Tuesday, August 16, 2016

JE UNA UHUSIANO NA UNACHOKIFANYA

Changamoto kubwa watu wengi wanayokutana nayo katika mambo wayafanyayo ni kukosa uhusiano wa kihisia baina yake na akifanyacho. Lazima kuwe na msingi na uhusiano wa kihisia na kinafsi baina yako wewe na unachokifanya.

Ukikosa huo uhusiano lazima ukose hisia ya kuridhia na kuridhika kwa kile ukifanyacho. Bado katika nafsi yako kunakuwa na utupu ambao husababisha hisia za upweke katika kila ukifanyacho. Kuna watu wengi wanafanya kazi au shughuli lakini wana upweke kwa yale wayafanyayo.

Nafsi yako inakosa uwiano na kile ukifanyacho. Uwezo wako unakosa msukumo kuelekea kile ukifanyacho. Ni changamoto kubwa pale unapotaka likizo ili upumzike kihisia ktk kile ukifanyacho maana kazi ya nafsi yako huwa haina likizo ya kihisia.

Ukiona msukumo wako unapungua na hauna ile shauku ya kuongeza msukumo kiutendaji katika jambo fulani ni dhahiri wewe na hilo jambo hamna uhusiano wa kimsingi wa kinafsi na kihisia. Lazima kuwe na uhusiano, tafuta jambo ambalo lina mahusiano na nafsi yako.

No comments:

Post a Comment