Thursday, May 25, 2017

KUTOKA KATIKA UCHOVU WA KINAFSI

Uchovu wa kinafsi ni hali ya nafsi ya mtu kukosa nguvu ya kusimama ili kuweza kuhimili mitikisiko hasi. Ni hali ambayo kama ikiingia humjenga mtu kutaka ukombozi wa kinafsi na pumziko.

Kila uchovu unahitaji pumziko lakini njia za kupata pumziko ina utofauti. Kuna pumziko la kudumu na lile lisilo la kudumu. Watu wengi wamekuwa wakishindwa kutofautisha mapumziko hayo kutokana na kukosa taswira hada hasa pale uchovu unapokuwa mkubwa.

Changamoto kubwa ni uchaguzi wa pumziko la nafsi yako maana waweza fanya uchaguzi wa kudumu au wa muda mfupi ambao utakupa uchovu mkuu baada ya ganzi ya pumziko hilo kuisha.

Ili uweze kuchagua pumziko la kudumu ni lazima ujue chanzo kikuu cha uchovu wako wa kinafsi maana vichocheo vya uchovu huo mara nyingi ni kama mchwa ambao hukula taratibu nguvu yako ya kinafsi na kukuacha mchovu.

Unaweza pata uchovu wa kinafsi pale unapojaribu jambo linashindikana au pale unapotaka kubadili jambo inashindikana, unapotaka kubadili hali fulani lakini inashindikana au inaweza ikawa jambo fulani linakushambulia kila wakati ambalo unajaribu kuliepuka, au yawezakana ni watu ndo wanakupa uchovu wa kinafsi pale wanapoila amani yako, wanaposhambulia nguvu yako ya kusimama, na kutenda yale yanayovuruga misingi yako. Unaweza pata uchovu wa kinafsi na pengine ukajaribu kupata pumziko lakini ukashindwa katika uchaguzi wako ni lipi pumziko hasa unalohitaji.

Ukishindwa kujua hasa ni pumziko gani unalohitaji waweza jikuta unapata pumziko la muda mfupi ambalo likawa kama kilevi cha nafsi kisichokupa suluhisho la kinafsi la kudumu bali kinakupa nafuu ya muda mfupi tu.

Ukitaka kuondoa uchovu wa kinafsi siku zote jaribu kujitia nguvu kwa kuelekea zaidi pale ambapo panakutia nguvu, panakupa amani, panakupa mguso chanya, pana uwiano na kile unachokiamini, na pana misingi ya kiutu yenye uhusiano na nafsi yako.

Uchovu wa kinafsi humkuta kila mtu kwa wakati fulani lakini tofauti inakuja katika uchaguzi wa mapumziko. Waweza jikuta unajiingiza katika pumziko la muda mfupi ambalo badala ya kuitia nguvu nafsi yako linazidi kukudhoofisha.

Chagua vyema pumziko la nafsi yako ili uweze kuushinda uchovu wa kinafsi.

Thursday, May 18, 2017

IMANI NI MSINGI WA AMANI YA NAFSI

Imani ni kuwa na hakika ya mambo yasiyoeleweka au ambayo hayajabainishwa kwa wakati huo. Imani hukupa nuru ya kutambua mafumbo ya kinafsi na maswali yasiyo na majibu yenye kuleta taharuki katika nafsi.

Nafsi inaweza kupitia mambo fulani ambayo yanaikosesha amani na kuifanya ibaki katika hamaki kutojua ni nini kinachofuata au nawezaje kutoka katika hali fulani ya mkwamo wa kihisia au kimtazamo na kiakili. Hapo ndipo imani huja kuleta amani.

Imani inatakiwa iongoze hisia na iziweke katika hali ya utulivu. Ni vigumu kupata tulizo la kihisia bila kuweka mfumo bora wa kiimani, Ukitazamia kutoka katika mkwamo huo, ukitazamia utulivu wa hisia na ukitazamia uzuri na mambo mema yajayo.

Muda wote imani hujengeka katika msingi imara wa hatma ya kesho yenye furaha, faraja na uzuri na pia hujengeka katika faida ya leo katika mazingira hayo magumu. Imani hutazama fundisho, hutazama uzuri na  hutazama uimara unaotokana na ugumu na changamoto husika.

Siku zote ukitaka kuwa na amani katika nafsi yako boresha mfumo wako wa imani, boresha mfumo wako wa kuamini, jikite katika kutengeneza imani zenye tija, imani zenye kukujenga na kukuimarisha. Na ukishapata msingi husika iache imani hiyo iamuru hisia zako zitii.

Imani ikisema nitatoka katika hii hali, ikasema nitavuka katika hili daraja la maumivu, ikasema nitapata kilicho bora, Hakuna hisia ya maumivu itakayoweza kukushikilia kwa muda mrefu au hata kukuzamisha. Utakuwa ni mtu mwenye amani muda wote.

Thibitisha imani zako kwa kuzipa msingi imara kwa kuzifanya sheria za nafsi yako. Imani juu ya uzuri wako, imani juu ya stahiki yako na yale unayoyatarajia na yenye kukupa amani ya nafsi, hakikisha unajijenga na kujithibitisha katika imani hizo kwa kusimama bila kuyumba kama hisia za taharuki na uchungu zikija.

Huwezi kuwa na amani ya nafsi kama huna imani na hali fulani, kama huna imani na jambo fulani, kama huna imani na watu fulani. Ni vyema ukajiimarisha katika imani na siku zote hakikisha imani yako inajengeka katika kweli. Huwezi jenga imani kwa kitu cha uongo. Imani lazima isimame katika misingi ya kweli, fikra chanya, ubora wa nafsi na utu.

Monday, May 15, 2017

CHUNGA MOYO WAKO

Chunga moyo wako maana hiyo ndiyo bustani ya amani na furaha yako. Nafsi yako hustawi katika bustani ya moyo wako. Katika bustani ya moyo wako kunaweza kuwa na maua ya furaha, amani na faraja au magugu ya maumivu na uchungu. Kuwa muangalifu sana kwa kuchunga moyo wako kila wakati ni nini kinachoota.

Kuna mawazo na maneno ambayo ukiyaruhusu yaingie moyoni yanaenda kuweka majeraha ambayo kupona kwake kutakuchukua muda sana. Majeraha hayo yatajenga mfumo wa kifikra wa kujihami ili kuzuia maumivu mengine. Hasara ya fikra za kujihami ni kwamba utashindwa kufurahia uhuru na uzuri wa maisha kwa kuwa utaishi kwa kujihami.

Moyo wako unatakiwa ulindwe kama ngome imara. Ukiruhusu maumivu au matatizo yakaingia katika bustani ya moyo wako yataenda kuotesha magugu ya mawazo na fikra hasi. Kuna maneno ukiyaruhusu kuingia siku moja yatautesa moyo wako wakati wote. 

Safisha moyo wako kwa kuondoa yale ambayo yanauumiza na kutesa moyo wako. Yale ambayo kila ukiyafikiria unasikia kama kichomi ndani ya moyo wako, yale ambayo kila ukiyapa nafasi katika akili yanakububujisha machozi ya uchungu moyoni mwako.

Tambua kuwa moyo wako unatakiwa kustawisha amani, furaha na upendo. Ukiwa na moyo wenye uchungu inageuka kuwa sumu inayodhoofisha nafsi yako na akili yako. Utakuwa mtu mwenye vifungo badala ya uhuru.

Chunga moyo wako na uache katika amani. Usiuache umekaa katika dimbwi la maumivu au usiuache ushikilie uchungu unaokuumiza, usiuache ushikilie maneno makali au misumari ya mitazamo hasi juu yako. Usiruhusu moyo wako udunde kwa kasi kwa kukosa amani au kuwa na taharuki, Jipe utulivu kwa kuruhusu uzuri na furaha istawishe moyo wako.

Ruhusu yale yenye furaha na amani na yenye uzuri na utulivu ndio yakae katika moyo wako. Stawisha moyo wako ili ukutunze na uachilie yale yenye furaha, amani na pumziko. Kama vile damu inavoingia na kutoka katika mkondo wa mishipa ya damu, wewe pia tengeneza mkondo wa kuingiza furaha nyingi, amani nyingi na faraja nyingi moyoni mwako kwa kukaa na watu au mazingira yatakayosaidia hivo vitu lakini ondoa moyoni mkondo wa maumivu, uchungu na yale yanayoutatiza moyo

Lazima kuwe na uwiano baina ya yanayotoka na yanayoingia, usipende kuingiza mawazo hasi, Itafute hiyo furaha na amani ili ustawishe bustani ya moyo wako.

Fikra chanya au mazingira chanya sio tu yale yanayokusukuma kufanikiwa bali pia kuustawisha moyo wako na kuuacha katika hali ya utulivu.

Saturday, May 6, 2017

ALWAYS KEEP A JOYFUL DEMEANOR

Our strength lies in our ability to always keep a joyful demeanor in the face of our problems-Nickvaleries

Life has its ups and downs, Life has negative situations that can hit us or hurt us and we find it hard to be joyful but joy has to be founded from our souls.

When we believe in our worth and have the mentality that there is always something better ahead and that we will always receive the desires of our souls then we generate a joyful spirit and demeanor.

There is no reason to stay in sorrow and pain when you know that the best is out there heading your way and you ought to be ready and step towards it. Pain and sorrow will try to drown you in a state of emotional stagnation but rise up, smile and say to yourself that am heading to my best. Darkness is for a night but joy comes in the morning.

Always choose to be joyful and find joy at whatever costs by changing your belief from a victim to a victor of circumstances. If things change dont stay there drowning yourself. Get up and heal your soul of the pain and choose to keep a joyful demeanor.

Just say to yourself it is well with my soul then believe that you are heading for the best out there. Tell your heart you are not hurt but you are strengthened then find your rythm and be happy. Smile for your beauty and peace awaits.

The Universe will always smile back if you smile at it. Its just a matter of time till you find love, happiness and joy again. But for now keep a joyful demeanor and attitude.

Tuesday, May 2, 2017

USICHUKULIE KILA JAMBO KIHISIA

Ukitaka kuwa na furaha usipende kuchukulia kila jambo kinafsi au kihisia. Kuna mambo mengine ni ya kifikra tu na yamekaa kimtazamo tu ambayo hayatakiwi kuchukuliwa kihisia.

Ukitaka kuwa na utashi wa kihisia na uweze kuratibu hisia zako katika mlengwa chanya yakupasa kuziacha hisia zako katika mfumo tulivo kadri uwezavyo. Kuna mambo ukiyachukulia kihisia utaziweka hisia zako kwenye mfumo wa taharuki kwa wakati mwingi na itakupunguzia msisimko wa maisha ulio katika muundo chanya.

Je wawezaje kutochukulia mambo kihisia? Tambua kuwa kila wazo au mtazamo unapaswa kupokelewa kiakili na kuratibiwa kabla ya kusukumwa na hisia fulani. Ni vizuri ukiratibu mawazo na mitazamo unayopokea na kuiratibu kabla ya kujua ni hisia gani uiachilie ili isukume hilo jambo.

Ni muhimu sana kulishikilia wazo au mtazamo katika mfumo chanya hata kama limekuja katika muundo hasi. Lione hilo wazo kama njia ya kukuboresha, yaone hayo maoni kama njia ya kukuboresha kisha yape hisia chanya ndipo uyapokee. Usikubali kuanza kupokea kihisia wazo ambalo hujariratibu kwa akili.

Mfano mtu anaweza kukwambia jambo ambalo unaona kabisa linaweza lisiwe chanya kwako, badala ya kulipokea kwa hisia hasi jaribu kuliona ilo jambo kama wazo la kukuboresha na sio kukuharibu, kisha chukua hisia ya amani na furaha kwa kutambua kuwa hilo wazo limekuja kukuboresha..kisha chukua hisia ya morali na ari ya kulitafutia ufumbuzi na kulishughulikia hilo jambo na sio vinginevyo. Ukilipokea kama vile limekuja kukuumiza utaingiwa na taharuki ya kinafsi pengine hata kujenga ukuta kulizuia hilo suala na kuonekana kuwa ni mtu dhaifu kinafsi pengine hata mtu hasiyependa kuambiwa ukweli.

Nakushauri tena usilipokee kila jambo kihisia kabla ya kuriratibu kiutashi na kiakili ili kukujenga utashi wa kihisia itakayokupa furaha wakati wote.