Thursday, May 18, 2017

IMANI NI MSINGI WA AMANI YA NAFSI

Imani ni kuwa na hakika ya mambo yasiyoeleweka au ambayo hayajabainishwa kwa wakati huo. Imani hukupa nuru ya kutambua mafumbo ya kinafsi na maswali yasiyo na majibu yenye kuleta taharuki katika nafsi.

Nafsi inaweza kupitia mambo fulani ambayo yanaikosesha amani na kuifanya ibaki katika hamaki kutojua ni nini kinachofuata au nawezaje kutoka katika hali fulani ya mkwamo wa kihisia au kimtazamo na kiakili. Hapo ndipo imani huja kuleta amani.

Imani inatakiwa iongoze hisia na iziweke katika hali ya utulivu. Ni vigumu kupata tulizo la kihisia bila kuweka mfumo bora wa kiimani, Ukitazamia kutoka katika mkwamo huo, ukitazamia utulivu wa hisia na ukitazamia uzuri na mambo mema yajayo.

Muda wote imani hujengeka katika msingi imara wa hatma ya kesho yenye furaha, faraja na uzuri na pia hujengeka katika faida ya leo katika mazingira hayo magumu. Imani hutazama fundisho, hutazama uzuri na  hutazama uimara unaotokana na ugumu na changamoto husika.

Siku zote ukitaka kuwa na amani katika nafsi yako boresha mfumo wako wa imani, boresha mfumo wako wa kuamini, jikite katika kutengeneza imani zenye tija, imani zenye kukujenga na kukuimarisha. Na ukishapata msingi husika iache imani hiyo iamuru hisia zako zitii.

Imani ikisema nitatoka katika hii hali, ikasema nitavuka katika hili daraja la maumivu, ikasema nitapata kilicho bora, Hakuna hisia ya maumivu itakayoweza kukushikilia kwa muda mrefu au hata kukuzamisha. Utakuwa ni mtu mwenye amani muda wote.

Thibitisha imani zako kwa kuzipa msingi imara kwa kuzifanya sheria za nafsi yako. Imani juu ya uzuri wako, imani juu ya stahiki yako na yale unayoyatarajia na yenye kukupa amani ya nafsi, hakikisha unajijenga na kujithibitisha katika imani hizo kwa kusimama bila kuyumba kama hisia za taharuki na uchungu zikija.

Huwezi kuwa na amani ya nafsi kama huna imani na hali fulani, kama huna imani na jambo fulani, kama huna imani na watu fulani. Ni vyema ukajiimarisha katika imani na siku zote hakikisha imani yako inajengeka katika kweli. Huwezi jenga imani kwa kitu cha uongo. Imani lazima isimame katika misingi ya kweli, fikra chanya, ubora wa nafsi na utu.

Monday, May 15, 2017

CHUNGA MOYO WAKO

Chunga moyo wako maana hiyo ndiyo bustani ya amani na furaha yako. Nafsi yako hustawi katika bustani ya moyo wako. Katika bustani ya moyo wako kunaweza kuwa na maua ya furaha, amani na faraja au magugu ya maumivu na uchungu. Kuwa muangalifu sana kwa kuchunga moyo wako kila wakati ni nini kinachoota.

Kuna mawazo na maneno ambayo ukiyaruhusu yaingie moyoni yanaenda kuweka majeraha ambayo kupona kwake kutakuchukua muda sana. Majeraha hayo yatajenga mfumo wa kifikra wa kujihami ili kuzuia maumivu mengine. Hasara ya fikra za kujihami ni kwamba utashindwa kufurahia uhuru na uzuri wa maisha kwa kuwa utaishi kwa kujihami.

Moyo wako unatakiwa ulindwe kama ngome imara. Ukiruhusu maumivu au matatizo yakaingia katika bustani ya moyo wako yataenda kuotesha magugu ya mawazo na fikra hasi. Kuna maneno ukiyaruhusu kuingia siku moja yatautesa moyo wako wakati wote. 

Safisha moyo wako kwa kuondoa yale ambayo yanauumiza na kutesa moyo wako. Yale ambayo kila ukiyafikiria unasikia kama kichomi ndani ya moyo wako, yale ambayo kila ukiyapa nafasi katika akili yanakububujisha machozi ya uchungu moyoni mwako.

Tambua kuwa moyo wako unatakiwa kustawisha amani, furaha na upendo. Ukiwa na moyo wenye uchungu inageuka kuwa sumu inayodhoofisha nafsi yako na akili yako. Utakuwa mtu mwenye vifungo badala ya uhuru.

Chunga moyo wako na uache katika amani. Usiuache umekaa katika dimbwi la maumivu au usiuache ushikilie uchungu unaokuumiza, usiuache ushikilie maneno makali au misumari ya mitazamo hasi juu yako. Usiruhusu moyo wako udunde kwa kasi kwa kukosa amani au kuwa na taharuki, Jipe utulivu kwa kuruhusu uzuri na furaha istawishe moyo wako.

Ruhusu yale yenye furaha na amani na yenye uzuri na utulivu ndio yakae katika moyo wako. Stawisha moyo wako ili ukutunze na uachilie yale yenye furaha, amani na pumziko. Kama vile damu inavoingia na kutoka katika mkondo wa mishipa ya damu, wewe pia tengeneza mkondo wa kuingiza furaha nyingi, amani nyingi na faraja nyingi moyoni mwako kwa kukaa na watu au mazingira yatakayosaidia hivo vitu lakini ondoa moyoni mkondo wa maumivu, uchungu na yale yanayoutatiza moyo

Lazima kuwe na uwiano baina ya yanayotoka na yanayoingia, usipende kuingiza mawazo hasi, Itafute hiyo furaha na amani ili ustawishe bustani ya moyo wako.

Fikra chanya au mazingira chanya sio tu yale yanayokusukuma kufanikiwa bali pia kuustawisha moyo wako na kuuacha katika hali ya utulivu.

Saturday, May 6, 2017

ALWAYS KEEP A JOYFUL DEMEANOR

Our strength lies in our ability to always keep a joyful demeanor in the face of our problems-Nickvaleries

Life has its ups and downs, Life has negative situations that can hit us or hurt us and we find it hard to be joyful but joy has to be founded from our souls.

When we believe in our worth and have the mentality that there is always something better ahead and that we will always receive the desires of our souls then we generate a joyful spirit and demeanor.

There is no reason to stay in sorrow and pain when you know that the best is out there heading your way and you ought to be ready and step towards it. Pain and sorrow will try to drown you in a state of emotional stagnation but rise up, smile and say to yourself that am heading to my best. Darkness is for a night but joy comes in the morning.

Always choose to be joyful and find joy at whatever costs by changing your belief from a victim to a victor of circumstances. If things change dont stay there drowning yourself. Get up and heal your soul of the pain and choose to keep a joyful demeanor.

Just say to yourself it is well with my soul then believe that you are heading for the best out there. Tell your heart you are not hurt but you are strengthened then find your rythm and be happy. Smile for your beauty and peace awaits.

The Universe will always smile back if you smile at it. Its just a matter of time till you find love, happiness and joy again. But for now keep a joyful demeanor and attitude.

Tuesday, May 2, 2017

USICHUKULIE KILA JAMBO KIHISIA

Ukitaka kuwa na furaha usipende kuchukulia kila jambo kinafsi au kihisia. Kuna mambo mengine ni ya kifikra tu na yamekaa kimtazamo tu ambayo hayatakiwi kuchukuliwa kihisia.

Ukitaka kuwa na utashi wa kihisia na uweze kuratibu hisia zako katika mlengwa chanya yakupasa kuziacha hisia zako katika mfumo tulivo kadri uwezavyo. Kuna mambo ukiyachukulia kihisia utaziweka hisia zako kwenye mfumo wa taharuki kwa wakati mwingi na itakupunguzia msisimko wa maisha ulio katika muundo chanya.

Je wawezaje kutochukulia mambo kihisia? Tambua kuwa kila wazo au mtazamo unapaswa kupokelewa kiakili na kuratibiwa kabla ya kusukumwa na hisia fulani. Ni vizuri ukiratibu mawazo na mitazamo unayopokea na kuiratibu kabla ya kujua ni hisia gani uiachilie ili isukume hilo jambo.

Ni muhimu sana kulishikilia wazo au mtazamo katika mfumo chanya hata kama limekuja katika muundo hasi. Lione hilo wazo kama njia ya kukuboresha, yaone hayo maoni kama njia ya kukuboresha kisha yape hisia chanya ndipo uyapokee. Usikubali kuanza kupokea kihisia wazo ambalo hujariratibu kwa akili.

Mfano mtu anaweza kukwambia jambo ambalo unaona kabisa linaweza lisiwe chanya kwako, badala ya kulipokea kwa hisia hasi jaribu kuliona ilo jambo kama wazo la kukuboresha na sio kukuharibu, kisha chukua hisia ya amani na furaha kwa kutambua kuwa hilo wazo limekuja kukuboresha..kisha chukua hisia ya morali na ari ya kulitafutia ufumbuzi na kulishughulikia hilo jambo na sio vinginevyo. Ukilipokea kama vile limekuja kukuumiza utaingiwa na taharuki ya kinafsi pengine hata kujenga ukuta kulizuia hilo suala na kuonekana kuwa ni mtu dhaifu kinafsi pengine hata mtu hasiyependa kuambiwa ukweli.

Nakushauri tena usilipokee kila jambo kihisia kabla ya kuriratibu kiutashi na kiakili ili kukujenga utashi wa kihisia itakayokupa furaha wakati wote.

Sunday, April 23, 2017

TAFUTA AMANI YA NAFSI

Hakuna jambo lenye msingi katika uimara na utashi wa nafsi kama amani ya nafsi - Nickvaleries

Huwezi kukua katika utashi wa nafsi pasipo kuwa na amani ya nafsi. Imani ikikaa katika nafsi humuwezesha mtu kustahimili misukosuko ya nje kwasababu kinachoweza kuzamisha meli sio bahari bali maji yanayoingia ndani ya meli.

Ukiweza kuiacha nafsi yako katika usalama kwa kujenga ukuta kuzuia yale yanayotokea yasiondoe amani ya nafsi utaweza kustahimili mengi. Ukikosa amani lazima utakosa imani na ukikosa imani hata utendaji wako na maneno yako yatakwenda kinyume na uhalisia.

Jiulize ni mambo gani ambayo unayaruhusu katika nafsi yako...Je yanaimarisha ngome za utulivu wako au yanabomoa amani ya nafsi yako na kukupa hali ya taharuki. Waweza kuwa na vyote ukakosa amani na ukikosa amani ukakosa imani huweza kuwa na furaha.

Hakuna furaha mahali palipokosa amani...Huwezi kuwa na furaha ya nafsi au kufurahia yale mazuri yanayokuzunguka kama ukikosa amani.  Tafuta kuwa na amani na jiimarishe kinafsi ukiziimarisha ngome za nafsi yako.

Jitahidi kujenga ngome zenye usalama ndani yako kiasi cha kusimama imara kinafsi hata kama mazingira ni yenye taharuki..sikiliza ulimwengu una taharuki na ukikosa amani jua huwezi kuwa na furaha.

Amani inaweza patikana kwa kuimarisha misingi ya uaminifu, mawasiliano, utashi wakihisia na utu. Tambua kwamba kila jambo linafanyika kuwa jema na wewe ni mwenye hatma njema na kuna mambo mengi mazuri ambayo yako mbele yako.

Taswira yako ni ya muhimu sana ukitaka kuwa na amani. Je unaangalia nini na unasikiliza nini? Hakikisha umejiimarisha kuratibu kila kinachoingia katika nafsi yako.

Usipende kuyapa muda mwingi mawazo na mazingira yanayoondoa amani yako. Itenge nafsi yako ili iwe na amani.


Tuesday, March 28, 2017

JENGA UTASHI WA KIHISIA

Uimara wa mtu katika nafsi umejikita zaidi katika utashi wake wa kihisia. Binadamu ni kiumbe chenye nafsi na nafsi ya mtu imeundwa katika mfumo wa hisia. Hisia za mtu pia zimeundwa katika mfumo wa utu wake. Kila mtu ana muundo wake wa kiutu ambao ndio msingi hasa wa uratibu wa hisia za mtu huyo.

Hisia ni misukumo na mihemko ya kinafsi ambayo hujitokeza kutoka kipindi hadi kipindi kutokana na mabadiliko ya ndani au nje. Yaweza ikawa mabadiliko ya kimazingira au mabadiliko ya tabia za mwili. Changamoto kubwa ya hisia ni kwamba ni kama upepo, huja na kufika katika kilele lakini baadaye hushuka katika ukawaida na pengine hushuka zaidi ya hapo.

Hapo ndipo wengi hujikuta wanasema leo najihisi niko chini sana kihisia au nimezama katika hisia na hata wengi hutumia kauli za vitabu vya dini na kusema leo nimezama katika bonde la uvuli wa mauti. Lakini hao hao watu nyakati nyingine utasikia anasema leo nina msisimko au leo niko hewani. Yote hayo ni mabadiliko ya kihisia.

Hisia zinaweza kuwa nzuri kama zikitumika vizuri lakini changamoto kubwa ni pale mfumo wa uratibu wa kimaamuzi katika akili unapofungwa katika hisia ambazo zinapanda na kushuka. Kuna ambao wamekuwa na utashi wakufikiria lakini wamekosa utashi wa kihisia.

Utashi wa kihisia ni uwezo wa kuratibu hisia zako na kuzielekeza vile unavotaka. Watu wengi tumekuwa na utashi wa ki akili lakini tumekosa jambo la muhimu sana ambalo ni utashi wa kihisia kupelekea yale tunayoyajenga kwa akili zetu yanaharibiwa na hisia zetu.

Waweza fikiria jambo zuri na ukaliwekea mikakati madhubuti lakini kinapofika kipindi cha mtikisiko unaogusa hisia ,wengi wetu tumejikuta tukiruhusu hisia zetu ziharibu hata ule mtazamo chanya wa yale tuliyoyajenga kwa akili zetu.

Watu wengi waliofanikiwa au wakuu wamejikuta wakianguka na kufanya maamuzi mabovu kwasababu ya kukosa utashi wa kihisia na wamejikuta wakizama katika dimbwi ambalo pengine kusababisha zile imaya walizozijenga kwa akili nyingi kuanguka kutokana na kukosa utashi wa kihisia.

Wekeza sana kuwa utashi wa kihisia uweze kutambua ni hisia zipi zinakujenga na zipi zinakubomoa. Hisia zipi zinakuimarisha na hisia zipi zinakudhoofisha, hisia zipi zinakuinua na hisia zipi zinakuangusha. Ukiwa na utashi wa namna hiyo utaweza kuzitumia hisia hizo ziweze kukutumikia na sio wewe kutumikia hisia zako.

Je wawezaje kuwa na Utashi wa kihisia

1. Pambanua hisia zako pindi zinapokuja na utambua mlengwa wa kila hisia.

2. Tambua chanzo cha hisia husika au mifumo sababishi ya kutokea kwa hisia hizo.

3. Jifunze kuzimudu hisia kila zinapokuja kwa kuifanya nafsi yako izungumze na hisia hizo

4. Tambua kuwa hisia sio jambo baya na wala sio udhaifu bali ni muundo wa kinafsi hivo hisia zako zikubali kuwa ni zako na wewe ndio mwenye kuwajibika kwa hisia hizo. Usitafute kisingizio juu ya hisia zako.

5. Jiimarishe katika uvumilivu ili uweze kuziratibu hisia zako na kuratibu mkondo wa hisia zako maana hisia ni kama mkondo wa maji

6. Pendelea kutenga muda wako wa upekee ukizungumza na nafsi yako ili uweze kuthibitika katika uimara wa kihisia.

Hakuna jambo la msingi na lenye kufaa kama kuwa na utashi wa kihisia maana maisha yako yanaweza kuwa yenye furaha na amani au kuwa na shida na maumivu kama hauna utashi wa kihisia.

Saturday, March 25, 2017

MUDA WAKO WA UPEKEE NA NAFSI YAKO

Ukitaka kuwa na furaha anza kwa kufurahia muda wako wa upekee.

Moja ya changamoto tulizonazo kama binadamu ni upweke. Upweke sio ukosefu wa wenza au watu wa kutuzunguka. Upweke ni pale mtu anaposhindwa kuufurahia upekee wake na anaposhindwa kuwa na uhusiano na uhalisia wa nafsi yake.

Kuna malalamiko mengi unasikia hata katika mahusiano mmoja wao anasema nilijihisi mpweke ndo maana nilikusaliti, au mwingine anaingia katika ulevi au hata mikanda ya ngono kwa sababu ya upweke. Tafsiri yetu ya upweke ni kukosa watu wa kutengeneza muungano wa kinafsi au watu wa kuburudisha nafsi zetu.

Nafsi ya binadamu kila wakati inahitaji kurutubishwa kwa kutengewa muda wa kupata uwepo. Nafsi yako ni utu wako wa ndani. Mtu wako wa ndani anahitaji wewe umtengee muda kumsikiliza, kumdadisi, kuzungumza naye, kumburudisha na hata kumponya na aina yeyote ya maumivu.

Lazima ujitengee muda wako wako bora wa kutengeneza mguso wa kimaelewano na nafsi yako. Watu wengi wameshindwa kuwa watu wa namna hiyo kupelekea kupigwa na upweke kila wakati anapokosa mguso wa nje wa watu wanaomzunguka.

Rafiki yako wa kwanza na wa karibu ni nafsi yako. Itengee muda nafsi yako ili ipate ukaribu wako. Na wakati wa kuzungumza na nafsi yako jua kwamba unaongea na mtu wako wa karibu. Acha kuongea na nafsi yako kwa ukali au kuihukumu kwa makosa ya nyuma. Itie moyo nafsi yako, ikumbushe uwezo wako. Panda mbegu chanya ndani ya nafsi yako, itie moyo, iponye kwa makosa ya nyuma na iahidi mambo mazuri huko mbele, iburudishe kwa lugha nzuri yenye mguso chanya lakini kuu kuliko yote iweke huru.

Watu wengi wamekuwa wakitumia wakati wao wa upekee kwa kulala, kuangalia mitandao ya kijamii au hata kutafuta magenge ya umbea kutafuta jambo la kufanya kuondoa upweke nk. Huo sio wakati wake. Huo ni wakati wa kujenga uhusiano na nafsi yako. Ni sawa na aina yeyote ya uhusiano. Lakini uhusiano wako na nafsi ndiyo jambo la msingi kwanza.

Ukiwa na tabia ya kuwa na muda mwingi na nafsi yako hautokuwa mtu wa kulalamika upweke. Na hautokuwa mtu wa kutafuta vileta msisimko vya nje kama pombe, anasa na ngono pale unapojihisi mpweke. Utaufurahia muda wako wa upekee, nafsi yako itarutubishwa na utakuwa ni mtu mwenye furaha muda mwingi.

Angalizo ni kwamba katika muda wako wa upekee na nafsi yako hakikisha unatengeneza mazingira chanya. Huwezi kutengeneza mazingira hasi ya mawazo na hisia hasi au muingiliano na mambo yasiyojenga halafu utegemee nafsi yako itajiachilia. Nafsi yako itajenga ukuta wa kujihami maana ndivo mwanadamu alivo kiakili katika maisha yanayoonekana kama mapambano.

Pia usipende kuipa nafsi yako maumivu yasiyokuwa na sababu na mara nyingi pale akili yako inaposhindwa kuendana na misingi ya nafsi yako. Na usipende kuipa nafsi yako vifungo kwa kufuata njia ambazo unajua nafsi yako haiwi huru kuchanua.

Thursday, March 16, 2017

KUWA NA UHUSIANO NA UHALISIA WAKO

Kila binadamu ana uhalisia wake na utofauti wake, binadamu wanaweza fanana tabia lakini kuna msingi wa ndani kabisa wa kinafsi unaowatofautisha. Huu msingi wa kinafsi ndio uhalisia wa yule mtu. Mtu yeyote anayetoka katika uhalisia wake anapoteza utambulisho wake na akipoteza utambulisho wake anapoteza mambo mengi ya kinafsi yaliyomo ndani yake maana inambidi atafute uhalisia mwingine na alazimike kuishi katika uhalisia huo.

Kuna mambo mengi ya kinafsi ambayo mtu hupoteza na kuu kuliko yote ni amani ya nafsi na furaha ya ndani. Hapo ndipo unakutana na mtu ana kila kitu lakini hana furaha wala amani, yamkini kuna mambo kadha wa kadha yanayomtatiza lakini kuu kuliko yote ni kupoteza uhalisia wake. Kuna mambo yanayompa mtu ujasiri wa ndani, kuna misingi ya kinafsi ambayo mtu anakuwa nayo inayompambanua. Akipoteza hivo vitu au akitoka nje ya hivo vitu utaona mabadiliko yake kimtazamo na hata kihisia.

Katika uratibu wa kihisia na kutengeneza uimara wa kihisia mtu lazima arudi katikà uhalisia wake. Watu wengi wamepoteza dira katika mambo mengi kwasababu walitoka katika uhalisia wao ndipo wanakuja kushtuka wameshapotea na wakajikuta wanaishi kama wahanga wa mambo pasipo kujua nini cha kufanya.

Jitambue na jitambulishe na jiimarishe katika uhalisia wako maana utakapokuja kutoka katika uhalisia huo utajaribu kuwa kitu au mtu ambaye haumuelewi hata wewe. Unakuwa kama mtu usiyejitambua, Rudi katika uhalisia wako ili urudishe ile morali na msukumo na msisimko wa ndani kufanya mambo.

Ukiwa katika uhalisia wako mazingira ndo yatalazimika kuendana na uhalisia wako lakini tofauti na hapo wewe ndo utalazimika kuendana na mazingira. Uhalisia hukupa wewe uhuru wa kujipambanua na kujiwasilisha katika jamii ili uwe na mguso chanya. Uhalisia wako ndio hupelekea wewe kutambua kusudi lako na hata kuongeza thamani yako ili ulitende kusudi lako. Hivo ni muhimu sana kuwa katika uhalisia wako.

Jamii au mazingira yasikufanye upoteze uhalisia wako. Jamii ndo inapaswa ipishe njia ili uhalisia wako uweze kuwa na mguso na hii itawezekana tu ukisimama katika kulinda uhalisia wako

Sunday, March 12, 2017

HOW TO DEAL WITH FEAR

Do you know that fear is false evidence appearing real? Sometimes in life you will be faced with situations whereby there will be evidences that are false appearing real. Fear will torment you and leave you paralysed. The only cure to fear is faith. Believe beyond circumstances. 

Clear your mind of the Past : You will always be free as your mind is free. The battlefield is always in your mind. Its a point where strongholds of the past are. The strong holds of fear and other dissapointments. Experience should make you wiser in terms of strategies and how you perceive life. But always free your mind as much as possible.

Something is about to happen in your life: Things happen all the time, good or bad but its always dark before dawn. We pass through darkness to experience the light. We pass through trouble to appreciate calmness. No darkness comes after darkness until afternoon passes. Always believe that the next phase of your life will always be better than the previous. Try to find the rainbow after the storm because its there. Dont be afraid that later will be like the former. There will always be changes in every stage of your life.

Find beauty and peace: You will never be happy unless you are at a state of beauty and peace and tranquility. We often look at the beauty without but not the beauty within. We all want to be in tune with our inner self. Our core values and our inner being, but we often times try to find this in the wrong places. We should always be in the quest to find beauty and nirvana and where its connected.

Wednesday, February 22, 2017

BENEFITS OF KNOWLEDGE AND ADVENTURE FOR EMOTIONAL INTELLIGENCE

Our minds and souls are constantly in need of exploration and discovery. The reason why we act differently and evolve is because our souls seek new horizons. Our minds need to be refreshend and expanded so as we can stable in our actions and in our ways. As it is said Lunacy is doing the same thing the same way and expecting different results.

We act in a lunacy form whenever we fail to expand our minds and let our souls explore its limitlessness. Knowledge is essential for expanding our minds increasing our possibilities and widening the limits that have been set by ignorance. We must grow in knowledge so as to be free. Emotional intelligence being the ability to perceive, assess and manage our emotions is a crucial attribute to our stability as human beings.

If we invest in knowledge while we let our souls experience wonder we invest in the attribute of emotional intelligence. We not only grow in our ability to manage our emotions but we develop control as to how we can relate our knowledge in a practical way to see wonder and adventure.

How can Knowledge and adventure be used simultaneously for emotional intelligence

1. Always read books of a specific topic in the specific moment at the specific place. That's Practical investment of knowledge.

2. Knowledge has to be put into practise, acquiring knowledge without practising it is a wastage of time. Ensure to always acquire the kind of knowledge you can practise.

3. Explore new horizons, listen don't let your life become a routine of activities that don't allow your soul to explore and experience the adventures of your life time.

4. Visit nature occasionally and meditate on it. This will open your mind and trigger your soul to explore the adventures of naturality.

Always remember that without emotional intelligence we will always be unstable human beings. If emotions aren't managed and assessed skillfully then we will always be human beings of so many imbalances and we will live life not realising the beauty of it.