.

Nickvaleries

Thursday, August 2, 2018

THE POWER OF THE ERASER

Dear Reader, today i want to unveil the power of the eraser. We as human beings are a component of time...We have past, present and future...We are always required to redeem time if we ought to live in dominion.

We came from the past, live at the present and heading the future...One thing to remember is the bible says God's purpose is to give us hope and a FUTURE...why so? The ministry of the PAST is the ministry of death...Engage the power of the eraser.

Whats the Power of the eraser...Apostle Paul says I no longer look at my past...i put it behind and i move towards the glory ahead....Listen, anytime you feel like revisiting your past or even curious ensure you have engaged the Power of the eraser.

Do you know most of the times whats behind you can pull you back...You dont move forward because you are loaded with the junk of the past...The fears, the pain, the worries, your past mindset....the words you said to yourself...past limitations.....ENGAGE THE ERASER.

You are not happy and you live in lack of confidence because you havent engaged the eraser...Listen those limiting thoughts might have been deposited at the past...Engage the eraser.

If you will ever have to live the best future learn to engage the eraser...Train your eyes not to set eyes on your past...Train your ears not to listen to the past...Remove past junk from your system..your surroundings and your life.

The Power of the eraser says I will set my eyes to the glory ahead, it proclaims i am a new creation all things have passed away all have become new, it shouts the latet glory is greater and better than that of old, it not only proclaims but acts to move forward.

If you keep on revisitting your past...loading and downloading past junk...listening to past stories and junk...Keeping past junkie stuff in your system...YOU are overloding your drive to the future.

Erase things of the past that dont have meaning now...The bible says Renew your Mind...

An eagle always shake off old feathers and gain new ones to fly...Hibernate your system then Refresh and renew...Dont back up past junk...Erase and fill yourself with new ones and present ones.

Dont syncronize your present to your past...Syncronize it to your future for you ought to move from glory to glory.

Nickvaleries

Friday, July 27, 2018

POWERFUL WAYS OF HAPPINESS IN THE WORLD

Have you realised that the happiness rate is decreasing in the world... People now lament, complain and cry more than ever

Jesus said in the world there is trouble but be of CHEER for i have overcomed the world.

The Kingdom of God isnt in food and drinks but joy and peace in the holy ghost....which means the kingdom of God isnt in materials but in the inward environment of the soul...There are those with so much materials but dont have the kingdom so never envy those with materials but find peace and joy.

Have you realised that the bible says seek the Kingdom of God and all others ( materials) will be added the he later says the kingdom of God is in joy and peace in the holy spirit...What do you understand??? Its simple...seek Joy and peace in your life and success will come...Some put it the other way round...NO, the reason you arent successful in the spirit is because you have no joy nor peace in you.

You complain too much instead of being joyful and praise the lord...You worry to much of money instead of having peace for he is able to do exceedingly, abundantly more than you can imagine....You worry and stress instead of Being at peace for all things work for Good for they that love God.

You will say you dont know what am going through...Well God knows and he is the one who said All things will work for good...Not I.

...Your mindset, speech and actions....One thing i have realised we as human beings should always evolve...and there is no greater pain than staying dormant....so each day make a goal and a devotion then hit it. Reduce your regrets by making everyday count...Do things that will make you happy and joyful daily.

So how can you find happiness in the world..

Its simple...Gravitate in Your identity, meditate in his promises...Focus on the light for so many times we fall into the temptation of following the darkness...

Listen search your spirit...understand your potentials, thank God for your strength and ask him to capitalize in your weakness.... Serve his kingdom with your God given talent. Invest in his kingdom...Change your perception and tie your life in your purpose.

Chase only what will cultivate your soul...Refuse to give you ear to negativity of the world...I believe the greatest transformation is in the way we use our tongues for in that area we find Life and death...

Happiness comes when you focus on God, his promises will give you peace...your mindset will change and you will be prophesying greatness.

Prophesy over your life more than you worry...Praise more than you complain...and another thing...Pray more than you stay in silent whining... Refuse to listen to any negative report from anyone that is contrally to the word of God.

Start a weekly devotion and fast...Say in this week i wont complain on anything, i will be thankful for all...and i will laugh at problems than cry and i will talk and prophesy of positive things like a crazy person and i wont talk bad words to hurt my spirit...then see the happiness you will find.

Nickvaleries

Friday, February 23, 2018

KITABU CHA UTASHI WA KIHISIA

NUNUA NAKALA YAKO SASA

Hiki ni kitabu cha kinafsi ambacho kimejikita katika kukuwezesha kutambua kwa upana wake dhana ya Hisia na namna unavoweza kuratibu hisia zako vyema

Pia kinatoa njia halisi za kiutendaji za kuiboresha nafsi yako katika nyanja ya kihisia ili uweze kuwa na mguso chanya katika jamii ya nafsi zinazokuzunguka

Pia kitabu hiki kinakuwezesha kutambua utu wako, vipawa vyako vya kinafsi na namna unavoweza kutumia hisia kama msukumo wa kuendesha vipawa vyako katika kuleta tija

Katika kitabu hiki kuna majibu yenye upana ya namna ya kujibu maswali ya kimahusiano na hata kutambua hisia za watu wengine ili uweze kuishi nao vizuri.

Kitabu hiki kina uhalisia na kinagusa kila nyanja na kila aina ya utu bila kusimama katika upande wa dini.

Ukisoma kitabu hiki kitakusaidia sana kinafsi na kihisia katika kukujenga kinafsi kuwa mtu bora na hakifungamani na mtazamo wa kwamba ni hadi uwe mhanga wa matatizo ya kihisia ndio unatakiwa ukisome.

Wasiliana nami katika account zangu za mitandao ya kijamii au email
nizzo43@gmail.com

Wednesday, September 27, 2017

FREEDOM OF THE SOUL

One of the greatest challenges to the soul is freedom. The soul is in constant craving for freedom and it always strive to acquire freedom by any means.

 In life no matter how successful you can be, freedom is crucial for your soul to flourish, freedom enhances security and grounds for expressing the attributes for impact. Unless souls are free there will always be constant struggle.

We can choose to be free by letting our souls sink into themselves and to discover what we are made of and choosing to connect. Connection is a product of freedom.

Without freedom there is no connection whatsoever thats why its our duty to always free ourselves from the ties of our souls.


Monday, September 11, 2017

NAFASI YA MAZUNGUMZO YAKO KATIKA UTASHI WAKO WA KIHISIA

Je wajua kuwa mazungumzo yako ni kipimo cha utashi wako wa kihisia? Je wajua ya kwamba mazungumzo yako yana mchango katika uimara wa utashi wako wa kihisia. Jiulize tu swali moja, unazungumza nini?

Mfumo wako wa mazungumzo au uwasilishaji mawazo yako ni kipimo cha utashi wako wa kihisia. Jinsi unavozungumza juu ya maswala yenye miguso ya kihisia ndivo jinsi utashi wako wa kihisia ulivo. Watu wengi hudhani kuwa uhuru wa kuzungumza katika kutoa mitazamo ya kihisia ni sawa na uhuru wa kuzungumza katika maswala ya kiakili na kifikra, hapana. Uhuru wa kihisia unahitaji mguso wa kinafsi na ufahamu wa aina ya utu wa nafsi husika.

Watu wengi wamejikuta wanazungumza katika lugha hasi yenye harufu ya ukosefu wa imani na ladha ya uchungu wa maumivu kwakuwa ndivo utashi wao wa kihisia ulivo. Wengi wanazungumza nyuma ya pazia la woga na hofu wakionekana ni watu wenye uimara mkubwa kifikra kumbe kihisia ni nafsi ambazo zina hofu hata ya kupatwa na mawimbi ya kihisia. Ukiweza tambua miundo ya lugha na mitazamo utatambua kuwa kuna changamoto kubwa katika utashi wa kihisia.

Tambua ya kwamba kimjazacho mtu ndicho kimtokacho. Inatakiwa tutambue ni nini haswa hutujaza nafsi zetu. Kuna mazungumzo tunayopenda kuyapa nafasi pengine kwa utamu wake  wa kimaudhui wenye kuburudisha nafsi zenye shauku ya kutaka ufahamu pengine hata kama maudhui haina tija wala faida lakini mazungumzo hayo ndiyo yanajaza nafsi zetu magugu yanayoenda kusababisha udhaifu wa kihisia. Shauku isiyo na nidhamu ni adhabu kwa hisia na nafsi. Lazima ujifunze kuratibu mazumgumzo.

Kuna mazungumzo pia tunayofanya ambayo hutudhoofisha nafsi zetu na kutupa misukosuko ya kihisia isiyo na tija. Hivo ni muhimu kutambua na kufahamu aina ya mazungumzo na mguso wake kwa hisia zako

Hatuwezi kuwa watu wenye nafsi imara na utashi wa kihisia bila kuwa watu wenye kuratibu aina ya mazungumzo tunayofanya. Ni jambo gumu sana kuwa mtu mwenye mazungumzo yasiyo na tija kuwa na utashi wa kihisia pengine ni rahisi hata ngamia kupenya katika tundu la sindano. Lazima uwe makini na mazungumzo yako.

Ratibu vyema mazungumzo yako ili safari yako ya utashi wa kihisia iweze kuimarika.

Wednesday, August 23, 2017

UDHIBITI BINAFSI

Nafsi isiyo na udhibibiti binafsi ni sawa na mji usiokuwa na kuta

Moja ya changamoto kubwa ya kinafsi ni ukosefu wa udhibiti binafsi. Udhibiti binafsi na uwezo wa kinafsi wa kuratibu na kuzuia kila ambacho kinaweza kuingia katika nafsi husika na hapo ndipo tabia ya udhibiti binafsi inapokuja. Ulimwengu ni kama jalala yenye kila aina ya mambo, yenye kuharibu nafsi, yenye kujenga, yenye kuleta tabia na mitazamo asi au chanya, hivo ukitaka usalama wa kinafsi ni lazima uwe na udhibiti binafsi.

Haijalishi kwamba umepewa macho, kinywa au masikio, uimara wako unatokana na kutumia milango hiyo katika mambo ya msingi pekee. Udhibiti binafsi sio tu kudhibiti haja za mwili wako bali pia ni kudhibiti milango inayoingiza habari ndani yako. Huwezi kuwa na uimara kama ni mtu wa kutazama kila kitu, mtu wa kusikiza kila kitu, mtu wa kuchangia kila kitu, mtu wa kufatilia kila kitu au mtu wa kuongea kila kitu, hapana. Hautakuwa mtu mwenye utashi mzuri wa kihisia na hata kiakili.

Kuna tamaa za kinafsi kama shauku ya kutaka kufahamu mambo yasiyo na tija kwako, au kutaka kusikiza maswala yasiyoongeza thamani kwako au kutaka kufatilia watu wasio katika mlengwa wa yale yanayokuhusu. Ni tamaa tu ya kinafsi kutaka kuburudishwa na yanayowatokea wengine pengine hata kama hayana faida kwako. Usichofahamu ni kwamba unaijaza nafsi yako na mambo ambayo yanaongeza mzigo au yanakupa mtazamo ambao hauna tija kwako. Hakuna changamoto kubwa kama uchaguzi. Pale unapokuwa katika mazingira yanayokupasa uchague kuburudisha nafsi au kujenga nafsi.

Tafuta burudani ya kinafsi kwa mambo yanayohusiana na mambo ya msingi yanayokujenga. Kuwa na udhibiti binafsi, na wengi ambao hawana udhibiti binafsi wamejikuta katika matatizo mengi ya msongo wa mawazo au hata mikwaruzano isiyo na tija na watu wengine. Hata kama jambo lipo mbele yako sio lazima uburudishe nafsi yako kulifatilia. Hata kama hoja iko mbele yako sio lazima kuburudisha nafsi yako kuchangia. Hata kama maneno yanasemwa juu yako sio lazima kuruhusu nafsi yako kujibu, hata kama una shauku ya kuwafatilia watu sio lazima uruhusu nafsi yako kuwafatilia. Kama jambo badala ya kukusaidia linakujaza ujinga dhibiti nafsi yako na uliache.

Hakika usipokuwa mtu wa kudhibiti nafsi yako utakuwa mtu mwenye kubeba kila aina ya uchafu.

Tuesday, June 20, 2017

ITAJIRISHE NAFSI YAKO

Nafsi yako ni hazina kubwa maana ndio kiunganishi cha mwili wako na uhai wako au tunaweza sema roho yako. Nafsi yenye nguvu ni ile inayoweza kudhibiti fikra na kuratibu hisia na kuziweka katika mfumo utakaoleta tija katika maisha na tija kwa yale yanayokuzunguka.

Nafsi imara ni ile inayoweza kuchuja fikra na mawazo na kuhakikisha yanaleta mguso chanya kwa hisia ili zilete msukumo wa utendaji. Huwezi kuwa na nafsi imara kama haudhibiti fikra zako na kama hauratibu hisia zako. Hisia zinatakiwa zipokee msukumo chanya kutoka katika fikra zilizoratibiwa vizuri.

Utatu wa kinafsi yaani hisia, akili na utashi unahitaji kuchunguzwa na kila mwenye nafsi. Inapaswa kama binadamu uhakikishe sheria au misingi ya imani yako imejikita kujenga nafsi imara na sio nafsi dhaifu. Je ni mambo gani yanaingia zaidi katika nafsi yako, je watu wanaokuzunguka wana mguso upi katika nafsi yako? Hayo mambo ni ya kuchunguza sana.

Waweza kuitajirisha nafsi yako kiasi cha kwamba ikawa inatoa misimamo na hisia zenye uwiano, ni jambo lenye changamoto pale akili yako na hisia zikawa na mgongano katika namna inavogusa watu. Utashi wa kimawazo usio na utashi wa kihisia siku zote hauleti matokeo sawa. Unaweza kuwa na utashi wa kimawazo ila pasipo na utashi wa kihisia ukasababisha maafa makubwa.

Je mawazo yako yanaleta mguso gani wa kihisia. Waweza jua jambo lakini ukaliwasilisha likasababisha maafa au hata maudhi. Tajirisha nafsi yako kiasi cha kwamba utashi wako wa kiakili uuwiane na utashi wako wa kihisia. Nikupe mfano wa zawadi, ukipeleka zawadi kwa mtu na umeinunua kwa gharama siku zote lazima uifunge katika boxi la zawadi na uliwekee gift paper. Vivyo hivo ukiwa unatoa madini ya mawazo, ushauri na marekebisho lazima utumie utashi wa kihisia ili anayepokea afurahishwe na kuguswa na zawadi yako.

Hata Kama zawadi ulioifunga sio nzuri sana ila namna ulivoifunga inaweza ikamgusa mtu na akaipokea.

Tajirisha nafsi yako kwa kuweka uwiano katika ukuaji wa utaahi wa kihisia na utashi wa kiakili

Thursday, May 25, 2017

KUTOKA KATIKA UCHOVU WA KINAFSI

Uchovu wa kinafsi ni hali ya nafsi ya mtu kukosa nguvu ya kusimama ili kuweza kuhimili mitikisiko hasi. Ni hali ambayo kama ikiingia humjenga mtu kutaka ukombozi wa kinafsi na pumziko.

Kila uchovu unahitaji pumziko lakini njia za kupata pumziko ina utofauti. Kuna pumziko la kudumu na lile lisilo la kudumu. Watu wengi wamekuwa wakishindwa kutofautisha mapumziko hayo kutokana na kukosa taswira hada hasa pale uchovu unapokuwa mkubwa.

Changamoto kubwa ni uchaguzi wa pumziko la nafsi yako maana waweza fanya uchaguzi wa kudumu au wa muda mfupi ambao utakupa uchovu mkuu baada ya ganzi ya pumziko hilo kuisha.

Ili uweze kuchagua pumziko la kudumu ni lazima ujue chanzo kikuu cha uchovu wako wa kinafsi maana vichocheo vya uchovu huo mara nyingi ni kama mchwa ambao hukula taratibu nguvu yako ya kinafsi na kukuacha mchovu.

Unaweza pata uchovu wa kinafsi pale unapojaribu jambo linashindikana au pale unapotaka kubadili jambo inashindikana, unapotaka kubadili hali fulani lakini inashindikana au inaweza ikawa jambo fulani linakushambulia kila wakati ambalo unajaribu kuliepuka, au yawezakana ni watu ndo wanakupa uchovu wa kinafsi pale wanapoila amani yako, wanaposhambulia nguvu yako ya kusimama, na kutenda yale yanayovuruga misingi yako. Unaweza pata uchovu wa kinafsi na pengine ukajaribu kupata pumziko lakini ukashindwa katika uchaguzi wako ni lipi pumziko hasa unalohitaji.

Ukishindwa kujua hasa ni pumziko gani unalohitaji waweza jikuta unapata pumziko la muda mfupi ambalo likawa kama kilevi cha nafsi kisichokupa suluhisho la kinafsi la kudumu bali kinakupa nafuu ya muda mfupi tu.

Ukitaka kuondoa uchovu wa kinafsi siku zote jaribu kujitia nguvu kwa kuelekea zaidi pale ambapo panakutia nguvu, panakupa amani, panakupa mguso chanya, pana uwiano na kile unachokiamini, na pana misingi ya kiutu yenye uhusiano na nafsi yako.

Uchovu wa kinafsi humkuta kila mtu kwa wakati fulani lakini tofauti inakuja katika uchaguzi wa mapumziko. Waweza jikuta unajiingiza katika pumziko la muda mfupi ambalo badala ya kuitia nguvu nafsi yako linazidi kukudhoofisha.

Chagua vyema pumziko la nafsi yako ili uweze kuushinda uchovu wa kinafsi.

Thursday, May 18, 2017

IMANI NI MSINGI WA AMANI YA NAFSI

Imani ni kuwa na hakika ya mambo yasiyoeleweka au ambayo hayajabainishwa kwa wakati huo. Imani hukupa nuru ya kutambua mafumbo ya kinafsi na maswali yasiyo na majibu yenye kuleta taharuki katika nafsi.

Nafsi inaweza kupitia mambo fulani ambayo yanaikosesha amani na kuifanya ibaki katika hamaki kutojua ni nini kinachofuata au nawezaje kutoka katika hali fulani ya mkwamo wa kihisia au kimtazamo na kiakili. Hapo ndipo imani huja kuleta amani.

Imani inatakiwa iongoze hisia na iziweke katika hali ya utulivu. Ni vigumu kupata tulizo la kihisia bila kuweka mfumo bora wa kiimani, Ukitazamia kutoka katika mkwamo huo, ukitazamia utulivu wa hisia na ukitazamia uzuri na mambo mema yajayo.

Muda wote imani hujengeka katika msingi imara wa hatma ya kesho yenye furaha, faraja na uzuri na pia hujengeka katika faida ya leo katika mazingira hayo magumu. Imani hutazama fundisho, hutazama uzuri na  hutazama uimara unaotokana na ugumu na changamoto husika.

Siku zote ukitaka kuwa na amani katika nafsi yako boresha mfumo wako wa imani, boresha mfumo wako wa kuamini, jikite katika kutengeneza imani zenye tija, imani zenye kukujenga na kukuimarisha. Na ukishapata msingi husika iache imani hiyo iamuru hisia zako zitii.

Imani ikisema nitatoka katika hii hali, ikasema nitavuka katika hili daraja la maumivu, ikasema nitapata kilicho bora, Hakuna hisia ya maumivu itakayoweza kukushikilia kwa muda mrefu au hata kukuzamisha. Utakuwa ni mtu mwenye amani muda wote.

Thibitisha imani zako kwa kuzipa msingi imara kwa kuzifanya sheria za nafsi yako. Imani juu ya uzuri wako, imani juu ya stahiki yako na yale unayoyatarajia na yenye kukupa amani ya nafsi, hakikisha unajijenga na kujithibitisha katika imani hizo kwa kusimama bila kuyumba kama hisia za taharuki na uchungu zikija.

Huwezi kuwa na amani ya nafsi kama huna imani na hali fulani, kama huna imani na jambo fulani, kama huna imani na watu fulani. Ni vyema ukajiimarisha katika imani na siku zote hakikisha imani yako inajengeka katika kweli. Huwezi jenga imani kwa kitu cha uongo. Imani lazima isimame katika misingi ya kweli, fikra chanya, ubora wa nafsi na utu.