Sunday, August 21, 2016

MSISIMKO WA MAISHA

Je umekosa msisimko wa maisha? Jizamishe katika kazi unayoiamini kwa moyo wako wote, iishi kazi hiyo, na utapata furaha ambayo haukuidhania-Dale Carnegie

Moja ya changamoto kubwa kwa watu sasa hivi ni kukosa msisimko na msukumo wa maisha, Moja ya viashiria vya kukosa msisimko wa maisha ni upweke, lawama na kukosa msukumo wa kufanya mambo. Watu wanakosa ile furaha ya kuamka jumatatu asubuhi, wengine hadi wanaingiwa na hisia hasi ikifika jumapili jioni.

Changamoto hii inatokana na mazoea ya watu ya kufanya mambo wasiyoyapenda, mambo ambayo hayana uhusiano na hulka zao. Watu wanafanya kazi lakini kwa lengo moja nalo ni kupata pesa pasipo kuwa na ridhaa katika nafsi zao. Kwa mujibu ya mwanasaikolojia Abraham maslow binadamu anasukumwa kukua na mambo mengi lakini kuu kuliko yote ni nafsi yake kuridhika.

Nafsi yako isiporidhika na kuridhia kazi unayofanya jua kabisa lazima utakosa msukumo na furaha katika kazi hiyo. Utaanza kuingiwa na hisia hasi kila unapokumbuka kwamba kesho yake kuna kazi. Steve Jobs aliwahi kusema kuwa kama hujapata kitu unachokipenda endelea kutafuta maana maana kuu ya maisha ni kutafuta kusudi lako na kulifanya.

Kama kwa mtazamo wa Dale carnegie inatupasa kujizamisha katika kazi tunayoiamini kwa mioyo yote na kuziishi kazi hizo utapata furaha na hautokaa kusubiri Jumatatu ifike uruke katika kazi ya moyo wako na uzuri ni kwamba ukiishi kazi ya moyo wako hautokuwa na likizo.

No comments:

Post a Comment