Sunday, August 28, 2016

HAKUNA AJALI, KILA JAMBO LINA KUSUDI

"Huwa hakuna ajali.. Bali kuna kusudi ambalo bado hatujalitambua "-Deepak Chopra

Katika moja ya mafundisho yake mhamasishaji na mkufunzi wa maswala ya kujitambua Deepak chopra alisema huwa hakuna ajali bali kuna kusudi ambalo bado hatujalitambua. Kauli hii ni yenye mtazamo chanya hasa pale tunapokosa majibu ya baadhi ya maswali tuliyonayo katika maisha.

Siku zote kusudi la jambo hufungwa katika muda na maarifa. Kuna usemi ambao wengi wetu huwa tunao hasa pale tunapokosa majibu huwa tunasema limetokea la kutokea tukiweka mtazamo kwamba jambo ilo ni kama muujiza au limetokea kutoka hali ya kutokuwepo. Lakini inatupasa tubadili mitazamo.

Katika kila jambo tusilopata majibu tutambue kuwa kuna kusudi ambalo halijadhiirishwa bado kwa wakati huo hivo inatupasa kutambua yatupasa kuwekeza katika kujikuza kimaarifa huku tukiendelea kutambua kuwa muda muafaka tutakuwa watu wenye ufahamu zaidi juu ya yale yanayotokea.

Hakuna jambo linalotokea kwa ajali...lazima kuwe na kusudi...iwe ni kukukumbusha jambo, kukufundisha jambo au kukuimarisha katika jambo. Lakini ni lazima tujenge tabia ya uvumilivu hadi pale tunapopata maarifa mapana ya jambo hilo.

Muda mwingi tumekuwa ni watu wa kuchukua maamuzi bila maarifa yeyote tunapokuwa katika hali ya kukosa ufahamu juu ya kusudi fulani. Inabidi turuhusu muda na kukua katika maarifa.Kuna ambao wanajifunga katika makubaliano baada ya dakika kumi na tano za hisia kali bila kuruhusu muda kupoza hisia hizo na kupata maarifa juu ya kusudi hilo kabla hawajachukua maamuzi.

Chukua muda wako vizuri huku ukikua ktk maarifa kutambua kusudi la jambo maana hakuna jambo linalotokea kama ajali.

Friday, August 26, 2016

KWANINI HATUTENDEI KAZI TUNAYOYAJUA

Changamoto kubwa tuliyonayo ni kujua sana, kusoma sana lakini hatutendi yale tunayoyajua. Ni sawa na kuingiza vitu vingi ndani yako lakini utoaji wake au utendaji wake ni mdogo. Wengi hawasongi mbele kwasababu wanajua sana lakini wanatenda kidogo.

Huwa najiuliza maswali mengi hasa pale napokijua kitu lakini nashindwa kukitendea kazi. Huwa najiuliza nini tatizo? Hasa hasa pale unapokuja kuona mtu mwingine akikitendea kazi kile ulichokijua wewe na akapiga hatua.

Hata maandiko husema muwe watendaji wa neno na sio wasikilizaji tu. Na yule ajuaye jambo na kutolitenda huhesabika kwake kama uovu.. Kwanini? Kwasababu ufahamu unapaswa kukuweka huru na sio kukufanya mfungwa. Unapojua kitu ni nafasi kwako kukifanyia kazi ili kikusaidie. Kukijua tu na kuishia pale haisaidii.

Ni kwanini watu hatutendei kazi yale tunayoyajua? Baada ya kutafakari na kuchunguza kwa makini nimekuja kugundua sababu kuu inayopelekea watu tusitendee kazi tunachokijua imefungwa katika mitazamo yetu na tabia zetu za ndani.

1. MTAZAMO BINAFSI: Hii ndiyo changamoto ya kwanza inayosababisha watu wasitendee kazi wanayoyajua. Watu wengi wana mitazamo binafsi iliyo asi ambayo hupambanua na kuua nguvu ya utendaji, ukiwa na mtazamo asi siku zote utakichambua unachokijua na kuua msukumo wako kukitendea kazi. Ni muhimu sana kujenga mtazamo binafsi ulio chanya.

2. KUKOSA UJASIRI : Watu wengi hawatendei kazi wanayoyajua kutokana na kukosa ujasiri wa kutenda. Wengi wamefungwa katika mitazamo ya watu wengine mfano ndugu wa karibu nk. Mawazo yao yakiyumbishwa kidogo wanakosa ujasiri wa kutenda. Zaidi ya vyote ni muhimu kuwa na ujasiri wa kufanya jambo hata ukikutana na vipingamizi. Lazima ujiamini katika kutenda.

3. IMANI HABA : Hili neno limekuwa lenye kufahamika sana hata katika vitabu vya dini, watu wengi hushindwa kutenda mambo kutokana na kuwa na imani isiyo thabiti. Lazima jambo unalolifahamu ulijengee msingi wa kiimani. Haiishii kulitambua bali inakupasa uliamini. Usipoliamini huwezi kulifanyia kazi

4. KUKOSA NIDHAMU: Nidhamu ni tabia ya ndani ambayo mtu huijenga. Nidhamu itakuwezesha kustahimili na kutoka katika comfort zone ( uwanda wa starehe) na kustahimili misukosuko na kuweza kusonga mbele. Nidhamu itakulazimu kufanya jambo hata usilojisikia kulifanya huku ukiwa na taswira ya matokeo chanya.

5. KUKOSA MIFUMO YA UTENDAJI: Hii ni changamoto kuu hasa pale unaposhindwa kuandaa mifumo ya utendaji kuhamisha nadharia kuwa vitendo. Mifumo ya utendaji ni malengo, muda, nguvu na uwezeshaji mwingine. Usipojenga mifumo bora ya utendaji itakuwia vigumu kutenda yale unayoyajua. Yakupasa uwekeze zaidi.
Pasipo kutathmini kwa makini hizo sababu tutaendelea kuwa watu wa kujua mambo pasipo kutenda.

ACHA KUJILINGANISHA NA WATU WENGINE

Moja ya changamoto ambayo huwafanya watu wengi wasiishi katika furaha ni tabia ya kujilinganisha na watu wengine. Washindi hawajipimi kwa maendeleo ya wengine bali kwa maendeleo waliyonayo jana. Bill gates muanzilishi wa Microsoft aliwahi kusema kuwa kujilinganisha na wengine ni kujitukana mwenyewe.

Ukipenda kujilinganisha na watu wengine kuna hatari ya kudharau uwezo wako na kuanza kutazama  madhaifu yako na hii itakujengea tabia ya kutofurahi hata kwa vitu ulivonavo huku ukiwa unatazama zaidi vitu vya wengine au mafanikio ya wengine.

Ukijilinganisha na wengine utaua msukumo wako wa mafanikio kwasababu kuna ambao wamekutangulia katika safari ya maendeleo, kuna ambao wamepitia vikwazo vingi au kuna ambao wamepitia njia rahisi zaidi hivo si busara kujilinganisha na watu.

Weka malengo yako na ujipime kwa malengo yako na siyo malengo ya watu wengine. Kila mtu ana malengo na mitazamo yake na dhana kuu ya maendeleo ni mfumo uliotumika na sio matokeo. Matokeo hayawezi kuwa sawa kama mifumo ni tofauti hivo ukitazama tu matokeo unaweza ingiwa na hasira kwa kutopata matokeo sawa na mwenzako.

Ukipenda kujilinganisha ma wengine utaishi kama kivuli na hautokuwa na utambulisho wako. Wanaoshindwa huangalia zaidi wanaoshinda badala ya kuangalia ushindi. Usiridhike na mafanikio yako ya nyuma...unaweza kuwa zaidi ya hapo.

JE UNAWEZAJE KUJENGA TABIA YA KUTOJILINGANISHA NA WENGINE

1. JITAMBUE : Inakupasa kujitambua wewe ni nani, vipawa vyako, uwezo wako, maarifa yako na yale unayoweza kuyafanya. Jipime kwa hayo mambo na ujiulize Je unaweza kufanya zaidi ya hapo?

2. JENGA MIFUMO: Siku zote husipokuwa na mifumo ya utendaji yako iliyojengwa na mitazamo uliyonayo kuhusu maisha lazima utajaribu kujilinganisha na matokeo yanayopatikana na mifumo inayotumiwa na wengine.

3. EPUKA MANENO YA WATU : Mara nyingi tunajikuta wahanga wa kujilinganisha na wengine kutokana na misukumo tunayoipata kutoka kwa watu wanaotuzunguka kama wazazi, watu wa karibu n.k...Lakini lazima uwe na uwezo wa kutotafakari sana maneno ya watu hasa wale wanaokushinikiza kuwa kama watu wengine.

4. KUMBUKA WEWE NDIO KIONGOZI WA MAISHA YAKO: Inakupasa utambue wewe ni kiongozi wa maisha yako, maisha yako ni kama kampuni hivo yakupasa kujua mtu pekee ambayo ana wajibika zaidi ni wewe. Hata mzazi wako sio kiongozi wa maisha yako zaidi yako wewe. Hii itakusaidia kuwa na mtazamo wa ubunifu zaidi juu ya maisha yako.

5. ANGALIA MBELE : Dereva bora ni yule anayeangalia mbele anapoendesha gari na sio kuangalia pembeni wanaomu overtake au walio ktk mwendo sawa na yeye. Siku zote usitumie muda wako mwingi kutazama wanaoku overtake. Unaweza jifunza jambo lakini si busara kujilinganisha na waƓ

Kumbuka kipimo pekee cha mafanikio yako ni malengo yako na uwezo wako na sio kujilinganisha na wengine.


Wednesday, August 24, 2016

JENGA TABIA YA UKIMYA

Napozungumzia tabia ya ukimya nazungumzia ukimya wa nafsi na ukimya wa tabia na hata mazingira kwa ujumla. Jamii kwasasa imezungukwa na vivutio na purukushani nyingi ambazo haziruhusu au hazisababisha ukimya. Shida kubwa ni kwamba baada ya purukushani za kila siku kinachobaki katika nafsi ni upweke unaotokana na kutojenga muda muafaka kusikiliza nafsi yako na kutafakari.

Ukimya kwanza unakuwezesha kujitambua kwa kuwa utakuwezesha kujitafakari kwa utulivu vipawa na uwezo wako na kukuwezesha kufikiri kwa makini juu ya hatma ya maisha yako.Pia ukimya utakuwezesha kutambua ni maeneo gani katika maisha yako yanahitaji uangalizi ili kukuongezea thamani. Pia utakuwezesha kusikiza miongozo inayotoka ndani ya nafsi yako.

Utajua ni nini unachotaka na ni nini unachokiamini kwasababu umezungukwa na kelele nyingi za maisha...Kelele za mitazamo ya watu, maneno ya watu na hata changamoto za maisha. Usipojenga tabia ya ukimya utakuwa ni mtu mwenye hisia za upweke mara kwa mara maana muda mwingi utajikuta umeenda tofauti na nafsi yako na kufuata mvuto wa kelele zinazokuzunguka.

Kumbuka palipo na ukimya ndipo maarifa, hekima na amani ya nafsi hukaa, pia katika ukimya kunajengeka tabia ya kuwa macho juu ya mahitaji na hisia za wengine. Mahusiano ya watu ambao hawajajenga tabia hii huwa na lawama, malalamiko na mikwaruzano ya hapa na pale kwasababu ya kukosa ule muamko na kuwa macho juu ya mahitaji na hisia za wengine.

Mambo ya kufanya na kuzingatia ili kujenga tabia ya ukimya:-
1. Pendelea kuwa na tabia ya kukaa mwenyewe ukitafakari juu ya maisha yako pasipo vurugu au purukushani kutoka kwa watu wengine

2. Jenga tabia ya kutembea au kutembelea maeneo yenye utulivu na malihai kama miti, bustani nk

3. Penda kuwa msikilizaji, mtazamaji na mtu anayetafakari zaidi kwa kile anachokiona.

4. Penda kupangilia vitu vizuri maana siku zote mlundikano wa vitu hautokuruhusu kuwa na muda mzuri wa kutafakari.

5. Jenga tabia za kiimani kama kusali na kusikiza nyimbo za taratibu zenye kuinua nafsi.

Tuesday, August 23, 2016

OUR ATTITUDE MATTERS

The process of human change begins within us. We all have tremendous potential. We all desire good results from our efforts. Most of us are willing to work hard and to pay the price that success and happiness demand.

Each of us has the ability to put our unique human potential into action and to acquire a desired result. But the one thing that determines the level of our potential, that produces the intensity of our activity, and that predicts the quality of the result we receive is our attitude.

Attitude determines how much of the future we are allowed to see. It decides the size of our dreams and influences our determination when we are faced with new challenges. No other person on earth has dominion over our attitude.

People can affect our attitude by teaching us poor thinking habits or unintentionally misinforming us or providing us with negative sources of influence, but no one can control our attitude unless we voluntarily surrender that control. No one else "makes us angry." We make ourselves angry when we surrender control of our attitude.

What someone else may have done is irrelevant. We choose, not they. They merely put our attitude to a test. If we select a violent attitude by becoming hostile, angry, jealous or suspicious, then we have failed the test.

If we condemn ourselves by believing that we are unworthy, then again,we have failed the test. If we care at all about ourselves, then we must accept full responsibility for our own feelings. We must learn to guard against those feelings that have the capacity to lead our attitude down the wrong path and to strengthen those feelings that can lead us confidently into a better future.

If we want to receive the rewards the future holds in trust for us, then we must exercise the most important choice given to humanity by maintaining total dominion over our attitude. Our attitude is an asset, a treasure of great value, which must be protected accordingly.

Beware of the vandals and thieves among us who would injure our positive attitude or seek to steal it away. Having the right attitude is one of the basics that success requires.

Monday, August 22, 2016

FAIDA YA JUU SANA KATIKA KAZI

Faida ya juu sana aipatayo mtu kwa kufanya kazi sio anachokipata katika kazi hiyo bali ni anachokuwa katika kazi hiyo -John Ruskin

Watu wengi hutenda mambo au hufanya kazi fulani ili apate mapato fulani mfano mafao, pesa nk. Si jambo baya kufanya kazi au kujishughulisha katika mambo fulani kwa mapato fulani lakini sio mtazamo endelevu wa maendeleo. Robert Kiyosaki aliwahi kusema kuwa katika kazi yeyote angalia zaidi hiyo kazi ina manufaa gani zaidi katika kukuongezea maarifa na thamani.

Wekeza zaidi katika kuongeza thamani na hiyo ndiyo iwe faida yako namba moja. Unapojali zaidi thamani inayoongezeka ndani yako unajijengea msingi wa maendeleo endelevu. Thamani ya mtu ni uwezo alionao ndani yake na thamani ya mtu itamuwezesha kuendelea katika mazingira tofauti tofauti.

Unapowekeza katika kuwa na maendeleo ya nafsi mfano mitazamo chanya, maarifa endelevu, uwezo wa kustahimili na tabia za uwajibikaji unajijengea thamani zaidi ya pesa unazopata.
Kama unachofanya kinakuza mfuko wako lakini hakikuzi nafsi yako na kukujenga basi hakikusaidii sana maana pasipo thamani ukija kupoteza hayo mafao ni vigumu kutengeneza mazingira ya kuzalisha.

Thamani yako itakuwezesha kuwa na ufanisi katika eneo lolote. Hivo kwa mujibu wa John Ruskin hiyo ndiyo faida ya juu sana unayoweza kuipata. Hivo badala ya kuangalia zaidi malipo utakayopata angalia zaidi mabadiliko au thamani unayopata au utakayopata katika jambo ulifanyalo.

Sunday, August 21, 2016

MSISIMKO WA MAISHA

Je umekosa msisimko wa maisha? Jizamishe katika kazi unayoiamini kwa moyo wako wote, iishi kazi hiyo, na utapata furaha ambayo haukuidhania-Dale Carnegie

Moja ya changamoto kubwa kwa watu sasa hivi ni kukosa msisimko na msukumo wa maisha, Moja ya viashiria vya kukosa msisimko wa maisha ni upweke, lawama na kukosa msukumo wa kufanya mambo. Watu wanakosa ile furaha ya kuamka jumatatu asubuhi, wengine hadi wanaingiwa na hisia hasi ikifika jumapili jioni.

Changamoto hii inatokana na mazoea ya watu ya kufanya mambo wasiyoyapenda, mambo ambayo hayana uhusiano na hulka zao. Watu wanafanya kazi lakini kwa lengo moja nalo ni kupata pesa pasipo kuwa na ridhaa katika nafsi zao. Kwa mujibu ya mwanasaikolojia Abraham maslow binadamu anasukumwa kukua na mambo mengi lakini kuu kuliko yote ni nafsi yake kuridhika.

Nafsi yako isiporidhika na kuridhia kazi unayofanya jua kabisa lazima utakosa msukumo na furaha katika kazi hiyo. Utaanza kuingiwa na hisia hasi kila unapokumbuka kwamba kesho yake kuna kazi. Steve Jobs aliwahi kusema kuwa kama hujapata kitu unachokipenda endelea kutafuta maana maana kuu ya maisha ni kutafuta kusudi lako na kulifanya.

Kama kwa mtazamo wa Dale carnegie inatupasa kujizamisha katika kazi tunayoiamini kwa mioyo yote na kuziishi kazi hizo utapata furaha na hautokaa kusubiri Jumatatu ifike uruke katika kazi ya moyo wako na uzuri ni kwamba ukiishi kazi ya moyo wako hautokuwa na likizo.

Friday, August 19, 2016

NJIA ZA KUDHIHIRISHA MAONO YAKO

"Whatever you vividly imagine, ardently desire, sincerely believe, and enthusiastically act upon must inevitably come to pass!" - Paul J. Meyer

Tafakari ya ufasaha ni ngazi ya kwanza kabisa ya kufikia unachokitaka. Mara nyingi huwa tunatafakari bila ufasaha. Tunabeba maono makubwa lakini hatukai chini kutafakari maono hayo kwa ufasaha. Ni muhimu kukaa chini kutafakari kwa ufasaha maono uliyonayo.

Hitaji kutoka ndani ya nafsi ni ngazi ya pili kwa mujibu wa paul meyer ya kufikia malengo. Lazima maono yako uyatengenezee sababu na msingi wa ndani wa kihisia. Tengeneza msukumo wa ndani wa uhitaji katika kufikia malengo yako...Lazima utengeneze sababu ya kwanini unatakiwa ufikie malengo hayo.

Amini kutoka moyoni ni ngazi ya tatu kwa mujibu wa Paul meyer, ni lazima uwe na imani thabiti juu ya maono yako na imani hiyo isitetereshwe na aina yeyote ya mazingira. Ukiwa na maono lakini ukashindwa kuyaamini maono yako jua hautoweza kuyafikia.

Kisha unatakiwa uchukue hatua kwa msisimko na mhemko chanya. Lazima uchukue hatua kwa msisimko na mhemko chanya la sivyo hutoweza kuyafanya hayo maono yako dhahiri. Hatua iliyo na msisimko itakuwezesha kushinda vipingamizi au misukumo na changamoto hasi.
Kwa mujibu wa Paul meyer chochote kitafanikiwa ukifata hizo njia.

FEAR OF THE UNKNOWN

The Fear of the unknown is the Psychological paralysis caused by mystery of the unknown. Its one of the greatest challenges to progress because it kills the enthusiasm and the morale to progress to the clouds of what you haven't experienced or what you don't know.

This has paralysed many people with big ideas, it has paralysed individuals and caused them to be ANTAGONISTS to the FORCE OF CHANGE. Human being delights in COMFORT ZONE and any idea of CHANGE that hasn't been experienced before is often excused by the fear of the unknown.

But you can overcome the FEAR OF THE UNKNOWN by evaluating the vision and putting it down into realistic attributes, then GRAB on FAITH and DISCIPLINE while exercising the POSITIVE MINDSET.
Negativity gives power to the FEAR OF THE UNKNOWN. In life we need to understand that we either CHANGE willfully or THE FORCE OF CHANGE affects us violently leaving us with scars. Now that requires us to overcome the fear of the unknown.

The unknown is a mystery and it should be approached with enthusiasm and the joy of exploration...for whatever you don't know holds a part of your soul you haven't discovered yet...Pursue the experience and let Go of the fear of unknown.

Believe that God is there in the unknown ready to make it known to you. Let your life be of adventures and explore new experiences and overcome the fear of the unknown that keeps you from knowing the unknown.

Tuesday, August 16, 2016

JE UNA UHUSIANO NA UNACHOKIFANYA

Changamoto kubwa watu wengi wanayokutana nayo katika mambo wayafanyayo ni kukosa uhusiano wa kihisia baina yake na akifanyacho. Lazima kuwe na msingi na uhusiano wa kihisia na kinafsi baina yako wewe na unachokifanya.

Ukikosa huo uhusiano lazima ukose hisia ya kuridhia na kuridhika kwa kile ukifanyacho. Bado katika nafsi yako kunakuwa na utupu ambao husababisha hisia za upweke katika kila ukifanyacho. Kuna watu wengi wanafanya kazi au shughuli lakini wana upweke kwa yale wayafanyayo.

Nafsi yako inakosa uwiano na kile ukifanyacho. Uwezo wako unakosa msukumo kuelekea kile ukifanyacho. Ni changamoto kubwa pale unapotaka likizo ili upumzike kihisia ktk kile ukifanyacho maana kazi ya nafsi yako huwa haina likizo ya kihisia.

Ukiona msukumo wako unapungua na hauna ile shauku ya kuongeza msukumo kiutendaji katika jambo fulani ni dhahiri wewe na hilo jambo hamna uhusiano wa kimsingi wa kinafsi na kihisia. Lazima kuwe na uhusiano, tafuta jambo ambalo lina mahusiano na nafsi yako.

Monday, August 15, 2016

HUWEZI FANIKIWA ZAIDI YA MAWAZO YAKO

Watu wengi hupenda mafanikio na kukua lakini hawafanikiwi wala kukua. Kwasababu ya sheria moja ambayo ni kwamba huwezi fanikiwa zaidi ya mawazo yako. Maisha yako ya nje ni zao la mawazo yako.

Hakuna jambo linaloweza kutokea kama hujalifikiria kwa wakati wowote katika maisha yako. Unaweza kupenda kufanikiwa lakini je ulishawahi kufikiria na kutafakari mafanikio. Huwezi kuwa na fikra za ukomo halafu uwe na ziada. Mfumo wako wa fikra unadhiirika kwa kauli zako na mitazamo yako juu ya jambo fulani.

Ukishakiri kwamba jambo haliwezekani ni kwasababu umefikiria haliwezekani na halitokuja kuwezekana kwako hadi ubadilishe jinsi unavoliwaza hilo jambo. Hapo pekee ndo utaweza kufungua ubongo wako juu ya njia za kuliweza.

Myles munroe alishawahi kusema ugumu wa jambo fulani unatokana na ufahamu wako juu ya jambo husika hivo badala ya kushikiria mtazamo wako, wekeza kupata ufahamu zaidi juu ya hilo jambo. Huwezi ishi nje ya mitazamo yako maana mitazamo yako siku zote itachonga muundo wa maisha yako.

Friday, August 12, 2016

PROBLEMS AS OPPORTUNITIES

The factor that triggers your creativity and activates your positive mind is pressing problems. It is only when you are experiencing the pressure of problems and obstacles that you are motivated to perform at your mental best. Facing and solving the inevitable problems and difficulties of life make you stronger and smarter, and bring out the very best in you.

Most people do not understand the nature of problems. Problems are a normal and necessary part of life. They are inevitable and unavoidable. Problems come in spite of your best efforts to avoid them. Problems, therefore, come unbidden.

The only part of a problem over which you have any control is your response to your problems. Effective people respond positively and constructively to problems. In this way, they demonstrate that they have developed high levels of “response-ability”. They have developed the ability to respond effectively when unexpected or undesired difficulties occur.

Problems of all kinds bring out your very best qualities. They make you strong and resourceful. The more pressing your problems, and the more emotion you invest in solving those problems,the more creative you will become. Each time you solve a problem constructively, you become smarter and more effective. As a result,you prepare yourself for even bigger and more important problems to solve.

Thursday, August 11, 2016

IMPACTS OF YOUR COMPANIONS TO YOUR SUCCESS

Learn to surround yourself with people who will make impact, encourage and support you. Don't waste most of your time with people who don't care about your future but cares about what you drink this weekend and always want you to depend on them than be independent.

Surround yourself with people who will assist you to chase your dreams and wish you to be independent in life than dependent. People who want to see you succeeding in life and take care of your own bill.

Most of us would have been successful by now but the company we keep is dragging us down because they enjoy when people depend on them. Is time to have people who wish us good than those who want us to depend on them.

Your company either makes you or breaks you. Your company is either a burden or a drive. You have to be careful with the company you keep if you want to succeed. Most successful people have success connections and they don't entertain people below their league because they believe they don't have any challenge to offer them.

If eagles fly alone no matter the crowd of other birds that fly together. Eagles fly with their kind. Thus its very important to choose well the company we hang out with.

There are three kinds of company, the comrades, the confidants, the constituents.
The Comrades are people who walk with you because you have a common goal and once the goal is gone they also leave. Most school friends and colleagues are comrades,
The constituents are people who walk with you because they want something from you and once they get what they want they go,most people fall in this that's why relationships fail and hurt, friendship break etc.
The confidants are the people who stick with you unconditionally...they will be with you in the valleys,hills, good times and bad times etc.
You have to evaluate well the company you keep if you want to succeed.

Wednesday, August 10, 2016

NANI MUANDAAJI WA SCRIPT YA MAISHA YAKO?

Ni utaratibu kwa waigizaji wa filamu kuandikiwa muongozo wa jinsi ya kucheza tamthilia au filamu kwa kuvaa uhusika wa watu walio katika nadharia. Wao huvaa uhusika na kucheza kwa muongozo wa mtayarishaji mkuu.

Katika maisha yako ni nani mtayarishaji mkuu wa script unazocheza? Kuna kipindi lazima uvae uhusika wa mtu fulani aliye katika nadharia nawe umuweke katika matendo lakini ni muhimu sana kutambua ni nani mtayarishaji mkuu wa script zako.

Mtayarishaji mkuu anaweza akawa Mzazi wako, ndugu zako na hata majirani zako inategemea na nani umempa funguo ya kukushurutisha, unapompa utayarishaji mkuu mtu mwingine unaishi katika maono au nadharia ya mtu mwingine. Naye ndo anakuwa mtengeneza utaratibu wa maisha yako. Ni sawa na mtumwa, yeye huishi akifata utaratibu wa Bwana wake.

Unapoacha kuwapa watu wengine utayarishaji mkuu wa script za maisha yako ndipo unapoanza kuishi maisha yako, ndipo unapoanza kuishi ndoto zako na maono yako, tofauti na hapo unakuwa mtumwa wa maono na nadharia za watu wengine.

Changamoto kubwa ni kutengeneza script ya maisha yako na usimame imara kama msimamizi mkuu kwa vitendo na usikilize mawazo yale yanayoendana na hiyo script yako na sio siri ni lazima utapata upinzani kutoka kwa wale ambao wanataka kuwa watayarishaji wa script ya maisha yako na mara nyingi ni watu wale ambao hata wao walitayarishiwa script za maisha yao wanataka kuendeleza utamaduni huo.

Andaa miongozo, andaa script na uhakikishe unajenga mianya ya watu watakaokuwezesha kucheza vizuri script yako, wawe ni marafiki, wakufunzi nk.
Kumbuka unaanza kuishi maisha yako pale unapokuwa mtayarishaji wa script ya maisha yako .