Thursday, September 22, 2016

UHURU NA UDHIBITI WA KIHISIA

Uhuru wa kihisia ni pale unapoweza kudhibiti na kuelekeza hisia zako katika muundo na mpangilio uutakao. Hili si jambo rahisi kwa maana hisia huja kutokana na mabadiliko ya ndani ya mwili na hata hujengeka katika msingi wa nafsi ya mtu hivo uhuru wa kihisia unawezekana pale tu unapojenga tabia inayoitwa Nidhamu.

Nidhamu itakuwezesha kudhibiti hisia zako kwa namna kwamba utaweza kuzielekeza au kuamua muitikio na hata namna ya kukabili hali fulani zinazojitokeza. Uhuru wa kihisia kwanza unajengwa na kuitambua nafsi yako....nguvu na mapungufu yake kisha kujenga msingi wa kimaamuzi unaotokana na sheria utakazozijenga katika akili yako.

Hisia ni kama upepo, huja na hupoa na pengine hata kupotea kabisa, upepo huo unaweza kuwa kimbunga kwako au unaweza kuwa kama kipupwe kutokana na misingi ya kinidhamu ulioijenga katika nafsi yako ambayo inakupa uhuru wa kuamua jinsi hisia zako zinavodhibitiwa. Kudhibiti hisia ni sawa na kujenga mifereji ili kudhibiti mikondo ya maji isilete madhara au isielekee kusikotakiwa.

Ukiwa mfungwa wa hisia inamaana utendaji wako au muitikio wako katika mambo utatokana na msukumo wa hisia ulizonazo. Umeshawahi kuwa hisia nzito juu ya mtu fulani au jambo fulani kwa wakati fulani na ukatamani kulifuatilia lakini baada ya muda unapoteza hiyo hisia? Na hii hasa ndio changamoto ya kufanya maamuzi kwa kufuata hisia.

Jenga utaratibu wa kinidhamu wa kuratibu hisia zako kisha zielekeze kuongeza msukumo ktk sheria ulizozijenga na wala usiruhusu hisia zako zikuelekeze kupingana na sheria zako...namaanisha usiruhusu hisia pinzani zipate nguvu. Hisia zote zielekeze unapotaka ziende. Na hii inahitaji mazoezi.

Warren buffet aliwahi kusema kuwa mtu asiyeweza kudhibiti hisia zake hawezi kudhibiti pesa zake. Na hilo ni jambo la kweli kabisa, usipoweza kuwa nidhamu ya kihisia huwezi kuwe na nidhamu ya kiuchumi

Pia usipokuwa na uhuru wa kihisia utakuwa mhanga wa maumivu mengi ikiwemo mahusiano au hata namna watu wanavoleta upinzani katika maisha yako. Watu wasio na uhuru wa kihisia mara nyingi hushindwa kuchanganua ni aina gani ya mahusiano ni mazuri kwao na yatakayowajenga, kwao hisia zikishatawala wanashindwa hata kuruhusu akili zao kuchanganua.

Maisha bila uhuru wa kihisia ni kama msitu maana kila aina ya mabadiliko yatakuwa na mguso kwako na utataka kuitikia kila ambavyo hisia zitakutuma. Lazima uwe huru kuzidhibiti hisia la sivyo zitakuzamisha.

Saturday, September 17, 2016

JENGA MSUKUMO WA NDANI

Binadamu yeyote hutenda mambo kutokana na msukumo fulani. Misukumo iko ya aina mbili. Kuna msukumo wa nje na msukumo wa ndani. Watu wengi hutenda mambo kutokana na msukumo wa nje ambao unahusisha mazingira fulani au faida na matokeo fulani. Sio jambo baya kuwa na misukumo ya nje inayopelekea wewe kutenda jambo lakini changamoto ni kwamba ukiwa na msukumo wa nje zaidi inaweza pelekea kuwa na mguso tofauti.

Misukumo ya nje inaweza kubadilika muda wowote na hii itakupelekea kupoteza kabisa ile ari ya utendaji. Unaposukumwa kutenda jambo kwa ajili ya faida fulani itapelekea kuwa na hamaki pale hasara inapokuja au kukosekana kwa faida husika. Ukisukumwa zaidi na mazingira jua hayo mazingira yanaweza kubadilika muda wowote mfano unaweza pangiwa kutoka Dar es salaam kwenda dodoma. Hii itakusumbua sana katika kupata uwiano wa kihisia.

Ni muhimu kujenga msukumo wa ndani uliojengwa katika msingi wa mambo matatu..Moja ni Uongozi wa maisha yako, Thamani na mwisho ni kusudi.

Uongozi wa maisha yako ni msukumo wa ndani ulio na mtazamo na uthibiti wa muelekeo wa maisha yako. Ukijua ya kwamba wewe ndio mwenye jukumu ya kutengeneza muelekeo wa maisha yako itakupa msukumo wa utendaji kwa maana utajua kila wakati kuwa unalolifanya linatengeneza muelekeo wa maisha yako.

Thamani ni msukumo wa ndani uliojijenga katika mtazamo kuwa kila jambo unalolitenda unalifanya ili likujengee uwezo na ufanisi, likufanye mtu mwenye uwezo zaidi na mwenye ufanisi zaidi...uwe mtu wa thamani na bora. Ndio maana faida kubwa katika kazi sio unachokipata baada ya kazi bali ni unavokuwa baada ya kazi ( Thamani yako)

Kusudi ni msukumo wa jambo uliojijenga katika mtazamo kuwa unafanya jambo kwasababu lina maana kwako na jamii inayokuzunguka. Utasukumwa kufanya jambo kwa sababu lina maana kubwa ndani yako na kwa jamii yako.

Ukiwa na misukumo hiyo mitatu ya ndani katika kila jambo ulifanyalo, kila siku utakuwa na ari na msisimko kufanya mambo na hautopoteza hamu ya kuamka asubuhi kuiendea siku kwa furaha.

Thursday, September 15, 2016

ACHA YA JANA...ISHI YA LEO

Usiruhusu yale ya jana yachukue muda mwingi wa leo- Willy rogers

Moja ya changamoto kubwa katika maisha yako ya leo ni kumbukumbu ya jana yako. Jana yako unaweza kuitumia katika tathmini yako kukuwezesha kuwa na mtazamo chanya na wa fadhila hasa ukikumbuka ulipotoka na kushukuru kwa hapo ulipo huku ukitazama unapoelekea.

Changamoto kubwa ni pale jana yako inapochukua muda mwingi kihisia na hata kimtazamo kiasi cha kukufanya kushindwa kuiishi leo yako. Jana yako inaweza kuwa mtego wako hasa pale unapokuwa na hisia zilizoshikamana na jana hiyo. 

Kuna watu wengi wameshindwa kuachilia jana yao kiasi cha kutotazama fursa katika leo yao na kuacha fursa hizo zikipotea.

Wengi wameingia katika mahusiano leo na kumbukumbu la jana yao...Wengi wao wanataka kuishi leo lakini bado hawajaachana na jana yao. Ukiona unatamani sana jana ni dhahiri umepoteza dira ya leo na kesho yako. Kuna mambo mengi ya jana bado hutaki kuyaachilia na yamekuwa mzigo kwa leo yako.

Huwezi furahia leo yako kama jana yako inachukua sehemu kubwa ya moyo wako, akili yako na nafsi yako. Wengi leo wanaingia katika mahusiano huku bado hawajaacha kutazamia mahusiano ya jana yao. Wanajaribu hata kulinganisha leo na jana yao. Kuna wengine ambao pia hawajaacha machungu ya jana yafe, bado wanayapa nafasi katika akili yao kufikia hatua ya kuteswa na hofu ya kuishi leo katika ukamilifu.

Sikiza leo haiwezi kuja kama jana haijafa, Kesho haiwezi tokea kama leo haijaisha. Acha kuchelewesha furaha ya leo, fursa ya leo, nuru ya leo kwa kuendelea kukaa katika giza la jana..Weka pembeni na uiishi leo yako kwa furaha. Acha ya jana yawe ya jana...Ganga ya leo.

Thursday, September 8, 2016

INVEST IN YOUR CHARACTER

One of the greatest investments you can make is investment of character. Character is the only virtue you can use to make an impact in your life. Unless you invest in your character your life wont be in alignment with Excellence.

All aspects of life are attributed to character. Your approach towards life will always depend on your character. That's why you should always invest in character. Those who impact people and even society are people who have distinguished themselves in character.

Invest in having moral strength, refuse to have a low mentality. Small things shouldn't intimidate you. Don't complain about things you cant change. Just be involved and take full responsibility over your life. Believe in yourself. Get rid of self doubts, invest in knowledge and your doubts will flee.

Create a suitable environment for you to grow, establish connections. Wherever you are be there, make an impact. Don't just follow the crowd, don't just be a follower, you are destined to be a leader and a leader must have character.

How you speak, how you act, how you approach matters, Your overall composure is necessary, Don't be panicky, be calm...Have an evaluative mindset. Be positive even when others seem negative...Let your light shine among men. Positive mindset attracts positivity.

Instill hope when there's discouragement, make people feel happy about life, be a person of humor and infect your domain with hope and joy. If you cant change it then no need to complain about it.
But one very important thing to remember is Whatever character you invest in will impact you and your generations

Tuesday, September 6, 2016

POWER OF PASSION IN PROGRESS

The greatest virtue one can have that assures progress is passion. Passion is the driving force of motivation. Without passion the heart lacks meaning, the actions lacks enthusiasm and the mind lacks creativity.

When you have passion you inspire innovation. When you always work in the circle of the usual that means you lack the passion.

Passion inspires excellence. If you lack the passionate heart concerning something then it isn't worth it. The bible says God looks for a passionate heart. When you are passionate about something you go the extra mile.

Passion develops Perseverance  which means you can push forward even when all odds are against you. Passion brings about internal peace and joy to do what you want. 

Which means you do something with the satisfaction. As the self actualization concept of Abraham Maslow with passion you have satisfaction which is the highest need of a person.

Always understand your passion and most of all develop passion about the things you do.

How can you develop passion to progress:-
1. Discover your talents and abilities : the greatest discovery a man can do isn't discovering an ipad, light bulb or anything tangible but the discovery of one's talents and abilities. Never undermine your talent discovery. A talent is something you do easily and effectively and excellently with little strength but brings maximum satisfaction and joy. A talent isn't a hobby..a hobby is something you love to do but a talent is something you can do excellently that others cant.

2. Love yourself : Realise that you are a limited edition and you are a miracle in this world. You aren't an accident nor is your life an accident. Troubles and mistakes don't define you but only shape you, people's opinion don't define you and you have so much greatness in you. You can do anything you put your mind into and you deserve all what life can offer, You deserve to be happy, live a good life and have good relationships. If you begin to look at yourself in that focus you begin to develop passion to progress.

3.  Have a Positive mindset: You need to have a mindset that things are working for good and you aren't at a disadvantage. Develop that positive mindset about life. Ignore the negative opinions that always come into your mind most of the times.
If you want to progress you must develop passion.

TENGENEZA UTARATIBU WA KIUONGOZI WA MAISHA YAKO

Pasipo utaratibu mambo huenda mrama. Pasipo uongozi thabiti lazima kuwe na machafuko. Ili uweze kuwa na uthibiti katika maisha lazima kuwe na utaratibu na lazima kuwe na uongozi thabiti. Wewe ni kiongozi wa maisha yako.

Usipokuwa na uongozi binafsi na utaratibu wako wa utendaji lazima utakuwa mtumwa wa uongozi na utaratibu wa mwingine. Mikwaruzo hutokea pale mamlaka zinapokinzana. Pale ambapo kunakosekana uwiano baina ya uongozi binafsi na uongozi unaokuzunguka. Pale ambapo kunakosekana uwiano baina ya utaratibu binafsi na utaratibu unaokuzunguka.

Usipokuwa kiongozi wa maisha yako utawapa wengine fursa ya kushinikiza mambo katika maisha yako na hii itakujengea hali ya kukosa furaha kwa maana utakuwa unashindana na nafsi yako inayotaka kuwa kiongozi lakini imekosa utaratibu wa kiungozi.

Uhuru siku zote una gharama, Huwezi kuwa huru kama unaogopa gharama ya kuwa huru. Nafsi yako inataka kuwa huru lakina usipojenga utaratibu na uongozi wa ndani wa hisia na maamuzi ni vigumu sana nafsi yako kuwa huru.

Je unawezaje kujenga utaratibu na uongozi wa maisha yako:-
1. Usisimame katika msingi wa hisia: siku zote ili kuwa na utaratibu na uongozi katika maisha lazima ujenge msingi imara katika nafsi yako. Na hisia sio msingi imara maana hisia hubadilika kila wakati, huwezi kuwa kiongozi wa maisha yako kama unaenda kwa hisia. Ukienda kwa hisia utajikuta unaendelea kuvipa nafasi vitu ambavyo havitakiwi kupewa nafasi kwa wakati huo.

2. Ongeza maarifa na ufahamu : Huwezi kuwa huru na kuwa kiongozi wa maisha yako kama ufahamu na maarifa yako vina ukomo. Hakuna jambo baya kama uhuru na ujinga. Huwezi kuwa mjinga halafu ukawa kiongozi wa maisha yako. Ujinga ni utumwa ndio maana kuna maandiko yanasema Utaijua kweli nayo kweli itakufanya huru.

3. Tengeneza sheria za maisha yako: lazima utengeneze msingi mgumu tofauti na hisia. Ukishakuwa na maarifa tengeneza sheria zako mwenyewe na hakikisha huzivunji sheria hizo maana ni changamoto na itakuumiza zaidi pale unapovunja sheria zako mwenyewe.

4. Fanya vitu kulingana na vipawa na karama zako : Huwezi kuwa kiongozi bora wa maisha yako kama haujipambanui na wengine. Usiwe mtu wa kufata upepo...Zig ziglar alishawahi kusema kuwa Uongozi sio kufuata njia iliyopitwa na watu bali ni kutafuta njia yako na kuacha alama. Ukiwa mtu wa kujilinganisha na wengine huwezi kuwa na utaratibu wako mwenyewe.

5. Jiamini : Dhana ya kujiamini ni pana sana. Katika jambo lolote lile usipojiamini huwezi fanya chochote, jiamini katika maamuzi yako, jiamini katika unayofanya. Wengi wanashindwa hata kufanya maamuzi magumu kwasababu ya kukosa kujiamini. Kama unataka kuwa kiongozi wa maisha yako jiamini ikiwemo huweze kufanya maamuzi na kuwa tayari kuwajibika kutokana na maamuzi yako.

* Hakuna jambo litakalokupa amani na furaha kama kutambua kuwa una uthibiti wa maisha yako. Ni jambo litakaloongeza ari ya utendaji wako na pia kukupa morali na msisimko wa kila siku wa maisha.

Sunday, September 4, 2016

PATA MAPUMZIMKO UONGEZE UFANISI

Moja ya mambo ambayo unatakiwa ujijengee katika maisha yako ni kupumzisha akili yako. Akili ambayo inakosa mapumziko huwa na uzito kuchukua hatua na hata kupata majibu ya maswali yanayokuzunguka.

Kupumzika ni zaidi ya kulala au kutofanya kazi bali kupumzisha akili ni kuacha kwa muda kufanya mambo fulani au kujishughulisha kwa mambo fulani. Maisha bila mapumziko hukosa msisimko na kuna wakati utajikuta bila ari ya utendaji kwasababu hukuweza kuupa mwili na akili mapumziko.

Muda wa kupumzika sio muda wa kuendelea kutumia simu au kuangalia runinga. Unachofanya pale ni kuendelea kuishughulisha akili na kujiweka wazi kwa fikra asi zinazochosha akili. Muda wa mapumziko ni muda wa kuweka pembeni stress na mawazo juu ya misukosuko na changamoto zinazokuzunguka.

Kuna watu ambao husema kupumzisha akili hakuyafanyi matatizo yaondoke, ni kweli lakini kupumzisha akili ni kuiwezesha kupata majibu ya matatizo hayo. Usidhani kuwa kupumzika ni kupoteza muda au kuwa mzembe.

Kuna usemi unasema kuwa "more than working hard, work smart", bila akili nguvu hupotea. Lazima akili ipumzishwe ili ilete ufanisi unaotakiwa. Njia nzuri ya kupumzika ni wakati wa kukaa kufurahia uzuri wa maisha na kutafakari mema.

Maandiko husema kuwa siku ya saba Mungu alipumzika na kufurahia uumbaji wake. Wakati wa mapumziko ni wakati wa kufurahi uzuri wa maisha. Katika wakati huu iache akili yako ifurahie uzuri wa maisha na mambo mazuri. Wengine hujitenga kabisa kwa muda na watu wengine.

Ukiona unakosa furaha ya maisha na msisimko wa kazi jiulize ni wakati gani uliopumzika, ni wakati gani umepumzisha nafsi yako, mara ya mwisho kufurahia uzuri wa maisha na kutafakari mazuri ni lini?

Friday, September 2, 2016

JINSI YA KUKABILIANA NA VIKWAZO

Moja ya changamoto tunazokumbana nazo katika maisha ni vikwazo vinavotukwamisha kufikia malengo au yale tunayoyahitaji. Kuna vikwazo vya nje na vikwazo vya ndani. Maana halisi ya kikwazo ni jambo linalokuzuia kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

Vikwazo vinaweza kuwa watu, tabia au hata mifumo ya utendaji. Unapokuwa mtu wa kutafakari maono yako na hapo ulipo utatambua ni aina gani ya kikwazo unachokumbana nacho. Kikwazo siku zote kina namna yake ya kukiangalia ili uweze kukiondoa au kukivuka.

Lazima ujitafakari ni kikwazo cha namna gani unachokumbana nacho na ni nini unaweza kufanya kukivuka hicho kikwazo. Pasipo kukaa chini kujitafakari vikwazo vinaweza kuwa sababu yako ya kulaumu, kulalamika na kujenga mtazamo asi wa maisha.

Njia pekee ya kuvuka kikwazo ni lazima kwanza ujue na uwe na picha halisi ya lengo lako au hatma yako, kisha lazima utulize akili na kisha ukitazame kikwazo kilichopo mbele yako na ukitambue kuwa ni kikwazo cha namna gani.

Kisha ni muhimu sasa kuangalia kikwazo hicho kina mguso gani katika mfumo wako wa kukabili mambo, je hicho kikwazo kinahitaji ufanye mabadiliko gani kwa upande wako, kisha yakupasa uangalie fursa zilizopo za kuweza kukivuka hicho kikwazo.

Kumbuka usipokaa ukatafakari utakuwa unavamia vikwazo na vinakuwa na mguso wa ndani katika nafsi yako kupelekea wewe kukosa kabisa ari na hata morali ya kufanya mambo kupelekea kukata tamaa na kupoteza kabisa mtazamo chanya na maisha.