Wednesday, November 23, 2016

MAKE YOUR THOUGHTS FUTURE ORIENTED

One of the greatest challenges to thinking is the directions of your thoughts, Are your thoughts future oriented or past oriented? Is the direction of your thoughts forward or backwards? Backward oriented thoughts are a resistance to future pursuit. The quest to the future needs a future oriented mindset.

If you are constantly thinking backwards rather than thinking forwards then you create a resistance in your forward movement. When you think backward you create a force that pulls you backwards to the past. But if you think forward you create a force that pulls you forward to your future.

You can never move in a direction where your thoughts aren't directed, Don't ever fall in the trap of the mind of thinking backwards. Thinking backwards is thinking about things past, its entertaining past thoughts, its your reluctance to delete the past from your system. The duty of the past is to give you a motivation to create a platform for the future you want. Once you find the gear of the future, drive in the future mode and set your mind there.

Never inter-change your present gear with your past gear, its dangerous, You can only change your present gear with your future gear to increase the momentum and increase a boost of enthusiasm. How do you inter change present gear with future gear....Its by consuming some of the future ideas and dreams and instill them in the present, You cant consume all of them or else your present will be crowded and you wont find pleasure in the process

Its very important to think forward, just analyse yourself in the times you sit down to think what are the directions of your thoughts? Present, Past or future. Ask yourself also when you want to act on something and thoughts come in your mind in your analysis where are those thoughts from? Past or future... If you realise that its your past that brings out most of your thoughts then its time to change.

Make the future be the source of your thoughts and let the future interchange gears of motivation in your quest to pursue life.

Monday, November 21, 2016

KIWANGO CHA MAANDALIZI YAKO KIKOJE?

Kuna dhana inayosema njia pekee ya kutabiri hatma yako ni kuitengeneza na ukishindwa kujiandaa unajiandaa kushindwa. Ni dhana zenye ukweli kabisa katika maisha yetu ya kila siku. Maandalizi ni jambo ambalo linaweza kukuonyesha hatma ya mchezo, yawezekana dhana hii isiwe na uhalisia wa jumla katika maeneo mengine hasa pale watu wanapojiandaa lakini bado wanashindwa. Jambo la muhimu ni je unajiandaa kwa kipimo gani na pia unajiandaa katika msingi upi.

Kutokujiandaa na kujiandaa kwa jambo lisilo na uwiano na hatma yako inaweza leta changamoto sawa jambo hilo linapofika. Kuna mambo yanaweza fika ukashindwa kuyahimili kwasababu hukuwa na maàndalizi imara kuyahimili hayo mambo.

Nataka nizungumzie juu ya maswali ambayo watu wanakuwa nayo hasa wanapokuwa wakisubiria jambo fulani litokee, mara nyingi hukaa wakitazama wengine ambao wanategemea jambo hilo hilo au lenye usawa wa namna hiyo wakisonga mbele na kulipata huku wao wakiendelea kusubiri, Maandalizi yanaweza kuwa ya muda mrefu au muda mfupi inategemea na uzito wa jambo lako.

Ukienda katika sehemu ya mgahawa ukaagiza chakula cha thamani sana au chakula kinachohitaji maandalizi utasubiri sana na pengine utashangaa mwingine anayekuja kuomba kinywaji akiandaliwa na kupata mapema, ukadhani labda unafanyiwa makusudi, hapana maandalizi ya chakula chako yanahitaji muda kwasababu umeomba chakula kinachohitaji umakini, muda na uwekezaji mkubwa kukiandaa, hivo haimaanishi kuwa umefanya makosa kuagiza chakula hicho.

Wengi wamejikuta wakibadilisha matazamio yao na kuamua kufanya mambo tofauti na matazamio yao kwasababu maandalizi yao yamekuwa ya muda mrefu. Tatizo halikuwa katika muda wa maandalizi bali tatizo lilikuwa katika uwezo wa kusubiri na misukumo ya kulitwaa jambo lile kwa wakati huo.

Cha msingi ni kuhakikisha unajiandaa katika kila jambo unalolihitaji, usiseme nitajiandaa hilo jambo likija, muda mwingine unaweza jiandaa lakini usifanikiwe kwa wakati huo, haimaanishi maandalizi yako hayakuwa na mantiki, hapana endelea na maandalizi. Katika maandalizi kuna tabia zinaimarika, kuna uwezo unajengeka ndani mwako ambao utakuwezesha kuwa na ufanisi katika hilo jambo litakapokuja.

Tambua kwamba maandalizi siku zote ni jambo endelevu, usichukie vipindi vya maandalizi na kila wakati jua unajiandaa kwa jambo fulani. Haijalishi maandalizi yako yanachukua muda gani. Usiupime muda wa maandalizi pima kiwango cha maandalizi yako. Maandalizi huongeza thamani yako na uwezo wako

Sunday, November 20, 2016

LEARN TO IGNORE

The race of life is the one with a lot of obstacles, a lot of hindrances and a lot of oppositions, we all know that and we all have experienced that at some point in life, but there comes the most critical of all a lot of intimidations. If you havent master the art of ignoring voices then you will always fall victim.

When you are walking your walk always know that there are people who will come to intimidate you and try to misfocus you with words. Listen always be ready for that for people will hit you where it hurts you the most, sometimes even people you cant imagine but always guide your heart and mind. Many have grabbed a victim mindset simply because they take everything thrown unto them personal

Don't be intimidated...Learn to ignore, choose not to give full attention to distractions, Its obvious that some will be people very close to you in whom there opinions can have a big impact in you, but one of the greatest thing you need to do is detach yourself from the emotions brought about by people. Its true that you might sometimes fall prey in the predatorial world but stand up, ignore the predators and move on. What doesnt kill you makes you stronger.

Just because people are close doesn't mean that their opinions of you will always be right. Don't let the pressure get into you...Don't be intimidated, learn to ignore the impacts of their words. Learn to ignore, Ignore the negative feelings, ignore the negative emotions. Ignore what seems to bring you down. I challenge you to ignore those voices that keep running through your mind all the times telling you that you are somebody's victim. No you arent. Train your mind to cancel off and ignore.

Say to yourself, i choose to ignore all distractions. One African proverb says a lion doesn't turn back when dogs bark, also the noise of frogs doesn't hinder the elephant from drinking water from the stream. When you have an understanding of what people go through then it wont trouble you when they voice out their opinions out of emotions. Just ignore and move on. Choose to mind your own business and move on. No need to give an airtime to the calls that dont compliment you. Focus on the good. 

Monday, November 14, 2016

USITAFAKARI MAJUTO, TAFAKARI FUNDISHO

Katika maisha tunapitia mambo mengi, njia nyingi na tunakutana na vitu vingi, nafasi nyingi na hata vipindi vingi ambavyo tunatakiwa tufanye maamuzi juu ya mambo kadha wa kadha tunayokutana nayo. Kama binadamu wenye uhuru wa kufanya uchaguzi na utashi kila wakati huwa tunatumia njia zozote zile tulizonazo kufanya maamuzi.

Maamuzi yetu ndiyo ambayo hutengeneza hatima ya maisha yetu au matokeo yanayokuja baada ya hapo. Maamuzi mazuri huleta matokeo mazuri na maamuzi mabaya pia huleta matokeo mabaya. Kila mtu ameshapitia hali ya kufanya maamuzi na kila mtu ametumia uhuru wake wa kinafsi kufanya maamuzi. Changamoto kubwa ni matokeo ya maamuzi yetu na jinsi tunavopokea matokeo ya maamuzi yetu.

Maisha siku zote ni safari endelevu yenye changamoto mbali mbali na safari hiyo huwa vumilivu pale inapoendeka kwa maarifa na ujuzi wa wapi unaelekea. Maisha huhitaji dira na dira ndo itakuelekeza kasi ya kwenda nayo hata njia za kupita kufikia hatma yako. Maarifa ni muhimu sana.

Mara nyingi tumekuwa na mapokeo tofauti tofauti ya matokeo ya maamuzi yetu ambayo wengi wetu yametusababishia kukwama kwa muda mrefu katika dimbwi la maumivu na tukaishia kulalamika, kulaumu, kuwa na mitazamo hasi na hata kupata matatizo mbali mbali ya nafsi. Mara nyingi tumekuwa watu wa majuto badala ya mafunzo

Jambo la muhimu ni kutafakari mafunzo uliyoyapata na uyatumie hayo kama mawe ya kukanyagia kwenda mbele, usikae unajilaumu au unatafakari kwa makosa ya nyuma hata kama yameleta matokeo mabovu katika maisha, badala ya kusema ningejua tafakari aya sasa umejua utafanya nini. Huwezi kubadilisha makosa ya nyuma ila unaweza kufanya mabadiliko ili makosa ya nyuma yasijirudie.

Wengi tunakaa zaidi tunatafakari majuto badala ya kutafakari mafunzo na kufanya yanayohitajika kusonga mbele halafu baadaye unajikuta unarudia kosa lile lile au unapita tena njia ile ile. Badili mtazamo hata kama matokeo ya maamuzi yako mabaya yanaendelea kukutesa kuwa na ujasiri wa kusema nitafanya hivi badala ya ningefanya hivi.

Kumbuka kila mtu ameshafanya kosa fulani ambalo limemgharimu au linamgharimu hadi sasa lakini cha msingi ni kutafakari funzo badala ya majuto.

Thursday, November 10, 2016

KUDHIBITI HISIA HASI

Magugu siku zote huota hata sehemu ambazo hazitakiwi, hayaitaji mbegu..yenyewe huota bila kupandwa wala nini, vivo hivo na hisia hasi, huwa haziitaji kazi kubwa kukaa katika nafsi yako. Zinaweza kukuhijia wakati wowote na kwa namna yeyote lakini hisia chanya zinahitaji kupangiliwa, kurutubishwa na kupaliliwa.

Moyo wako kuna wakati unaweza patwa na hisia hasi ambazo zinakuja kutokana na jambo lolote, inawezekana ni uchovu wa kimwili au kiakili, mtu fulani kukukatisha tamaa, mtu fulani kuzungumza na wewe vibaya nk...yamkini ni mtu wako wa karibu, au mtu ambaye ana mguso wa tofauti ndani ya moyo wako. Lakini ni vyema ukatengeneza mzani wa kupima hisia hasi na kuzikata badala ya kuzipa hifadhi kwa muda mrefu ndani yako.

Ukizipa hifadhi kwa muda mrefu zina tabia ya kuchoma nafsi yako na kila zikichoma nafsi yako zinakujengea hali ya kutaka kuzitoa. Na hapo wengi wamejikuta wakizitoa kwa msukumo unaosababisha maafa zaidi. Njia pekee ya kuzidhibiti hisia hasi ni kupumzisha nafsi yako kwa muda huku ukijaribu kuingiza hisia chanya.

Hisia chanya zinahitaji nidhamu kuziimarisha ndani ya nafsi yako, kwasababu asilimia kubwa ya watu wamezungukwa na mazingira hasi mfano ndugu walalamishi, marafiki wasiojali, wapendwa wasiokuelewa na wasioheshima uhuru wako na furaha yako. Inabidi ujipe likizo ya kinafsi. Ikiwezekana jijengee utaratibu hata wa kufunga kuendekeza hisia hasi kwa kipindi fulani kama jinsi ambavyo dini hufunga chakula au starehe fulani waweza funga kutoziendekeza hisia hasi.

Jenga utaratibu katika maisha yako wa kutozipa hifadhi hisia hasi wala kuziendekeza kwa muda mrefu. Hisia ni mfano wa mimea, kuna mimea bora na kuna magugu. Hisia hasi ni kama magugu. Tafuta kuwa mtu mwenye hisia chanya kila wakati. Ni sawa na chumba chenye uchafu na kila aina ya takataka...usipoweza kuondoa visivohitajika, chumba kitajaa na hewa itakuwa haizunguki vizuri. Usipoweza kupunguza hifadhi ya hisia hasi ndani ya nafsi yako, nafsi yako itajaa na hewa nzuri ya mazingira chanya haitozunguka vizuri ndani yako.


Tuesday, November 8, 2016

INVEST IN YOURSELF

How do you picture yourself? How do you see your life? How do you see your soul? How do you see your spirit? Do you see any area you can add more value in you. There is still more you can add in your life. You still have room for more. Invest in excellence. You still have more you can add.

Listen when you stop growing you start dying. And dying can start from your soul, mind and even your spirit. You slowly start to settle for whats below you. You slowly start to settle for what doesn't compliment you. Listen challenges should boost you to invest in yourself more.

Negative thinking will just drown you in negativity. Choose to direct your thoughts towards creating value in life. You can still be the best version of yourself. Refuse to settle in despair. Life is bigger than that...rise higher. A country like america invested in every sector to be the world superpower. Invest in every sector of your life. Your health, your skills, your financial life. Invest more and let you be needed for the value you have.

Feed your faith and your fears will flee, choose to distinguish yourself...Don't fit in, fit out with character and excellence. Be the best version of yourself for when you do that you will always stand out with an impact. Commit yourself in being a person of value and character. Enrich your soul with everything needful for you. Don't settle down crying and complaining. It wont help.

Walk in wisdom, choose to be a man of excellence. Focus on being a person that impacts the world and inspire people. Be the best person you would feel great to be around. Doubts should not be part of you, worry should leave you. Let you soul free to enjoy the beauty of life without regrets. Any pain you have, use it for greatness. Don't drown in it. Use it. Your purpose is greater than anything.


Friday, October 28, 2016

IMANI YAKO HUJENGA KAWAIDA YAKO

Imani mara nyingi hutokana na uzoefu juu ya jambo fulani, uzoefu huo hujiimarisha katika ubongo wako na kutengeneza mfumo wa kisheria ambao utatawala mitazamo yako na utakujengea kawaida yako. Na mara nyingi kawaida hiyo hujenga utamaduni ambao utakusanya mambo ya kuthibitisha na kuendana na utamaduni huo.

Unapojenga imani fulani siku zote imani hiyo huvuta mazingira husika ya kuthibitisha imani hiyo. Mfano unapojenga imani kuwa katika mahusiano jinsia fulani sio ya kuaminika imani hiyo huvuta mazingira hayo, imani hiyo itakuongoza kuchagua watu wasioaminika na hata itakujenga kutafuta mazingira yasio aminifu katika mahusiano yako ili kuthibitisha imani hiyo.

Siku zote akili hujisikia furaha pale inapothibitisha mitazamo yake na malengo yake..ndio maana siku zote ukithibitisha jambo ulilokuwa na wasiwasi nalo hata kama linaumiza akili yako itasema nilijua tu....tafsiri ya neno nilijua ni kuipa thamani akili yako kwa uthibitisho huo na kuijengea thamani kwa imani hiyo.

Ni muhimu utambue kuwa unatakiwa kutafakari sana kabla hujakiweka kitu kama imani yako kwasababu imani hiyo itakutengenezea kawaida yako. Na siku zote kawaida yako ndio ulimwengu wako. Watu wengi wamejijengea kawaida mbaya hadi pale jambo zuri linapokuja wanalikataa na kuliona haliwastahili. Kuna watu wamejijengea kawaida kiasi cha kwamba jaribio lolote la kutoka hapo ni maumivu kwao.

Usijenge msingi wa kiimani ambao unaona kabisa ni asi kwasababu huo msingi utavuta mazingira ya kuthibitisha hayo uliyoyaweka kama sheria. Hakikisha kabla hujaliamini jambo na kuliweka katika akili yako litafakari. Usije kufungwa na kawaida ambayo itakutesa. Mfano mtu anaweza akaja kukwambia yaani mie kila mahusiano yangu naumizwa...unamuuliza je unadhani kwanini....mtu anakwambia mie nadhani nina mkosi au wanaume wote ni wahuni, au wanawake wote hawaaminiki...Tayari kishajenga imani ambayo inavuta mazingira kuthibitisha imani hiyo.

Ni jambo la muhimu sana kuongeza maarifa juu ya jambo usilolijua badala ya kujijengea imani ambazo zitakujengea kawaida yako. Pia ni kubadilisha taswira yako, ni nini hasa unaangalia au ni wapi hasa mtazamo wako ulipo maana taswira siku zote hukutengenezea imani itakayokujengea kawaida itakayovuta mazingira kuthibitisha mambo husika.

Tuesday, October 25, 2016

UTUMIE VEMA MUDA WA KUSUBIRI

Moja ya changamoto katika maisha ni pale ambapo matarajio yetu yanachelewa, pale ambapo unasubiri jambo fulani likamilike. Ni sawa na kupanda mbegu chini ya ardhi na kusubiri mti uchipuke. Muda mwingi tumekuwa tukiona wakati huo ni mrefu na hata kuingiwa na hisia za huzuni na kuchoka pale tunapoona matokeo yamekawia.

Inapaswa ujifunze kuwa wakati wa kusubiri huwa mrefu na wenye uchungu pale ambapo kwa muda huo unasimama katika mambo mengine huku ukisubiria. Hata mkulima huwa akipanda mbegu hakai akisubiria. 

Jizamishe katika mambo uyapendayo hadi usahau kuwa ulikuwa unasubiria jambo fulani.
Subira yenye furaha ni ile subira ambayo unaifanya huku unaendelea kufanya mambo uyapendayo. Hata katika mahusiano yakupasa kuwekeza pia kuhusiana na nafsi yako wakati uko katika mahusiano na mtu mwingine, mahusiano haimaanishi uiache nafsi yako katika ukame ukisubiria muitikio wa nafsi unayohusiana nayo.

Mfano umepanga kukutana na mtu na hajafika huwa unafanya nini huku ukisubiri?, mfano upo katika foleni sehemu huwa unafanya nini ukisubiria?, mfano umeingia katika mgahawa chakula kimechelewa huwa unafanya nini ukisubiria? Dunia haitakiwi kusimama wakati wewe ukisubiria muitikio wa mtu au jambo. Endelea kufurahisha nafsi yako kwa kufanya yale uyapendayo la sivyo utakuwa unaingiwa na huzuni ukiona jambo linachelewa.

Unasubiri jambo gani katika maisha, iwe katika mahusiano au eneo lolote, usisimamishe dunia ya nafsi yako ukisubiria, kuna mambo mengi unaweza kufanya wakati unasubiria kuna vitabu hujasoma, kuna tabia na vipawa unaweza vikuza, kuna marafiki unaweza wasiliana nao, unaweza kwenda kutembea. Kuna mambo mengi nafsi yako ingependa kuyafanya na bado hujayafanya...tumia huo muda.

Jifunze pia kutembea na kitabu kidogo cha kunakiri mambo au yafundishe macho yako kuona uzuri wa mambo yanayokuzunguka, jenga akili ya kudadisi, andika mambo unayoyaona, changamoto mbalimbali, sikiliza audio za kukujenga, waweza enda kusaidia mtu mwingine, tembelea marafiki na jamàa na mzungumze, kuna sehemu unaweza itajika kusubiri muitikio wa jambo fulani, wewe endelea kuishi dunia iliyomo nafsini mwako.

Hata katika mahusiano watu wamekuwa wakilaumiana kwakuwa husubiri miitikio ya watu fulani lakini huchelewa kuitikia, wakati unasubiri waweza fanya mambo mengine, waweza andika mambo yanayokufurahisha katika mahusiano nk, jizamishe katika mambo ya nafsi yako na vipawa vyako, wekeza katika ufahamu wako.

Sunday, October 23, 2016

TENGENEZA MKONDO MZURI WA MAWASILIANO

Moja ya changamoto katika maisha ni pale tunaposhindwa kutengeneza mkondo mzuri wa mawasiliano na hii upelekea mikwaruzano na hata hali ya taharuki na hata hali ya mashaka juu ya mustakabali mzima wa mambo.

Mahusiano pasipo mawasiliano mazuri ya kinafsi ni chanzo kikubwa cha huzuni na hata kuumizana, waweza kuwa na nia njema lakini ukishindwa kutengeneza mkondo mzuri wa mawasiliano unaweza eleweka vibaya. Au unaweza kumuumiza mtu mwingine, ni muhimu sana ukawa mtu wa kuwa unazungumza.

Ni lazima ujenge hali nzuri na msingi imara ili uweze kuwasiliana na mwenzako au yule ambaye unataka kuwasilisha kile unachoona kinakutatiza. Wakati mwingi huwa tunadhani kwamba ni lazima tutafute misamiati mizuri ya mawasiliano, ni kweli pia kuna wakati unaweza kuwasilisha jambo fulani likapokelewa usivyodhania ndo maana kuna wakati unaweza kuwa na hofu fulani.

Ni muhimu kujenga msingi wa uwazi na ukweli na uwe huru maana pasipo uhuru wa nafsi juu ya jambo fulani huwezi kujenga mkondo mzuri wa mawasiliano ndio maana ni muhimu kuwa na msingi mzuri wa kihisia ukitaka kuwa na mkondo mzuri wa mawasiliano...Tambua ya kwamba unapokuwa huru kuzungumza ndio utakuwa na uhuru wa kuwa vile unavotaka.

Kuna sauti nyingi ambazo zinaweza kuja katika akili yako kukuzuia kujenga mkondo mzuri wa mawasiliano, kukosa amani ya nafsi, hofu au hata kutotaka kufikiriwa au kutazamiwa vibaya ndio maana inakupasa uwe na uhuru na amani ya nafsi na utambue kuwa wewe ni nafsi huru na unatakiwa uwe huru kuwasilisha yaliyo katika nafsi yako.

Jifunze kuzungumza kama unadhani huwezi kuzungumza yaliyo ndani ya nafsi yako, tambua nafsi yako ina uzuri na ukuu ambao kama ukishindwa kuzungumza inakuwa vigumu kueleweka....iache nuru yako ing'ae...usihofie kuzungumza. Usipozungumza unaweza jikuta upo katika hali ya taharuki na ukaishi kama mfungwa wakati ukisema ukweli utakuwa huru

Hekima ni kutambua njia na muda muafaka wa kuzungumza lakini mawasiliano ya nafsi ni jambo la msingi sana, yatakuweka huru. Ukitaka sana kufurahisha watu pia inaweza kuwa changamoto yako kuzungumza, pia usipotaka kuwaumiza watu inaweza kuwa changamoto yako kuzungumza lakini ni vyema ukawa huru katika nafsi.

Monday, October 17, 2016

BADILI TASWIRA WAKO

Changamoto kubwa katika maisha ni kuwa na mitazamo mibovu. Taswira uliyonayo juu ya mambo inatokana na hazina uliyoweka moyoni mwako. Jinsi unavowekeza ndani yako ndo jinsi unavojenga taswira nzuri katika maisha yako. Mambo unayoyaona mazito kwako inatokana na nguvu au hazina uliyowekeza ndani yako.

Usipowekeza katika kukua siku zote hautakuwa mtu mwenye taswira nzuri....ukiwa na hazina ndogo au nguvu ndogo ya kiroho siku zote taswira yako itakuwa na tatizo...na ukikosa taswira nzuri utakuwa ni mtu mwenye kulaumu na kuona kama maisha hayakutendei haki. Maisha yapo siku zote lakini wenye nguvu ndio wanaoweza kustahimili hivo wekeza kuwa na nguvu katika nafsi yako.

Chukua kila tatizo linalokuja kwako na ulione kama jiwe la kwenda kiwango kingine. Chukua maumivu na uyaone kama fursa ya kujiimarisha zaidi roho yako. Usilalamike, wewe ni kiongozi wa maisha yako na kila jambo hufuata mkondo unaouweka wewe. Hukuzaliwa umfurahishe kila mtu hivo acha kufungwa katika mawazo au shuruti za watu. Unatakiwa uwe huru.

Ili taswira yako iwe nzuri ibadilishe, unapokuwa unatafuta taswira ya picha na camera lazima uhakikishe picha ya maisha yako unaiweka katika mraba, kuna vitu vya kuondoa katika taswira hiyo, unaweza kubadili umbali nk. Vivyo hivo katika maisha yako ukitaka upate taswira unayoitaka kuna watu inabidi uachane nao, kuna mambo inabidi uachane nayo, kuna vitu inabidi uviondoe katika taswira. Haijalishi vikoje kama unaona havipo katika taswira yako yakupasa uviondoe.

Usipokua, siku zote taswira yako itakuwa ndogo, kuna mambo mengine hujayajua au kuna mambo mengine huyaoni kwasababu huna taswira nzuri na hii hutokana na kutokuwa na hazina na nguvu ndani yako.


Thursday, October 13, 2016

SAUTI TATU KATIKA MAHUSIANO

Mahusiano yetu huguswa na sauti ambazo zinaleta changamoto na ni sauti ambazo zinamchango katika uimara wa mahusiano yako au kuanguka kwa mahusiano yako. Bila sauti hizo kuwa katika uwiano  sawa basi sauti moja ikiizidi nyenzake inaweza sababisha changamoto.

Sauti hizo zimegawanyika katika makundi matatu, ya kwanza ni sauti ya nafsi ; Hii ni sauti ambayo kila mtu anakuwa nayo kiasili nayo ni sauti ya uhuru, furaha na amani. Kila nafsi inataka kuwa katika uhusiano ambapo itakuwa huru na yenye furaha na amani, sauti hii inalia kutoka ndani ya nafsi ya mtu na ndio maana kuna ambao husema kuwa katika uhusiano ambao utakuwa huru na mwenye furaha na amani.

Sauti ya pili ni sauti ya Jamii; hii ni sauti inayotoka katika jamii inayotuzunguka juu ya mahusiano yetu. Hii sauti inaweza ikawa sauti ya wazazi au sauti ya malezi na makuzi ambayo tumeyapitia. Sauti hii mara nyingi hutuambia kuwa ni nani anatufaa, au ni nani tunatakiwa tuwe naye au ni mahusiano gani ambayo inabidi tuwe nayo.

Sauti ya tatu ni sauti ya akili zetu; Binadamu huwa na hali ya kupenda kutafakari na kutumia akili katika kufanya maamuzi na pengine kuna wakati hutumia zaidi akili katika mambo fulani juu ya nini hasa jambo sahihi la kufanya.

Ili kujenga uhusiano imara lazima hizi sauti ziwe na uwiano...sauti ya nafsi inabidi iwe kama msingi itakayobeba sauti nyingine zote. Sauti ya nafsi ikizifunika sauti nyingine zote unaweza pelekea kufanya mambo ambayo yanaweza kutokubalika katika jamii na ukajikuta unakosa kabisa ushirikiano na wengine lakini sauti ya jamii ikiizidi sauti ya nafsi utajikuta unaingia katika mahusiano ambayo katika jamii unasifika lakini ndani ya nafsi yako unakosa furaha na unakuwa na upweke ambao jamii haiwezi kukusaidia.

Pia inakupasa sauti ya nafsi iwe na uwiano na sauti ya akili ili akili yako iweze kuwekeza zaidi...maana nafsi na akili zikiwa na uwiano ile amani na furaha hudhiirika katika fikra za ubunifu zaidi katika kuimarisha mahusiano hayo.

Kama unaona sauti ya jamii ni kubwa na inakutisha hakikisha sauti ya nafsi na sauti ya akili vinaungana kuishurutisha sauti ya jamii itulie.

Changamoto na jambo la msingi kwa kila mtu ni kuhakikisha hizo sauti zina uwiano ili kujenga mahusiano imara.


Monday, October 3, 2016

TAMBUA UNACHOTAKA KATIKA MAISHA

Moja ya changamoto kubwa ambayo watu wengi huwa tunayo ni kutofahamu nini tunachotaka au tunachohitaji katika maisha. Watu wengi hudhani wanajua wanachokitaka au wanachokihitaji lakini ukiangalia matendo yao utatambua kuwa wengi hawajui wanachokitaka katika maisha. Usipojua unachotaka katika maisha utakuwa ni mtu wa kuzunguka zunguka kujaribu jaribu kila kitu kuona kina mguso gani kwako.

Kuna dhana nyingi sana ambazo tunazo ju ya yale tunayotaka katika maisha na unaweza ukapewa kila ulichodhani unakitaka kisha ukaja kugundua kuwa bado kuna kitu kingine unachokitaka. Na utakuwa ni mtu usiye na furaha wala amani kwasababu hujui unachokitaka. Pengine hata ukawa mtu mwenye lawama katika kila jambo kwasababu wewe mwenyewe hujui unachokitaka.

Pengine pia unaweza jua unachokitaka lakini unadhani ni jambo la kufikirika, huo mtazamo unaweza kukufanya ukaendelea kuwa kama mtumwa anayezunguka jangwani asijue anapoelekea. Kuna mwanafilosofia mmoja aliwahi kusema kuwa Watu wengi hawajui wanachokitaka hadi uwaonyeshe wanachokitaka. Ni muhimu sana kujua unachokitaka.

Njia pekee ya kujua unachokitaka ni kujitathmini nafsi yako na kujitambua utu wako ndipo utajua ni nini unachohitaji. Mwanafilosofia mmoja aliwahi kusema kuwa kama hakuna adui ndani adui wa nje hawezi kutudhuru. Nafsi yako ya ndani imeundwaje? Pengine ushawahi kujiuliza ni jambo gani linakupa amani na unaamini ndio jambo ambalo ukilipata kama msingi wa maisha yako utaweza kupata mambo mengine yote?

Kila nafsi inahitaji uhuru na amani na furaha na wengi wetu tumedhani tukipata vitu basi nafsi yetu ndo itakuwa imepata inachotaka. Hapana!! Nafsi yako inahitaji kukua na jambo lolote linaloweza kuinyanyua nafsi yako ndilo jambo unalohitaji. Nafsi yako inahitaji thamani na jambo linaloweza kuipa thamani nafsi yako ndilo unalohitaji. Nafsi yako inahitaji amani na jambo lolote linaloweza kukupa amani ya nafsi ndilo unalohitaji.

Ukishajua msingi hasa wa mahitaji ya nafsi yako itakuwezesha kutambua ni nini unachohitaji katika maisha, iwe ni katika uchaguzi wa kazi, iwe ni katika mahusiano au nyanja yeyote ya maisha. Utatambua marafiki wa nafsi yako, utatambua hata mwenzi wa nafsi yako, utatambua hata kusudi la maisha yako.

Saturday, October 1, 2016

USIOGOPE KUKUTANA NA HOFU YAKO

Moja ya changamoto tunazopitia katika maisha ni hofu ya kukutana na hofu zetu na hofu ya mguso utakaotokana na hofu zetu. Huwezi kuwa huru kutoka katika hofu unayohofia kukutana nayo. Siku zote kuwa tayari kukutana na hofu zako na jivike ujasiri wa kuweza kuzidhibiti hofu zako.

Katika maisha lazima uwe na ujasiri wa kusonga mbele na kujua kuwa iko siku utakutana na hofu zako. Lazima ujipange jinsi ya kukabiliana na hofu yako na uwe jasiri maana hofu yako siku zote ndio gereza lako. Kuna wakati katika maisha inakubidi kuvuka daraja lenye kutia hofu kwa ujasiri ukitazamia maono uliyonayo katika maisha.

Amani ya nafsi ikishakaa ndani yako itakupa ujasiri wa kukabiriana na hofu yako ndio maana mwanafilosofia mmoja aliwahi kusema kuwa kama hakuna adui ndani ...adui wa nje haweza kutuathiri. Na hapa anapozungumzia adui sio lazima awe adui anayekupinga bali kuna maadui wa furaha yako na maono makubwa ambao wanaweza kuja kama watu wa karibu wakikushauri au mazingira fulani yakikukwamisha.

Lazima ujivike ujasiri na useme kwa jambo lolote nitasonga mbele na niko tayari kukutana na hofu yangu. Bila kuwa na huo ujasiri hofu yako itaendelea kukuzuia kusonga mbele. Na njia pekee ya kuweza kuishinda hofu yako ni kuwa mkweli kwa nafsi yako, kuwa mkweli kwa kile nafsi yako inataka na pia kuikubali amani iliyo ndani yako maana amani ya nafsi siku zote ni ya msingi sana. Ukisha kuwa mkweli uweke wazi ukweli ulio ndani yako, usiuogope, wala usiogope jinsi watu watakavoupokea huo ukweli.

Njia ya maisha siku zote ni ya kufanya maamuzi na kusonga mbele. Muda wa kukaa kutafakari kwa sababu ya hofu iliyo mbele yako ni kujikwamisha mwenyewe. Songa mbele kama una imani na kweli iliyo ndani yako. Amini tu kwamba kila jambo linafanyika kuwa jema. Maamuzi siku zote hutujenga, pasipo maamuzi tutaendelea kukaa katika hali ya mazoea ambayo pengine yangekuja kutuumiza.
Kuwa jasiri na Hofu zako zitakimbia. Usipokuwa jasiri hofu zako zitaendelea kukufunga sehemu ulipo.

Thursday, September 22, 2016

UHURU NA UDHIBITI WA KIHISIA

Uhuru wa kihisia ni pale unapoweza kudhibiti na kuelekeza hisia zako katika muundo na mpangilio uutakao. Hili si jambo rahisi kwa maana hisia huja kutokana na mabadiliko ya ndani ya mwili na hata hujengeka katika msingi wa nafsi ya mtu hivo uhuru wa kihisia unawezekana pale tu unapojenga tabia inayoitwa Nidhamu.

Nidhamu itakuwezesha kudhibiti hisia zako kwa namna kwamba utaweza kuzielekeza au kuamua muitikio na hata namna ya kukabili hali fulani zinazojitokeza. Uhuru wa kihisia kwanza unajengwa na kuitambua nafsi yako....nguvu na mapungufu yake kisha kujenga msingi wa kimaamuzi unaotokana na sheria utakazozijenga katika akili yako.

Hisia ni kama upepo, huja na hupoa na pengine hata kupotea kabisa, upepo huo unaweza kuwa kimbunga kwako au unaweza kuwa kama kipupwe kutokana na misingi ya kinidhamu ulioijenga katika nafsi yako ambayo inakupa uhuru wa kuamua jinsi hisia zako zinavodhibitiwa. Kudhibiti hisia ni sawa na kujenga mifereji ili kudhibiti mikondo ya maji isilete madhara au isielekee kusikotakiwa.

Ukiwa mfungwa wa hisia inamaana utendaji wako au muitikio wako katika mambo utatokana na msukumo wa hisia ulizonazo. Umeshawahi kuwa hisia nzito juu ya mtu fulani au jambo fulani kwa wakati fulani na ukatamani kulifuatilia lakini baada ya muda unapoteza hiyo hisia? Na hii hasa ndio changamoto ya kufanya maamuzi kwa kufuata hisia.

Jenga utaratibu wa kinidhamu wa kuratibu hisia zako kisha zielekeze kuongeza msukumo ktk sheria ulizozijenga na wala usiruhusu hisia zako zikuelekeze kupingana na sheria zako...namaanisha usiruhusu hisia pinzani zipate nguvu. Hisia zote zielekeze unapotaka ziende. Na hii inahitaji mazoezi.

Warren buffet aliwahi kusema kuwa mtu asiyeweza kudhibiti hisia zake hawezi kudhibiti pesa zake. Na hilo ni jambo la kweli kabisa, usipoweza kuwa nidhamu ya kihisia huwezi kuwe na nidhamu ya kiuchumi

Pia usipokuwa na uhuru wa kihisia utakuwa mhanga wa maumivu mengi ikiwemo mahusiano au hata namna watu wanavoleta upinzani katika maisha yako. Watu wasio na uhuru wa kihisia mara nyingi hushindwa kuchanganua ni aina gani ya mahusiano ni mazuri kwao na yatakayowajenga, kwao hisia zikishatawala wanashindwa hata kuruhusu akili zao kuchanganua.

Maisha bila uhuru wa kihisia ni kama msitu maana kila aina ya mabadiliko yatakuwa na mguso kwako na utataka kuitikia kila ambavyo hisia zitakutuma. Lazima uwe huru kuzidhibiti hisia la sivyo zitakuzamisha.

Saturday, September 17, 2016

JENGA MSUKUMO WA NDANI

Binadamu yeyote hutenda mambo kutokana na msukumo fulani. Misukumo iko ya aina mbili. Kuna msukumo wa nje na msukumo wa ndani. Watu wengi hutenda mambo kutokana na msukumo wa nje ambao unahusisha mazingira fulani au faida na matokeo fulani. Sio jambo baya kuwa na misukumo ya nje inayopelekea wewe kutenda jambo lakini changamoto ni kwamba ukiwa na msukumo wa nje zaidi inaweza pelekea kuwa na mguso tofauti.

Misukumo ya nje inaweza kubadilika muda wowote na hii itakupelekea kupoteza kabisa ile ari ya utendaji. Unaposukumwa kutenda jambo kwa ajili ya faida fulani itapelekea kuwa na hamaki pale hasara inapokuja au kukosekana kwa faida husika. Ukisukumwa zaidi na mazingira jua hayo mazingira yanaweza kubadilika muda wowote mfano unaweza pangiwa kutoka Dar es salaam kwenda dodoma. Hii itakusumbua sana katika kupata uwiano wa kihisia.

Ni muhimu kujenga msukumo wa ndani uliojengwa katika msingi wa mambo matatu..Moja ni Uongozi wa maisha yako, Thamani na mwisho ni kusudi.

Uongozi wa maisha yako ni msukumo wa ndani ulio na mtazamo na uthibiti wa muelekeo wa maisha yako. Ukijua ya kwamba wewe ndio mwenye jukumu ya kutengeneza muelekeo wa maisha yako itakupa msukumo wa utendaji kwa maana utajua kila wakati kuwa unalolifanya linatengeneza muelekeo wa maisha yako.

Thamani ni msukumo wa ndani uliojijenga katika mtazamo kuwa kila jambo unalolitenda unalifanya ili likujengee uwezo na ufanisi, likufanye mtu mwenye uwezo zaidi na mwenye ufanisi zaidi...uwe mtu wa thamani na bora. Ndio maana faida kubwa katika kazi sio unachokipata baada ya kazi bali ni unavokuwa baada ya kazi ( Thamani yako)

Kusudi ni msukumo wa jambo uliojijenga katika mtazamo kuwa unafanya jambo kwasababu lina maana kwako na jamii inayokuzunguka. Utasukumwa kufanya jambo kwa sababu lina maana kubwa ndani yako na kwa jamii yako.

Ukiwa na misukumo hiyo mitatu ya ndani katika kila jambo ulifanyalo, kila siku utakuwa na ari na msisimko kufanya mambo na hautopoteza hamu ya kuamka asubuhi kuiendea siku kwa furaha.

Thursday, September 15, 2016

ACHA YA JANA...ISHI YA LEO

Usiruhusu yale ya jana yachukue muda mwingi wa leo- Willy rogers

Moja ya changamoto kubwa katika maisha yako ya leo ni kumbukumbu ya jana yako. Jana yako unaweza kuitumia katika tathmini yako kukuwezesha kuwa na mtazamo chanya na wa fadhila hasa ukikumbuka ulipotoka na kushukuru kwa hapo ulipo huku ukitazama unapoelekea.

Changamoto kubwa ni pale jana yako inapochukua muda mwingi kihisia na hata kimtazamo kiasi cha kukufanya kushindwa kuiishi leo yako. Jana yako inaweza kuwa mtego wako hasa pale unapokuwa na hisia zilizoshikamana na jana hiyo. 

Kuna watu wengi wameshindwa kuachilia jana yao kiasi cha kutotazama fursa katika leo yao na kuacha fursa hizo zikipotea.

Wengi wameingia katika mahusiano leo na kumbukumbu la jana yao...Wengi wao wanataka kuishi leo lakini bado hawajaachana na jana yao. Ukiona unatamani sana jana ni dhahiri umepoteza dira ya leo na kesho yako. Kuna mambo mengi ya jana bado hutaki kuyaachilia na yamekuwa mzigo kwa leo yako.

Huwezi furahia leo yako kama jana yako inachukua sehemu kubwa ya moyo wako, akili yako na nafsi yako. Wengi leo wanaingia katika mahusiano huku bado hawajaacha kutazamia mahusiano ya jana yao. Wanajaribu hata kulinganisha leo na jana yao. Kuna wengine ambao pia hawajaacha machungu ya jana yafe, bado wanayapa nafasi katika akili yao kufikia hatua ya kuteswa na hofu ya kuishi leo katika ukamilifu.

Sikiza leo haiwezi kuja kama jana haijafa, Kesho haiwezi tokea kama leo haijaisha. Acha kuchelewesha furaha ya leo, fursa ya leo, nuru ya leo kwa kuendelea kukaa katika giza la jana..Weka pembeni na uiishi leo yako kwa furaha. Acha ya jana yawe ya jana...Ganga ya leo.

Thursday, September 8, 2016

INVEST IN YOUR CHARACTER

One of the greatest investments you can make is investment of character. Character is the only virtue you can use to make an impact in your life. Unless you invest in your character your life wont be in alignment with Excellence.

All aspects of life are attributed to character. Your approach towards life will always depend on your character. That's why you should always invest in character. Those who impact people and even society are people who have distinguished themselves in character.

Invest in having moral strength, refuse to have a low mentality. Small things shouldn't intimidate you. Don't complain about things you cant change. Just be involved and take full responsibility over your life. Believe in yourself. Get rid of self doubts, invest in knowledge and your doubts will flee.

Create a suitable environment for you to grow, establish connections. Wherever you are be there, make an impact. Don't just follow the crowd, don't just be a follower, you are destined to be a leader and a leader must have character.

How you speak, how you act, how you approach matters, Your overall composure is necessary, Don't be panicky, be calm...Have an evaluative mindset. Be positive even when others seem negative...Let your light shine among men. Positive mindset attracts positivity.

Instill hope when there's discouragement, make people feel happy about life, be a person of humor and infect your domain with hope and joy. If you cant change it then no need to complain about it.
But one very important thing to remember is Whatever character you invest in will impact you and your generations

Tuesday, September 6, 2016

POWER OF PASSION IN PROGRESS

The greatest virtue one can have that assures progress is passion. Passion is the driving force of motivation. Without passion the heart lacks meaning, the actions lacks enthusiasm and the mind lacks creativity.

When you have passion you inspire innovation. When you always work in the circle of the usual that means you lack the passion.

Passion inspires excellence. If you lack the passionate heart concerning something then it isn't worth it. The bible says God looks for a passionate heart. When you are passionate about something you go the extra mile.

Passion develops Perseverance  which means you can push forward even when all odds are against you. Passion brings about internal peace and joy to do what you want. 

Which means you do something with the satisfaction. As the self actualization concept of Abraham Maslow with passion you have satisfaction which is the highest need of a person.

Always understand your passion and most of all develop passion about the things you do.

How can you develop passion to progress:-
1. Discover your talents and abilities : the greatest discovery a man can do isn't discovering an ipad, light bulb or anything tangible but the discovery of one's talents and abilities. Never undermine your talent discovery. A talent is something you do easily and effectively and excellently with little strength but brings maximum satisfaction and joy. A talent isn't a hobby..a hobby is something you love to do but a talent is something you can do excellently that others cant.

2. Love yourself : Realise that you are a limited edition and you are a miracle in this world. You aren't an accident nor is your life an accident. Troubles and mistakes don't define you but only shape you, people's opinion don't define you and you have so much greatness in you. You can do anything you put your mind into and you deserve all what life can offer, You deserve to be happy, live a good life and have good relationships. If you begin to look at yourself in that focus you begin to develop passion to progress.

3.  Have a Positive mindset: You need to have a mindset that things are working for good and you aren't at a disadvantage. Develop that positive mindset about life. Ignore the negative opinions that always come into your mind most of the times.
If you want to progress you must develop passion.

TENGENEZA UTARATIBU WA KIUONGOZI WA MAISHA YAKO

Pasipo utaratibu mambo huenda mrama. Pasipo uongozi thabiti lazima kuwe na machafuko. Ili uweze kuwa na uthibiti katika maisha lazima kuwe na utaratibu na lazima kuwe na uongozi thabiti. Wewe ni kiongozi wa maisha yako.

Usipokuwa na uongozi binafsi na utaratibu wako wa utendaji lazima utakuwa mtumwa wa uongozi na utaratibu wa mwingine. Mikwaruzo hutokea pale mamlaka zinapokinzana. Pale ambapo kunakosekana uwiano baina ya uongozi binafsi na uongozi unaokuzunguka. Pale ambapo kunakosekana uwiano baina ya utaratibu binafsi na utaratibu unaokuzunguka.

Usipokuwa kiongozi wa maisha yako utawapa wengine fursa ya kushinikiza mambo katika maisha yako na hii itakujengea hali ya kukosa furaha kwa maana utakuwa unashindana na nafsi yako inayotaka kuwa kiongozi lakini imekosa utaratibu wa kiungozi.

Uhuru siku zote una gharama, Huwezi kuwa huru kama unaogopa gharama ya kuwa huru. Nafsi yako inataka kuwa huru lakina usipojenga utaratibu na uongozi wa ndani wa hisia na maamuzi ni vigumu sana nafsi yako kuwa huru.

Je unawezaje kujenga utaratibu na uongozi wa maisha yako:-
1. Usisimame katika msingi wa hisia: siku zote ili kuwa na utaratibu na uongozi katika maisha lazima ujenge msingi imara katika nafsi yako. Na hisia sio msingi imara maana hisia hubadilika kila wakati, huwezi kuwa kiongozi wa maisha yako kama unaenda kwa hisia. Ukienda kwa hisia utajikuta unaendelea kuvipa nafasi vitu ambavyo havitakiwi kupewa nafasi kwa wakati huo.

2. Ongeza maarifa na ufahamu : Huwezi kuwa huru na kuwa kiongozi wa maisha yako kama ufahamu na maarifa yako vina ukomo. Hakuna jambo baya kama uhuru na ujinga. Huwezi kuwa mjinga halafu ukawa kiongozi wa maisha yako. Ujinga ni utumwa ndio maana kuna maandiko yanasema Utaijua kweli nayo kweli itakufanya huru.

3. Tengeneza sheria za maisha yako: lazima utengeneze msingi mgumu tofauti na hisia. Ukishakuwa na maarifa tengeneza sheria zako mwenyewe na hakikisha huzivunji sheria hizo maana ni changamoto na itakuumiza zaidi pale unapovunja sheria zako mwenyewe.

4. Fanya vitu kulingana na vipawa na karama zako : Huwezi kuwa kiongozi bora wa maisha yako kama haujipambanui na wengine. Usiwe mtu wa kufata upepo...Zig ziglar alishawahi kusema kuwa Uongozi sio kufuata njia iliyopitwa na watu bali ni kutafuta njia yako na kuacha alama. Ukiwa mtu wa kujilinganisha na wengine huwezi kuwa na utaratibu wako mwenyewe.

5. Jiamini : Dhana ya kujiamini ni pana sana. Katika jambo lolote lile usipojiamini huwezi fanya chochote, jiamini katika maamuzi yako, jiamini katika unayofanya. Wengi wanashindwa hata kufanya maamuzi magumu kwasababu ya kukosa kujiamini. Kama unataka kuwa kiongozi wa maisha yako jiamini ikiwemo huweze kufanya maamuzi na kuwa tayari kuwajibika kutokana na maamuzi yako.

* Hakuna jambo litakalokupa amani na furaha kama kutambua kuwa una uthibiti wa maisha yako. Ni jambo litakaloongeza ari ya utendaji wako na pia kukupa morali na msisimko wa kila siku wa maisha.

Sunday, September 4, 2016

PATA MAPUMZIMKO UONGEZE UFANISI

Moja ya mambo ambayo unatakiwa ujijengee katika maisha yako ni kupumzisha akili yako. Akili ambayo inakosa mapumziko huwa na uzito kuchukua hatua na hata kupata majibu ya maswali yanayokuzunguka.

Kupumzika ni zaidi ya kulala au kutofanya kazi bali kupumzisha akili ni kuacha kwa muda kufanya mambo fulani au kujishughulisha kwa mambo fulani. Maisha bila mapumziko hukosa msisimko na kuna wakati utajikuta bila ari ya utendaji kwasababu hukuweza kuupa mwili na akili mapumziko.

Muda wa kupumzika sio muda wa kuendelea kutumia simu au kuangalia runinga. Unachofanya pale ni kuendelea kuishughulisha akili na kujiweka wazi kwa fikra asi zinazochosha akili. Muda wa mapumziko ni muda wa kuweka pembeni stress na mawazo juu ya misukosuko na changamoto zinazokuzunguka.

Kuna watu ambao husema kupumzisha akili hakuyafanyi matatizo yaondoke, ni kweli lakini kupumzisha akili ni kuiwezesha kupata majibu ya matatizo hayo. Usidhani kuwa kupumzika ni kupoteza muda au kuwa mzembe.

Kuna usemi unasema kuwa "more than working hard, work smart", bila akili nguvu hupotea. Lazima akili ipumzishwe ili ilete ufanisi unaotakiwa. Njia nzuri ya kupumzika ni wakati wa kukaa kufurahia uzuri wa maisha na kutafakari mema.

Maandiko husema kuwa siku ya saba Mungu alipumzika na kufurahia uumbaji wake. Wakati wa mapumziko ni wakati wa kufurahi uzuri wa maisha. Katika wakati huu iache akili yako ifurahie uzuri wa maisha na mambo mazuri. Wengine hujitenga kabisa kwa muda na watu wengine.

Ukiona unakosa furaha ya maisha na msisimko wa kazi jiulize ni wakati gani uliopumzika, ni wakati gani umepumzisha nafsi yako, mara ya mwisho kufurahia uzuri wa maisha na kutafakari mazuri ni lini?

Friday, September 2, 2016

JINSI YA KUKABILIANA NA VIKWAZO

Moja ya changamoto tunazokumbana nazo katika maisha ni vikwazo vinavotukwamisha kufikia malengo au yale tunayoyahitaji. Kuna vikwazo vya nje na vikwazo vya ndani. Maana halisi ya kikwazo ni jambo linalokuzuia kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

Vikwazo vinaweza kuwa watu, tabia au hata mifumo ya utendaji. Unapokuwa mtu wa kutafakari maono yako na hapo ulipo utatambua ni aina gani ya kikwazo unachokumbana nacho. Kikwazo siku zote kina namna yake ya kukiangalia ili uweze kukiondoa au kukivuka.

Lazima ujitafakari ni kikwazo cha namna gani unachokumbana nacho na ni nini unaweza kufanya kukivuka hicho kikwazo. Pasipo kukaa chini kujitafakari vikwazo vinaweza kuwa sababu yako ya kulaumu, kulalamika na kujenga mtazamo asi wa maisha.

Njia pekee ya kuvuka kikwazo ni lazima kwanza ujue na uwe na picha halisi ya lengo lako au hatma yako, kisha lazima utulize akili na kisha ukitazame kikwazo kilichopo mbele yako na ukitambue kuwa ni kikwazo cha namna gani.

Kisha ni muhimu sasa kuangalia kikwazo hicho kina mguso gani katika mfumo wako wa kukabili mambo, je hicho kikwazo kinahitaji ufanye mabadiliko gani kwa upande wako, kisha yakupasa uangalie fursa zilizopo za kuweza kukivuka hicho kikwazo.

Kumbuka usipokaa ukatafakari utakuwa unavamia vikwazo na vinakuwa na mguso wa ndani katika nafsi yako kupelekea wewe kukosa kabisa ari na hata morali ya kufanya mambo kupelekea kukata tamaa na kupoteza kabisa mtazamo chanya na maisha.

Sunday, August 28, 2016

HAKUNA AJALI, KILA JAMBO LINA KUSUDI

"Huwa hakuna ajali.. Bali kuna kusudi ambalo bado hatujalitambua "-Deepak Chopra

Katika moja ya mafundisho yake mhamasishaji na mkufunzi wa maswala ya kujitambua Deepak chopra alisema huwa hakuna ajali bali kuna kusudi ambalo bado hatujalitambua. Kauli hii ni yenye mtazamo chanya hasa pale tunapokosa majibu ya baadhi ya maswali tuliyonayo katika maisha.

Siku zote kusudi la jambo hufungwa katika muda na maarifa. Kuna usemi ambao wengi wetu huwa tunao hasa pale tunapokosa majibu huwa tunasema limetokea la kutokea tukiweka mtazamo kwamba jambo ilo ni kama muujiza au limetokea kutoka hali ya kutokuwepo. Lakini inatupasa tubadili mitazamo.

Katika kila jambo tusilopata majibu tutambue kuwa kuna kusudi ambalo halijadhiirishwa bado kwa wakati huo hivo inatupasa kutambua yatupasa kuwekeza katika kujikuza kimaarifa huku tukiendelea kutambua kuwa muda muafaka tutakuwa watu wenye ufahamu zaidi juu ya yale yanayotokea.

Hakuna jambo linalotokea kwa ajali...lazima kuwe na kusudi...iwe ni kukukumbusha jambo, kukufundisha jambo au kukuimarisha katika jambo. Lakini ni lazima tujenge tabia ya uvumilivu hadi pale tunapopata maarifa mapana ya jambo hilo.

Muda mwingi tumekuwa ni watu wa kuchukua maamuzi bila maarifa yeyote tunapokuwa katika hali ya kukosa ufahamu juu ya kusudi fulani. Inabidi turuhusu muda na kukua katika maarifa.Kuna ambao wanajifunga katika makubaliano baada ya dakika kumi na tano za hisia kali bila kuruhusu muda kupoza hisia hizo na kupata maarifa juu ya kusudi hilo kabla hawajachukua maamuzi.

Chukua muda wako vizuri huku ukikua ktk maarifa kutambua kusudi la jambo maana hakuna jambo linalotokea kama ajali.

Friday, August 26, 2016

KWANINI HATUTENDEI KAZI TUNAYOYAJUA

Changamoto kubwa tuliyonayo ni kujua sana, kusoma sana lakini hatutendi yale tunayoyajua. Ni sawa na kuingiza vitu vingi ndani yako lakini utoaji wake au utendaji wake ni mdogo. Wengi hawasongi mbele kwasababu wanajua sana lakini wanatenda kidogo.

Huwa najiuliza maswali mengi hasa pale napokijua kitu lakini nashindwa kukitendea kazi. Huwa najiuliza nini tatizo? Hasa hasa pale unapokuja kuona mtu mwingine akikitendea kazi kile ulichokijua wewe na akapiga hatua.

Hata maandiko husema muwe watendaji wa neno na sio wasikilizaji tu. Na yule ajuaye jambo na kutolitenda huhesabika kwake kama uovu.. Kwanini? Kwasababu ufahamu unapaswa kukuweka huru na sio kukufanya mfungwa. Unapojua kitu ni nafasi kwako kukifanyia kazi ili kikusaidie. Kukijua tu na kuishia pale haisaidii.

Ni kwanini watu hatutendei kazi yale tunayoyajua? Baada ya kutafakari na kuchunguza kwa makini nimekuja kugundua sababu kuu inayopelekea watu tusitendee kazi tunachokijua imefungwa katika mitazamo yetu na tabia zetu za ndani.

1. MTAZAMO BINAFSI: Hii ndiyo changamoto ya kwanza inayosababisha watu wasitendee kazi wanayoyajua. Watu wengi wana mitazamo binafsi iliyo asi ambayo hupambanua na kuua nguvu ya utendaji, ukiwa na mtazamo asi siku zote utakichambua unachokijua na kuua msukumo wako kukitendea kazi. Ni muhimu sana kujenga mtazamo binafsi ulio chanya.

2. KUKOSA UJASIRI : Watu wengi hawatendei kazi wanayoyajua kutokana na kukosa ujasiri wa kutenda. Wengi wamefungwa katika mitazamo ya watu wengine mfano ndugu wa karibu nk. Mawazo yao yakiyumbishwa kidogo wanakosa ujasiri wa kutenda. Zaidi ya vyote ni muhimu kuwa na ujasiri wa kufanya jambo hata ukikutana na vipingamizi. Lazima ujiamini katika kutenda.

3. IMANI HABA : Hili neno limekuwa lenye kufahamika sana hata katika vitabu vya dini, watu wengi hushindwa kutenda mambo kutokana na kuwa na imani isiyo thabiti. Lazima jambo unalolifahamu ulijengee msingi wa kiimani. Haiishii kulitambua bali inakupasa uliamini. Usipoliamini huwezi kulifanyia kazi

4. KUKOSA NIDHAMU: Nidhamu ni tabia ya ndani ambayo mtu huijenga. Nidhamu itakuwezesha kustahimili na kutoka katika comfort zone ( uwanda wa starehe) na kustahimili misukosuko na kuweza kusonga mbele. Nidhamu itakulazimu kufanya jambo hata usilojisikia kulifanya huku ukiwa na taswira ya matokeo chanya.

5. KUKOSA MIFUMO YA UTENDAJI: Hii ni changamoto kuu hasa pale unaposhindwa kuandaa mifumo ya utendaji kuhamisha nadharia kuwa vitendo. Mifumo ya utendaji ni malengo, muda, nguvu na uwezeshaji mwingine. Usipojenga mifumo bora ya utendaji itakuwia vigumu kutenda yale unayoyajua. Yakupasa uwekeze zaidi.
Pasipo kutathmini kwa makini hizo sababu tutaendelea kuwa watu wa kujua mambo pasipo kutenda.

ACHA KUJILINGANISHA NA WATU WENGINE

Moja ya changamoto ambayo huwafanya watu wengi wasiishi katika furaha ni tabia ya kujilinganisha na watu wengine. Washindi hawajipimi kwa maendeleo ya wengine bali kwa maendeleo waliyonayo jana. Bill gates muanzilishi wa Microsoft aliwahi kusema kuwa kujilinganisha na wengine ni kujitukana mwenyewe.

Ukipenda kujilinganisha na watu wengine kuna hatari ya kudharau uwezo wako na kuanza kutazama  madhaifu yako na hii itakujengea tabia ya kutofurahi hata kwa vitu ulivonavo huku ukiwa unatazama zaidi vitu vya wengine au mafanikio ya wengine.

Ukijilinganisha na wengine utaua msukumo wako wa mafanikio kwasababu kuna ambao wamekutangulia katika safari ya maendeleo, kuna ambao wamepitia vikwazo vingi au kuna ambao wamepitia njia rahisi zaidi hivo si busara kujilinganisha na watu.

Weka malengo yako na ujipime kwa malengo yako na siyo malengo ya watu wengine. Kila mtu ana malengo na mitazamo yake na dhana kuu ya maendeleo ni mfumo uliotumika na sio matokeo. Matokeo hayawezi kuwa sawa kama mifumo ni tofauti hivo ukitazama tu matokeo unaweza ingiwa na hasira kwa kutopata matokeo sawa na mwenzako.

Ukipenda kujilinganisha ma wengine utaishi kama kivuli na hautokuwa na utambulisho wako. Wanaoshindwa huangalia zaidi wanaoshinda badala ya kuangalia ushindi. Usiridhike na mafanikio yako ya nyuma...unaweza kuwa zaidi ya hapo.

JE UNAWEZAJE KUJENGA TABIA YA KUTOJILINGANISHA NA WENGINE

1. JITAMBUE : Inakupasa kujitambua wewe ni nani, vipawa vyako, uwezo wako, maarifa yako na yale unayoweza kuyafanya. Jipime kwa hayo mambo na ujiulize Je unaweza kufanya zaidi ya hapo?

2. JENGA MIFUMO: Siku zote husipokuwa na mifumo ya utendaji yako iliyojengwa na mitazamo uliyonayo kuhusu maisha lazima utajaribu kujilinganisha na matokeo yanayopatikana na mifumo inayotumiwa na wengine.

3. EPUKA MANENO YA WATU : Mara nyingi tunajikuta wahanga wa kujilinganisha na wengine kutokana na misukumo tunayoipata kutoka kwa watu wanaotuzunguka kama wazazi, watu wa karibu n.k...Lakini lazima uwe na uwezo wa kutotafakari sana maneno ya watu hasa wale wanaokushinikiza kuwa kama watu wengine.

4. KUMBUKA WEWE NDIO KIONGOZI WA MAISHA YAKO: Inakupasa utambue wewe ni kiongozi wa maisha yako, maisha yako ni kama kampuni hivo yakupasa kujua mtu pekee ambayo ana wajibika zaidi ni wewe. Hata mzazi wako sio kiongozi wa maisha yako zaidi yako wewe. Hii itakusaidia kuwa na mtazamo wa ubunifu zaidi juu ya maisha yako.

5. ANGALIA MBELE : Dereva bora ni yule anayeangalia mbele anapoendesha gari na sio kuangalia pembeni wanaomu overtake au walio ktk mwendo sawa na yeye. Siku zote usitumie muda wako mwingi kutazama wanaoku overtake. Unaweza jifunza jambo lakini si busara kujilinganisha na waô

Kumbuka kipimo pekee cha mafanikio yako ni malengo yako na uwezo wako na sio kujilinganisha na wengine.


Wednesday, August 24, 2016

JENGA TABIA YA UKIMYA

Napozungumzia tabia ya ukimya nazungumzia ukimya wa nafsi na ukimya wa tabia na hata mazingira kwa ujumla. Jamii kwasasa imezungukwa na vivutio na purukushani nyingi ambazo haziruhusu au hazisababisha ukimya. Shida kubwa ni kwamba baada ya purukushani za kila siku kinachobaki katika nafsi ni upweke unaotokana na kutojenga muda muafaka kusikiliza nafsi yako na kutafakari.

Ukimya kwanza unakuwezesha kujitambua kwa kuwa utakuwezesha kujitafakari kwa utulivu vipawa na uwezo wako na kukuwezesha kufikiri kwa makini juu ya hatma ya maisha yako.Pia ukimya utakuwezesha kutambua ni maeneo gani katika maisha yako yanahitaji uangalizi ili kukuongezea thamani. Pia utakuwezesha kusikiza miongozo inayotoka ndani ya nafsi yako.

Utajua ni nini unachotaka na ni nini unachokiamini kwasababu umezungukwa na kelele nyingi za maisha...Kelele za mitazamo ya watu, maneno ya watu na hata changamoto za maisha. Usipojenga tabia ya ukimya utakuwa ni mtu mwenye hisia za upweke mara kwa mara maana muda mwingi utajikuta umeenda tofauti na nafsi yako na kufuata mvuto wa kelele zinazokuzunguka.

Kumbuka palipo na ukimya ndipo maarifa, hekima na amani ya nafsi hukaa, pia katika ukimya kunajengeka tabia ya kuwa macho juu ya mahitaji na hisia za wengine. Mahusiano ya watu ambao hawajajenga tabia hii huwa na lawama, malalamiko na mikwaruzano ya hapa na pale kwasababu ya kukosa ule muamko na kuwa macho juu ya mahitaji na hisia za wengine.

Mambo ya kufanya na kuzingatia ili kujenga tabia ya ukimya:-
1. Pendelea kuwa na tabia ya kukaa mwenyewe ukitafakari juu ya maisha yako pasipo vurugu au purukushani kutoka kwa watu wengine

2. Jenga tabia ya kutembea au kutembelea maeneo yenye utulivu na malihai kama miti, bustani nk

3. Penda kuwa msikilizaji, mtazamaji na mtu anayetafakari zaidi kwa kile anachokiona.

4. Penda kupangilia vitu vizuri maana siku zote mlundikano wa vitu hautokuruhusu kuwa na muda mzuri wa kutafakari.

5. Jenga tabia za kiimani kama kusali na kusikiza nyimbo za taratibu zenye kuinua nafsi.

Tuesday, August 23, 2016

OUR ATTITUDE MATTERS

The process of human change begins within us. We all have tremendous potential. We all desire good results from our efforts. Most of us are willing to work hard and to pay the price that success and happiness demand.

Each of us has the ability to put our unique human potential into action and to acquire a desired result. But the one thing that determines the level of our potential, that produces the intensity of our activity, and that predicts the quality of the result we receive is our attitude.

Attitude determines how much of the future we are allowed to see. It decides the size of our dreams and influences our determination when we are faced with new challenges. No other person on earth has dominion over our attitude.

People can affect our attitude by teaching us poor thinking habits or unintentionally misinforming us or providing us with negative sources of influence, but no one can control our attitude unless we voluntarily surrender that control. No one else "makes us angry." We make ourselves angry when we surrender control of our attitude.

What someone else may have done is irrelevant. We choose, not they. They merely put our attitude to a test. If we select a violent attitude by becoming hostile, angry, jealous or suspicious, then we have failed the test.

If we condemn ourselves by believing that we are unworthy, then again,we have failed the test. If we care at all about ourselves, then we must accept full responsibility for our own feelings. We must learn to guard against those feelings that have the capacity to lead our attitude down the wrong path and to strengthen those feelings that can lead us confidently into a better future.

If we want to receive the rewards the future holds in trust for us, then we must exercise the most important choice given to humanity by maintaining total dominion over our attitude. Our attitude is an asset, a treasure of great value, which must be protected accordingly.

Beware of the vandals and thieves among us who would injure our positive attitude or seek to steal it away. Having the right attitude is one of the basics that success requires.

Monday, August 22, 2016

FAIDA YA JUU SANA KATIKA KAZI

Faida ya juu sana aipatayo mtu kwa kufanya kazi sio anachokipata katika kazi hiyo bali ni anachokuwa katika kazi hiyo -John Ruskin

Watu wengi hutenda mambo au hufanya kazi fulani ili apate mapato fulani mfano mafao, pesa nk. Si jambo baya kufanya kazi au kujishughulisha katika mambo fulani kwa mapato fulani lakini sio mtazamo endelevu wa maendeleo. Robert Kiyosaki aliwahi kusema kuwa katika kazi yeyote angalia zaidi hiyo kazi ina manufaa gani zaidi katika kukuongezea maarifa na thamani.

Wekeza zaidi katika kuongeza thamani na hiyo ndiyo iwe faida yako namba moja. Unapojali zaidi thamani inayoongezeka ndani yako unajijengea msingi wa maendeleo endelevu. Thamani ya mtu ni uwezo alionao ndani yake na thamani ya mtu itamuwezesha kuendelea katika mazingira tofauti tofauti.

Unapowekeza katika kuwa na maendeleo ya nafsi mfano mitazamo chanya, maarifa endelevu, uwezo wa kustahimili na tabia za uwajibikaji unajijengea thamani zaidi ya pesa unazopata.
Kama unachofanya kinakuza mfuko wako lakini hakikuzi nafsi yako na kukujenga basi hakikusaidii sana maana pasipo thamani ukija kupoteza hayo mafao ni vigumu kutengeneza mazingira ya kuzalisha.

Thamani yako itakuwezesha kuwa na ufanisi katika eneo lolote. Hivo kwa mujibu wa John Ruskin hiyo ndiyo faida ya juu sana unayoweza kuipata. Hivo badala ya kuangalia zaidi malipo utakayopata angalia zaidi mabadiliko au thamani unayopata au utakayopata katika jambo ulifanyalo.

Sunday, August 21, 2016

MSISIMKO WA MAISHA

Je umekosa msisimko wa maisha? Jizamishe katika kazi unayoiamini kwa moyo wako wote, iishi kazi hiyo, na utapata furaha ambayo haukuidhania-Dale Carnegie

Moja ya changamoto kubwa kwa watu sasa hivi ni kukosa msisimko na msukumo wa maisha, Moja ya viashiria vya kukosa msisimko wa maisha ni upweke, lawama na kukosa msukumo wa kufanya mambo. Watu wanakosa ile furaha ya kuamka jumatatu asubuhi, wengine hadi wanaingiwa na hisia hasi ikifika jumapili jioni.

Changamoto hii inatokana na mazoea ya watu ya kufanya mambo wasiyoyapenda, mambo ambayo hayana uhusiano na hulka zao. Watu wanafanya kazi lakini kwa lengo moja nalo ni kupata pesa pasipo kuwa na ridhaa katika nafsi zao. Kwa mujibu ya mwanasaikolojia Abraham maslow binadamu anasukumwa kukua na mambo mengi lakini kuu kuliko yote ni nafsi yake kuridhika.

Nafsi yako isiporidhika na kuridhia kazi unayofanya jua kabisa lazima utakosa msukumo na furaha katika kazi hiyo. Utaanza kuingiwa na hisia hasi kila unapokumbuka kwamba kesho yake kuna kazi. Steve Jobs aliwahi kusema kuwa kama hujapata kitu unachokipenda endelea kutafuta maana maana kuu ya maisha ni kutafuta kusudi lako na kulifanya.

Kama kwa mtazamo wa Dale carnegie inatupasa kujizamisha katika kazi tunayoiamini kwa mioyo yote na kuziishi kazi hizo utapata furaha na hautokaa kusubiri Jumatatu ifike uruke katika kazi ya moyo wako na uzuri ni kwamba ukiishi kazi ya moyo wako hautokuwa na likizo.

Friday, August 19, 2016

NJIA ZA KUDHIHIRISHA MAONO YAKO

"Whatever you vividly imagine, ardently desire, sincerely believe, and enthusiastically act upon must inevitably come to pass!" - Paul J. Meyer

Tafakari ya ufasaha ni ngazi ya kwanza kabisa ya kufikia unachokitaka. Mara nyingi huwa tunatafakari bila ufasaha. Tunabeba maono makubwa lakini hatukai chini kutafakari maono hayo kwa ufasaha. Ni muhimu kukaa chini kutafakari kwa ufasaha maono uliyonayo.

Hitaji kutoka ndani ya nafsi ni ngazi ya pili kwa mujibu wa paul meyer ya kufikia malengo. Lazima maono yako uyatengenezee sababu na msingi wa ndani wa kihisia. Tengeneza msukumo wa ndani wa uhitaji katika kufikia malengo yako...Lazima utengeneze sababu ya kwanini unatakiwa ufikie malengo hayo.

Amini kutoka moyoni ni ngazi ya tatu kwa mujibu wa Paul meyer, ni lazima uwe na imani thabiti juu ya maono yako na imani hiyo isitetereshwe na aina yeyote ya mazingira. Ukiwa na maono lakini ukashindwa kuyaamini maono yako jua hautoweza kuyafikia.

Kisha unatakiwa uchukue hatua kwa msisimko na mhemko chanya. Lazima uchukue hatua kwa msisimko na mhemko chanya la sivyo hutoweza kuyafanya hayo maono yako dhahiri. Hatua iliyo na msisimko itakuwezesha kushinda vipingamizi au misukumo na changamoto hasi.
Kwa mujibu wa Paul meyer chochote kitafanikiwa ukifata hizo njia.

FEAR OF THE UNKNOWN

The Fear of the unknown is the Psychological paralysis caused by mystery of the unknown. Its one of the greatest challenges to progress because it kills the enthusiasm and the morale to progress to the clouds of what you haven't experienced or what you don't know.

This has paralysed many people with big ideas, it has paralysed individuals and caused them to be ANTAGONISTS to the FORCE OF CHANGE. Human being delights in COMFORT ZONE and any idea of CHANGE that hasn't been experienced before is often excused by the fear of the unknown.

But you can overcome the FEAR OF THE UNKNOWN by evaluating the vision and putting it down into realistic attributes, then GRAB on FAITH and DISCIPLINE while exercising the POSITIVE MINDSET.
Negativity gives power to the FEAR OF THE UNKNOWN. In life we need to understand that we either CHANGE willfully or THE FORCE OF CHANGE affects us violently leaving us with scars. Now that requires us to overcome the fear of the unknown.

The unknown is a mystery and it should be approached with enthusiasm and the joy of exploration...for whatever you don't know holds a part of your soul you haven't discovered yet...Pursue the experience and let Go of the fear of unknown.

Believe that God is there in the unknown ready to make it known to you. Let your life be of adventures and explore new experiences and overcome the fear of the unknown that keeps you from knowing the unknown.

Tuesday, August 16, 2016

JE UNA UHUSIANO NA UNACHOKIFANYA

Changamoto kubwa watu wengi wanayokutana nayo katika mambo wayafanyayo ni kukosa uhusiano wa kihisia baina yake na akifanyacho. Lazima kuwe na msingi na uhusiano wa kihisia na kinafsi baina yako wewe na unachokifanya.

Ukikosa huo uhusiano lazima ukose hisia ya kuridhia na kuridhika kwa kile ukifanyacho. Bado katika nafsi yako kunakuwa na utupu ambao husababisha hisia za upweke katika kila ukifanyacho. Kuna watu wengi wanafanya kazi au shughuli lakini wana upweke kwa yale wayafanyayo.

Nafsi yako inakosa uwiano na kile ukifanyacho. Uwezo wako unakosa msukumo kuelekea kile ukifanyacho. Ni changamoto kubwa pale unapotaka likizo ili upumzike kihisia ktk kile ukifanyacho maana kazi ya nafsi yako huwa haina likizo ya kihisia.

Ukiona msukumo wako unapungua na hauna ile shauku ya kuongeza msukumo kiutendaji katika jambo fulani ni dhahiri wewe na hilo jambo hamna uhusiano wa kimsingi wa kinafsi na kihisia. Lazima kuwe na uhusiano, tafuta jambo ambalo lina mahusiano na nafsi yako.

Monday, August 15, 2016

HUWEZI FANIKIWA ZAIDI YA MAWAZO YAKO

Watu wengi hupenda mafanikio na kukua lakini hawafanikiwi wala kukua. Kwasababu ya sheria moja ambayo ni kwamba huwezi fanikiwa zaidi ya mawazo yako. Maisha yako ya nje ni zao la mawazo yako.

Hakuna jambo linaloweza kutokea kama hujalifikiria kwa wakati wowote katika maisha yako. Unaweza kupenda kufanikiwa lakini je ulishawahi kufikiria na kutafakari mafanikio. Huwezi kuwa na fikra za ukomo halafu uwe na ziada. Mfumo wako wa fikra unadhiirika kwa kauli zako na mitazamo yako juu ya jambo fulani.

Ukishakiri kwamba jambo haliwezekani ni kwasababu umefikiria haliwezekani na halitokuja kuwezekana kwako hadi ubadilishe jinsi unavoliwaza hilo jambo. Hapo pekee ndo utaweza kufungua ubongo wako juu ya njia za kuliweza.

Myles munroe alishawahi kusema ugumu wa jambo fulani unatokana na ufahamu wako juu ya jambo husika hivo badala ya kushikiria mtazamo wako, wekeza kupata ufahamu zaidi juu ya hilo jambo. Huwezi ishi nje ya mitazamo yako maana mitazamo yako siku zote itachonga muundo wa maisha yako.

Friday, August 12, 2016

PROBLEMS AS OPPORTUNITIES

The factor that triggers your creativity and activates your positive mind is pressing problems. It is only when you are experiencing the pressure of problems and obstacles that you are motivated to perform at your mental best. Facing and solving the inevitable problems and difficulties of life make you stronger and smarter, and bring out the very best in you.

Most people do not understand the nature of problems. Problems are a normal and necessary part of life. They are inevitable and unavoidable. Problems come in spite of your best efforts to avoid them. Problems, therefore, come unbidden.

The only part of a problem over which you have any control is your response to your problems. Effective people respond positively and constructively to problems. In this way, they demonstrate that they have developed high levels of “response-ability”. They have developed the ability to respond effectively when unexpected or undesired difficulties occur.

Problems of all kinds bring out your very best qualities. They make you strong and resourceful. The more pressing your problems, and the more emotion you invest in solving those problems,the more creative you will become. Each time you solve a problem constructively, you become smarter and more effective. As a result,you prepare yourself for even bigger and more important problems to solve.

Thursday, August 11, 2016

IMPACTS OF YOUR COMPANIONS TO YOUR SUCCESS

Learn to surround yourself with people who will make impact, encourage and support you. Don't waste most of your time with people who don't care about your future but cares about what you drink this weekend and always want you to depend on them than be independent.

Surround yourself with people who will assist you to chase your dreams and wish you to be independent in life than dependent. People who want to see you succeeding in life and take care of your own bill.

Most of us would have been successful by now but the company we keep is dragging us down because they enjoy when people depend on them. Is time to have people who wish us good than those who want us to depend on them.

Your company either makes you or breaks you. Your company is either a burden or a drive. You have to be careful with the company you keep if you want to succeed. Most successful people have success connections and they don't entertain people below their league because they believe they don't have any challenge to offer them.

If eagles fly alone no matter the crowd of other birds that fly together. Eagles fly with their kind. Thus its very important to choose well the company we hang out with.

There are three kinds of company, the comrades, the confidants, the constituents.
The Comrades are people who walk with you because you have a common goal and once the goal is gone they also leave. Most school friends and colleagues are comrades,
The constituents are people who walk with you because they want something from you and once they get what they want they go,most people fall in this that's why relationships fail and hurt, friendship break etc.
The confidants are the people who stick with you unconditionally...they will be with you in the valleys,hills, good times and bad times etc.
You have to evaluate well the company you keep if you want to succeed.

Wednesday, August 10, 2016

NANI MUANDAAJI WA SCRIPT YA MAISHA YAKO?

Ni utaratibu kwa waigizaji wa filamu kuandikiwa muongozo wa jinsi ya kucheza tamthilia au filamu kwa kuvaa uhusika wa watu walio katika nadharia. Wao huvaa uhusika na kucheza kwa muongozo wa mtayarishaji mkuu.

Katika maisha yako ni nani mtayarishaji mkuu wa script unazocheza? Kuna kipindi lazima uvae uhusika wa mtu fulani aliye katika nadharia nawe umuweke katika matendo lakini ni muhimu sana kutambua ni nani mtayarishaji mkuu wa script zako.

Mtayarishaji mkuu anaweza akawa Mzazi wako, ndugu zako na hata majirani zako inategemea na nani umempa funguo ya kukushurutisha, unapompa utayarishaji mkuu mtu mwingine unaishi katika maono au nadharia ya mtu mwingine. Naye ndo anakuwa mtengeneza utaratibu wa maisha yako. Ni sawa na mtumwa, yeye huishi akifata utaratibu wa Bwana wake.

Unapoacha kuwapa watu wengine utayarishaji mkuu wa script za maisha yako ndipo unapoanza kuishi maisha yako, ndipo unapoanza kuishi ndoto zako na maono yako, tofauti na hapo unakuwa mtumwa wa maono na nadharia za watu wengine.

Changamoto kubwa ni kutengeneza script ya maisha yako na usimame imara kama msimamizi mkuu kwa vitendo na usikilize mawazo yale yanayoendana na hiyo script yako na sio siri ni lazima utapata upinzani kutoka kwa wale ambao wanataka kuwa watayarishaji wa script ya maisha yako na mara nyingi ni watu wale ambao hata wao walitayarishiwa script za maisha yao wanataka kuendeleza utamaduni huo.

Andaa miongozo, andaa script na uhakikishe unajenga mianya ya watu watakaokuwezesha kucheza vizuri script yako, wawe ni marafiki, wakufunzi nk.
Kumbuka unaanza kuishi maisha yako pale unapokuwa mtayarishaji wa script ya maisha yako .