Tuesday, March 28, 2017

JENGA UTASHI WA KIHISIA

Uimara wa mtu katika nafsi umejikita zaidi katika utashi wake wa kihisia. Binadamu ni kiumbe chenye nafsi na nafsi ya mtu imeundwa katika mfumo wa hisia. Hisia za mtu pia zimeundwa katika mfumo wa utu wake. Kila mtu ana muundo wake wa kiutu ambao ndio msingi hasa wa uratibu wa hisia za mtu huyo.

Hisia ni misukumo na mihemko ya kinafsi ambayo hujitokeza kutoka kipindi hadi kipindi kutokana na mabadiliko ya ndani au nje. Yaweza ikawa mabadiliko ya kimazingira au mabadiliko ya tabia za mwili. Changamoto kubwa ya hisia ni kwamba ni kama upepo, huja na kufika katika kilele lakini baadaye hushuka katika ukawaida na pengine hushuka zaidi ya hapo.

Hapo ndipo wengi hujikuta wanasema leo najihisi niko chini sana kihisia au nimezama katika hisia na hata wengi hutumia kauli za vitabu vya dini na kusema leo nimezama katika bonde la uvuli wa mauti. Lakini hao hao watu nyakati nyingine utasikia anasema leo nina msisimko au leo niko hewani. Yote hayo ni mabadiliko ya kihisia.

Hisia zinaweza kuwa nzuri kama zikitumika vizuri lakini changamoto kubwa ni pale mfumo wa uratibu wa kimaamuzi katika akili unapofungwa katika hisia ambazo zinapanda na kushuka. Kuna ambao wamekuwa na utashi wakufikiria lakini wamekosa utashi wa kihisia.

Utashi wa kihisia ni uwezo wa kuratibu hisia zako na kuzielekeza vile unavotaka. Watu wengi tumekuwa na utashi wa ki akili lakini tumekosa jambo la muhimu sana ambalo ni utashi wa kihisia kupelekea yale tunayoyajenga kwa akili zetu yanaharibiwa na hisia zetu.

Waweza fikiria jambo zuri na ukaliwekea mikakati madhubuti lakini kinapofika kipindi cha mtikisiko unaogusa hisia ,wengi wetu tumejikuta tukiruhusu hisia zetu ziharibu hata ule mtazamo chanya wa yale tuliyoyajenga kwa akili zetu.

Watu wengi waliofanikiwa au wakuu wamejikuta wakianguka na kufanya maamuzi mabovu kwasababu ya kukosa utashi wa kihisia na wamejikuta wakizama katika dimbwi ambalo pengine kusababisha zile imaya walizozijenga kwa akili nyingi kuanguka kutokana na kukosa utashi wa kihisia.

Wekeza sana kuwa utashi wa kihisia uweze kutambua ni hisia zipi zinakujenga na zipi zinakubomoa. Hisia zipi zinakuimarisha na hisia zipi zinakudhoofisha, hisia zipi zinakuinua na hisia zipi zinakuangusha. Ukiwa na utashi wa namna hiyo utaweza kuzitumia hisia hizo ziweze kukutumikia na sio wewe kutumikia hisia zako.

Je wawezaje kuwa na Utashi wa kihisia

1. Pambanua hisia zako pindi zinapokuja na utambua mlengwa wa kila hisia.

2. Tambua chanzo cha hisia husika au mifumo sababishi ya kutokea kwa hisia hizo.

3. Jifunze kuzimudu hisia kila zinapokuja kwa kuifanya nafsi yako izungumze na hisia hizo

4. Tambua kuwa hisia sio jambo baya na wala sio udhaifu bali ni muundo wa kinafsi hivo hisia zako zikubali kuwa ni zako na wewe ndio mwenye kuwajibika kwa hisia hizo. Usitafute kisingizio juu ya hisia zako.

5. Jiimarishe katika uvumilivu ili uweze kuziratibu hisia zako na kuratibu mkondo wa hisia zako maana hisia ni kama mkondo wa maji

6. Pendelea kutenga muda wako wa upekee ukizungumza na nafsi yako ili uweze kuthibitika katika uimara wa kihisia.

Hakuna jambo la msingi na lenye kufaa kama kuwa na utashi wa kihisia maana maisha yako yanaweza kuwa yenye furaha na amani au kuwa na shida na maumivu kama hauna utashi wa kihisia.

Saturday, March 25, 2017

MUDA WAKO WA UPEKEE NA NAFSI YAKO

Ukitaka kuwa na furaha anza kwa kufurahia muda wako wa upekee.

Moja ya changamoto tulizonazo kama binadamu ni upweke. Upweke sio ukosefu wa wenza au watu wa kutuzunguka. Upweke ni pale mtu anaposhindwa kuufurahia upekee wake na anaposhindwa kuwa na uhusiano na uhalisia wa nafsi yake.

Kuna malalamiko mengi unasikia hata katika mahusiano mmoja wao anasema nilijihisi mpweke ndo maana nilikusaliti, au mwingine anaingia katika ulevi au hata mikanda ya ngono kwa sababu ya upweke. Tafsiri yetu ya upweke ni kukosa watu wa kutengeneza muungano wa kinafsi au watu wa kuburudisha nafsi zetu.

Nafsi ya binadamu kila wakati inahitaji kurutubishwa kwa kutengewa muda wa kupata uwepo. Nafsi yako ni utu wako wa ndani. Mtu wako wa ndani anahitaji wewe umtengee muda kumsikiliza, kumdadisi, kuzungumza naye, kumburudisha na hata kumponya na aina yeyote ya maumivu.

Lazima ujitengee muda wako wako bora wa kutengeneza mguso wa kimaelewano na nafsi yako. Watu wengi wameshindwa kuwa watu wa namna hiyo kupelekea kupigwa na upweke kila wakati anapokosa mguso wa nje wa watu wanaomzunguka.

Rafiki yako wa kwanza na wa karibu ni nafsi yako. Itengee muda nafsi yako ili ipate ukaribu wako. Na wakati wa kuzungumza na nafsi yako jua kwamba unaongea na mtu wako wa karibu. Acha kuongea na nafsi yako kwa ukali au kuihukumu kwa makosa ya nyuma. Itie moyo nafsi yako, ikumbushe uwezo wako. Panda mbegu chanya ndani ya nafsi yako, itie moyo, iponye kwa makosa ya nyuma na iahidi mambo mazuri huko mbele, iburudishe kwa lugha nzuri yenye mguso chanya lakini kuu kuliko yote iweke huru.

Watu wengi wamekuwa wakitumia wakati wao wa upekee kwa kulala, kuangalia mitandao ya kijamii au hata kutafuta magenge ya umbea kutafuta jambo la kufanya kuondoa upweke nk. Huo sio wakati wake. Huo ni wakati wa kujenga uhusiano na nafsi yako. Ni sawa na aina yeyote ya uhusiano. Lakini uhusiano wako na nafsi ndiyo jambo la msingi kwanza.

Ukiwa na tabia ya kuwa na muda mwingi na nafsi yako hautokuwa mtu wa kulalamika upweke. Na hautokuwa mtu wa kutafuta vileta msisimko vya nje kama pombe, anasa na ngono pale unapojihisi mpweke. Utaufurahia muda wako wa upekee, nafsi yako itarutubishwa na utakuwa ni mtu mwenye furaha muda mwingi.

Angalizo ni kwamba katika muda wako wa upekee na nafsi yako hakikisha unatengeneza mazingira chanya. Huwezi kutengeneza mazingira hasi ya mawazo na hisia hasi au muingiliano na mambo yasiyojenga halafu utegemee nafsi yako itajiachilia. Nafsi yako itajenga ukuta wa kujihami maana ndivo mwanadamu alivo kiakili katika maisha yanayoonekana kama mapambano.

Pia usipende kuipa nafsi yako maumivu yasiyokuwa na sababu na mara nyingi pale akili yako inaposhindwa kuendana na misingi ya nafsi yako. Na usipende kuipa nafsi yako vifungo kwa kufuata njia ambazo unajua nafsi yako haiwi huru kuchanua.

Thursday, March 16, 2017

KUWA NA UHUSIANO NA UHALISIA WAKO

Kila binadamu ana uhalisia wake na utofauti wake, binadamu wanaweza fanana tabia lakini kuna msingi wa ndani kabisa wa kinafsi unaowatofautisha. Huu msingi wa kinafsi ndio uhalisia wa yule mtu. Mtu yeyote anayetoka katika uhalisia wake anapoteza utambulisho wake na akipoteza utambulisho wake anapoteza mambo mengi ya kinafsi yaliyomo ndani yake maana inambidi atafute uhalisia mwingine na alazimike kuishi katika uhalisia huo.

Kuna mambo mengi ya kinafsi ambayo mtu hupoteza na kuu kuliko yote ni amani ya nafsi na furaha ya ndani. Hapo ndipo unakutana na mtu ana kila kitu lakini hana furaha wala amani, yamkini kuna mambo kadha wa kadha yanayomtatiza lakini kuu kuliko yote ni kupoteza uhalisia wake. Kuna mambo yanayompa mtu ujasiri wa ndani, kuna misingi ya kinafsi ambayo mtu anakuwa nayo inayompambanua. Akipoteza hivo vitu au akitoka nje ya hivo vitu utaona mabadiliko yake kimtazamo na hata kihisia.

Katika uratibu wa kihisia na kutengeneza uimara wa kihisia mtu lazima arudi katikà uhalisia wake. Watu wengi wamepoteza dira katika mambo mengi kwasababu walitoka katika uhalisia wao ndipo wanakuja kushtuka wameshapotea na wakajikuta wanaishi kama wahanga wa mambo pasipo kujua nini cha kufanya.

Jitambue na jitambulishe na jiimarishe katika uhalisia wako maana utakapokuja kutoka katika uhalisia huo utajaribu kuwa kitu au mtu ambaye haumuelewi hata wewe. Unakuwa kama mtu usiyejitambua, Rudi katika uhalisia wako ili urudishe ile morali na msukumo na msisimko wa ndani kufanya mambo.

Ukiwa katika uhalisia wako mazingira ndo yatalazimika kuendana na uhalisia wako lakini tofauti na hapo wewe ndo utalazimika kuendana na mazingira. Uhalisia hukupa wewe uhuru wa kujipambanua na kujiwasilisha katika jamii ili uwe na mguso chanya. Uhalisia wako ndio hupelekea wewe kutambua kusudi lako na hata kuongeza thamani yako ili ulitende kusudi lako. Hivo ni muhimu sana kuwa katika uhalisia wako.

Jamii au mazingira yasikufanye upoteze uhalisia wako. Jamii ndo inapaswa ipishe njia ili uhalisia wako uweze kuwa na mguso na hii itawezekana tu ukisimama katika kulinda uhalisia wako

Sunday, March 12, 2017

HOW TO DEAL WITH FEAR

Do you know that fear is false evidence appearing real? Sometimes in life you will be faced with situations whereby there will be evidences that are false appearing real. Fear will torment you and leave you paralysed. The only cure to fear is faith. Believe beyond circumstances. 

Clear your mind of the Past : You will always be free as your mind is free. The battlefield is always in your mind. Its a point where strongholds of the past are. The strong holds of fear and other dissapointments. Experience should make you wiser in terms of strategies and how you perceive life. But always free your mind as much as possible.

Something is about to happen in your life: Things happen all the time, good or bad but its always dark before dawn. We pass through darkness to experience the light. We pass through trouble to appreciate calmness. No darkness comes after darkness until afternoon passes. Always believe that the next phase of your life will always be better than the previous. Try to find the rainbow after the storm because its there. Dont be afraid that later will be like the former. There will always be changes in every stage of your life.

Find beauty and peace: You will never be happy unless you are at a state of beauty and peace and tranquility. We often look at the beauty without but not the beauty within. We all want to be in tune with our inner self. Our core values and our inner being, but we often times try to find this in the wrong places. We should always be in the quest to find beauty and nirvana and where its connected.